Wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru

Wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru

Safi sana halmashauri za dar ziige pia
Huko kuna mijihela sana

Ova
 
WATU wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru.

Ni baada ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema jijini Mwanza, kupitisha sheria ndogo za ada na ushuri ambazo tayari zimepata baraka za Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Barua iliyosainiwa na Emmanuel Kaponoke, Afisa Utamaduni wa halmashauri hiyo ya tarehe 15 Januari 2021 kwenda kwa walengwa, inabainisha ada hizo.

Washereheshaji (MC) watapaswa kulipa Sh.50,000 kwa sherehe moja huku wapambaji kumbi za burudani/sherehe watalipa Sh.30,000.

Wamiliki wa kumbi, unaochukua watu kati ya 100-200 ni Sh.50,000 kwa siku, ukumbi unaochukua watu kati ya 201-500 atalipa Sh.100,000.

Wapishi wa vyakula kwa siku moja ya tukio atapaswa kulipa Sh.30,000 na wapiga picha za video na mnato watapaswa kulipa Sh.30,000 huku muziki ikiwa ni Sh.30,000

“Kamwe, mmiliki wa ukumbi asiruhusu sherehe kufanyika ndani ya ukumbi wake bila kibali cha halmashauri,” inaeleza sehemu ya barua hiyo

“Ikumbukwe, ada hii ni kwa ajili ya kubali cha halmashauri tu na si gharama ya kukodi ukumbi.”

Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria ya nchi bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
 
39283333-2643-4E54-B456-FB7F6E7ED7C7.jpeg


26124632-BD0B-41CC-B744-8620821FB658.jpeg


☝️ Hayo ndio mamlaka walio nayo kwa mujibu wa wizara ya fedha 👉
Wizara ya fedha wapo very specific kwenye mambo ya tozo na kodi za halmashauri inayoweza fanya kwa mamlaka zao.

Kwa mujibu wa maelezo hawana mamlaka ya kucharge services kama kukodisha kumbi za starehe, ku charge ma MC na wengine wote; wanachoweza fanya kwa sababu azijawekwa kwenye list yao ni kudai percentage in levy based on those services turnover (mapato ya mwaka) lakini si kuwawekea watu kiwango kabla ya kazi.

Kibongo bongo ndio ishatoka kwa nchi ambayo hakuna tax lawyers wa kutosha.

Unajiuliza hivi huko TAMISEMI kabla ya kuruhusu mambo kama haya huwa wana refer kwenye sheria kwanza na kuuliza wizara ya fedha kama hawana uhakika au watu huwa wanajiamulia tu; pili wanamaanisha nini wanapotaka watu wajiajiri na kutengeneza ajira wakati kutwa wengine wanawaza tozo tu.
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
Watu watafanyia sherehe majumbani mwao!
wait and see
 
Hakuna asiyependa kulipa kodi mkuu tatizo kodi kubwa na zinaumiza... fikiria kuna baadhi ya kumbi ndogo za kawaida mc analipwa 50k halafu unamwambie huyo mc alipe tozo ya 50k inaingia akilini kweli.?? Yaana afanye kazi hela yote serekali ichukue?
Kuna biashara zina kodi na tozo zaidi ya 4 unafikiri kuna kufaidi au kuumia?
Yeah true wangejitahidi kuweka kwa asilimia...
kadiri mtu anavyopata
 
WATU wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru.

Ni baada ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema jijini Mwanza, kupitisha sheria ndogo za ada na ushuri ambazo tayari zimepata baraka za Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Barua iliyosainiwa na Emmanuel Kaponoke, Afisa Utamaduni wa halmashauri hiyo ya tarehe 15 Januari 2021 kwenda kwa walengwa, inabainisha ada hizo.

Washereheshaji (MC) watapaswa kulipa Sh.50,000 kwa sherehe moja huku wapambaji kumbi za burudani/sherehe watalipa Sh.30,000.

Wamiliki wa kumbi, unaochukua watu kati ya 100-200 ni Sh.50,000 kwa siku, ukumbi unaochukua watu kati ya 201-500 atalipa Sh.100,000.

Wapishi wa vyakula kwa siku moja ya tukio atapaswa kulipa Sh.30,000 na wapiga picha za video na mnato watapaswa kulipa Sh.30,000 huku muziki ikiwa ni Sh.30,000

“Kamwe, mmiliki wa ukumbi asiruhusu sherehe kufanyika ndani ya ukumbi wake bila kibali cha halmashauri,” inaeleza sehemu ya barua hiyo

“Ikumbukwe, ada hii ni kwa ajili ya kubali cha halmashauri tu na si gharama ya kukodi ukumbi.”

Hii sera ya makusanyo zaidi na kufikia malengo inachagizwa na shughuli za maendeleo za taifa
 
Hii maana yake ukitaka kuoa au kuolewa ongeza gharama hizo kwenye budget yako. Carnal Gaddafi aliwalipa watu wake ile waoe sisi tunailipa serikali kuoa.

Kweli mitano tena.
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
Acha ujinga.Ujanjaujanja uko wapi hapo?
Kumiliki ukumbi au kupika kwenye sherehe ni ujanjaujanja? Tatizo unakurupukia mada tu bila kuisoma na kuielewa.
 
Kuna kodi mpaka ya wanaotumia baiskeli
Ngoja wailete nayo

Ova
 
Duu! Yaani tumekosa ubunifu wa vyanzo vya mapato mpaka tukatoze ushuru na ada kwenye sherehe za harusi? Vipi kama watu wote wakiamua kuchukuana kimyakimya bila sherehe, hayo mapato ambayo sasa yataingizwa kwenye makisio ya hizo halmashauri je yatatoka wapi?

Alafu unakuta hao hao wote unaowaongezea ushuru huo na ada walishasajiliwa na kupewa leseni na halmashauri hiyo na wanalipa kodi TRA, Je na hizi tozo ni za nini? mfano mmiliki wa ukumbi tayari ana leseni inayomruhusu kufanya biashara hiyo na analipa kodi TRA ambayo amekadiriwa kulingana na mapato anayopata kutokana na ukodishaji wa ukumbi huo, Je hizo tozo tena za nini wakati kila siku serikali inajitapa kuwa imepunguza mlolongo wa tozo kuweka mazingira wezeshi ya biashara je na hizi tozo za kila sherehe zinatoka wapi?

Mama lishe wa migahawa ndio wanaoshikia dili za upishi wa hizo sherehe ambapo serikali ya wanyonge imejitapa kuwawezesha kupata vitambulisho vya mjasiria mali vya Tsh 20,000/= na wasitozwe kodi nyingine, Je hapa kuna maana gani ya kulipia hiko kitambulisho Tshs 20,000/year wakati natozwa 30,ooo per trip?

Nashauri tozo hizo ziangaliwe upya kama kweli serikali ina nia ya kuwezesha wananchi kukuza mitaji yao hasa ukilinganisha na ukweli kuwa haohao tunaowawekea tozo za kulipa mara mbilimbili wanakuwa na mikopo kwenye halmashauri ambako nako pia wanapeleka marejesho kila mwezi, tujiulize kwa kasi na viwango hivi vya kupitisha hizi tozo wajasiria mali hawa watasalimika kweli?
 
Back
Top Bottom