Wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru

Wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru

Nashauri yafuatayo kwa wanasengerema;
1.Punguzeni kufanya sherehe
2.Mkifanya sherehe,fanyieni majumbani.
3. Kama ni sherehe ya harusi fanyieni misikitini au makanisani.
4.Kukiwa na ulazima wa ukumbi,basi nenda na msosi wako au wageni wako wakale nyumbani.

NB: Vijana oeni ki-mila,epukeni usumbufu usio wa lazima.

Hapo mtakuwa mmewapa elimu hao wanaofikiria kuvuna hata
wasipopanda.
 
Umesoma degree makaratasi ukapata kazi serikalini ukapewa na cheo basi ndo mwisho wa matumizi ya fikra zako. Kila kinacholetwa unaamua kwa kuangalia maslahi yako na mabosi wako, kazi yako kubwa ni kutia saini kila kitu bila kutafakari kiundani mambo husika.

Hakuna mwanadamu asiyekuwa mbinafsi, kauli hii inajidhiirisha wazi kabisa.

Tuna viongozi wachache sana. Wengi wapo tu wakisubiri kila kitu atafuniwe yeye ni kumeza tu.

Ukikaa kufikiria sababu za msingi za baadhi ya maamuzi yanayofanywa na kiongozi mpaka mtu unabaki unajiuliza huyu kweli nati zimekaa sawa?

Ifikie hatua kila mmoja awe flexible, kama unaona mazingira ya nchi yako hayakupi support kwa kile ulichonacho ili kuiinua, tafuta namna nenda nchi yoyote ambayo unaona uko mambo yako yataenda sawa.

Tumepoteza na tunaendelea kupoteza vipaji vingi sana hapa kwetu Tanzania na pia tumekuwa na ushabiki wa vitu vidogo hata visivyo na msingi, yaani wenzetu washafanya huko mda mrefu na hawaoni jipya, sisi kwetu mambo hayo yanaonekana kuwa mapya na ya kustaajabisha na tunadiriki kutoa pongezi kana kwamba ni muujiza umefanywa.

Umasikini wa kifikra unatutesa sana siyo siri.

Hata vyanzo vya mapato na wasomi wetu wote tulionao hakuna wa kuja na njia bora za kuongeza pato la taifa na wapo maofisini wanakula viyoyozi huku mjasiriamali mwenye nia ya dhati na ubunifu wa kutosha akiminywa na mazingira magumu ya biashara yake aliyotumia nguvu na akili kuianzisha.

Haya mambo yanauma sana aisee, na hapo watakuja kujitetea na hoja za kwenye makaratasi theory za vitabu walizosoma miaka mingi huko nyuma bila hata kuangalia uhalisia wa huyu raia kwa wakati huo na mazingira halisi.



The problem with Africa is, those with ideas has no power and those with power has no ideas.

Prof Lumumba
 
Na itakuwaje kama ma-MC wanajitolea bure?
Au wapishi wanapika bure?
Hapa ukienda mahakamani unawashinda kirahisi hawa maboya.
La sivyo kila anayepika au kufanya kazi ya u-MC awe analipwa(aingize kipato).
Mwisho,Nina wasiwasi na elimu za viongozi watu hasa madiwani.
 
dept.jpg
 
Hawa watu hawana akili kabisa sengerema ni wilaya ndogo sana kuna ukumbi gani pale mwenye ukumbi atoe 220,000 au 270,000 kwa ajili ya halmashauri?
Sengerema asili yake ni wasukuma na wasukuma wengi wanapenda kufanyia sherehe zao manyumbani au kwenye jamii yake.Anyway sasa hivi sherehe tutakuwa tunafanyia makanisani na penyewe waje wadai kodi..
Mfumo mbovu kabisa wa kutafuta mapato..sasa hivi kijana kuoa inakuwa adhabu..
Kusanyiko lolote too, hata ufanyie nyumbani au kanisani, tozo iko palepale ndugu
 
Kama mpishi ni hoteli au catering ambayo tayari inalipa kodi za serikali je hii pia inamuhusu
 
hyo pesa ni kodi au ni kwa ajili ya nini? kwani mwanye hukumbi hana leseni ya biashara/ na wapiga mziki si wana leseni ya biashara na wanalipia? sigara tu ni hatari na mnatuuzia! ama kweli mitano tena.😳
 
Waongezee na hii....

-kila chombo Cha usafiri kitakayoshiriki Kwenye msafara wa maharusi
- gari = 50,000
-bajaji= 30,000
-pikipiki= 20,000
-baskeli= 10,000
 
Wakulaumiwa Ni hao madiwani waliopitisha izo tozo za kihuni
 
Back
Top Bottom