Nuzulati
JF-Expert Member
- Nov 25, 2020
- 10,094
- 37,314
Kwa hiyo hutaki ndoa unataka kuolewa mkuu?Ndoa sio kutoishi na mwanamke hatutaki kitu inaitwa ndoa mkuu inatuingiza kwenye ujinga kama wa dr mwaka
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa hiyo hutaki ndoa unataka kuolewa mkuu?Ndoa sio kutoishi na mwanamke hatutaki kitu inaitwa ndoa mkuu inatuingiza kwenye ujinga kama wa dr mwaka
Hawa wanaopingaga ndoa ukiangalia Historia zao zina shida sanaKumekuwa na mijadala mingi sana inayowazuia vijana kuoa au kuolewa, kubwa sana ni kukataa kuoa. Hiyo ni kutokana na mfumo wa maisha ya sasa yalivyo. Ndoa nyingi hazidumu na uaminifu ndani ya ndoa umepungua sana kiasi kwamba wanandoa kusalitiana limekuwa jambo la kawaida na ndio sababu ya ndoa nyingi kuvunjika.
Pamoja na yote hayo haipaswi kuwepo na mjadala wa kuhamasishana watu wasioe/kuolewa au wasiingie kwenye ndoa. Katika hilo kuna watu wanaingia mkenge kwa kufata mkumbo au kumuiga mtu fulani kwa kuwa hataki kuoa/kuolewa nami sioi/siolewi. Hiyo sio poa kabisa kwa sababu watu wanatofautiana na kila mtu ana changamoto zake, changamoto za mke wa fulani haziwezi kuwa sawa na changamoto za mke wa fulani au za mume wa fulani haziwezi kuwa sawa na mume wa fulani. Halafu wengi wanaokataa kuoa/kuolewa wana changamoto za kisaikolojia ambazo wamezipata either kwa kushuhudia au kusimuliwa.
Kwahiyo nawaomba vijana ambao hamjaoa au kuolewa msiogope kuingia kwenye ndoa. Usiangalie na kulinganisha na ndoa ya fulani kwani ndoa yako haiwezi kufanana na hao wengine.
Kubali Ndoa
Ndoa ni Baraka
Ndoa ni Furaha
Ndoa ni Heshima
Umepita mulemule😀Wengi wao ni
Wazazi wao walikwepa majukumu ya malezi bora eg Mume kuendekeza michepuko na kusahau familia,Mke kuwekeza kumlisha limbwata Mume na kusahau kujaza upendo kwa watoto
Watoto waliotelekezwa kwa ndugu
Watoto wa michepuko
Mimba zisizo tarajiwa kisha zikakanwa
Waliopatikana kwa matokeo ya ubakaji. Mabazazi yanayobaka yalaaniwe yanatuharibia jamii
Waliokacha shule na kukimbilia kuvuta vijiweni,dating za kipuuzi,kula kimasihara
Waliopatikana vilabu vya matapu tapu
etc etc etc
ukishakuwa na watoto kusema kweli hakuna haja ya ndoa, unakomaa na kutafuta hela , kulea watoto wako vizuri na kuenjoy maishaNina watoto wawili hivyo nawaza yote hayo pia.
#YNWA
Well said, lakini kuishi na watoto pamoja ni vizuri zaidi. Imagine umemzalisha dada halafu humuoi hapo itabidi umchukue mtoto uishi nae, kama hutamchukua ataenda kulelewa na baba wa kambo au utampeleka kwa ndugu zako akalelewe huko. Huoni kama hilo ni tatizo mtoto kulelewa na mzazi mmoja?ukishakuwa na watoto kusema kweli hakuna haja ya ndoa, unakomaa na kutafuta hela , kulea watoto wako vizuri na kuenjoy maisha