Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 22,379
- 41,294
Siku hizi kuna wajasiriamali Wengi Sana WA vyakula sehemu mbalimbali.
Ukiingia online karibu kila kitongoji kina wapishi mbalimbali wanapika kuanzia pilau,Biriani n.k.
Na wengine wanakuwa maarufu Sana.
Sasa basi kuna aina ya wanawake usiombe umpeleke sehemu muende Kula chakula Kwenye restaurant inayovuma Kwa upishi labda wa pilau au Biriani au chochote kile...inakuwa kama mtu "kachokozwa"...
Ni mwendo wa kuponda na kukosoa mapishi mwanzo mwisho.
Utasikia viungo vimezidi Sana au pilau hili bado Sana kuna kitu hakija kaa sawa..mara hivi mara vile.......yaani unaweza kukuta ulipompeleka mtu anasifika mji mzima lakini yeye kazi "kukosoa Tu"....na sometimes mapishi yake unayajua hata robo haingii.
Huwa inanishangaza Sana wanawake wa aina hii tatizo lao ni insecurity au wivu?
Hata kama ulipoenda Kula kweli umekuta chakula kinakasoro huwezi Kula ukaenda zako bila kukosoa ...?..au kukosoa ndo kunafanya wewe uonekane unajua sana?
Kinacho nishangaza wako Wengi wenye tabia hii.
Mnaenda sehemu badala ya Ku enjoy Tu chakula au mandhari mtu anakuwa busy Sana kutafuta makosa ama ya chakula au watoa huduma..... wanawake wenye hii tabia wanaboa sana.
Hebu nikumbushe maana ni kitambo sasa....
Nilikuwa nakosoa chakula au niliposhiba niliomba kufungiwa take away aka to go...😁😁😁?? (Kasinde is a food monger 🤭🤭).
Itabidi turudie ili nijikague kama nina hiyo tabia ama sina...😃.
Pole kwa hekaheka, nifikishie salamu zangu za heri tafadhali.