Wanaume (baadhi) wa Tanzania kufurahia Sensa, Low IQ!

Wanaume (baadhi) wa Tanzania kufurahia Sensa, Low IQ!

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Majibu ya Sensa yameonyesha kwamba Wanawake ni wengi zaidi kuliko Wanaume, baadhi ya Wanaume wanaona ni jambo zuri kwao, lakini ni wajinga kwani wasichokijua ni kwamba Wanaume ni wachache kuliko Wanawake kwa sababu Wanaume wanakufa mapema kuliko Wanawake, Kibaologia uwiano kati ya Wanawake na Wanaume ni 1:1 Dunia nzima ila human factors kama vita, umaskini, njaa, magonjwa vinachangia nani aishi muda mrefu klk mwingine.

Hivyo Wanaume walipaswa wajiulize ni kwanini ni wachache? Ni kwanini wanakufa mapema? Kwa maana uwiano wa watoto wa kiume kike wanaozaliwa ni karibia sawa yaani 1:1 sasa nini kinatokea baada ya kuzaliwa hata Wanaume wapungue?

Next time angalia tu mtaani kwenu kuna wajane wangapi kulinganisha na wanaume waliopoteza wake zao kwa kifo?
 
Hiyo ni nature wewe

Hata Wanyama pori ni hivyo hivyo

Hauelewi Biology labda, nature hata kwenye Animal kingdom ratio ya Wanawake wanaume 1:1, kunaweza kuwa na tofauti ndogo sana lkn huwa 1:1 na ndiyo maana Population ziko stable.

Labda nikuulize nini msamiati wa Kiswahili wa Mwanaume aliyefiwa na Mume? Mwanamke ni Mjane, je mwanaume?
 
Hauelewi Biology labda, nature hata kwenye Animal kingdom ratio ya Wanawake wanaume 1:1, kunaweza kuwa na tofauti ndogo sana lkn huwa 1:1 na ndiyo maana Population ziko stable.

Labda nikuulize nini msamiati wa Kiswahili wa Mwanaume aliyefiwa na Mume? Mwanamke ni Mjane, je mwanaume?
Mgane
 
Mkuu Kijakazi kimahesabu bado tu ni kama tuko sawa, nashangaa watu wanashabikia wakati ni asilimia moja tuu!

Watu niliokuwa nawaheshimu wenye busara kama Matola jana wamekuja na nyuzi kibaao
 
Hauelewi Biology labda, nature hata kwenye Animal kingdom ratio ya Wanawake wanaume 1:1, kunaweza kuwa na tofauti ndogo sana lkn huwa 1:1 na ndiyo maana Population ziko stable.

Labda nikuulize nini msamiati wa Kiswahili wa Mwanaume aliyefiwa na Mume? Mwanamke ni Mjane, je mwanaume?
Mgane, ila ratio hii inaapply tu wanyama wazaao mtoto mmoja, ila kwa ndege kama kuku huzaa majike wengi kuliko vidume.
 
Kweli wewe shule ulienda kushiriki na sio kujifunza. .

Kwa nini? Mbona inajulikana na scientific community Dunia nzima kwamba ratio ni almost 1:1, ila kuna human factors mfano India Wanaume ni wengi sababu ya social environment na siyo biological, India mtoto mwanamke akijua ana mimba jinsia KE anafanya abortion hali inayopelekea wanaume kuwa wengi zaidi lkn hiyo ni social factor na siyo biological!
 
Siyo kweli, Dunia nzima ratio ni 1:1, hata kwenye Animal Kingdom ratio ya jike/dume ni 50/50, na ndiyo maana population ziko stable!
Hiyo ratio ya 50/50 umeitoa wapi wakati kila nchi ratio ya wanawake ni kubwa
 
Mgane, ila ratio hii inaapply tu wanyama wazaao mtoto mmoja, ila kwa ndege kama kuku huzaa majike wengi kuliko vidume.
Sijui ni ndege gani hao lkn kwenye Animal kingdom ratio ni 1:1 it’s a well established fact na inatambulika Dunia nzima, ila kuna human factors kama abortion, vita, njaa n.k. hizo zote huaffect idadi.
 
Hiyo ratio ya 50/50 umeitoa wapi wakati kila nchi ratio ya wanawake ni kubwa
Ni kubwa sababu ya human factors na siyo biological isitoshe kuna nchi nyingi tu Wanaume ni wengi zaidi mfano India na sababu ni cultural, Wanawake hupendelea mtoto wa kiume hivyo kuna abortion kubwa sana ya jinsia KE hali inayopelekea kuwa na wanaume wengi zaidi.
 
Basi chukuwa data za watoto wanaozaliwa kila siku.

Wapi zinapatikana? Labda TZ ni unique lkn Dunia nzima hata UN inatambua kwamba ratio ni ~1:1, isipokuwa sehemu zenye matatizo kama vita Wanaume hupungua na hivyo hupelekea kuwa na wanawake wengi.
 
Ni kubwa sababu ya human factors na siyo biological isitoshe kuna nchi nyingi tu Wanaume ni wengi zaidi mfano India na sababu ni cultural, Wanawake hupendelea mtoto wa kiume hivyo kuna abortion kubwa sana ya jinsia KE hali inayopelekea kuwa na wanaume wengi zaidi.
Kwa hiyo kusingekuwa inafanyika hiyo abortion bado nature ingefavour wanawake tu kama nchi nyingine
 
Back
Top Bottom