Wanaume tuwe makini tuwapo na wake zetu kwenye mizunguko

Wanaume tuwe makini tuwapo na wake zetu kwenye mizunguko

Ha ha haaaa!! umenikumbusha tulikuwa tunaenda moshi mjini na brother wangu sasa tulikuwa tuko watatu, mimi ,brother pamoja na mke wake, ila mke wake alikuwa amekaa siti ya nyuma alafu amenyamazaaaa kimya muda mrefu sisi ndio tunapiga story!

tukasimamishwa na trafiki wa kike pale KIA kwakweli alikuwa mzuri yule dada masikini nadhani ndio alikuwa anaanza kazi maana hata kuuliza maswali alikuwa anaogopa! alipoturuhusu tuondoke tukaanza kumsifia yule dada,

ghafla broo akasema 'NAKWAMBIA MOSHI KUNA WATOTO ASIKWAMBIE MTU" ghafla tukashtulia na sauti ya shemeji ikisema "NDIO MAANA MLIKUWA MNANILAZIMISHA MNISHUSHE KWETU NISALIMIE NA NYIE MUENDE KWENYE MIHANGAIKO,

KUMBE NDIO MIPANGO YENU KUJA HUKU MOSHI LEO KWA WATOTO" kimya kikatawala kidogo ila brother alirudi na topic mpya tena kwa ukali, "sasa unachokasirika ni nini!!? si nikweli kila kona MOSHI utaona watoto wanaenda shule!!? kila kona hebu ona wale kule eenhh ona wee ona tu mwenyewe kila mahali ni watoto wako busy na kwenda shule"

Mkuu hukuchukua namba ya huyo traffic unirushie?
 
Juzi kati nikiwa na wife wangu katika mizunguko ya hapa na pale town ghafla akapita dada mmoja amevalia skirt nyeusi fupi mno na high heels bila shaka dada yule atakuwa mtu wa kusin kwani alikuwa na umbo la kibantu haswa na mrefu wa haja.

Nilikuwa kwenye speed ndogo ghafla nikajikuta nasema Dah shiiit, huku nikimtolea macho yule dada ni kama vile nilikuwa sikumbuki nipo wife pembeni taratibu wife akaniuliza Baba nini shida? Ikabidi nibadili topic.''Nikamwambia pumbaf kabisa hivi umeona huyu dada kitu alichavaa? Kwanini wanawake mnashindwa kujiheshimu lakini, uvaaji gani huu na siku mke wangu uvae hivyo walahi nakupa talaka siku hiyohiyo"

Wife kiupole akadhani kweli nimekasirishwa na uvaaje wa yule dada kumbe nilistaajabu umbo na uzuri aliokuwa nao yule dada, akaniambia lakini wanaume wengine ndio wanawapendaga wanaovaa hivyo. Nikaongeza kwa sauti ya ukali "hakuna kitu wife uvaaji gani huu wa kijinga kabisa bwana.

Story zikabadilika toka hapo tukaendelea na mambo yetu moyoni nasema leo ningeshtukiwa sijui ingekuaje? Dada zangu chonde chonde na vivazi vyenu jamani.

Ila mimi nilishangaa uumbaji uliotukuka tu.


ni hatareeee sanaaaaa

 
Haahaaaa mkuu umenichekesha sana

Ila ufahamu kuwa wanawake wana akili sana, wanakumbukumbu sana na wanajua kuunganisha matukio

Siku moja ukibugi tu anaunganisha dots na kupata mchoro kamili

Take note of this au ujitahidi nawe uwe na kumbukumbu za kutosha na uendelee ku-pretend the same way through out kwa watu waliovaa nguo fupi na kuumbika sana

Aisee umeongea ukweli kabisa unaweza ukawa unampotezea mwanamke events nyingi thn kuna siku umejisahau anakukumbusha every event...utasikia unamkumbuka yule binti wa siku ile mwenye gauni la pink pale sheli...eeh?

Saa hizo unajing'ata na kuunganisha sound za kutoa
 
Dah mie leo mchana nilikuwa na my wife wangu, tuko kwa gari yetu inayotumia petroli, tukapita karibu na baa moja..ambayo mie siku zote, nilijua ni kibaa uchwara, lakini kwa kuwa leo tulipita karibu sana..nikaona nyama choma za nguvu kwenye jiko na harufu nzuri ya misosi inayoenda na kinywaji. Afu wateja kibao mle kwa baa.

