Wananchi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini tunakupongeza Rais Samia, ziara ya Rais kama hii haijawahi tokea toka uhuru

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,207
Reaction score
13,839

Rais Samia akiwa Iringa

Kama kumbukumbu zangu ziko sawa, ziara ya Rais Mama Samia Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini imevunja rekodi.
Sikumbuki Rais aliyezungukia mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa tena kiwilaya na kuimaliza. Kwetu Mbeya Rais kaenda Chunya, Mbeya vijijini, Rungwe na Kyela.

Marais wengine toka enzi za Mwalimu waliishia aidha kufungua miradi kwa siku moja na kuondoka siyu hiyo hiyo.
Rais Mwinyi, Rais Mkapa, Rais Kikwete, Rais Magufuli wote walikuwa a one day visit presidents. Na kama walikaa zaidi basi ni wakati wa kampeni za Urais tu.

Hivyo Rais mama Samia amejipatia sifa kubwa kwa kuonekana na watu wengi katika mikoa hii.

Kilichobaki sasa ni kutekeleza ahadi zote zilizo ahidiwa na hao marais wengine, na hazikutekelezwa.

Viva Rais Samia.
Your browser is not able to display this video.
 
Hivi nyie mataga,badala moamvane na Gali zenu,mmegeuka kusubili teuzi kwa kusifia viti ambavo haipo,nyanda za juu kusini unapafahamu?
 
Kwa uelewa wangu Mikoa ya huko ndio pekee ambayo Uislamu haujatamalaki (bado), labda ni kwa ajili kuifungua na kueneza β€œinjiliβ€œ , who knows?
Watu wengi hawajui hilo.
Lakini kuna machifu waliofanya kazi kubwa kuzuia waarabu kupita na kufika mikoa hiyo.
Kuna Chief Mkwawa(Hehe) na Chief Merere(Safwa) waliokuwa wakali sana sehemu hizo.
 
Watu wengi hawajui hilo.
Lakini kuna machifu waliofanya kazi kubwa kuzuia waarabu kupita na kufika mikoa hiyo.
Kuna Chief Mkwawa(Hehe) na Chief Merere(Safwa) waliokuwa wakali sana sehemu hizo.

Sasa Waarabu wamerudi kivingine na akina Mkwawa hawapo tena sijui kama safari hii watapona huko chini!
 
Naunga mkono hoja!
 
Viva Mama Viva
 
Duh !!!....

Kwahio wale ambao walikuwa hawana teknolojia ya sasa ya kuweza kuwafikia watu kwa dakika na kutatua Kero kwa urahisi hawakukaa kama huyu ambaye angeweza kupunguza gharama kwa kufanya vitu remotely ?

Hivi hii Ziara / Kampeni yake imetumia kiasi gani cha Kodi kama gharama ? Na ni kipi alichofanya ambacho kisingeweza kufanyika vinginevyo..., Anyway bora kutumia muda wake huku na kuvunja rekodi za ndani kuliko zile alizovunja huko USA bila hata kukutana na Mwenyeji Wake...

Sio mbaya aendelee kuzunguka ila itapendeza zaidi tukijua gharama ya hio mizunguko / kampeni
 
Sema wewe ndio unampongeza usitusemee wote bhana
 
Ni vema kafika ili aone wenzake vitu vingi walivyoahidi wakati wa kampeni zao havikufanyika.
Ilikuwa usanii wa kupata kura tu!
 
Sema wewe ndio unampongeza usitusemee wote bhana
Akija kwako mgeni kma Mama Samia si ustaarabu wala tabia yetu ,hasa kwa watu wa sehemu zetu kujifungia na kula "mbalagha" kichoyo.
Hujalelewa vizuri.
 
Akija kwako mgeni kma Mama Samia si ustaarabu wala tabia yetu ,hasa kwa watu wa sehemu zetu kujifungia na kula "mbalagha" kichoyo.
Hujalelewa vizuri.
Mgeni wako sio mgeni wangu ukimshukuru unamshukuru wewe sio kwaniaba yangu mwanafyale hayo ndio malezi
 
Ni vema kafika ili aone wenzake vitu vingi walivyoahidi wakati wa kampeni zao havikufanyika.
Ilikuwa usanii wa kupata kura tu!
Kwamba dunia ya Sasa hana Network ya kujua nini Kimefanyika mpaka Afike ? All I need is transparency kujua gharama pia ili tuweze kuona kama tunaweza kufanya hizi ziara / kampeni cheaply....

Pia since hawa wanafika na kuelezea jinsi ilani ya Chama chao ianvyofanya kazi basi wasiwabane na wengine wapite vilevile na kuelekezea jinsi yanayotakiwa kufanyika hayafanyiki... (Kumbuka pia huyu atajuaje kwamba vitu havifanyiki wakati hata mabango alisema hataki kuyaona)
 
Wakati mwingine napata kigugumizi na kwikwi saana juu ya sifa hizi za"haijapata tokea" wakati ule wimbo bora kabisa ulikuwa ndiyo huui huu, mpaka bunge likaweka azimio la kumpongeza kwa "ushindi mnono wa uenyekiti wa SADC". Sasa kama aliambiwa haijapata kutokea, leo Tena mwingine anaambiwa haijapata tokea. Mm naomba ufafanuzi. HII HAIJAPATA TOKEA " ni kwa vipi Tena wakati ni miaka Sita tu iliyopita? Au tunasahau ya Jana na kukumbuka ya Leo tu??
 
Binadamu wanafki sana
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Damn!
 
Chawa kama chawa masopakyindi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…