Wanasayansi wa kiafrika ndio wanaoikuza Amerika na Ulaya, kwanini wasiikuze Afrika yao?

Wanasayansi wa kiafrika ndio wanaoikuza Amerika na Ulaya, kwanini wasiikuze Afrika yao?

kwani tunasoma ili tupate pesa au tunasoma ili tusolve matatizo yetu hivi wakina newton na eistein wangekuwa wanafanya kazi ili walipwe hivi kuna nchi ingeweza kuwalipa
Lengo la kusoma ili upate hela. Kusolve matatizo ni issue ya ziada. Ingekuwa kusoma ili u-solve matatizo watu wangefanya kazi kwa kujitolea. Masilahi kwanza mambo mengine ndiyo yanafuata
 
umezungumzia wanasayansi ila hujazungumzia kada nyingine wao wakiona mwafrika kama ana kipaji hata cha michezo wanampa uraia kuna kipindi afrika kusini walikuwa wanalalamika kuhusu wao ksomesha manesi lakini wakimaliza wanaenda kufanya kazi ulaya na marekani ambapo wanalipwa pesa nzuri ila nawashangaa sana viongozi wa afrika wanapokutana na viomgozi wa ulaya kujadiliana juu ya wahamiaji haramu wakati tatizo la wahamiaji haramu limesabababishwa na wao wenyewe kwa wamechukua kuanzia rasilimali watu mpaka rasilimali fedha ambazo ni fedha zinazoibwa huku afrika ili kuendeleza nchi zao.Wao wanataka vitu vizuri kutoka afrika lakini vibaya hawavitaki wanasahau kuwa kama wangeacha vitu vizuri huku wimbi la kukimbilia ulaya lingepungua
 
HII NI LIST YA WANASAYANSI KUTOKA AFRICA NA KAZI WANAZOZIFANYA KWENYE MATAIFA MAKUBWA

EGYPT
1. Euclid of Alexandria
huyu ni founder wa geometry ni mzaliwa wa egypt
amefanya kazi katika European Space Agency's (ESA) na ameunda euclid space craft
220px-Euklid-von-Alexandria_1.jpg


2. Sameera Moussa
huyu ni ni mwanafizikia aliyebobea kwenye maswala ya nyukilia na ni mzawa wa egypty ana doctorate ya atomic radiation na alifia huko California, united state
220px-SameeraMoussa.jpg


3.Ahmed Hassan Zewail
Huyu ni wa Egypt ni mwanzilishi wa femtochemistry anafanya kazi amerca
185px-Ahmed_Zewail_HD2009_Othmer_Gold_Medal_portrait.JPG


Eritrean
1. Haile Debas
huyu ni mfanya sugery, mwanafizikia na ni academic adminstrator katika chuo kikuu cha California ni mzawa wa africa

Carthage
1. Abbas Ibn Firnas
huyu ni mwanafizikia mchemia na engineer alifanya kazi huko spain ila ni mzawa wa carthage africa

Morocco
1. Rachid Yazami
huyi ni morocan alifanya research kuhusu lithium battery na graphite anode anafanya kazi katika French National Centre for Scientific Research (CNRS) ni wa kwaza kugundua intercalation ya lithium kwenye graphite katika electrochemical cell
220px-Rachid_Yazami_2011.JPG

Ethiopean

1. Sossina M. Haile

huyu ni profesa na mchemia pia ni mwanafizika na ni mhandisi anafanya kazi california instute of technology huyu aligundua solid acid fuel cells

2. Kitaw Ejigu
Ethiopian engineer and Chief of Spacecraft and Satellite Systems engineer at NASA.
KENYAN
1. Calestous Juma
Huyu ni professor pia ni mfanya kazi katika havard university ni mzawa wa kenya

MALI
1. Cheick Modibo Diarra
Huyu ni aerospace engineer amechangia kukamilika kwa mission nyingi za NASA mfano kupatikana kwa njia ya kwenda kwenye sayari ya mars , galileo space craft na kuchunguza sayari ya mars
NIGERIAN
1. John Uzo Ogbu
huyu ni professor alikuwa anachunguza maswala ya intelligence kuendana na rangi ya ngozi (race) inasemekana alikuwa na IQ kubwa ni mzawa wa nigeria lakini alikuwa anafundisha na kuishi California

