Wanasayansi Wagundua Mfumo Mpya wa Kinga ya Mwili

Wanasayansi Wagundua Mfumo Mpya wa Kinga ya Mwili

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Mfumo mpya wa kinga ya mwili umegunduliwa. Upo katika sehemu ya mwili inayojulikana kwa kusaga protini. Mfumo huo una muundo wa siri unaoweza kutapika kemikali zinazoua bakteria.

Watafiti kutoka Israel wanasema ugunduzi huu utabadilisha uelewa wetu wa jinsi mwili unavyolindwa dhidi ya maambukizi. Utafiti huu unatoa nafasi mpya ya kutafuta dawa mpya za antibiotiki ili kukabiliana na tatizo linaloongezeka la wadudu ambao ni sugu kwa dawa zetu za sasa.

Mfumo huu upo katika proteasome – eneo dogo ambalo lipo katika kila seli ya mwili. Kazi yake kuu ni kukata protini kongwe na kuzifanya vipande vidogo ili ziweze kuchakatwa na kutengenezwa kuwa protini mpya.
Source: BBC News

Ugunduzi huu unazidi kuthibitisha unabii wa Danieli kuwa siku za mwisho maarifa yataongezeka.
"Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya, ukatie muhuri kitabu hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka." (Danieli 12:4)

Israeli imebarikiwa katika maeneo mengi ya kiuchumi, kiteknolojia na kiafya kama Mungu alivyoahidi:
"Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; Nami nitawabariki wakubarikio, na yeye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa."( Mwanzo 12:2-3).
Usithubutu Kuilaani Israeli.jpg
 
Mfumo mpya wa kinga ya mwili umegunduliwa. Upo katika sehemu ya mwili inayojulikana kwa kusaga protini. Mfumo huo una muundo wa siri unaoweza kutapika kemikali zinazoua bakteria.

Watafiti kutoka Israel wanasema ugunduzi huu utabadilisha uelewa wetu wa jinsi mwili unavyolindwa dhidi ya maambukizi. Utafiti huu unatoa nafasi mpya ya kutafuta dawa mpya za antibiotiki ili kukabiliana na tatizo linaloongezeka la wadudu ambao ni sugu kwa dawa zetu za sasa.

Mfumo huu upo katika proteasome – eneo dogo ambalo lipo katika kila seli ya mwili. Kazi yake kuu ni kukata protini kongwe na kuzifanya vipande vidogo ili ziweze kuchakatwa na kutengenezwa kuwa protini mpya.
Source: BBC News

Ugunduzi huu unazidi kuthibitisha unabii wa Danieli kuwa siku za mwisho maarifa yataongezeka.
"Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya, ukatie muhuri kitabu hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka." (Danieli 12:4)

Israeli imebarikiwa katika maeneo mengi ya kiuchumi, kiteknolojia na kiafya kama Mungu alivyoahidi:
"Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; Nami nitawabariki wakubarikio, na yeye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa."( Mwanzo 12:2-3).
View attachment 3265867
Je, Ni Kweli Atakayeilaani Israeli Anaweza Kulaaniwa?
Kulingana na historia na Maandiko Matakatifu, wale walioilaani na kuishambulia Israeli walikumbwa na maangamizi makubwa. Hivyo ni heri na ni hekima kusimama upande wa taifa ambalo Mungu mwenyewe amelibariki.

Hebu tuangalie madhara waliyoyapata watu walioilaani na kuishambulia Israeli...
 
Madhara waliyoyapata watu walioilaani na kuishambulia Israeli...
Farao wa Misri na Mapigo Kumi (Kutoka 7-12)
Farao aliwatesa Waisraeli, lakini Mungu alimletea mapigo kumi mazito sana, na hatimaye jeshi la Farao lilikumbwa na maangamizi baharini.
 
Mfalme wa Moabu – Balaki na Balaamu (Hesabu 22-24)
Balaki alitaka Balaamu awalaani Waisraeli, lakini Mungu akamzuia Balaamu, na badala yake akawabariki. Baada ya hilo, Moabu waliadhibiwa na Mungu.
 
Waashuru na Kuanguka kwa Ninawi (Nahumu 1-3)
Waashuru waliiharibu Israeli Kaskazini, lakini baadaye Mungu aliuangamiza Ninawi, mji wao mkuu, kama adhabu.
 
Nebukadneza na Babeli (Yeremia 25:12-14, Danieli 4)
Nebukadneza aliiteka Yerusalemu na kuliharibu hekalu la Mungu, lakini baadaye Mungu alimwadhibu kwa kumfanya atembee kama mnyama kwa miaka saba!
 
Daah Siku nafikia akili za ki mateka kama hizi za mtoa mada naomba mniuwe tuu sitakuwa na faida katika hi dunia tena.

Hebu tumiaeni hata robo ya akili zenu nyie watu wa dini jamani ..
kuna muda unaweza dhani mtu hana Ubongo kichwani, Unaweza dhani mtu kichwa chake ni kama kifuniko cha mwili kwa namna dini zimewafanya mataira.
 
Mfalme Herode Agripa I (Matendo 12:1-23)
Herode alidhulumu Wakristo wa Kiyahudi na akaamuru kuuawa kwa Yakobo, lakini Mungu alimwadhibu kwa kifo cha ghafla kupitia malaika wa Bwana.
 
Hitler na Ujerumani ya Nazi
Adolf Hitler alianzisha Holocaust, akiwatesa Wayahudi mamilioni, lakini baadaye Ujerumani ya Nazi ilianguka vibaya katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
 
Jamani hili somo si kila siku nawapa hamjapata kuelewa hadi leo?Israel iliyotajwa kwenye biblia sio hii Israel mnayosema leo(Israel ya kisiasa).Acheni kuchanganya mambo(Biblia inataja uzao wa Jacob kama Isreal .Watoto 12 wa Jacob ndio maana halisi ya Israel.Unajua wapo wapi?unadhani ni hawa kina Netanyahu?sio kweli)
 
Dola ya Kirumi na Kuanguka Kwake
Warumi waliiharibu Yerusalemu mnamo mwaka 70 BK, lakini baadaye Dola ya Kirumi iliporomoka, na kuanguka kutokana na maangamizi ya ndani na nje.
 
Jamani hili somo si kila siku nawapa hamjapata kuelewa hadi leo?Israel iliyotajwa kwenye biblia sio hii Israel mnayosema leo(Israel ya kisiasa).Acheni kuchanganya mambo(Biblia inataja uzao wa Jacob kama Isreal .Watoto 12 wa Jacob ndio maana halisi ya Israel.Unajua wapo wapi?unadhani ni hawa kina Netanyahu?sio kweli)
Ntakurudia...
 
Je, Ni Kweli Atakayeilaani Israeli Anaweza Kulaaniwa?
Kulingana na historia na Maandiko Matakatifu, wale walioilaani na kuishambulia Israeli walikumbwa na maangamizi makubwa. Hivyo ni heri na ni hekima kusimama upande wa taifa ambalo Mungu mwenyewe amelibariki.

Hebu tuangalie madhara waliyoyapata watu walioilaani na kuishambulia Israeli...
Uzwazwa mtupu. Mbona walioingamiza ni wazungu na wanaendelea kutesa?
 
wanasayansi wa ccm wamegundua kutumia simba na yanga wafike kama wasira.
 
Back
Top Bottom