Wanasiasa wa Upinzani kuweni makini mnapofanya mahojiano na Media za Nje

Kama ameongea hivyo kwenye issue ya COVID19 huyo ni tatizo. Haiwezekani madaraka yakufanye ufanye chochote ili ufanikiwe bila kujali uzalendo.

Hivi uzalendo ni kupiga risasi wanaokukosoa?

Magufuli na wenzake huko CCM na serikali yao yote siyo wazalendo unless uwe hujui maana ya "uzalendo" na "mtu mzalendo"....

Huyu ni tyrant, muuaji na mwizi bila shaka yoyote...

Very unlucky and unknowingly, you're defending these...!!
 
Kama ameongea hivyo kwenye issue ya COVID19 huyo ni tatizo. Haiwezekani madaraka yakufanye ufanye chochote ili ufanikiwe bila kujali uzalendo.

Kama ni kweli kwa hili Lisu alipaswa kujibu kwa kulinda image ya nchi, lakini unatarajia nini kama hivi vyombo vyetu kila akiongea wanakata asisikike? Sijasikia hayo majadiliano ili nijiridhishe na alichojibu, ili niweze kuwa katika mazingira mazuri ya hitimisho. Ni vyema vyombo vya hapa nchini vikaacha kuwa biased na kumuhoji yeye hayo maswali wanayotaka aweke uzalendo, sio mambo ya kumbania kisha kuacha ahojiwe na watu wengine.
 
Wakisema Lissu bado hajapona ama amepewa mulungula na watu fulani...baadhi ya watu wanahamaki. Hata hivyo, dawa yake na wale wanaomuunga mkono kwa kutaka kuizamisha Tanzania inachemshwa na wananchi. Atainywa na atapona.
 
Halafu mbaya zaidi mwezi ujao zinaanza kampeni vipi atahutubia wananchi kwa YouTube au atawakusanya tu na kuwatoa mhanga kwenye corona.?
Hajajiandaa wala kuandaliwa kuwa mgombea Urais. Anaongea kiharakati mno kuliko jukumu analotakiwa ku face. Kwasasa nchi ipo kwenye diplomacy tension na Kenya sababu ya COVID19 na kila mmoja anataka nchi yake kunufaika.

Hapo alipaswa kujua aseme nini au ikibidi aseme hilo ni swala la ndani na tunaoshauri serikali kwa utaratibu tuliojiwekea na kuhusu hali ya sasa no comments sababu hakuna takwimu rasmi na pia wananchi wanaendelea na maisha bila hofu.

Anaposema watu wanakufa amesikia kwa nani? Huyu wasipomuweka chini wakamtoa hasira na uanaharakati tutashuhudia kampeni kituko safari hii.
 

"Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko." Moja ya imani za chama pendwa ambayo ilibakia kwenye makaratasi.

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Vitabu vya dini vinasema "usiseme uongo."

Mchana utaendelea kuwa mchana hata kama binafsi ungependa vipi iwe usiku.

Kujidanganya hakutatusaidia:

Watanzania, Kuukimbia ukweli hakutatusaidia

Heko Lissu kwa kuusema ukweli. Hauko peke yako. Wanaokumbatia janja, ghiliba, hadaa, na yote ya namna hiyo watakutana nasi October 2020 at our best.

Wanasahau kuwa wahanga wa ugonjwa huu wana ndugu na jamaa zao. Eti kuwa kwa njaa zao wao binafsi, basi kila mmoja na wahanga wote waingie kwenye ushabiki tu wa fulani dhidi ya fulani.

Mtoa mada tambua ushabiki wa kwenye Mbao FC, Ndanda, Mbeya City, Namungo FC nk, hauna nafasi kunapokuja masuala halisi na hasa yenye kuhusisha maisha ya watu.
 
Huyo jamaa yenu ni roporopo by birth wala hajaanza leo.

Ni sawa na kumwambia bata asinye kinyesi rojorojo.😁!
 

..Jpm anawaambia wananchi wasichukue tahadhari.

..TL anawaambia wananchi wachukue tahadhari.

..huu utaratibu wa kuenenda kiholela-holela wakati dunia ikihangaika kukabiliana na covid19 inatishia watu wa nje kujumuika na sisi.

..pia tukionekana hatuko makini ktk kuchukua tahadhari tunaweza kusababisha mataifa mengine yatuzuie kusafiri kwenda nchini kwao.

..Tunamshukuru kwamba covid19 haijatupiga ukilinganisha na mataifa mengine, lakini ni UJINGA kuenenda kana kwamba tunaitafuta covid19.
 
Kwa hiyo Marekani wanapotangaza maambukizi ya Covid-19 na kuonesha wanaongoza duniani ni kukosa uzalendo.

Watanzania mbona mnapenda nchi iongozwe kienyeji enyeji hivyo. Tunaenda shule ili tupractice professionalism sio uswahili.
 

..hivi CCM mmewahi kuwaunga mkono wapinzani ktk jambo gani?

..mbona kila siku mnawachafua na kujaribu kuwaaminisha wananchi kwamba wapinzani ni watu wabaya?
 
Yani wanaofanya CCM iendelee kuwa madarakani ni hao hao wapinzani kwa kushindwa kujitambua na kutambua nafasi zao.

Ni bora shetani unaemjua siku zote, kuliko...
Shetani ni shetani tu, ukikaa vibaya anakumiminia risasi 38, ogopa shetani.
 
lisu anaendelea na drama zake za risasi wakati akisubiri ilani ya uchaguzi itoke kwa mabeberu huko.
 
A country with no data, a chiefdom type of leadership.
 
Kabisa anahitaji washauri ili aongee kama Rais mtarajiwa sio mwanaharakati wa mitaani.

Watanzania hakuna anaependa kuona Wala kusikia adha za corona..

Lisu asicheze na hisia za wahisani zaidi kuliko za Watanzania wa kawaida ambao hawawezi kumudu lockdown ya hata siku tatu.

Toka amefika Tanzania amekuwa kwenye mikusanyiko muda wote bila tahadhali yoyote Ile, Ina maana hahofii Covid-19.

Atuambie ndani ya familia yake aliyoiacha Tanzania wamekufa wangapi kwa corona ama ndani ya Chadema pamoja na misongamano yote Ile wamekufa viongozi na wajumbe wangapi pamoja na familia zao.

Aendelee kupigania Uhuru wa kujieleza na sheria za mitandao za ajabu ajabu.
 
CCTV camera ziling'olewa na majambazi wenzako
 
Tumeficha data, ukiugua utajijua mwenyewe na familia yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…