Wanaume ndiyo viumbe pekee wanaoweza kukaa pamoja na kupiga ‘story’ kwa saa 6 bila kujuana majina yao

Akhsante sana na kwako pia SABATO NJEMA mpendwa
 
Mie sasa karibu miezi minne kuna jamaa pale basketball ground simujui jina ila kila siku tupo pale.
Mkuu uko mkoa gani,na wilaya gani na huo ground ya Basketball unachezea wapi mm ni mdau wa huo mchezo napenda sana Bball mm niko Dar
 
Mimi maisha ya chuo nilikuwa najichanganya kila idara iwe kwa walevi, Walokole, wazee wa movies, wazee wa games, wazee wa mikeka, wazee wa kutembea usiku kucheki soka, group discussion za watafuta GPA kubwa. Kote huko ukinikuta utafikiri ni mwenyeji. Mpaka wadau wengine wakawa wananihisi ni mtu wa usalama taifa kumbe nimezoea tu maisha ya kujichanganya na watu
 
Hujaelewa mada tulia soma vizuri. Au ngoja nikusaidie mfano mpo kwenye usafiri wanaume mnaweza jikuta mnapiga story kwa muda mrefu bila kuulizana majjna zaidi ya kuitana mwamba,bro. Hajamaanisha story za kujichanganya au kufatana na watu mbali mbali
Wadada nyie mnafuatanaga wale mashosti kama kumbikumbi
 
Mkuu wewe Ni mhaya?
 
Bora yako wewe mi na baba yangu hadi leo hatujuani majina mi namsalimia "big niaje" ye ananijibu "Ni yechu tu dingilai"
 
Naongezea.

Unafukuzia Mtoto, anakusikiliza mnabadilishana/mnapeana namba za simu. Cha ajabu wewe ukiwa unasevu namba unamuuliza jina lake kisha unasevu kwa jina alilokutajia, yeye wala hakuulizi jina lako ila anaisevu namba yako na mtawasiliana kama kawaida.

Maajabu haya
 
Mi jana tu hapo nauli zimepanda halafu nilikuwa naenda vituo viwili vinavyofuata na ata sina haraka [narudi maskani] nikaona isiwe tabu.

Basi nikaamua kuonesha msisitizo kwamba natembea; kula nauli, literally - kununua hindi la kuchoma🤣🤣. Halafu nikatembea zangu

Sasa njiani nakutana na jamaa anaswaga ndama katoka kumnunua[so yeye ilikuwa lazima atembee] tumepiga stori hadi nafika nakatisha na hakuna aliyeondoka na hata idea ya jina la mwenzie.
 
Noma sana
 
Hata siku kadhaa mnaweza kuwa mnakutana story kibao mnaachanazhadi kuja kufahamiana it takes time.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…