2. Bisi Ezerioha

huyu ni professor, engeneer huyu ndie mgunduzi na mtengenezaji wa honda pia ameshiriki katika utengenezaji wa Hyundai Motor America mhshimiwa huyu pia anatengeneza injini za magari pia
220px-Bisi_before_a_race-_2013-09-24_11-08.jpg


SOUTH AFRICA

1. Aaron Klug
Huyu ni mchemia na biophycist alijishindia tuzo kwa kugundua crystallographic electron microscopy pia amegundua structure ya tobacco mosaic virus huyu ni director wa maabara ya molecular biology huko cambridge

2. Sydney Brenner
huyu amebobea kwenye genetic alipata tuzo noble prize kwenye phsiology or medicine anafanya kazi kwenye maabara ya molecular biology huko cambridge england pia ni mwanzilishi na mmiliki wa California instute of molecular bilology kwa kipindi cha maisha yake

3. Christiaan Barnard
huyu ni mpasuaji bingwa wa moyo pia alifanikiwa kuhamisha moyo kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa mara ya kwanza duniani hajareportiwa sehemu aliyokuwa anafanyakazi nnje ya africa lakini alionekana kuondoka sana africa na alikufa mwaka 2001

SUDANI
1. Mohammed Ibrahim
Huyu engineer na ni billionaire pia aliwahi kuishi british na kufanya kazi huko katika vitengo vya telecomunication aliajiriwa na british telecom huyu ni mwanzilishi wa mtandao wa celtel
220px-Mo_Ibrahim.jpg


2. Ali M. El-Agraa
huyu ni mwanauchumi bingwa amefanya kazi british, usa, na japan nchi ambazo sasa zinaonekana kukua kiuchumi mno

200px-Editing_Ali_M._El-Agraa.JPG


3. Mohamed Osman Baloola
huyu ni biomedical engineer pia ni mtafiti na mwendesha research kuhusu diabetes anafanya kazi uarabuni katika Ajman University of Science and Technology

220px-Mohamed_Osman_baloola.jpg

TANZANIA
1. Felix A. Chami
Felix A. Chami is an archaeologist from Tanzania. He is a professor at Dar es Salaam University. Dr. Chami discovered, on the island of Mafia and Juani, artefacts that revealed East Africa as being integral to the Indian Ocean trade huyu yupo africa na anafanya kazi africa alichogundua imebidi nikiweke kwenye lugha ya fumbo ili mjiulize kwanini kabaki africa
220px-Professor_Felix_Chami.jpg

UGANDA
1. Kwatsi Alibaruho
Huyu ni director wa kurusha vifaa vya anga anafanya kazi National Aeronautics and Space Administration (NASA) alishadirect human spaceflight mwaka 2005 pia anahusika kumanage na kucarry space shuttle flight
220px-Kwatsi_Alibaruho_-_flight_director.jpg

AFRICA TUNA LIST YA WANASAYANSI WENGI AMBA O NI WAZAWA WA AFRICA LAKINI SASA WANAYATUMIKIA MATAIFA MAKUBWA BADALA YA TAIFA LAO PIA WENGINE WANAONEKANA KUTAFUTA URAIA KWENYE MATAIFA HAYO

1. Je hii ni akili na wanasababu mdhubuti kufanya hivyo? je kuna watu wa mataifa makubwa kama amerca wanakuja kulitumikia tafa dogo africa?

2. Je tukisema waafrica wanatamaa ya pesa na si wazalendo wa nchi zao tunakosea? unafikiri hawa wanasayansi wangefanya kazi kwenye mabara yao africa tungekuwa bado maskini?

3. Je unafikiri hawa wanasayansi wangefanya kazi africa kungekuwa na mgogoro mkubwa na mataifa makubwa na huenda wangefanikiwa kuwaua?

