Wanaotesa mpaka kuua, huwa wanavuta bangi kwanza au wanaua kavukavu bila kupata chochote cha kuwaondolea ubinadamu na eneo huwa ni sound proof?

Duniani kuna mambo ya ajabu sana!!
 
Je wangapi mkimkamata mwizi mnaweza kumpiga na kumuua?? Je ni kweli wote wanaomshabulia mwizi na kumuua anakuwa amewaibia wote?? Kama unaweza kumuua mwizi basi jua unaweza kumuua binadamu yoyote. Kikubwa ni sababu tu!
Kuna kitu kinaitwa chuki?? Hao wauwaji mara nyingi wanakuwa na chuki sana na watu wanaowafanyia ukatili huo. Unajua hata maisha ya kawaida ukishachukiana na mtu ni rahisi sana kumfanyia kitu chochote.leo hii wangapi wako tayari kuwaona wabaya wao wakiteseka?? Kipi kinakufanya ujisikie raha ukimuona adui Yako anapitia machungu na magumu?

Mtoa mada nikupe mfano kidogo ulio hai! Unademu wako ama mkeo unampenda sanaa lkn baada ya mda mkeo akabadilika upendo kwako haupo Tena, unakuja kuchunguza unagundua kumbe ni rafiki Yako ndie anaekumegea mkeo na kamteka kabisaa!! Basi jamaa anakuvimbia sana kitaa, anajigamba kwamba kakunyang'anya mke na hauna Cha kumfanya, anasema mkeo kampendea show konk ambazo kwako alikua hazipati. Kufupisha stori je jamaa huyo ataendelea kuwa rafiki Yako?? Vipi ukimuona unajisikiaje?? Vipi siku ukimkuta mahari jamaa wanampa mkong'oto na analia kwa uchungu, utamhulumia ama utawambia jamaa waongeze mkong'oto kwani kilio chake kinakuburudisha???

Sasa mtoa mada: Hawa wauaji Cha kwanza kabisa wanachojengewa ni kukichukia kitu. Ogopa sana mtu anaekwambia Mimi kuwa CHADEMA Bora mniuwe. ama mimi kuwa CCM Bora mnichinje. Mtu wa hivyo anakuwa na chuki iliyopitiliza na kitu flani kwa hivyo wote anao waona wanakipenda kitu hicho asichokipenda yeye basi anawachukia sana na yuko tayari kuwafanya chochote maana maumivu Yao ndio furaha kwake.
But yote wa yote Mimi nalia na siasa za chuki ndo zimeleteleza yote haya, wanasiasa wetu wahimize upendo miongoni mwetu, wawambie watu uchadema na uccm ni utofauti wa mitazamo tu, Hawa wanaamini hivi na wale wanaamini vile lkn msingi wa yote sote tunajenga nyumba Moja haina haja ya kugombania ufito.
 
Hatuna tofauti na fisi wanaotafuna mnyama alie hai mpaka mnyama anakata roho huku wao wakiendelea kumla nyama tena wanagombania.
Kisayansi Binadamu ni mnyama tu kama wanyama wengine tofauti yake kubwa ikiwa ni consciousness ya kuelewa mambo mengi, uwezo wa kuongea na uwezo wa kutumia nyenzo kwa ufanisi zaidi zikiwemo hizo watesaji wanazotumia .
 
Ukatili hauhusiani na kabila, kuna Wazaramo makatili sana pia.
 
Ukatili hauhusiani na kabila, kuna Wazaramo makatili sana pia.
Ukatili wa mzaramo na ukatili wa mkurya 😊

Unataka kusema Nini ndugu yangu umringanishe mkwere , mzaramo na mkurya kwenye ujasir,ushupavu,ukatili N.K

Wazaramo unawaonea labda kwenye ushirikina TU.
 
Sasa bangi inahusikaje humu ? Bangi haina undugu na uovu acheni upotoshaji
Bangi ni Kama kichocheo kwa hao makatili kupata hamasa ya kuwatesa kikatili.

Kuna wavuta bangi wengi sana ambao ni watu wa amani ie. Marastaman wengi wanavuta msuba na ni watu peace sanaa ✌️
 
Nilipitia pia maelezo ya jamaa mmoja ni ex - SF wa Guatemala (kaibiles) aliwahi naswa kama POW's anakwambia mtu aliye fit katika interrogation ni hatari na mbaya zaidi ajue pia wewe ni mtu mwenye mafunzo.
 
Basi tunatofautiana mkuu,me niliwahi kushuhudia postmortem,nikaona yule maiti anavyokatwa mara mkono,mara apasuliwe kifua...daahhh...sitaki kukumbuka asee ile kitu.
Ok sijawahi shuhudia hiyo postmortem, labda sijui inavyotisha, ila mimi ni mtu wa barabarani, nimeshuhudia ajali kadhaa ambazo watu timamu wanakata roho huku naona.
Maiti inatisha, ila hatua ya binadamu anapotaka kuwa maiti inatisha zaidi
 
Dunia ina mengi...
 
Ganja itoe hapo
hao ni wahuni wenye leseni ya kuteka na kuua.
 
kuna wale professsional wamesomea...wapo kwa ajili ya kuua tu serikalini, sasa imetokea miaka kadhaa marais wanajifanya hawataki kusaini wapate ruhusa ya kuwanyonga waliohukumiwa kifo....hawawanyongaji hawapati mahali kwa kutekeleza kazi zao......wanakuja nje huku wanadhani wameruhusiwa na rais kuteka raia.....raia akizingua kidogo au wamemhisi tofauti tu wanapita naye ilimradi tu watimize takwa lao la kutesa na kuua, na unashangaa watu rundo kupotea na kukutwa wameuliwa lakini mwenye nchi ana amani anafurahia....kule kutia saini tu anajinasibu yeye hapendi. Upande wa pili watu wa visasi na chuki binafsi na wivu nao wapo busy kuteka, kutesa na na kuua...wakibainika wakahukumiwa kunyongwa ..mkuu wa nchi anagoma kuweka saini kuruhusu watu wanyongwe.....alafu anajitapa hadharani kwamba mimi siwezi tia sahihi yangu mtu anyongwe...hapo unatarajia uuaji nchini utaisha ?, kwa njia ipi sasa?. Binadamu tuna safari ndefu sana..yaani huku unawindwa na nyoka, kule simba, huku mamba, kule mbwa, huku wachawi, kule binadamu wauaji, wezi, tandu, mara ukwepe ng'nge, ukwepe ajali, mara uumwe U.T.I....unajikuta unamtumainia Bwana na kubaki hai inakuwa ni Kristo kufa inabaki Faida tu...shida zinakuwa nyingi aisee😎
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…