Tetesi: Wanasheria wa Paul Makonda wanajipanga kumburuza mahakamani Tundu Lissu kwa defamation case ya kumuita na kumtangaza muuaji.

Kama wahenga wasemavyo " Wacha inyeshe tujue panapovuja" mimi najisemea tu " Tibua tope tuone waliko kambare" Yangu ni hayo tu, sina wanasheria mimi.
 
Inasemekana hadi ratiba ya mazishi walishaiandaa jamaa kwenda kuzikwa Singida eti ? 😭😭

Risasi zote zile kama kuua tembo jamani 🙆‍♂️🤦‍♀️😭😭😭
Baada ya kufika nyumbani area D, dereva alimsihi bosi wake asishuke kwenye gari alimwambia kuna magari yalikuwa yanawafuatilia moja wapo ni hilo limesimama nyuma yetu, dereva na mheshimiwa Lissu waliwaona waliokuwa kwenye gari lililokuwa limesima nyuma yao baada ya kufika nyumbani area D, mmoja alishuka kutoka nyuma ya hiyo gari na kuongea na aliye kuwa mbele, baada ya hayo maongezi alirudi kwenye gari, likageuzwa nakuondoshwa kwa kasi sana, (kwa mbio), na ndipo shambulio lilianza, swali je waliokuwa kwenye gari la wasijulikana waliwatambua?, je hao bado wanaishi?
 
Mwambie bwana Tako atulize, akienda huko ataumbuka! Maana atatueleza kwa Mh. Kebwe alipita kufanya nini huo usiku wa tarehe 17 kuamkia 18 September? Na alikuwa anatoka wapi?
 
Ila kwa musiba membe alipata kitu hadi anaingia kaburini?? Tena membe alifatwa hadi na Pengo akaambiwa asamehe ila akajifanya kukomaa, ila kilichofata nini??? Kazila hizo bilioni za Musiba ??
 
Hivi unajua Tundu Lissu huwa hatishiwi kwenda mahakamani? Huko ni kama nyumbani kwake!
 
Mwambie bwana Tako atulize, akienda huko ataumbuka! Maana atatueleza kwa Mh. Kebwe alipita kufanya nini huo usiku wa tarehe 17 kuamkia 18 September? Na alikuwa anatoka wapi?
Uzuri ni mahakama ya bongo sio za mabeberu itaeleweka tu atashinda nani hata ikibidi kwenda gamboshi.......membe reloaded inaweza tokea
 
Unacho ongea upo sahihi kabisa kuna vita vingine upaswi kupigana kwa sababu unaweza kudhani kuwa adui yako ni huyo unayejibizana naye kumbe yeye kapangwa tu aanzishe choko choko kisha anatokea Adui mwingine nyuma anakumaliza na kitu kizito. Ukitaka kupigana usiangalie nguvu ya Adui yako tu angalia na nguvu za marafiki zake.
 
Huko mahakamani ndiko tutalijua jina halisi la mkuu wa mkoa wa Arusha kama ni Makonda au Bashite, vyeti vitasema.
 
Na ndicho tunachotaka, muuaji ajitokeze hadharani
 
Kwa hapa Mkuu umenichekesha sana kama na Wewe ni mmoja ya Watetezi wa PCM mapema sana mnapoteza pambano na TAL anaondoka na points zote tatu muhimu. Yaani umejichanganya na kujikoroga kama rangi za kutengenezea mabatiki na ukindu.
Wewe ulitakiwa kujikita kwenye hoja yako uliyoileta sio kuanza kuandika na mambo ya maliasili za Taifa. Yaani Mkuu inaonekana umepaniki mnoo na watu kama nyinyi mnaopaniki TAL ndio huwa anawapenda sana kwa sababu umeingia kwenye mfumo mpaka umepoteana 🤣🤣🤣
 
Utakua unaota
 
Hao watekaji walipenda starehe,wanalala hoteli!!
Tayari wameacha record zao siku waliolala,na zitakuwa zimehifadhiwa kwa ishahidi probably
 
BAN YA USA INAYOMHUSU MAKONDA INASEMA ANAHUSIKA KUPOKA HAKI YA KUISHI YA WATU USHAHIDI WANAO WA PICHA NA SAUTI
 
Umesema nchi yetu haitawaliwi na sheria za Uingereza. Vipi kuhusu mkataba wa DP WORLD unasemaje?
Kwa kukuelimisha wewe na wale wenye fikira kama zako, nchi yetu au nchi nyingine yo yote haiwezi kushitakiwa kwenye mahakama ya nje ambayo haijaridhia conventions zake.

Mahakama ambazo tulisharidhia ni zile zinazohusu wawekezaji wa kutoka nje (foreign investors) for obvious reasons za kulinda mitaji yao wanayowekeza kwetu. Hivyo sisi tuliridhia kuwa wanachama wa MIGA Convention (Multilateral Investment Guarantee Agency) na ICSID (International Court for Settlement of Investment Disputes). Hivyo mkataba wa uwekezaji wa DP-WORLD uko kwa mjibu wa sheria hizo za uwekezaji. Hawa ndiyo wanaweza kamata ndege zetu wakitushinda kesi ya uwekezaji huko ICSID. Sasa huyo Tundu Lissu wako ni foreign investor na kupigwa kwake risasi kunahusikaje kwenye hizi mahakama? Atakamataje ndege zetu kama anavyotamba kukusudia?

Mahakama pekee ya kimataifa kwa tuhuma za makosa ya jinai ambayo tulisharidhia ni International Court of Justice (ICJ). This is the principal judicial organ of the United Nation whose role is to settle legal disputes submitted to it by states and issue advisory opinions to relevant authorized UN organs. Ni states ndizo hupeleka mashitaka kwenye mahakama hiyo na siyo mtu binafsi. Mmeona hivi karibuni state ya Afrika Kusini ilivyo mfungulia Benjamin Netanyahu, waziri mkuu wa Israel mashitaka ya mauwaji ya kimbali ya wapalestina na ikashinda kesi. Sasa ni lini Tundu Lissu amekuwa ni state wa kuruhusiwa kumfungulia Paul Makonda, mkuu wa mkoa wa Arusha mashitaka ya mauaji huko ICJ? Huo siyo ufyatu wa akili?

Hiyo Jumuiya ya Madola ya Uingereza haina tofauti la kundi la WhatsApp la urafiki wa waliosoma shule fulani pamoja ( ex classmates). Administrators wa group hilo ni waingereza wakiongozwa na mfalme wao. Unaweza kuingia na ku left wakikuzingua. Hata uki left baada ya muda unaweza kujiunga tena. Halina mamulaka ya kisheria ya kukulazimisha kufanya jambo lo lote. Hizo mahakama za London hazina judicial powers kwa nchi zilizo kwenye hiyo WhatsApp group ya Commonwealth countries kama ambavyo Tundu Lissu na jasusi wake wa kimataifa Robert Amsterdam wanavyotaka kuwaaminisha.
 
Head to head.
Lissu 4:0 Bashite.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…