cocochanel
Platinum Member
- Oct 6, 2007
- 27,885
- 76,043
Mkuu mimi nimekubali sio kila mahusiano yataishia kwenye ndoa je Zuchu atakubali
Ndio maana nimesema wanawake tumetofautiana mkuu
Diamond mpango wa kuoa yoyote hana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu mimi nimekubali sio kila mahusiano yataishia kwenye ndoa je Zuchu atakubali
Ndio maana nimesema wanawake tumetofautiana mkuu
Ndio ukweli mkuu hata kama kosa ni lake ili mradi tu ameumia basi ni atakurogaaaa
Ongeza nyama kidogo mkuuMaisha niliyoishi mimi na mama yangu ni funzo tosha kwangu. Aise hivi visasi vya kimapenzi vinaumiza mno watu wasio na hatia, japo mimi ni mwanaume ila sishauri wanaume wenzangu kuendekeza tamaa za kutamani kila mwanamke.
ukishamzalishamwanamke huyo huyo nenda kaishi naye acha kutafuta wanawake wengine waoneeni huruma viumbe visivyo na hatia.
usiombe kisasi cha mwanamke mchagga halafu ni mshirikina.
Kuna wajibu wa kuwa na sheria kali kuhusu mambo haya uchumba miaka 5 then amemtumia kiasi cha kutosha bila kuoana kuna wajibu wa kuwa ana kanuni na kama zipo basi jamii iihelimisweInaumiza sana sana sana
Sasa hivi kumekuwa na matukio yakishamiri ya wanandoa kufariki baada ya ndoa ama siku chache kabla ya ndoa( mimi pia ni muhanga wa kukutwa na hilo tukio japo ilikuwa ni kabla ya ndoa nikapoteza mchumba kwa ajari.. hili sitaki kulizungumzia)
Kama wewe ni mfuatiliaji wa mitandaoni haswa page za kusherehesha utagundua hili jambo, hiki kitu kimekuwa kikipamba moto mno, wanaume kwa wanawake wanafariki muda mchache baada au kabla ya ndoa…
Ukipitia comments nyingi utakuta ni wanawake ndio wamecomment na nyingi zikiwa kama zinafikisha ujumbe kwa wanaume..
Wanaume acheni kuwaumiza mioyo wanawake ambao hamna malengo ya kuwaoa
Hiko hivi wanawake hatufanani kuna kina sisi ambao ukusema mahusiano yamekwisha unihitaji basi nitakubaliana na hali na kusahau na kusonga mbele kama injili, sasa omba mahusiano yako ukutane na kina sisi
Usije ukakutana na kina wale ambao hawajuagi kusamehe wala kusahau utajutaa kwanini ulizaliwa mwanaume,,, hao wanawake ndio hao sasa wabeba visasi ambao wako tayari kwenda kokote kufanya jambo lolote ili mradi akukomoe
Ndio hapo sasa unaposikia bwana/ bibi harusi kafariki miezi 2 baada ya ndoa ama siku 2 kabla ya harusi.. unasababisha watu wasiokuwa na hatia kudhulumiwa uhai wao
Imefikia hatua mpk unaogopa mwanaume atakaenioa ex wake alisamehe na kusahau au na mimi nitajumuishwa kwenye kisasi
Usiseme nimeachana nae kwa amani, wengine huonyesha hivyo mbele yako ukimpa kisogo ndio anaenda kukusemelea kwa babu yake
Nimeleta hili kwasababu kuna mwanaume mwenzenu huko kashasababisha vifo kwa mke na mtoto wake kisa ex wake
Wanaume mnatuhusisha kwenye matatizo ambayo hatuhusiki.. mimi siwezi kujua kila kitu kuhusu mwanaume anaetaka kunioa ukizingatia tumekutana ukubwani.. matokeo yake wanawake ndio tunateswa na ma ex zenu kwasababu zenu ambazo sisi hazituhusu
Imagine unaolewa na mwanaume kumbe alishaishi kinyumba na mwanamke mwinginee kwa ZAIDI Ya Miaka 10 na watoto wa 3,, hivi unafikiri mwanamke kama huyo, akisema analipa kisasi inakuaje??
