Wanasiasa mjifunze kufanya kazi na wenye itikadi nyingine kwa lengo la kuleta maendeleo

Wanasiasa mjifunze kufanya kazi na wenye itikadi nyingine kwa lengo la kuleta maendeleo

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Mwaka 1992 Tanzania ilitangaza kuwa ni nchi ya vyama vingi. 2020 bado kuna viongozi wanao simama majukwaani na kusema mkichagua upinzani hatuleti maendeleo.

Sifa kubwa ya kiongozi ni kuweza kuwaongoza wale anao wajibika nao kisheria katika mamlaka yake. Kiongozi anaefuata kanuni za haki bila kupendelea wa kabila lake, wa dini yake au wa chama chake. Ataweka imani yake kwa anaowaongoza na wata msaidia kukitokea matatizo kwakua anasimamia haki.

Kama wazazi tunashauriwa kuwapeleka watoto shuleni hata kama una uwezo wa kukodi mwalimu wa kuwafundisha watoto wako nyumbani. Shuleni mtoto anaanza kujifunza kuishi na watu wengine mbali na wale anaotoka nao nyumba moja. Mtoto ataanza kutunza vifaa vyake visiibiwe, kuwahi dawati kama hayatoshi kwakua hapa mama wala baba hayupo kukuita ukae kwenye kiti chako.

Chama kitakachounda serikali baada ya uchaguzi kiwe na lengo la kutuletea maendeleo katika haki bila kutubagua.
 
Nchi ilikuwa inakwenda kwenye muelekeo wenye kuridhisha tu, ijapokuwa CCM ilikuwa imekwishapoteza dira na muelekeo sahihi toka ilipoingia awamu ya pili ya utawala ktk nchi yetu. Utawala wa awamu ya tano ndiyo umegeuka kuwa mzigo kwa taifa letu.

Licha ya chama tawala ktk utawala huu kukosa maarifa ktk kuiongoza nchi na kudumisha umoja na udugu ndani ya taifa letu. Imegeuka kuwa ndiyo chanzo cha kuvunjilia mbali misingi hii muhimu ya taifa letu. Tuna kiongozi wa ajabu kabisa kuwahi kutokea kuliongoza taifa letu.

Badala ya kuilinda, kuitii na kuitetea katiba ambayo aliapa kufanya hivyo kabla kukabidhiwa madaraka. Yeye ameamua kwa makusudi kwenda kinyume chake. Hajali wala haambiliki, tena awapo hadharani haoni haya kutamka bayana mambo yasiyozingatia masharti ya katiba na sheria nyingine za nchi yetu nzuri ya Tanzania.

Ni muda sahihi umefika sasa tumpumzishe siku ya tarehe 28-10-2020. Na badala yake tumuunge mkono na kumuamini Tundu Lissu, ambaye atatuletea katiba mpya ambayo itakuwa ni sehemu sahihi ya kujitathimini kama taifa tuliteleza wapi na wala siyo hapa tulipoangukia tayari.
 
Nchi ilikuwa inakwenda kwenye meuelekeo wenye kuridhisha tu, ijapokuwa CCM ilikuwa imekwishapoteza dira na muelekeo sahihi toka ilipoingia awamu ya pili ya utawala ktk nchi yetu. Utawala wa awamu ya tano ndiyo umegeuka kuwa mzigo kwa taifa letu.

Licha ya chama tawala ktk utawala huu kukosa
Chama kilichopo madarakani kinaposhindwa kufanya kazi na viongozi wa upinzani wanatuchanya wananchi. Hatuelewi maana ya kuwa na vyama vingi.
 
Dada Sky, hao ni washamba na malimbukeni tu, kama vile ambavyo imekwisha ongelewa na watu mbalimbali.

Mtu mwenye matamanio ya kuufuta kwa namna yoyote ile upinzani wa vyama vya kisiasa ambao upo kikatiba, ni lazima yeye ndiye tatizo kubwa kwa taifa na wala si wananchi.
 
Huyo mwanasiasa unaemfundisha hilo ni mshamba sana, kama hatambui hilo hastahili kuongoza taasisi yoyote kwasababu atasababisha mgawanyiko mkubwa sana kwa wale anaowaongoza.
 
Ukweli mchungu kwa sasa CCM kama Chama Dola wamesha poteza muelekeo wa kisiasa ,kwa sasa Siasa siasa za CCM sio za ushawishi tena bali kulazimisha/vitisho/kutumia dola kubaki Madarakani.

Chama chochote ni kuwa na ushawishi kama ilivyo kwa Chadema na Lissu ,wana washawishi Wananchi kwa Sera zenye kujenga.Hawa nunui Watu /hawa wapandishi kwenye Malori/hawa wanunulii tisheti na makofia hawatumii Wasanii kama kivutio ila Watu wana kuja kwenye Mikutano yao kwa hiari yao.

Ukisha ona Mgombea yeyote anawagawa Wananchi wake (kwa sababu yeyote ile) huyo amesha filisika Sera hana vission hana chochote Kichwani na yupo tayari kufanya lolote ili kusalia Madarakani ,matokeo ya Utawala wa Mtu wa namna hii sio mazuri ni mabaya wakati wote sababu ya hila alizo zitumia awali ili kushika Madraka.
 
Jpm hawezi, Kwake maendeleo ni ccm tu, jpm ameharibu kabisa msingi wa kisiasa wa nchi yetu.kwake kubagua wananchi kwa msingi ya kisiasa ni kawaida.

Huyu ame kanyaga Katiba katika mambo mengi sana ikiwemo ya kuzuia Shughuli za Siasa kama Mikutano ya Vyama vya Siasa.Ubovu wa Katiba tulio nayo ni kuwa hashitakiwi sasa na baada ya kutoka Madarakani.Hebu tizama huu mfumo ulivyo mmbovu ,alie Madarakani anakuwa na nafasi kubwa na yenye kufuru hapo hata ule usawa wa kuwa Watu wote ni sawa mbele ya Jamii haupo.
 
In a real sense when your not voted means that voters disqualified you in the position... Your not enough to save them.... They hate you in other way so as a human being we have feelings, been president want modify that.

So itategemea aina ya mtu katika kutafsiri uongozi, jambo la msingi kukumbuka tafsiri yangu sio yako the same applied to our Head of State.

Na mtu anatumia alichonacho mfano usitegemee kama ikiwa huna busara utaitumia. Maana huna. So utatumia ulichonacho.
 
Kufanya kazi na Wasaliti wa Nchi Chadema ni laana
 
Chama kilichopo madarakani kinaposhindwa kufanya kazi na viongozi wa upinzani wanatuchanya wananchi. Hatuelewi maana ya kuwa na vyama vingi.
Dawa yao ni kuwa mwaga wasituletee ubaguzi kwa visingizio vyovyote.Hata mume na mke ndani ya nyumba wanatofautiana je iweje wato 60m+.
 
Back
Top Bottom