Wanaume naomba mnijibu tafadhali

Hao ni wavulana ndio wanafanya hivyo mkuu.
Mwanaume kamili akifika nyumbani anaacha pesa zake zote na kuzitolea maagizo kwa kila kiasi, then yeye ndie anachukua kiasi kidogo kwaajili ya matumizi yake binafsi kwa siku inayo fuata.
Umesema sahihi Mkuu

Kipaumbele cha kwanza familia

Unampatia wife kibunda chote kisha unamwelekeza, kwenye kile kiasi utachukua shilingi 50,000 utampa Mzee Moh'med kwaajili ya chakula cha Kuku

Shilingi 45,000 utalipia school bus ya mtoto

Haipendezi Mkeo kukuomba hela ya Matumizi Kwa Kila Siku

Kama una nafasi mpe ya mwezi mzima ili apange bajeti yeye mwenyewe
 
Exactly yaani unaacha hela ya emergence au ya vitu visivyokuwa na ulazima na hiyo hela sio lazima itumike kila siku.
Ni maisha ya umaskini tu hayo kuna siku nilidamkia mitaa ya tandika kule mwembe yanga nikaenda shop kununua maji nikakuta mtoto katumwa kununua sukari vijiko 5 nilishangaa na kujifunza kwamba haya maisha yetu kuna gap kubwa sana la kipato na moangilio wa maisha
 

Utakuta mtu leo ameenda dukani kanunua nyanya mbili,kitunguu kimoja ,mafuta ya kupikia kibaba kimoja ,kesho anaenda tena kununua nyanya mbili,kitunguu,mafuta ya kupikia kibaba kimoja ,kesho kutwa hivyo hivyo wakati angeweza kununua tu nyanya 6 ,vitunguu vitatu na mafuta vibaba vitatu hizo siku mbili akawa na stock.

Ya nin kila siku uende dukani kununua unga nusu wakati kuna unga ulifungwa wa kilo 3 hadi 5? Siyo kwamba hana hela ya kununua hivyo vitu kwa pamoja la hasha anayo sema ni mentality tu washajijengea.
 
Usishangae mkuu kwamba mtu hana hio hela ya kununua hilo furushi la vitunguu na unga. Vidole havilingani mkuu! Kuna mtu kipato chake ni buku 7 kwa siku akitoa nauli anabakia na buku 5 ndio akabalansie mambo ya maskani.

Mke akipewa elfu 4 kesho ndio mambo ya vitunguu vya 300 dagaa za buku jero, unga nusu, nyanya mbili na karoti moja, sukari robo yanapotokea.
 
Swali, Ungekuwa na hio laki nne ungeweza kumpa mumeo elfu 20 kila siku? Chukulia hio laki 4 unayo wewe.
 

Hao nawaelewa kuna wale ambao wanayo hiyo hela ,utakuta mtu kabisa hadi ana kausafiri ka kutembelea lakini na yeye ndiyo wale wale kila siku kwenda kununua mchele kilo moja.
 
Kuna mjinga alipewa million 10 za site na mumewe akahifadhi, akachomoa laki 2 kimya kimya akamtumia baba yake siku hela inahitajika ikakautwa iko 9.8M 🤣alikula makofi hakuamini kisha akatimuliwa aende kwa huyo huyo baba yake.

Baba mkwe akapiga simu tu kumuombea msamaha mwanae arudi. Wanawake wajinga sana wakiona hela.
 
Hao ni wavulana ndio wanafanya hivyo mkuu.
Mwanaume kamili akifika nyumbani anaacha pesa zake zote na kuzitolea maagizo kwa kila kiasi, then yeye ndie anachukua kiasi kidogo kwaajili ya matumizi yake binafsi kwa siku inayo fuata.
Umuachie sharifa bunda ndani bila maelekezo si atamaliza maduka sinza kununua mawigi ya kila aina😂 na kubandika kope na kucha.
 
Wanawake tuna akili kama za watoto,nilivyokuwa mdogo baba alikuwa anaweka pesa kwenye mfuko wa shati sasa nikiomba akisema hana nilikuwa simuelewi kabisa...kumbe zilikuwa zina mambo kibao ya kusolve..😅
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 We ukiona bunda unajua zote za biskuti zile 😁
 
Wanawake wa hivi mkuu bure kabisa
 
Wanawake tuna akili kama za watoto,nilivyokuwa mdogo baba alikuwa anaweka pesa kwenye mfuko wa shati sasa nikiomba akisema hana nilikuwa simuelewi kabisa...kumbe zilikuwa zina mambo kibao ya kusolve..😅
Vipi baada ya kukua na kuanza jitegemea , unamshauri nini ,huyu mwenzako mleta mada
 
Wanaume hatuachi hela, tunaacha kadi mama ajichotee mwenyewe anavyotaka akiridhika ajue yeye mwenyewe karidhika wapi.

Mimi nitajuaje atakachohitaji ghafla wakati sipo?
Hujui Dunia wewe , kadi kama kuacha inaachwa ya famili account tu na lazima elewa bajet ya pesa iliyotoka imetumika vipi, unaacha kadi ajichotee , unaongea nini ,wewe sio mwanaume na kama mwanaume umerogwa sio bure ,
 
Kabisa mkuu , unaokoa gharama ya muda hata fedha .
Manake unakuta mtu ananunua nyanya 1 sh 150 wakati fungu moja la nyanya sh 400 unapata nyanya 4 hata vitunguu ni hivyohivyo .
Kuna watu wana uwezo huo ila hawafanyi hivyo kwa sababu za ajabu sana mfano kuna jamaa yangu analalamika akinunua vitu in a bulk mke wake anagawa kwa mashoga zake
 
Mtoa mada kaona mumew anajali mchepuko Zaid ndo kilichomuuma
Mchepuko wapi, nyie wanawake ambao mmeolewa na ambao mpo na mausiano , ukiona mwenzako amekaa na mwanamke mwenzio mnafikili ni mchepuko wake? Kwani hawezi kuwa mfanyabiashara mwenzake au rafiki/ mtu wa karibu katika kufanikisha mambo yake zikiwemo izo pesa mnazolalamika ni ndogo.

Itoshe kusema wazee wetu wanaishi kwenye ndoa mpaka Mungu anawachukua ,ila kwa sasa wanawake wenda sio wote sijui wamekumbwa na shetani gani,
 
Acha iyo , kuna shule moja hivi , mkurugenzi alijichanganya kwenye nafasi mbalimbali za shule akaweka na ndugu zake mkewe ,siku ya siku ikachotwa pesa katika account ya shule na kununuliwa gari ya baba mkwe,
Mkurugenzi alipogundua iyo gari aliipiga bei na kuwatimua kwenye nafasi zao
 
Kampeni ya haki kwa wanaume inatakiwa kuanza kwa haraka sana hali ni mbaya sasa, leo msione wanaume wanatembea barabarani ,majumbani kwao hapakali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…