Wananchi kuweka Mageti ya ukaguzi mitaani ni ishara ya kushindwa kwa Jeshi la Polisi

Wananchi kuweka Mageti ya ukaguzi mitaani ni ishara ya kushindwa kwa Jeshi la Polisi

Ulinzi shirikishi ni jambo muhimu kila sehemu. Police wachache, na waliopo wana vipaumbele vyao. Baadhi ya mitaa ilipaswa iwe na mlango mmoja wa kuingilia na kutokea ili kuepusha matukio ambayo raia wanaokaa eneo hilo wanaweza yazuia. Nchi nyingi zinafanya hivyo.
 
Pathetic fool!! Ulinzi shirikishi wakati polisi wanalipwa mishahara kwa kodi za wananchi ili kuwalinda???
Ulizi shirikishi Tanzania umeanza siku nyingi sana.Ulinzi huu ulibadilika jina ukawa ulinzi wa sungusungu.Haya yalifanyika miaka ya tisini wakati wazir wa mambo ya ndani akiwa mrema.Na hawa polisi wengine walikuwa hawajazaliwa.Na polisi walikuwepo wa nyakati hizo.Inaonekana huna idea kabisa ya haya mambo.
 
Uwiano wa idadi ya askari kwa wananchi unatakiwa uweje?tusipongeze wala kulaumu
 
Sasa hivi maeneo mengi ya Mkoa wa DSM wananchi kwa umoja wao wameamua kuajiri walinzi binafsi na kuweka Vizuizi vya ukaguzi kwenye mitaa , ukifika kigamboni au Mbezi Beach ni lazima wenyeji wako wathibishe ujio wako mbele ya walinzi , vinginevyo utaishia njiani .

Pamoja na pongezi hizi kwa Wananchi kwa kuamua kujilinda Wenyewe na wahalifu , lakini kuna tafsiri kwamba jambo hili ni ishara ya Polisi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya Halali baada ya kuelemewa na MAJUKUMU YASIYOWAHUSU YA KISIASA .
Polisi wapo busy na CHADEMA
 
Kwa swala hili mkuu acha tujilinde maana km huku kigamboni tuna uhaba wa vituo vya polisi vibaka walianza kuja kuiba ila baada ya sisi kuanza lindo sasa tunalala usingizi safi kabisa pia kama ww si mharifu unaogopa nn kuhojiwa ukisimamishwa na walinzi wetu.
Kwa mawazo yangu uhaba wa vituo vya polisi sio tatizo. Tatizo ni kutokuwa na polisi wanaozunguka mtaani kutuhakikishia usalama wetu. Hawa kwa kuzunguka mtaani ndio wangewajua watu wanaoishi humo na wangeweza kuitikia mapema pale tukio la uhalifu linapotokea. Vituo vya polisi vinawageuza watu wa mezani ambao wanangojea kuitwa tukio likitokea. Hali hii ndio inapelekea kuwa ukiripoti tukio unaambiwa kamkamate unayemshuku uwaletee! Kwa maneno mengine kazi yao wame outsource kwa raia. Kwa wenzetu, kituo cha polisi ni mtaani ambako wana patrol kwa kutumia miguu, baiskeli au magari. Tuache kuwajengea vituo, tuwanunulie baiskeli.

Amandla....
 
Kwa mawazo yangu uhaba wa vituo vya polisi sio tatizo. Tatizo ni kutokuwa na polisi wanaozunguka mtaani kutuhakikishia usalama wetu. Hawa kwa kuzunguka mtaani ndio wangewajua watu wanaoishi humo na wangeweza kuitikia mapema pale tukio la uhalifu linapotokea. Vituo vya polisi vinawageuza watu wa mezani ambao wanangojea kuitwa tukio likitokea. Hali hii ndio inapelekea kuwa ukiripoti tukio unaambiwa kamkamate unayemshuku uwaletee! Kwa maneno mengine kazi yao wame outsource kwa raia. Kwa wenzetu, kituo cha polisi ni mtaani ambako wana patrol kwa kutumia miguu, baiskeli au magari. Tuache kuwajengea vituo, tuwanunulie baiskeli.

Amandla....
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]mkuu baiskeli kweli si bora hata pikipiki watawahi sehem ya tukio
 
Hao ni wahuni, wezi, wabakaji, majambazi na wabambikiaji kesi FEKI dhidi ya Watanzania wasio na hatia ambao sasa HAWAHESHIMIWI na Watanzania wengi sana.
Sasa hivi maeneo mengi ya Mkoa wa DSM wananchi kwa umoja wao wameamua kuajiri walinzi binafsi na kuweka Vizuizi vya ukaguzi kwenye mitaa , ukifika kigamboni au Mbezi Beach ni lazima wenyeji wako wathibishe ujio wako mbele ya walinzi , vinginevyo utaishia njiani .

