Wanaotaka kuzua taaruki kuhusu Afya ya Makamu wa Rais wapuuzwe sawa na wanaozusha kujiuzulu kwa KM CCM

Wanaotaka kuzua taaruki kuhusu Afya ya Makamu wa Rais wapuuzwe sawa na wanaozusha kujiuzulu kwa KM CCM

Mapema Sana Ccm Wanafarakana
Hakuna hicho kitu bro. Katika vyama vyote vya siasa tulivyonavyo, hao jamaa wanajua sana kumaliza figisu ndani kwa ndani. Wanaparuana sana lakini mwisho wa siku wanakua wamoja. Kumbuka enzi za JK wakati wa kumpata mgombea kunako 2015, waligawanyika sana. Mwisho wa siku wakakaa pamoja na kuja na jina la Mwendazake. Ugomvi ukaishia pale
 
Mambo ya hovyo sana wanafanya. Hili la kutafuta hawara na kutumia nudes ni ukosefu wa watu wenye akili,busara na maarifa. Mijitu iko kwenye ngono 24/7. Ulimbukeni kwenye matumizi ya teknolojia ni mbaya sana.

Katibu Mkuu apimwe kwa utendaji wake. Najiuliza hata ingekuwa lengo ni kumtoa, mbona makatibu wakuu wengine walitoka kwenye hiyo nafasi bila picha za uchi? Why Chongolo? Ame perform vizuri sana wamekosa sababu za msingi za kuwapa wanachama imebidi wamtafute hawara amuangamize? Was he that successful? Taarifa zake za kimaadili zimeshindwa kushughulikiwa na walio juu yake na kumuondoa kwa staha kama wengine? Wamemkosa kote kwingine wameishia kwenye nudes? Aibu kwa Chama Chetu,anayefanya hivi ni adui wa CCM.

Akilipiza na yeye kwa kutoa mapicha ya mahawara wa viongozi wenzie au uovu wao hatari zaidi si tutafika 2030 kila siku tunaangalia porn twitter na whatsaapp? Idiots. Mijitu miovu ikipata pesa na nguvu inaangamiza taifa kabisa.

Imefika mahali tuna wahuni ndani ya chama mpaka tunasaidiwa na wapinzani kukemea yanayoendelea?
 
Natambua mtandao mbaya umerejeshwa kazini ila wakimtegemea Mungu watavuka salama. Waovu siku zote kwa Mungu ni chukizo. Waovu wakipewa madaraka madhara lazima yawepo hasa kwa watu wema na waadilifu......mimi personally nawaombea wale wote wenye uadilifu waweze kusimama dhidi ya kundi la waovu linalopigana usiku na mchana kurejesha ukatili kwenye siasa za nchi na ustawi wa watu wake.
Ina maana wanajulikana, kama nia yako ni njema ungeishauri mamlaka iwashughulikie hao waliorejeshwa badala ya waliotumwa
 
Mamndenyi nawe verified unaamini uzushi wa Kigogo na wale wanaopush hashtag? CCM ina tovuti, ina X account, kote huko hawajaandika habari ya Katibu wao. Kwa ni ni usiwaamini wao? Au na wewe una puch agenda za Makonda na wenzake?
Tuambieni makamu wetu wa raisi yuko wapi? Acheni porojo.

Alafu huyo mnaemtetea mbona hajakanusha?
 
Kuelekea kikao cha Mkutano Mkuu wa CCm kuna propaganda zinaendelea zikisema Mzee Mpango anaumwa wakati huohuo zikidai KM CCM amejiuzulu

Hawa watu wa tweeter wapuuzwe, tufike wakati tubaki na verified information tu. Tunapokuwa na viongozi wa kisiasa wanaoandika na kupost kila kinachovumishwa kwenye mitandao kunawaondolea kuaminika kwenye jamii.

Kiongozi wa kisiasa jaribu kuchuja habari unayoweka kwenye mitandao ya kijamii. Nimtakie Mzee wetu Mpango maisha mema na afya tele zaidi kulitumikia Taifa. Nimtakie Mdogo wetu Chongolo uvumilivu kipindi hiki ambacho ameletewa watu wanaotaka aonekane kama hana hadhi ya kuwadhibiti kusema.

Natambua mtandao mbaya umerejesha kazini ila wakimtegemea Mungu watavuka salama. Waovu siku zote kwa Mungu ni chukizo. Waovu wakipewa madaraka madhara lazima yawepo hasa kwa watu wema na waadilifu......mimi personally nawaombea wale wote wenye uadilifu waweze kusimama dhidi ya kundi la waovu linalopigana usiku na mchana kurejesha ukatili kwenye siasa za nchi na ustawi wa watu wake.
Waasisi wa taharuki ni CCM
Wanapopelekewa taharuki wakae kwa utulivu
 
Jana usiku saa tatu niliona jf swali la kuomba kujulishwa na mleta mada akasema" mnataka hadi itokee kama 3/21? . Baada ta dakika tano sikuona uzi huo tena. Ndiyo naona kivingine leo.
 
Wengi walitabiri baada ya Ujio wa PCM chama kinaweza kugawanyika, na ndicho kilichotokea.

Kwasasa kuna movement kubwa inayotaka timu yao ichukue full power Chamani na Serikalini.

Ngoja tuone mwisho wa haya yanayoendelea.

Ila jambo la kuzingatia ni kuwa "Chama Imara huunda Serikali Imara".
 
Wengi walitabiri baada ya Ujio wa PCM chama kinaweza kugawanyika, na ndicho kilichotokea.

Kwasasa kuna movement kubwa inayotaka timu yao ichukue full power Chamani na Serikalini.

Ngoja tuone mwisho wa haya yanayoendelea.

Ila jambo la kuzingatia ni kuwa "Chama Imara huunda Serikali Imara".
Polepole alisemaga tuwakatae wahuni !
Ngoja tuone !🙏
 
Back
Top Bottom