4. je wanasayansi wa africa wanalazimishwa kufanya kazi kwenye mataifa makubwa na kutishiwa kuuliwa hivyo wanaogopa kufa



ILA NIMEGUNDUA WANASAYANSI WENGI WA KIAFRICA WANAOJULIKANA DUNIA NA NI WAZAWA WA SOUTH AFRICA BADO WANAFANYA KAZI SOUTH AFRICA JAPO SIJAWAWEKA KWENYE LIST HAPO

UMEGUNDUA NINI? africa tunajiona tuna wanasayansi wengi lakini wanaofahamika ulimwenguni pote ni wachache mfano kwa tanzania anafahamika mmoja kwani tunamaporofesa wangapi kwenye vyuo vyetu je wametendewa haki kutotajwa kwenye hii list?


nawasilisha
Hii list angekosekana mchaga
 
Mi nadhani pia nchi zetu za Kiafrika pia zinachangia sana kuwafifisha wataalamu wetu

Wee fikiria nchi kama DRC au Burundi au Sudan zimejaa migogoro ya kivita na kisiasa alafu unawaambia Wanasayansi wabaki pale wafanye nini cha maana?! Hata raia tu wakawaida wanakimbia nchi kuokoa maisha yao Sembuse Wanasayansi wabaki?!

Mataifa mengi ya Kiafrika yamejaa siasa za ufisadi, na Siasa za ukabila badala ya kujali maendeleo, wanasiasa wanalipwa zaidi hela nyingi kuliko hata Wanasayansi,, unakuta mbunge ni darasa la saba analipwa hela nyingi kuliko mhadhiri au profesa wa chuo kikuu alafu bado unawaambia Wanasayansi wetu wabaki Afrika?! Huoni Hata maprofessa wanakimbilia kwenye siasa kuliko kubaki kwenye taaluma zao?! Sio kwamba hawana uzalendo bali serikali zetu zimesababisha hayo yote badala ya kujali taaluma za Wanasayansi wetu wao wanajali sana siasa kuliko sayansi,, inauma sana



Pia hawaweki mkazo katika ugunduzi na ubunifu wa kisayansi,, hivi ni bajeti kiasi gani inawekwa kwenye ugunduzi Na Utafiti wa kisayansi?! Sasa hata mwanasayansi mfano wa spacecraft akibaki hapa nchini atafanya utafiti au ugunduzi wa kitu gani kama hakuna bajeti au fund ya utafiti wa kitu hicho?!

Bora waende tu kwenye mataifa hayo yanayo wajali Wanasayansi na kutenga fedha kwaajili ya utafiti ili kuendeleza ugunduzi wao kuliko kubakia Wakiwa marecturers hapa bongo mpaka kifo chao,,,
 
Wangeuawa zamani tu,tena kama huyo mwenye celtel angeshapigwa risasi.
Hata mack aliyegundua facebook asingefika popote na fb yake wala whatsapp,angepigwa risasi na yeye.
Nata mimi nikiwa scientist sifanyi ujinga huo wa kukaa humu tena hususani Tanzania.
Huyo mrusho satellite angeambiwa aishushe haraka sana la sivyo atapigwa kipigo cha mbwa koko.
sawa hii ni sababu wew unafikiri tutabadili vipi mtazamo wa serikali zetu za africa hasa africa mashariki?
 
Tatizo kwenye nchi za kiafrika hawathaminiwi na hawapewi kipaumbele kbs mana wanasiasa ambao ni viongozi huku kwetu Africa wanapenda watu waendelee kuw wajinga wajinga ili wawatawale milele

Kuna case moja huko Zanzibar vijana kujaribu kuunda helikopta lakini kilichotokea waliwekewa vikwazo kibao ikiwemo kuwa eti hawana kibali wala leseni ya kurusha kifaa cha angani
 
Africa i

Mtu akitengeneza kitu badala apewe karakana na uwanja wa majaribio utasikia hairuhusiwi iko kitu maana hakijathibitishwa. Nyumbu nyumbu tu Africa haitaendelea. Kuna tatizo.