Pamoja na pongezi hizi kwa Wananchi kwa kuamua kujilinda Wenyewe na wahalifu , lakini kuna tafsiri kwamba jambo hili ni ishara ya Polisi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya Halali baada ya kuelemewa na MAJUKUMU YASIYOWAHUSU YA KISIASA .
 
Kwa swala hili mkuu acha tujilinde maana km huku kigamboni tuna uhaba wa vituo vya polisi vibaka walianza kuja kuiba ila baada ya sisi kuanza lindo sasa tunalala usingizi safi kabisa pia kama ww si mharifu unaogopa nn kuhojiwa ukisimamishwa na walinzi wetu.
Kama vile hujamuelewa mtoa mada. Sio kwamba napingana na wewe au yeye anapingana na wewe ila rudia tena kusoma ile uweze kuelewa mantiki ya hoja yake.
 
Pathetic fool!! Ulinzi shirikishi wakati polisi wanalipwa mishahara kwa kodi za wananchi ili kuwalinda???
subiri siku uje kubakwa,mashtaka kwa polisi kuzembea utayaleta hapa jf.

nyinyi ndio wale wanaume mlikuwa mnajifungia na wake zenu saa moja usiku kisa panyaroad.
 
Sasa hivi maeneo mengi ya Mkoa wa DSM wananchi kwa umoja wao wameamua kuajiri walinzi binafsi na kuweka Vizuizi vya ukaguzi kwenye mitaa , ukifika kigamboni au Mbezi Beach ni lazima wenyeji wako wathibishe ujio wako mbele ya walinzi , vinginevyo utaishia njiani .

Pamoja na pongezi hizi kwa Wananchi kwa kuamua kujilinda Wenyewe na wahalifu , lakini kuna tafsiri kwamba jambo hili ni ishara ya Polisi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya Halali baada ya kuelemewa na MAJUKUMU YASIYOWAHUSU YA KISIASA .
hata kununua kufuli na kuweka mlango imara kwako ni ishara kwamba jeshi halifanyi kazi yake sawa sawa!!

ni kama unataka kusema kila nyumba na mtaa,awepo polisi mmoja analinda.

kila siku nakwambia mkuu,wewe akili zako zimeliwa na siasa,zimegoma kabisa kufanya kazi kwa kujitegemea.
 
Kwa upande mmoja uko sawa, upande mwingine uko wrong. Jukumu ya serikali ni kusaidia kulinda watu na mali, lakini haiwezi kulinda kila mtu na mali yake. Labda iwe na askari milion 50 halafu sijui nani atawalipa.
 
Hivi askari polisi mmoja anahudumia watanzania wangapi?, Isije ikawa askari polisi mmoja anahudumia watanzania elfu mbili. [emoji15][emoji15]
 
Sasa hivi maeneo mengi ya Mkoa wa DSM wananchi kwa umoja wao wameamua kuajiri walinzi binafsi na kuweka Vizuizi vya ukaguzi kwenye mitaa , ukifika kigamboni au Mbezi Beach ni lazima wenyeji wako wathibishe ujio wako mbele ya walinzi , vinginevyo utaishia njiani .

Pamoja na pongezi hizi kwa Wananchi kwa kuamua kujilinda Wenyewe na wahalifu , lakini kuna tafsiri kwamba jambo hili ni ishara ya Polisi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya Halali baada ya kuelemewa na majukumu yasiyowahusu ya kisiasa .
Neighbourhood watch
 
umetaja maeneo mawili tu. mbezi beach na kigamboni? ni sehem ndogo sana ya hii nchi.
labda kama wananchi nchi nzima wameweka vizuizi.
umeweka as if ni tanzania nzima wananchi wote wamefanyahikokitu kumbe wapi. asilimia kubwa nchini hawajachukua hatua hizo.
suala la ulinzi binafsi limekuwepo miaka mingi sana. si kitu cha juzi wala jana.
lakin asilimia kubwa hawawezi ku afford hizo services.
Na hata huko ni baadhi ya mitaa tu. Ni upuuzi kuweka kizuizi kwenye barabara ya umma mtu asipite mpaka aseme anaenda kwa nani. Kwahio siwezi kukatiza mtaa huo nikatokea mtaa mwingine kuendelea na safari yangu? au mitaa yao haitoki upande mmoja?
 
Na hata huko ni baadhi ya mitaa tu. Ni upuuzi kuweka kizuizi kwenye barabara ya umma mtu asipite mpaka aseme anaenda kwa nani. Kwahio siwezi kukatiza mtaa huo nikatokea mtaa mwingine kuendelea na safari yangu? au mitaa yao haitoki upande mmoja?
una hoja
 
Gated Community ndio mpango mzima, Duniani huko huwezi ingia tu mitaa yoyote na kuzurura hovyo. Tunafurahi Tanzania nako sasa zinakuja hizo ili kina Yakhe wakae kwao na kina Mangi wawe Salama.
 
Back
Top Bottom