Wanauchumi nipeni bajeti nikiwa na buku 3 natoboa vipi siku

Wanauchumi nipeni bajeti nikiwa na buku 3 natoboa vipi siku

skia chukua hapo majani ya chai ya hamsini chemsha chai tia kwenye chupa hiyo elfu 2 mia tisa toa mia tano kachukue chapata mbili piga hapo asubui unabakiwa na elfu mbili mia nne hamsini, mchana kaza usile jioni nenda kwa mama ntilie akupe hata ubwabwa wa 500 au buku ikiwa ukoko freshi hapo utabakiwa na elfu moja mia nne ya kesho yake tena
mkuu unaishi wapi vitu bei rahisi hivi!.. yani chapati 2 ni shilingi miatano!..
 
Wanazuoni na walioboboa kwenye uchumi hapa naishije Kwa siku

Nikiwa na buku 3 na ramani zimegoma

Hapo iwepo breakfast, lunch na dinner na nitambe Kwa mtaa

Naomba ushauri wa kina, me ni Mtanganyika mwenzenu
Mchele nusu na robo 1200
Mafuta 500
Cabbage 500
Karot na kitunguu 200.
Jumla 2400
600 unatamba nayo kitambaa.

Hapo mchawi gas huna gas pikia gas asilia ( Kuni).
Nusu na robo, unakula asubuhi, mchana na usiku.
 
Kama hauna familia na upo DSM

Hakikisha Una hivi vitu
Hotpot
Chupa ya chai

Unachofanya ukipika Ahsubui unaweka katika hotpot unatoboa hadi usiku na kiporo unapata

Chai the same.

Na ikiwa vifaa hauna

Usikae mbali na eneo linaitwa Buguruni pale supu utapata 500 ,ugali au wali hautozidi 1000 na usiku 1000
Utabaki na 500 ya kupata Lita moja ya maji .
Jitafute unaweza kuwa comedian mzuri 😅😨🎽
 
sasa cjajua uko mkoa gani.
coz iyo buku tatu kuna mikoa unaweza tumia kwa siku fresh kabisa.
toa location yako mkuu.
 
Mchele nusu na robo 1200
Mafuta 500
Cabbage 500
Karot na kitunguu 200.
Jumla 2400
600 unatamba nayo kitambaa.

Hapo mchawi gas huna gas pikia gas asilia ( Kuni).
Nusu na robo, unakula asubuhi, mchana na usiku.
Una CPA ya mambo ya uchumi wa kati
 
Sema na nafsi yako kuwa leo mko kwenye msimu wa kwaresma/Ramadhani hivyo mtafunga siku nzima. Hiyo buku tatu iweke kwenye wallet yako itakupa ujasiri wa kuwa nina hela na itaondoa hofu.

Ikifika saa moja usiku muda wa kufungua/kuvunja funga yako nenda kwenye kijiwe cha kahawa toa mia 5, hapo upate vikombe vya kahawa na kashata hadi ushibe.

Rudi nyumbani oga maji baridi, kunywa maji ya kuchemsha nyumbani au hata ya bomba lala usingizi wa amani huku kwenye wallet umebakiwa na 2,500 ya kuanza nayo kesho.

Leo isikutishe, unaimudu. Kesho huijui, ipangilie vyema.

Kila la Kheri.
Sema hiyo sio kufunga,nikujishindisha njaa
 
Wanazuoni na walioboboa kwenye uchumi hapa naishije Kwa siku

Nikiwa na buku 3 na ramani zimegoma

Hapo iwepo breakfast, lunch na dinner na nitambe Kwa mtaa

Naomba ushauri wa kina, me ni Mtanganyika mwenzenu
Kula buku kwa mama ntilie
Kula buku kwa mama ntilie
Kula buku kwa mama ntilie

Then siku imeisha
 
Sema na nafsi yako kuwa leo mko kwenye msimu wa kwaresma/Ramadhani hivyo mtafunga siku nzima. Hiyo buku tatu iweke kwenye wallet yako itakupa ujasiri wa kuwa nina hela na itaondoa hofu.

Ikifika saa moja usiku muda wa kufungua/kuvunja funga yako nenda kwenye kijiwe cha kahawa toa mia 5, hapo upate vikombe vya kahawa na kashata hadi ushibe.

Rudi nyumbani oga maji baridi, kunywa maji ya kuchemsha nyumbani au hata ya bomba lala usingizi wa amani huku kwenye wallet umebakiwa na 2,500 ya kuanza nayo kesho.

Leo isikutishe, unaimudu. Kesho huijui, ipangilie vyema.

Kila la Kheri.
kama kuna kufunga mwambie aende msikitini au kanisani au kwa mchungaji au shehe ajifanye kama anaenda kusalimia hapo anavizia msosi tu wa usiku alafu hiyo buku tatu aweke mfukoni au akachukue karanga atembeze kwenye mabanda umiza
 
Kula mipakani mara mbili,kati kati ya mchana na asubuhi,na kati kati ya usiku na jioni,buku jero mara mbili imeisha hiyo
 
Milo miwili yaani breakfast-lunch (brunch) inapigwa moja. Venue kwa mama lishe, piga ubeche wa chini/ukoko unalainishwa na mchuzi wa maharage, full plate ni buku tu, unashiba na kushushia kandoro.

Usiku saa mbili kwa mama lishe tena, ugali mboga saba kwa buku jero, shushia maji ya kandoro.

Unarudi home na chenji ya jero!!
 
Asubuhi piga neutral.

Mchana nunua maandazi ya buku kunywa na maji (maji yawe kama chai). Itabaki buku 2.

Usiku nenda kwa mama lishe yeyote wa kilocal mwambie unataka ukoko wa buku 2. Utapata ukoko mwingi sana na mboga nyingi kwa ajili ya kuulainisha. Utakula mpaka utauangalia.
 
Milo miwili yaani breakfast-lunch (brunch) inapigwa moja. Venue kwa mama lishe, piga ubeche wa chini/ukoko unalainishwa na mchuzi wa maharage, full plate ni buku tu, unashiba na kushushia kandoro.

Usiku saa mbili kwa mama lishe tena, ugali mboga saba kwa buku jero, shushia maji ya kandoro.

Unarudi home na chenji ya jero!!
Mtaalam
 
Back
Top Bottom