Wananchi Chunya wamwambia RC Chalamila wagonjwa wanaotapika damu wako 22, RC aagiza wapelekwe hospitali ya Rufaa

Wananchi Chunya wamwambia RC Chalamila wagonjwa wanaotapika damu wako 22, RC aagiza wapelekwe hospitali ya Rufaa

inaleta taharuki, bora uende kimya kimya tuu

Si kuwa taarifa sahihi zinawafanya watu kuwa makini zaidi?

Haka ka hali ka kuonana wengine kama watoto wadogo kanakera na kupalilia chuki tu:

 
Sasa ule waraka unakuwaje? Kiukweli yule mama ni mkurupukaji mno na alimuoteshea kibarua majani daktari wa watu...kazi kujali kumfurahisha mwamfulani wkt watu wanateketea.... ITV sa itakuwaje..wataombwa radhi?
Acha kuwa mjinga!Na hili limezidi kuwa tatizo kwa watanzania wote. Yule Mama hafanyi vile kwa matakwa yake.Anafanya vile kumuwakilisha Magufuli. Ile siyo yule Mama ni Magufuli.Asipofanya vile hana kazi, hana tonge la kila siku! Mzizi wa tatizo ni Magufuli.
 
Tusiongelee possibilities kwenye uhai wa binadamu. Kama ni sumu au maji yaliyochaguliwa kuna maabara za kuchunguza hayo yote. Tusianze kupiga ramli kama wale wapiga manyanga.
Na huwezi kuacha kuweka pissibilities kwa aina ya dalili zinazotajwa, na pia inaonesha si ugonjwa unaoambukiza ndio maana kwa muda mrefu upo eneo hilohilo.

Sasa na hao Madaktari waliosomeshwa huko Chunya miaka yote hiyo hawakufanya chochote kujua tatizo ni nini?...maana nawasikia hapa wanasema ni tatizo la muda mrefu.
 
Na sidhani hata kama ni sawa kusema "Ugonjwa usiojulikana"....ni vizuri tu kusema "Ugonjwa ambao bado haujafahamika chanzo chake".

Matumizi ya hayo maneno ya mwanzo ni ya kutishana zaidi bila msingi wowote, na hutumiwa sanasana na Jamii vivu na tegemezi, ambao badala ya kuingia maabara kujua tatizo ni nini mnakaa kulalamika mkisubiri "Mabeberu" waje ndio watuambie tatizo ni nini.

Sanasana tutakimbilia kwenye imani za kishirikina tu wala hakuna cha zaidi hapo.
 
Back
Top Bottom