Mkuu ziara kama hii imekuwa ikililiwa na wananchi wa Nyanda za Juu Kusini kwa muda mrefu maana marais wengi waliopita hasa Magufuli ni kama walnyanyapaa maeneo hayo.
Ziara ni vile vile Rais kuwatatulia wananchi kero zao za muda mrefu.
Ndio raha ya kiongozi kufanya ziara maana anapata Hali Halisi na kuona na pia akiwauliza wananchi watamwambia shida za Moja kwa Moja..
Naendelea na kuleta summary ya mambo ambayo yatatatuliwa,nimetaja mambo makubwa kwa Mbeya na Njombe sasa ni zamu ya Iringa..
Kwa Mkoa wa Iringa,
-Ujenzi na Upanuzi wa uwanja wa ndege wa Iringa awamu ya pili ilinkuwezesha ndege kubwa kutua na kukuza utalii,
-Kuanza ujenzi wa barabara ya km 201 ya Iringa hadi Ruaha NP,ilikwama toka uhuru.
-Kuanza ujenzi wa barabara ya Iringa Bypass Ili kuondoa malori makubwa kupita katikati ya Mji.
-Kuanza ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mgololo,
-Kuanza ujenzi wa barabara ya Nyororo/Mafinga hadi Mtwango kwa kiwango cha lami,
-Kuanza ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Madibira/Mbarali kwa kiwango cha lami,
-Kuanza ujenzi wa barabara ya Ipogolo-Kilolo hadi Idete na kutoboa Mlimba Kwa kiwango cha Lami,
-Mafinga Mjini kupata km 4 za lami chini ya mradi wa Tactic ,
-Kufuta kabisa tatizo la maji mjini Mafinga chini ya mradi wa miji 28,
-Kufuta kabisa tatizo la Maji Mufindi Kaskazini zaidi ya bil.58 zimewekwa,
-Kufuta kabisa shida ya Maji Kwa watu wa Jimbo la Kalenga,zaidi ya bil.60 zitajenga Bwawa kwa ajili ya maji ya nyumbani na umwagiliaji.
-Pia Serikali imepata pesa za mkopo dola mil.350 sawa na zaidi ya sh.Bil.800 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa REGROW kuimarisha utalii kwenye Kanda ya Kusini hususani hifadhi za Ruaha,Kitulo na Katavi..