Wanawake jifunzeni kuwatunza na kuwaheshimu wafanyakazi wenu wa ndani yasije kuwatokea haya anayopitia mzazi mwenzangu

Hawawezi upo sahihi. Kuna tension fulani ya kuonesha umaza house ambayo sio ya lazima
 
Nipe namba yake PM mkuu
 
Unamtesa mtoto wa watu, mara fimbo mara makofi mwishowe afe afu ufie jela kisa ujinga tu. Alafu bado huyohuyo unaemtesa unamuachia akuangalizie vifaranga vyako ukienda kutafuta mia mia zako. Hivi hizi akili huwa zikoje jamanii???

Tangia udogo wangu mbaka utu uzima sijawahi ona msaidizi wa kazi akipigwa. Nimeona juzi kwa macho yangu. Alooo nilifuraaaa, nikasimama katikati. Unajua mbaka mwili unauma kwa zile hasira mana kumuonea mtu kisa yupo kwako na unaona hana msaada basi kwako faida etiii!!!

Kama wapo wamama wa staili hizi waache huu ujinga. Sio sawa hata kidogo. Mtoto wako nawewe anakua hujui kesho atakaa kwa nani. Vipi uone anapigwa kama wewe unavofanya kwa watoto wa wenzio???

Ni kweli wapo wengine hawana adabu na vijitabia vya hovyo. Mrudishe alipotoka uendelee na mambo yako. Ila ujinga wa kutesa watoto wa watu sio sawa kabisaa.

Ova
 
Kwa kweli madada wanapaswa wapewe maua yao. Wazazi wengi tunafeli kuwanyanyasa madada wa kazi lkn hatuoni umuhimu wao.

Binafsi ninaishi na mdada ki ukweli namlea kama binti yangu. Licha ya mshahara namnunulia mahitaji yote ya mtoto wa kike. Na ikitokea familia yake inachangamoto basi natoa msaada.
Na mwezi uliopita nilijikusanya nikamnunulia simu ya laki mbili na nusu. Sifanya haya kwa sababu nina kipato kikuba la hasha natambua thamani yake ya kunilelea mwanangu wakati mimi sipo.

Kuna siku nilisafiri kikazi kufika usiku wa manane dogo kaanza kutapika,,,akachukua kadi ya mtoto akampeleka hospitali hapo kanipigia simu sijapokea nami simu nilikuwa nimeweka chaji. Kulipokucha ndo nikampigia akanipa taarifa hizo.

Japo si wadada wote wanajielewa lakin kama alivyosema mtoa mada tuishi nao kwa haki kwa sababu nao ni binadamu.

Mungu awabiriki wote wanaowatendea vizuri wadada na kuwachukulia kama sehemu ya familia yao.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…