Wanasheria Waelimisheni Viongozi Wetu Kitu Kinachoitwa "Vicarious Liability", Hata Kama Wewe Hujaua, Kama Muuaji ni Mtu Wako, Then Unawajibika Wewe

Kuna nazi na koroma mkuu! Nazi Itajua kupembua kilicho cha kweli na cha uongo, koroma litazoa kila kitu!
 
Umeelezea kwa kirefu sana kama vile unawafundisha watu wengi ambao ni wageni wa haya mambo. Pia umetumia Busara kubwa kuwasilisha ujumbe wako kwani unajua hatawewe unapigwa chabo ukijilengeshe tu kwenye 18 zao na wewe unaliwa kichwa. Ukisha onja nyama ya mtu uachi hata siku moja. Wamesha onja nasikia huwa haitaji kuwekwa chumvi.
 
Sasa wewe "Paskali" si unakutana nao huko high street, na pia kuna vituo kama uongozi institute, si mgekuwa mnawapa kozi fupi kuhusu uchumi, Sheria, na utawala bora
 
Mkuu Steve, Steven Joel Ntamusano,
Kwanza naomba nikuhakikishie Rais Samia ni mkweli kabisa, kama ni kuua, ameua sisimizi tuu, ila anajua watu wake wanafanyaga nini, akiwa VP alimtembelea Lissu hospitalini Nairobi na kulihakikishia taifa, wale sio watu wao, watu wetu ukikosa mbili unaandika maelezo!.

Kanuni ya vicarious liability anatamka mamlaka ndio inabeba the final responsibility kwa matendo ya maofisa wake, hivyo kama ni watu wake, anapaswa kusafisha. Ile 1976 Nyerere aliwasafisha!.

Mazingira ya baadhi ya matukio haya suggest sio "wasiojulikana" bali ni 'wasiojulikana', hivyo kwa vile kwa mujibu wa Katiba yetu, the right to life iko kwenye katiba yetu, ila kuna mazingira fulani inaondolewa na mamlaka pekee ya kusaini death warrant ni mamlaka moja tuu, President of URT, ikitokea wamefanya walichokifanya bila kumhusisha au kumdanganya hao watu ni dissidents, they deserve to be eliminated, vicarious liability inasema the one responsible ni mamlaka na sio watekelezaji.

Ndio maana tumewahi kushauri TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!

Hivyo kama kuna watu wake wanatenda vitendo hivyo behind the closed doors, awashughulikie vinginevyo watamponza bure yeye na karma ikaja kumshukia.

Sisi wenye jicho la tatu, tunaumia sana jinsi watu wake wanavyomset na issues za uhaini just to justify vitendo vyao viovu!. Uhaini My God!. Kuna Uwezekano Anadanganywa na Kadanganyika? I Don't Believe This!. Sitatizwi na Uongo Wao, Natatizwa na The Motives Behind Such Lies! hili la uhaini nimeliendeshea darasa humu na magazetini Ijue Katiba ya JMT kwa Jicho la Mtunga Katiba: Watanzania Tusishabikie Uhaini. Hukuna Uhaini wa Kauli na Maneno, Uhaini ni Mipango na Matendo

Mtu Watanzania waliomkabidhi dhamana ya maisha yao ni mtu mmoja, watumishi wote wa umma, wanafanya kazi kwa niaba ya mtu mmoja tuu, the big boss, wakiharibu kazi wanatakiwa kuwajibishwa, wasipowajibishwa then the vicarious liability shifts to the boss!.

Waswahili wana kamsemo chao cha mchelea mwana kulia, hulia yeye!.

P
 
Sasa wewe "Paskali" si unakutana nao huko high street, na pia kuna vituo kama uongozi institute, si mgekuwa mnawapa kozi fupi kuhusu uchumi, Sheria, na utawala bora
Thanks, this is food for thought.
P
 
Ile hotuba ni ya hovyo sana tangu kuumbwa kwa Tanganyika.
 
Kiserikali na family matters ni ‘Strict liability’ this can be used on criminal and sometimes civil cases (depends on the demand of evidence required).

Kibiashara ni ‘vicarious liability’ only, mainly applied in tort law and not applicable in criminal cases.

Kwenye ‘vicarious liability’ you don’t need a ‘mens rea’. Ili kutaka muhusika wa juu ahusike kwa sababu. Only ‘actus reus’ is enough maana unaemshtaki anaweza asiwe na uwezo kukulipa fidia kwa makosa yake (in civil cases)..

Kwenye jinai lazima uonyeshe ‘actus reus’ and ‘mens rea’ ili mtu unae mtuhumu awe implicated kwenye case husika

Ndio maana uwezi tumia ‘vicarious liability’ kwenye criminal case, labda utatumia strict liability kuna hiyo possibility (ya kupata ‘mens Rea’) maana ni lazima uonyeshe unaemtuhumu alikuwa na uelewa wa crime husika.

Liability depends on direct partcipation in criminal cases, not vicariously.
 
Hadi mi huwa najiuliza: 'hivi huyu ni yule S. Suluhu wa Bunge la Katiba kweli, au ni crony from no where tumepandikiziwa? '

Maana haendani na naibu Spika wa Bunge la Katiba, yaani ni watuwa wili tofauti kabisa!

Ninakosa sana raha na Rais huyu mimi.
 
Sijawahi muona Rais ameshika tofali akijenga shule, ila tunaambiwa rais kajenga shule au Rais anachimba mtaro wa kupitisha mabomba ya maji, lakini tunaambiwa raisi kapeleka maji mji flan, ni mfano tu.
Hivyo anavikubali kuwa kafanya yeye.
 
Mnasemaga Eti kwenye Siasa Mungu hayupo huko !!
Au nasema uongo ??!
 
The Culprit is "Fear for change" ndio maana inatumika nguvu kubwa kutuaminisha kuwa mabadiliko yataleta machafuko🤣 ilihali nafsi za watu zIshachafukwa tayari. Tuitunze tunu ya Amani!!!
 
Kwa kauli ile kuna kitu hakipo sawa kabisa nchi hii!
Huenda kuna "raisi" mwingine zaidi ya mama na anatakiwa atuambie ni nani huyo!
 
Hii rule inafanyakazi mahali ambapo uongozi sio ajira.
La, uongozi huku ni kulana a.k.a survival of the fittest
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…