Sasa kwa akili za kiongozi wa malaika unategemea ipo siku Afrika itatoka
ila kwa mfano aliyetengenezaga lile gari kwa kipindi kile hata angepewa support bado asingeweza kuliingizia taifa kipato kikubwa kwakuwa hata yangetengenezwa hayo magari yasingeweza kuuzwa nje ya tanzania pili yasingeweza kupambana sokoni na magari yanayingizwa nchini kutokana na ubora wake. je uanafikiri kungekuwa na uwezo wowote wa kuzuia magari kutoka mataifa makubwa yazuiliwe kuuzwa tanzania ili magari yatakayotengenezwa hapa yapate soko?

kikubwa mtu ili apewe support na kuliletea faida taifa anapaswa kuvumbua kitu ambacho hakijawahi kugunduliwa duniani hapo ndipo technologia ya huyo mtu itakuwa na manufaa na kuuzika kwa bei kubwa.
 
Jibu ni rahisi, hakuna haja ya kusema wana tamaa ya pesa ama c.yo wazalendo. Ni kwa sbb hakuna nchi za kiafrika zilizojikita seriously kwenye uendelezaji wa sayansi na teknolojia ama hata R&D.
si kweli kwa south africa wamejitahidi sana ila kwanini kwa hapa tanzania hii sera ya viwanda inasuasua kutimizwa na pia kuna mgogoro mkubwa kwenye hii serikali yetu inayodai inataka kuunda tanzania ya viwanda
 
Sasa huko Bongo tunazibiwa na kuongozwa na Bashite.

Kwa nini tusisepe tu?
hilo nalo ni tatizo tukisema viongozi watu wanapaswa kuwa watu wenye elimu kubwa kuna watu watajitokeza na kupinga hili na watadai kila mtu ana hakli ya kuongoza na matokeo yake wakipewa hiyo haki kama walivyopewa sasa nchi inakuwa na sera mbovu na kila siku tunakutana na miswada ya ajabu kwenye mabunge yetu badala ya kupambana kujikwamua
 
Jibu mbona Dogo sana ,angalia mshahara wa mbunge na wa Mwalimu,hapo ndio utapata jibu.

Nchi za afrika husani Tanzania haiungi mkono profession Bali inaunga mkono politics.
Mi nadhani pia nchi zetu za Kiafrika pia zinachangia sana kuwafifisha wataalamu wetu

Wee fikiria nchi kama DRC au Burundi au Sudan zimejaa migogoro ya kivita na kisiasa alafu unawaambia Wanasayansi wabaki pale wafanye nini cha maana?! Hata raia tu wakawaida wanakimbia nchi kuokoa maisha yao Sembuse Wanasayansi wabaki?!

,
je tanzania ya sasa imekuja kwa sera ya viwanda itafanikiwa? je ni kwanini? na kama haitafanikiwa pia ni kwanini?

unafikir serikali kuna inapokosea mpaka sasa kumekuwa na minong'ono mpaka watu wamekuwa na haka kamsemo "TANZANIA YA VIBANDA" badala ya "TANZANIA YA VIWANDA" Je watu ndio wanakosea kufanya hivyo au serikali ndio inakosea na ikapelekea watu kuleta huo msemo na suluhisho lake ni lipi?
 
Tatizo kwenye nchi za kiafrika hawathaminiwi na hawapewi kipaumbele kbs mana wanasiasa ambao ni viongozi huku kwetu Africa wanapenda watu waendelee kuw wajinga wajinga ili wawatawale milele

Kuna case moja huko Zanzibar vijana kujaribu kuunda helikopta lakini kilichotokea waliwekewa vikwazo kibao ikiwemo kuwa eti hawana kibali wala leseni ya kurusha kifaa cha angani
unafikiri hao wanasiasa wanafanya hivyo huku wakitambua umuhimu wa kuwa na technologia au wanafanya hivyo kwakuwa elimu yao ni ndogo au hawana elimu kabisa kuhusu hili
 
Back
Top Bottom