Wanaume wanapenda kwa vipande sio kitu kizima

Wanaume wanapenda kwa vipande sio kitu kizima

Hata unipe nini lakini hutoweza kunitosheleza hivo lazima nitatoka nje tu na nitarudi ndani kikubwa nakuheshimu na natimiza majukumu wewe niache tu wala usiumie roho.

Stupidity [emoji706] kwahiyo muachwe tu mlete magonjwa eti simply because hamuwezi kutulia, wanawake kibao hawatoshelezwi mbona wametulia wanawavumilia au na wao wakatafute watu wengine huko wa kuwatosheleza, kujiendekeza tu.[emoji57][emoji57]
Usiwe na hasira sasa
 
Ndio maana umeyapenda maneno ya mama Mghwira [emoji23][emoji23][emoji23]

Ila eti wanasemaga "utazunguuka mabucha yote nyama ni ile ile" sa sijui kweli au vip[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Hii kauli si ya kweli, mabucha kweli ni yaleyale ila nyama inapishana utamu
 
Kaongea fact mwambie aagize k vant nakuja kulipa na mnyama pendwa kilo ndizi kwa mbali.
 
Hamna lolote Ni kujiendekeza tu,Ni wanaume wangapi wametulia na mwanamke mmoja?

Sent using Jamii Forums mobile app
Upo sahihi Dada..mimi nimeoa nikiwa 31 na nilioa nikiwa clean kabisa kabisa sikuwahi kudondoka hata mara moja tangu utoto..nilikuwa kuwa na mchumba kabla na tulidumu more than 5 years without sex.

Ingawa ilitokea bahati mbaya hatukuoana...ila nimeoa my first girl kumjua ndio huyu mke wangu. Na sijawahi toka nje ya ndoa na siatatoka huu ni mwaka wa 13.
Hata yeye aje asaliti mie sitafanya huo ujinga kamwe.
Majaribu ni mengi mno mno mno lakini msimamo wangu unayazidi majaribu yote no matter what.
Ni kweli wapo wanaume wengi tuu sio mmoja wala Wawili ambao ni waaminifu mno..most of my friends wapo hivyo...wapo walioa na ambao bado..but those are very good men.
 
Wanawake wao wanapenda nini

Sent using Jamii Forums mobile app
Wote ni sawa tuu..wanaume ni vipande na wanawake pia..ni uamuzi tuu wa kuchagua which part is best for your life,you choose one and stay for ever..kuna maandiko yanasema enyi wanadamu kamwe hamtaweza kutimiza tamaa za miili yenu..tamaa ni kama mtihani tuu ambao kila mwanadamu amepewa.
Hakuna mwaka zitaisha labda uwe mgonjwa hoi kabisa...
Ni kuamua ni kuamua ni kuamua tuu.
Mimi kama mwanaume niliapa kamwe siwezi kupangiwa au kuendeshwa na kiungo tuu cha mwili never never.
Uanaume ni kujitawala na kujicontrol..kuvumilia magumu na mateso.
Daima najiona mimi ndio mwanaume strong mbabe nisie shindwa na vitamaa mshenzi.
 
Umenifurahisha sana, Allah akubarikie mamaangu.

Hivi inakuwaje watu wengine wasomi kabisa lakini hawajui kuwa mwanaume akikupenda wewe kwa sababu ya digirii yako na ingilishi yako huyohuyo atampenda mwengine kwa sababu ya mahabbat. Na huwezi kupewa vyote kwani we nani. Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi wa kumpa huyu hiki na akampa mwengine kile.

Mama wewe ni mshauri wa kimataifa asante sana.
 
Jana katika pita pita zangu mitandaoni nikakutana na lile sakata la yule Bi. Mkubwa aliechezea vitasa mjini Moshi baada ya kuhusishwa na fumanizi flani.

Katika hali ambayo iliamsha hisia zangu zaidi ni mahojiano ambayo yalifanyika kati yake na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira ambapo mwisho wa siku aliamua kutoa ufafanuzi flani juu ya lile tukio kama kuhitimisha.

Alisema, "Kupendwa ni haki ya kila mtu hivyo hakuna sababu ya wanawake kupiga wenzao maana kimsingi hakuna kosa kwenye kupenda. Isitoshe mwanaume huwa anapenda kwa vipande vipande (sections) na huwa hapendi mwanamke mzima. Kwako atapenda pua, kule sikio, kule macho n.k. Wanawake wamejaaliwa nguvu ya pekee ya kupenda mtu katika uzima wake hivyo ni vyema wangejifunza kuishi na hilo badala ya kuumizana."

Kimsingi naona mama Anna Mghwira ametuinua kinamna flani japo ChrisMauki alitupondea. Pia, kamaliza ule utata wa siku nyingi kuhusu wanaume kuwa haturidhiki na mke mmoja, jamani warembo sie tunapenda kipande flani tu kwa kila mwanamke na ndio maana tunahangaika kukamilisha mwili mzima. Mtuelewe tafadhali wala msipigane 😂😂😂
Aulizwe yeye Anna Mgwira kaolewa na WANAUME wangap?au ameshawah kuishi na WANAUME wangap?
 
Aulizwe yeye Anna Mgwira kaolewa na WANAUME wangap?au ameshawah kuishi na WANAUME wangap?
Ukipata majibu nami nitag nije kisoma, maana kabla ya kwenda Kilimanjaro nilikuwa namuona na gari ya zambarau tu.
 
Back
Top Bottom