Wanaume kwanini tunashoboka kwa wanawake wasiotutaka na wenye nyodo?

Sio wenye nyodo tu, hata wanapenda kushoboka na wanawake Malaya na wasiotulia wakapata mtu mtulivu kazi kumsumbua kutwa kucha. Hata kwenye jamii wanawake wavicheche wanawahi kuolewa kuliko wale ambao wanastaha...
 
Sio wenye nyodo tu, hata wanapenda kushoboka na wanawake Malaya na wasiotulia wakapata mtu mtulivu kazi kumsumbua kutwa kucha. Hata kwenye jamii wanawake wavicheche wanawahi kuolewa kuliko wale ambao wanastaha...
Mwanaume anaoa anahitaji utulivu,Mwanaume hawezi kumwacha demu mtulivu akaoa malaya.

Yaani ufikirie kutafuta hela, kulea familia na bado ufikirie umalaya wa mkeo,hayupo huyo mwanaume na kama wapo basi wachache.
 
Hongera
 
Kitasa 10k+5k ya ufundi=15k,
Mkuu amekupiga buku 5k huyo mdada,yaani amekupiga kwa mara ya pili😃😃😃
 
Sio wenye nyodo tu, hata wanapenda kushoboka na wanawake Malaya na wasiotulia wakapata mtu mtulivu kazi kumsumbua kutwa kucha. Hata kwenye jamii wanawake wavicheche wanawahi kuolewa kuliko wale ambao wanastaha...
Maringo na dharau ndo changamoto kubwa kwa wanawake wengi, sio kweli Wanaume wanapenda wanawake Malaya hapana

Wanawake wanao wahi kuolewa ni wale wasio na maringo na dharau na sio kwa Sababu ni malaya

wanawake wengi ambao wanachelewa kuolewa ni wale wenye maringo na dharau
 
Binti: Hallow habari Davy
Mimi: Safi , we nani?
Binti: We ni Davy ?
Mimi: Ndio
Binti: Uko wapi?
Mimi: Kilosa (jina nimetunga ).

Binti akakata simu. Mimi nikapiga baada ya yeye kukata(nilikuwa nishamtambua )

Mimi: Mbona unakata?
Binti: Nilikuwa namtafuta Davy ila sio wa huko kilosa itakuwa nimekosea namba.
Mimi: Wala hujakosea, mimi na wewe tunafahamiana wewe ni fulani tulibadilishana namba tulipokutana maeneo fulani, nilipiga kimya kutokana na wewe kutotoa ushirikiano. Ila sasa hivi niko kilosa kikazi.

NB: ukweli huyu binti nilikutana nae sehemu na kumuomba namba. Ila alikuwa hatoi ushirikiano wa kujibu ujumbe au kupokea simu , nikaamua kumpotezea. Na ukweli siku aliyonipigia alikuwa hamtafuti Davy mimi. Ila niliamua kuongea nae zaidi ili kumkumbusha tu kuwa mimi sio wa kuletewa nyodo kisa tu anasoma chuo fulani cha kata.

Tukaendelea na mazungumzo, binti akaongeza umakini baada ya kusikia neno 'kikazi'

Binti: Kwa hiyo huku kabla hujahama ulikuwa unafanya kazi wapi?

Mimi: (nikamtajia sehemu niliyokuwa nafanya kazi baada ya hapo tukaagana).

Akitarajia nitamtafuta,
Siku ya kwanza,ya pili ikapita bila kutafutana.

Siku ya tatu ujumbe unaingia kwa namba nyingine ya yule binti kwenye simu yangu: Mambo?

Mimi: poa, nani?

Hakujibu, akanipigia na kuanza kujielezea kwa kirefu huku akinikumbusha kwamba tuliongea juzi na akinilaumu kiaina kwamba sijamtafuta tangu siku ile tulipoongea.

Mimi nikamuahidi nitamtafuta baadae kwa vile niko 'bize'. Ukweli ni kwamba sijamtafuta, sitamtafuta.

Ushirikiano wa mwanzo ndio unaoongea kila kitu, akileta nyodo mwanzoni akirudi baadae usimpe ushirikiano.
 
Hizi ndo nyuzi sasa. Siyo kila siku wanaune wanalialia au kujipiga risasi. Dawa ya kiburi jeuri.
 
Nimekuwazaga sana nikaona kila kitu sio ukweli mengine unatunga 🤣🤣🤣
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Namna hiyo
 
Binafsi kuwashobokea hivi viumbe kwasana sinaga ni vile ukiwa sirias namm napita humo ukiwa simple namm napita humo
Japo wengn wananambya nakuwa sirias san mda mwing adi wanaogopa adi kunisemesha wengn bt mm sijali nafata mambo yangu tu
 
Nyumba zako ziko wapi nije nipange?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…