Kama huna nia ya kuoa acha kumpotezea binti wa watu muda wake.. wanawake huwa tunatunza visasi moyoni anaweza kusema amekusamehe kumbe anakutafutia timing akumalize
Nawasilisha kama hivyo
Wanawake na sisi tujiongoze. Unakaa na mtu mwaka , miaka bila ndoa halafu unaendelea kuwa naye. Tutumie akili zetu kujua hapa hakuna future. Utaroga wangapi? Kutwa kucha utakuwa unabadilisha waganga. Tujifunze kumuacha ende, kwani kuna maisha bila wao. Atakuja ambaye ni wako.Kuna wajibu wa kuwa na sheria kali kuhusu mambo haya uchumba miaka 5 then amemtumia kiasi cha kutosha bila kuoana kuna wajibu wa kuwa ana kanuni na kama zipo basi jamii iihelimiswe
Mkuu tunatakiwa kuwaache Wanawake kiujanja na siyo una muache mwanamke kwa ghafra inatakiwa umuache taratibu mpaka akija kushtuka kashazoea, Na pia Ukimuacha Mpenzi wako anatakiwa hasijue kama umeoa na ata akijua iwe meditation miaka zaidi ya miwili uko, Na yeye kama atakua kasha zalishwa au kaolewa.Hakunaga kuachana kwa amani trust me… kuachana na mtu umetangaza nae vita… ila sasa upiganaji wake wa hiyo vita ndio kunatofautiana silaa, wenginee wanatumia risasi wengine makombora ya nyukliya
Mkuu umesema ukweli mtupu vijana ukitaka kufurahia ujana ingia kwenye Mahusiano na mabinti wa chuo lakini ukiingia kwenye mahusiano na Wanawake wenye miaka 28 na kuendelea utapata shida sana, Wanawake wenye kuanzia miaka 28 na kuendelea wao wanataka ndoa kwa udi na uvumba kwasababu wao wameshatumika sana, Sasa wanatafuta boya mmoja sasa kijana makini hawezi kukubali kuoa Mwanamke aliyepitia mahusiano na Wanaume zaidi ya sita.Tongoza wanafunzi , hasa wa chuo kama huna malengo ya kuoa, hao hawana visasi , ni pesa yako tu.
Hawa wawanawake wa mtaani wako open kwa ndoa,hawajui chochote hata kama ni maamuzi ya kichwa cha chini yamefanyika but no malengo,yeye ikimfata tu kesho yake anaelezea ukoo mzima kuwa amepata mchumba, sasa jichanganye umuache na asikie unaenda kuoa kwingine , kila rangi hutaacha kuona[emoji28]
Duh! Aisee 🤔Ngoja niwape story! Umekimbusha kitu
I have a good friend of mine! Ni Rafiki yangu haswa.
Ananiamini mno! Nimekuwa mshauri wake wa mambo mengi yangu tukiwa A Level na uzuri tupata nafasi ya kusoma chuo kimoja degree yangu ya kwanza.
Jamaa angu akipata mchumba ila ukweni wakazingua ila jamaa alimpenda sana yule Binti, baadae wakatengana
Kwenye mishemishe za maisha jamaa akapata manzi wa kutuliza hisia tu, gafla akampa mimba.
Hapo hapo kule ukweni wakamwita na kumwambia nyie owaneni tu.
Huyu manzi mwenye mimba baada ya kujua Hilo! Maana nilimwambia nenda na mweleze ukweli, kwa sababu hamkua na mahusiano yenye Malengo yoyote!
Manzi akakubali jamaa aoe ila mimba akasema hatoi! Tukamwambia tutalea mtoto.
Kumbe yule Binti kaondoka na kisasi! Ndoa imeisha baada ya mwezi shemu akapata na yeye mimba! Huwezi amini iliharibika na akaanza kuumwa sana.
Katika kuchunguza tukajua yule dada kashapoteza wadada wawili kwa uchawi!
Nikwambie Abeee ! Hii ishu niache Mimi ni deal nayo shemu atakaa sawa ... Baada ya Kufanya ninayoyajua ndo shemeji yangu kapona.
Hii michezo ipo
Mkuu jiandae ulete mkasa mzima tujifunze kituHizi michezo ya visasi ipo sanaa, kuna rafiki wa jamaa yangu aliachana na binti tena kwa amani miaka ya 2010.
Jamaa akaja kupata mchumba mwingine 2013 akiwa kwenye shirika moja kubwa nchini linamlipa pesa nzuri.
Mwaka huo huo, Jamaa akaenda kikazi mkoa flani, by coincidence akakutana na yule X wake maeneo ya Mnadani wakabadilishana namba za simu.