Nikamwambia my wife wangu, "kumbe hii baa ni nzuri ee.. .?". Akajibu, "inavyoonekana ni baa nzuri..." then nikajilipua, "inawezekana kuna mademu wazuri pia hapo...?" Akaniangalia usoni amenikazia macho; nami nikawa namuona kwa jicho la pembe huku nimeng'ang'ania usukani...akaniambia "si uende ukahakikishe..." Ukimya ulitawalaka muda, na mada ikaishia hapo!

Ila lazima nitarudi kula zile nyama dadeeek!
 
Mungu fundi ujue,kuna vitu alitulia sheikh...maana unaweza sahau kama uko na wife hapo pembeni
 
Haaa ama kweli,mpaka wife mwenyewe anaamua kumhusisha mmewe kuhusu kazi za Mungu! sasa hebu acha niulize,kama wife anakuuliza hivyo anakuwa anategemea umjibuje mfano alafu hiyo topic anaimaliza nani?
 
Hhhhhaaaaaaaaa tuwe tunaachana tuangalie tu tu buanaa
 
kuna watu waongo humu!! Hata ukicheka inatosha si lazima uzushe kisa na wewe. Kha!
 
kaka kuna siku na mie kidogo inikute, kwani tulikuwa tunatoka kwenye mihangaiko mie na my wife wangu, wakati naendesha gari nikamuona binti kaumbika nilimpiga jicho mara 1 nikabaki namtathmini, kumbe wife ananitizama usoni na mie nikawa nishamstukia nikajifanya kama sijaona, basi ilimtoka mwenyewe du mume wangu umeona yule dada alivyoumbika nikajifanya kuuliza yuko wapi kumbe hajui mie nishamuona muda mrefu, kwani kuna siku tukiwa jangwani sea breeze nilishawahi pigwa kofi mpaka nikaona nyote kisa macho kung'ang'ania kwa binti 1 mrembo aliyekuwa anatoka kupata shower rain

hahahahaaaa! kaaaazi kwelikweliiiiiii!!
 
Inatokeaga unaweza panga kula wali samaki kisha unafika hotelini unamkuta mtu anakula ugali nyama choma nawe ukatamani
 
Hv na wake zenu wakianza kushangaa wanaume njian mkiwa wote nanyi mtajickiaje!! Siyo kuwa hawapend kushangaa wanaume magentlemen njian ila tu wanalinda heshima ya mume wake. Bas na wanaume pia walinde heshma za wake zao pind wanapokuwa wote njian. Shangaa hvyo vituko ukiwa peke yako..
 
We jamaa nahisi utakuwa ni Mhaya au Mjita...

Nilipoanza kusoma nikadhani "hilo gari lako linalotumia petrol" linahusiana na stori inavyoendelea kumbe umeandika kama mbwembwe...

Umenifanya nimkumbuke kibopa mmoja wa Kihaya aliyekuw anamuuliza mlinzi, "kwa magari yenye full tank tunapark wapi?"...


Dah mie leo mchana nilikuwa na my wife wangu, tuko kwa gari yetu inayotumia petroli, tukapita karibu na baa moja..ambayo mie siku zote, nilijua ni kibaa uchwara, lakini kwa kuwa leo tulipita karibu sana..nikaona nyama choma za nguvu kwenye jiko na harufu nzuri ya misosi inayoenda na kinywaji. Afu wateja kibao mle kwa baa.

Nikamwambia my wife wangu, "kumbe hii baa ni nzuri ee.. .?". Akajibu, "inavyoonekana ni baa nzuri..." then nikajilipua, "inawezekana kuna mademu wazuri pia hapo...?" Akaniangalia usoni amenikazia macho; nami nikawa namuona kwa jicho la pembe huku nimeng'ang'ania usukani...akaniambia "si uende ukahakikishe..." Ukimya ulitawalaka muda, na mada ikaishia hapo!

Ila lazima nitarudi kula zile nyama dadeeek!
 
Utajuaje kama gari lake linatumia petrol?????


We jamaa nahisi utakuwa ni Mhaya au Mjita...

Nilipoanza kusoma nikadhani "hilo gari lako linalotumia petrol" linahusiana na stori inavyoendelea kumbe umeandika kama mbwembwe...

Umenifanya nimkumbuke kibopa mmoja wa Kihaya aliyekuw anamuuliza mlinzi, "kwa magari yenye full tank tunapark wapi?"...

Hapo kasahau kuandika ukubwa wa engine tu...
 
Back
Top Bottom