Wanasayansi wa kiafrika ndio wanaoikuza Amerika na Ulaya, kwanini wasiikuze Afrika yao?

kwani tunasoma ili tupate pesa au tunasoma ili tusolve matatizo yetu hivi wakina newton na eistein wangekuwa wanafanya kazi ili walipwe hivi kuna nchi ingeweza kuwalipa
Lengo la kusoma ili upate hela. Kusolve matatizo ni issue ya ziada. Ingekuwa kusoma ili u-solve matatizo watu wangefanya kazi kwa kujitolea. Masilahi kwanza mambo mengine ndiyo yanafuata
 
umezungumzia wanasayansi ila hujazungumzia kada nyingine wao wakiona mwafrika kama ana kipaji hata cha michezo wanampa uraia kuna kipindi afrika kusini walikuwa wanalalamika kuhusu wao ksomesha manesi lakini wakimaliza wanaenda kufanya kazi ulaya na marekani ambapo wanalipwa pesa nzuri ila nawashangaa sana viongozi wa afrika wanapokutana na viomgozi wa ulaya kujadiliana juu ya wahamiaji haramu wakati tatizo la wahamiaji haramu limesabababishwa na wao wenyewe kwa wamechukua kuanzia rasilimali watu mpaka rasilimali fedha ambazo ni fedha zinazoibwa huku afrika ili kuendeleza nchi zao.Wao wanataka vitu vizuri kutoka afrika lakini vibaya hawavitaki wanasahau kuwa kama wangeacha vitu vizuri huku wimbi la kukimbilia ulaya lingepungua
 
Hii list angekosekana mchaga
 
Mi nadhani pia nchi zetu za Kiafrika pia zinachangia sana kuwafifisha wataalamu wetu

Wee fikiria nchi kama DRC au Burundi au Sudan zimejaa migogoro ya kivita na kisiasa alafu unawaambia Wanasayansi wabaki pale wafanye nini cha maana?! Hata raia tu wakawaida wanakimbia nchi kuokoa maisha yao Sembuse Wanasayansi wabaki?!

Mataifa mengi ya Kiafrika yamejaa siasa za ufisadi, na Siasa za ukabila badala ya kujali maendeleo, wanasiasa wanalipwa zaidi hela nyingi kuliko hata Wanasayansi,, unakuta mbunge ni darasa la saba analipwa hela nyingi kuliko mhadhiri au profesa wa chuo kikuu alafu bado unawaambia Wanasayansi wetu wabaki Afrika?! Huoni Hata maprofessa wanakimbilia kwenye siasa kuliko kubaki kwenye taaluma zao?! Sio kwamba hawana uzalendo bali serikali zetu zimesababisha hayo yote badala ya kujali taaluma za Wanasayansi wetu wao wanajali sana siasa kuliko sayansi,, inauma sana



Pia hawaweki mkazo katika ugunduzi na ubunifu wa kisayansi,, hivi ni bajeti kiasi gani inawekwa kwenye ugunduzi Na Utafiti wa kisayansi?! Sasa hata mwanasayansi mfano wa spacecraft akibaki hapa nchini atafanya utafiti au ugunduzi wa kitu gani kama hakuna bajeti au fund ya utafiti wa kitu hicho?!

Bora waende tu kwenye mataifa hayo yanayo wajali Wanasayansi na kutenga fedha kwaajili ya utafiti ili kuendeleza ugunduzi wao kuliko kubakia Wakiwa marecturers hapa bongo mpaka kifo chao,,,
 
sawa hii ni sababu wew unafikiri tutabadili vipi mtazamo wa serikali zetu za africa hasa africa mashariki?
 
Tatizo kwenye nchi za kiafrika hawathaminiwi na hawapewi kipaumbele kbs mana wanasiasa ambao ni viongozi huku kwetu Africa wanapenda watu waendelee kuw wajinga wajinga ili wawatawale milele

Kuna case moja huko Zanzibar vijana kujaribu kuunda helikopta lakini kilichotokea waliwekewa vikwazo kibao ikiwemo kuwa eti hawana kibali wala leseni ya kurusha kifaa cha angani
 
ila kwa mfano aliyetengenezaga lile gari kwa kipindi kile hata angepewa support bado asingeweza kuliingizia taifa kipato kikubwa kwakuwa hata yangetengenezwa hayo magari yasingeweza kuuzwa nje ya tanzania pili yasingeweza kupambana sokoni na magari yanayingizwa nchini kutokana na ubora wake. je uanafikiri kungekuwa na uwezo wowote wa kuzuia magari kutoka mataifa makubwa yazuiliwe kuuzwa tanzania ili magari yatakayotengenezwa hapa yapate soko?

kikubwa mtu ili apewe support na kuliletea faida taifa anapaswa kuvumbua kitu ambacho hakijawahi kugunduliwa duniani hapo ndipo technologia ya huyo mtu itakuwa na manufaa na kuuzika kwa bei kubwa.
 
Jibu ni rahisi, hakuna haja ya kusema wana tamaa ya pesa ama c.yo wazalendo. Ni kwa sbb hakuna nchi za kiafrika zilizojikita seriously kwenye uendelezaji wa sayansi na teknolojia ama hata R&D.
si kweli kwa south africa wamejitahidi sana ila kwanini kwa hapa tanzania hii sera ya viwanda inasuasua kutimizwa na pia kuna mgogoro mkubwa kwenye hii serikali yetu inayodai inataka kuunda tanzania ya viwanda
 
Sasa huko Bongo tunazibiwa na kuongozwa na Bashite.

Kwa nini tusisepe tu?
hilo nalo ni tatizo tukisema viongozi watu wanapaswa kuwa watu wenye elimu kubwa kuna watu watajitokeza na kupinga hili na watadai kila mtu ana hakli ya kuongoza na matokeo yake wakipewa hiyo haki kama walivyopewa sasa nchi inakuwa na sera mbovu na kila siku tunakutana na miswada ya ajabu kwenye mabunge yetu badala ya kupambana kujikwamua
 
true ila dawa ya tatizo ni kulikimbia au kulisolve? wew umebadili uraia wa tz pia?
Moja wapo ya condition ya kuwa astronauts
Kwa nchi kama USA lazima uwe raia wao!..

Bahati mbayaa bongo hawana double!..
Nadhani utaelewa

Log out
 
Jibu mbona Dogo sana ,angalia mshahara wa mbunge na wa Mwalimu,hapo ndio utapata jibu.

Nchi za afrika husani Tanzania haiungi mkono profession Bali inaunga mkono politics.
je tanzania ya sasa imekuja kwa sera ya viwanda itafanikiwa? je ni kwanini? na kama haitafanikiwa pia ni kwanini?

unafikir serikali kuna inapokosea mpaka sasa kumekuwa na minong'ono mpaka watu wamekuwa na haka kamsemo "TANZANIA YA VIBANDA" badala ya "TANZANIA YA VIWANDA" Je watu ndio wanakosea kufanya hivyo au serikali ndio inakosea na ikapelekea watu kuleta huo msemo na suluhisho lake ni lipi?
 
unafikiri hao wanasiasa wanafanya hivyo huku wakitambua umuhimu wa kuwa na technologia au wanafanya hivyo kwakuwa elimu yao ni ndogo au hawana elimu kabisa kuhusu hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…