Wanaoomba kulipiwa mahari Al Hikma wafika 1,000, wapo wanawake, wanatakiwa 50 tu

Wanaoomba kulipiwa mahari Al Hikma wafika 1,000, wapo wanawake, wanatakiwa 50 tu

Quran 2:97

Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur’ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.”


ADUI WA JIBRIL (GABLIEL) NI SHETANI NDIE ALIYEMSHUSHIA MTUME QURAN.
 
kijana mwenye akili timamu hataenda kutafuta aibu ya kujitakia kulipiwa mahari
Huna akili , kuna watu wanalipiwa ufadhili wa masomo na watu au serikali vyuoni mtu anaomba kwenye pesa ya mkopo alipiwe angalau ada ili aweze kusoma .

Udini unakusumbua na utakuua kwa kuteseka pasipo na sababu za msingi.
 
Huoni wametangaza na vitu vingine kwenye habari kama semina ya ndoa au umekurupikia mada ?
Kindness na ukarimu, issue zinazofanana na wito wa ndani na upenzi wa dhati wa jambo husika, mfano, ualimu, uwe na utashi kwanza ndipo uusomee!, semina kwa mtu ambaye hana utashi ispokuwa tu wakati umemlazimu kufanya ndoa, patakuwa na shida.
 
Alitangaza 50 tu wamejitokeza zaidi, kama huyu sheikh ana imani ya Mungu anatakiwa awalipie mahari wote waliojitokeza. Usaili wa nini kwenye mambo ya imani?
Huna akili na itakuwa ajabu kichwa kama chako kuwa na familia inayokutegemea,anza na serikali kwa nini inatoa mkopo vyuoni na kwa vijana wachache ikiwa waombaji ni wengi kwa nini wasitoe kwa wote ?
 
Kindness na ukarimu, issue zinazofanana na wito wa ndani na upenzi wa dhati wa jambo husika, mfano, ualimu, uwe na utashi kwanza ndipo uusomee!, semina kwa mtu ambaye hana utashi ispokuwa tu wakati umemlazimu kufanya ndoa, patakuwa na shida.
Wewe ulitakaje ?
 
Mkaja wa bibi wanatoa?

Inawezekana wao wana watu wao wa kwenda kwa wazazi wa binti kubageini. Ktk hali ya kawaida itabidi wazazi/walezi wakubali maana watabigwa aya na khadithi mpaka mtu ataona aibu,atashusha 'bei'
Kwenye uislamu hakuna mkaja wa bibi wala babu, ni binti anaulizwa anahitaji mahari yake iwe nini atakayotaja mwanaume unatakiwa ulete. Apatiwe binti mahari yake sio ya wazazi wala walezi.
 
Wewe ulitakaje ?
Elimu kwa wazazi itolewe wasiwe vikwazo kwa vijana wao wanapopata wenza, endapo mahari itatakiwa kuwa laki 2,basi kijana atakapokuwa hata japo na kianzio cha hamsini, ndoa ifungwe bila shida.
 
Back
Top Bottom