Wananchi wengi wakilipa kodi ndio wataweza kuwadhibiti viongozi wao. Lakini sio kwa nchi yetu ambayo walipakodi hawafiki hata robo ya idadi

Hakuna mwananchi asiyelipa kodi sema wafanyabiashara ambao kimsingi ni mawakala tu wa kodi ndiyo wengine wanazila hizo kodi wanazokusanya toka kwa wananchi.
 
Huna Elimu ya Kodi ndio shida,ndio Maana Kodi kubwa tunawekewa kwenye Indirect Tax,Ili ionekane hulipi,Kila mtanzania analipishwa Kodi isiyo ya Moja Kwa Moja.mpaka Watoto wachanga wanalipa.
 
Kodi ipi unayosema hii hii inayoishia kwenye mikono ya majitu ya ccm na family zao ama ipi...
Unamfatiliaga CAG ww lakini na report zake au unabwabwaja tu hapa tulipe kodi ili wale mema ya nchi vzuri si wanachuku mikopo huko acha wachukue mpk nchi iuzwe tu

Unafatiliaga bajeti bungeni ww huonagi mfano bajeti ni laki 1 hapo matumizi ya kawaida elfu 85, maendeleo elfu 15 nani alipe kado kwa mtindo huo.
 
Unafikiri nini kusema walipa kodi ni wachache?
Unafikiria nini mtu kuambiwa haulipi kodi wakati kila huduma unayopata unalipa VAT?
Huyo hajui kitu hajui kwamba hata mfuko wa cement ukiondolewa kodi tunaweza nunua hata elfu 10 tu, hajui kila bajeti ikisomwa ndiyo inayoamua vitu vpande bei au visipande sababu ya kodi huyo ni kichaa.
 
Huyo hajui kitu hajui kwamba hata mfuko wa cement ukiondolewa kodi tunaweza nunua hata elfu 10 tu, hajui kila bajeti ikisomwa ndiyo inayoamua vitu vpande bei au visipande sababu ya kodi huyo ni kichaa.

Wéwe ndio huelewi hata ninachozungumzia.

Huo mfuko wa cement unaosema unauhakika gani umelipiwa kodi? Hilo ndio swali
 
Wéwe ndio huelewi hata ninachozungumzia.

Huo mfuko wa cement unaosema unauhakika gani umelipiwa kodi? Hilo ndio swali
Ujue we jamaa huwa ninakukubali sn lakin nashangaa leo unaandka pumba tu. Hivi hujui kila bidhaa unaponunua ile bei si halisi inakuwa si halisi sababu ya kodi. Uliwahi jiuliza kwann petrol Zambia 🇿🇲 bei iko chini kuliko tz na wakati mafuta hayo yanapita hapa bongo issues ni kodi. Nenda kafanye utafiti kiwanda cha cement utapata majibu kwann cement inauzwa bei hiyo. Wakati wangeweza uza hata elfu 10.
 
Mkuu, pata kwanza elimu ya mlipa kodi ndiyo uje umwage madini yako hapa.

Raia yeyote wa nchi hii aliyepo hai ni mlipa kodi bila kujali umri ama status yake.

Kwa mfumo wetu wa kodi usivyo rafiki, watu wengine wanalipa kodi zaidi ya mara moja: mf.

Mfanya kazi anakatwa Payee kwenye mshahara wake, akienda Bank kutoa pesa anakumbana na tozo za miamala, akienda dukani kununua bidhaa anakumbana na Vat.

Na hiyo Vat ipo kila kona ya mauzo, hivyo bidhaa moja inaweza kulipiwa Vat zaidi ya moja.

Kifupi ni hivyo kuna utitiri wa kodi usio na mpangilio kwa kila mwananchi.
 
Halafu zinaishia kuliwa na kundi la mchwa
 
Kuna wakati unaoneka critical thinker (na nadhani ni kweli), huu upuuzi wa leo umeutoa wapi?
 
Wafanya kazi na waajiriwa ndio kundi pekee linalokamuliwa kodi
 
Ukinunua bidhaa hardware wanakupa risiti ya kutembelea. Yaani bidhaa za laki 4 unapewa risiti ya elfu 20. Tena duka lipo mita 500 tu kutoka TRA.
 
Kuna wakati unaoneka critical thinker (na nadhani ni kweli), huu upuuzi wa leo umeutoa wapi?
Umemtukana lakini yuko sahihi kwa kiwango kikubwa..

Watu wengi wameongelea VAT - lakini kwenye nchi yetu VAT compliance ni chini ya asilimia 8. Wakati huo huo bidhaa nyingi za vyakula zimesamehewa kodi ya VAT. Hivyo, watu wengi hawalipi na wanaolipa hawadai risiti.

Pia, umewahi kujiuliza kwa wale wafanyakazi wanaolipa direct tax na bado wanalipa hizo indirect?? Kwa hiyo ni muhimu kundi la wanaolipa direct tax liongezeke la sivyo kulipa indirect tax sio excuse kwa kweli.
 
Nnaponunua bidhaa iwe jumla au rejareja obvious nimelipa kodi,nnaposafiri nimelipa kodi,nikinunua vocha/kutuma hela/kutoa hela nimelipa kodi.Nnapoenda hos nnalipa kodi yaan kiujumla kila nnachotaka kukifanya hapa Tz nnalipa kodi there is no anywhere kwenye uafadhali.
Nchi hizo zilizoendelea ambazo unahisi watu wengi wanalipa kodi(according to you) actually hawatozwi na kuumizwa na gharama kama huku kwetu.Niambie nchi gani iliyoendelea mtu akitaka kununua gari analipa kodi zaidi ya thaman ya gari tena inaeza enda mara mbili!!!???
Bidhaa ambayo kwenye mataifa yaliyoendelea unaezaipata kwa sh 120,000/- kwa hapa unaeza ipata kwa sh 450,000/- na imetengenezwa China ikasafirishwa kupelekwa huko Ulaya ama pia ikasafirishwa from China to Tz.
Mkuu kiufupi sema kwamba shida ni corruption,Ufisadi na ulaf ni tatizo.Gharama za viongozi wa nchi yetu ni kubwa compared.Hapo bado wizi unaofanyika kwenye idara za Serikali unategema nn?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…