Usiku jamaa akaona asilale kinyonge, akamchek X aje kumpa Kampani. Ebwana eeeh! That was a fatal mistake.
Hii story ni ndefu kidogo ntakuja kuiandikia uzi separate nikitulia.
Mimi niliambiwa live ntarogwa😂 lakini Bado nadunda, ukiona limenifika Allah kaliandika hakuna kukwepa, vinginevyo hakuna linalonifika💪.Inaumiza sana sana sana
Sasa hivi kumekuwa na matukio yakishamiri ya wanandoa kufariki baada ya ndoa ama siku chache kabla ya ndoa( mimi pia ni muhanga wa kukutwa na hilo tukio japo ilikuwa ni kabla ya ndoa nikapoteza mchumba kwa ajari.. hili sitaki kulizungumzia)
Kama wewe ni mfuatiliaji wa mitandaoni haswa page za kusherehesha utagundua hili jambo, hiki kitu kimekuwa kikipamba moto mno, wanaume kwa wanawake wanafariki muda mchache baada au kabla ya ndoa…
Ukipitia comments nyingi utakuta ni wanawake ndio wamecomment na nyingi zikiwa kama zinafikisha ujumbe kwa wanaume..
Wanaume acheni kuwaumiza mioyo wanawake ambao hamna malengo ya kuwaoa
Hiko hivi wanawake hatufanani kuna kina sisi ambao ukusema mahusiano yamekwisha unihitaji basi nitakubaliana na hali na kusahau na kusonga mbele kama injili, sasa omba mahusiano yako ukutane na kina sisi
Usije ukakutana na kina wale ambao hawajuagi kusamehe wala kusahau utajutaa kwanini ulizaliwa mwanaume,,, hao wanawake ndio hao sasa wabeba visasi ambao wako tayari kwenda kokote kufanya jambo lolote ili mradi akukomoe
Ndio hapo sasa unaposikia bwana/ bibi harusi kafariki miezi 2 baada ya ndoa ama siku 2 kabla ya harusi.. unasababisha watu wasiokuwa na hatia kudhulumiwa uhai wao
Imefikia hatua mpk unaogopa mwanaume atakaenioa ex wake alisamehe na kusahau au na mimi nitajumuishwa kwenye kisasi
Usiseme nimeachana nae kwa amani, wengine huonyesha hivyo mbele yako ukimpa kisogo ndio anaenda kukusemelea kwa babu yake
Nimeleta hili kwasababu kuna mwanaume mwenzenu huko kashasababisha vifo kwa mke na mtoto wake kisa ex wake
Wanaume mnatuhusisha kwenye matatizo ambayo hatuhusiki.. mimi siwezi kujua kila kitu kuhusu mwanaume anaetaka kunioa ukizingatia tumekutana ukubwani.. matokeo yake wanawake ndio tunateswa na ma ex zenu kwasababu zenu ambazo sisi hazituhusu
Imagine unaolewa na mwanaume kumbe alishaishi kinyumba na mwanamke mwinginee kwa ZAIDI Ya Miaka 10 na watoto wa 3,, hivi unafikiri mwanamke kama huyo, akisema analipa kisasi inakuaje??
Kama huna nia ya kuoa acha kumpotezea binti wa watu muda wake.. wanawake huwa tunatunza visasi moyoni anaweza kusema amekusamehe kumbe anakutafutia timing akumalize
Nawasilisha kama hivyo
Wanaorogwa huwa hawasemi mkuuMimi niliambiwa live ntarogwa😂 lakini Bado nadunda, ukiona limenifika Allah kaliandika hakuna kukwepa, vinginevyo hakuna linalonifika💪.
Tena wengine wanakuroga hata kosa huna, basi tu uonevu.
Hayo yote ya nini … kama huna malengo na mtu achana nae mapemaMkuu tunatakiwa kuwaache Wanawake kiujanja na siyo una muache mwanamke kwa ghafra inatakiwa umuache taratibu mpaka akija kushtuka kashazoea, Na pia Ukimuacha Mpenzi wako anatakiwa hasijue kama umeoa na ata akijua iwe meditation miaka zaidi ya miwili uko, Na yeye kama atakua kasha zalishwa au kaolewa.
Wengine hujuaHivi familia zao au wanaooana anayebaki anajua je kuwa huyu au yule ni sababu ya mchezo kaondolewa?