DOKEZO Wanasiasa na mipango ovu ya kuiua eGA

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mfumo wa tanesco marope alivyosema tuu vile nikajua wanaanza kutafuta pesa za uchaguzi hawa vyura wa kijani.
All in all mkurugenzi wenu wa E-GA hali na watu wengi au yuko upande wa kundi hasimu ndio maana wanataka kumng'oa
ohoo kula na wengine tena ? washirikiane kutafuna keki ya wananchi ?
 
Hakuna mfumo ambao hauwezi kutengenezwa na watu wa ndani

Na hakunaga mfumo mdogo mkuu
 
Yes RAIS ni taasisi kubwa ana jua ndio maana hata sisi tunasema hapa , lakini haimaanishi ana endorse hio move.
wanasiasa waovu wanapambana kutaka kumruka asijue ujanja wao , lakini bahati nzuri kamba yao imejulikana
siyo kweli hakuna jambo ambalo rais halijui,hapo unawadanganya wananchi.rais ni taasisi ambayo ina kila kitu.ina mashushushu kila kona ndo maana alijua hata mabilioni yaliyokopwa kwa dhamana feki na kutoroshwa nje ya nchi.hivyo tusidanganyane kuwa rais hajui kinachoendelea.
 
Point ya msingi ni kwamba mpaka mkataba mkubwa kama huu unasainiwa ni lazima rais ajue. Refer ule mkataba wa ndege mpaka raid akawa anasema kaletewa hesabu kubwa!

Inshort lazima rais ajie, sasa tujiulize rais kajua alafu akaidhinisha akiwa anajua kwa kufanya hivyo kwanza ataua vipaji vya ndani na pili kuingiza taifa hasara kwa kulipa mapesa makubwa?
 
"Kuna wanasiasa wanalipwa ili waseme"
 
Kwa tatizo la ajira lilivyo kubwa kuua taasisi yenye vijana wengi namna hio ni kuua ajira , pili unatengeneza ombwe kubwa sana la usiri serikalini , sio kila mfumo wa kutengenezwa na wazungu , ni sawa na kuuza ramani ya handaki kwa adui
 
sijasema Raisi kuna mambo hajui , ninachosema ni kuwa rais anaweza kupotoshwa , akapewa ukweli usio ukweli , na hapo ndipo ninasema rais anakua hajui .
Mfano watu wamdanganye rais afute E-GA wampe sababu za uongo huwezi sema rais ana husika
 
Hakuna mfumo ambao hauwezi kutengenezwa na watu wa ndani

Na hakunaga mfumo mdogo mkuu
Complexity ya hiyo mifumo naijua mkuu. ERP za TANESCO na TRA ni very very complex. Bado hatuna technological capability ya kuiunda hiyo mifumo.
 
Mkuu Twilumba heshima kwako. Nashukuru kwa uliyoandika, naomba kama kuna yeyote aliye karibu na Mama yetu amnong'eneze huu ufisadi uliopo "pipeline". Hivi hao mafisadi "papa" hawana huruma na nchi hii? Kama alichosema Mkuu poisonous hapo juu ni kweli. namshauri Mkuu Maxence Melo tuanzishe harakati za kuupinga huu mpango muovu kupitia hii platform yetu.
Ahsante
 
Complexity ya hiyo mifumo naijua mkuu. ERP za TANESCO na TRA ni very very complex. Bado hatuna technological capability ya kuiunda hiyo mifumo.
Limsingi mkuu ni kwamba , tech maturity haiwezi lingana na ya silcon valley .
Lakini si sawa kuua taasisi ili mifumo hata ambayo iko katika capacity ya wazawa ikodishwe nje.
Mfumo kama wa kumanage rasilimali watu unanunua nje kwa Billion nyingi ni kweli haufanyiki ndani huo?
 
Wanaua man power ya ndani halafu kesho wanasema ajira hazipo
Ni sawa na walivyofanya kuua viwanda vya ndani ili waagize sukari, mafuta, mchele na unga toka nje
 
wazalendo wa kweli ni kama ninyi , sauti zenu zipazwe na sisikike , ipo siku sauti na maumivu haya yatamfikia mwenye kufanya maamuzi ya mwisho , ili wasimwingize chaka hao watu , tuliokoe taifa na midomo ya mamba wenye njaa kali ya kulitafuna hili taifa . Tunayasema haya tukiwa na uhakika na yanayoendelea jikoni , sio ramli na wahusika wanajua ni ukweli . Tumsaidie RAIS awashtukie mpango wao mchafu watu hawa
 
Wanaua man power ya ndani halafu kesho wanasema ajira hazipo
Ni sawa na walivyofanya kuua viwanda vya ndani ili waagize sukari, mafuta, mchele na unga toka nje
Waliua nguvu kazi ya viwanda vya ndani ambavyo kwa sasa vingekua vimeajiri wananchi wengi sana , na huenda vingepunguza tatizo la ajira,.
kwa sasa nchi imeingia kwenye uelekeo wa kidigital badala vijana wetu tuwawezeshe wawe wazuri tunashiriki kuwakata mikono wawe tegemezi kwa mataifa ya nchi ili watu flani wapate 10% ni aibu na laana
 
Tatizo nchi haina rais bali inaongozwa na genge la wahalifu...
Hapa ninatofautiana na wewe, Rais hawezi kuwa mwanasheria, mtaalamu wa IT , hakimu etc.
Lakini kuna wasaidizi wake ambao wanapaswa wamshauri kwenye maeneo hayo yote .
Hao ndio wanaweza kumpotosha .
Kwa hili la E-GOV kuna genge ambalo limeapa limpotoshe makusudi ili limshushie credibility maana akiifuta tu E-GOV au akiiweka kwenye namna ambayo itadhoofika watu watamlaumu Rais .
Na hapo ndipo sisi tunamshtua Rais asiingie kwenye huo mtego
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