Wanawake wanasema Kimewashuka: Threads za Lissu aanzishe chama, wamefarakana, Lema sijui na Kigaila kawaje zimeisha jana baada ya Hotuba ya Mbowe

kuna siku watu watakuja kumjua mlamba asali kuwa ndio adui namba mbili wa nchi hii baada ya sisiemu.
 
kuna siku watu watakuja kumjua mlamba asali kuwa ndio adui namba mbili wa nchi hii baada ya sisiemu.
 
Mbowe amesema kweli, lazima kuwe na uhuru wa kuongea katika Chama, pia kukubaliana kutokubaliana katika hoja na kusonga mbele.
 
YOTE NI MEMA, LAKINI NGOJA TUPATE KATIBA MPYA AMBAYO RAIS HATAKUWA NA MAMLAKA YA KUCHOTA PESA KUWAPA WASANII, KUHONGA/KUNUNUA WAPINZANI, KUCHEZEA ANAVYOTAKA KAMA ANYOFANYA MAMA YETU SAMIA
Kama huwezi kujilinda mwenye na kudhibiti mitandao unayoitumia katiba haina maana mfano whatsap wakiamua kuzima ama hata hii jf ikizimwa tutarudi kwenye ujima, tuseme, wakizima internet tena huwa wanapenda kuzima kipindi cha uchaguzi mkuu
 
Ok atwist situation na kuharmonise mambo then ajiuzulu

Kujiuzulu ni Heshima, Nakumbuka 1985; Nyerere alipotangaza kujiuzulu wengi walihofu na kuogoba mabadiliko

Mbowe ajiuzulu huu ndo muda muafaka
Huo ni wivu tu dhidi yake,mbowe ndo kiongozi anayetakiwa haswaa,mi nashangaa mpinzani wako kukupa machaguo!,adui yako akikusifia jiangalie mara nyingi zaidi wapi umekosea?
 
Peter Msigwa kalala na viatu jana.
 
Unafanisha chadema ya slaa na huu upuuzi wa chadema ya leo?
Slaa hakuwahi kufanya kazi mazingira magumu kama Lissu aliyebaki kupambana Magufuli peke yake;
1. Slaa alikimbia Chadema baada ya kunyimwa kugombea urais...huu ni ubinafsi.

2. Lissu alipigwa risasi kuliko binadanu yeyote au hata mnyama lkn hakufikiria kuacha siasa kama mdudu Slaa bali ameimarika zaidi ...huu ni uzalendo wa hali ya juu.

3. Ccm haijawahi kumwogopa Slaa lakini Lissu tangu enzi za Mkapa...Lissu alipambana kuwatetea wanyinge zaidi ya 300 kule nyamongo walipokuwa wakionewa na aerikali kwa kigezo cha uwekezaji...Slaa ana rekodi gani?

4. Lissu amekuwa muwazi kiasi hata amethubutu kupinga baadhi ya mambo anayoyataka Mbowe yanayibeba ccm hasa mwafaka fake....Slaa angethubutu?
 
Paulo Makonda aliwahi kutuonya juu ya kuzitegemea mahakama zetu kupata haki, analijua hilo.
 
Tundu LISU sio bwana mdogo zitokabwe

ukigusa LISu umegusa idara ya Sheria ya chama yote(msingi wake ni TUndulisu na mbowe hakumlea LISu kama alivyomlea zito kabwe Toka ujanawake...

mbowe na LISu walikutana kwenye SHIDA yachama kwelikweli na LISu alikiokoa chama na wanachama mana mzee lupaso hakuwa na mchezo

Rejeeni ,hukumu ya kifungo Cha maisha kwa chacha wangwe na wale wezake 29 waliofungwa miaka 30

LISu akiwa Hana gari huko tarime mishe zake anajipigia akiwa na baiskeli akizunguka vijiji vya nyamongo

Mbowe sio bwege,na anakwambia komeni kabisa mdogowake LISu na yeye damudamu na kwa Sasa Yuko uzinduni wa kampeni Kanda ya kati na akimaliza ataenda Kanda ya Viktoria

kimsingi,wale chambia guzi...inauma ila ndohivyo
 
Nyuzi za kuitabiria mabaya CHADEMA na ramli chonganishi zilikuwa nyingi sana.. In fact kuna hela ndefu zilimwagwa kwa ajili ya hii project.. 😂
Chawa walicheza rhumba haswa. Wanaangalia hata mtu akipiga chafya wanakuja kupost. Wengine wanasema kwann hawakwenda eneo la tukio kuombea waathirika na badala yake waliwaombea wakiwa kwenye kikao.
Blablablaaqq
 
Chairman aache hadaa na uongo kwa wanachadema bana,

mnasongaje mbele Kwa pamoja hali ya kua mnatofautiana mtazamo na uelekeo ?🤣

huo si uongo wa mchana huo ndrugo zango? vita gani mtashinda na mnapigana risasi wenyewe kwa wenyewe ndrugo zango?🤣


Chairman acha uongo bana dah!

eti hakuna ufa wakati Makamu Mwenyekiti yuko against na chama katika mambo mengi sana ya Chadema kama chama. Lakini pia mnyukato wa Kigaila na Lema, lakini pia mnyukano wa Kigaila na Lisu sio ufa kweli ndrugo zango?🤣
 
Kwani Msaliti Lissu anasemaje? Na ni kwa nini Lissu na Lema hawakuhudhuria mkutano wa Mwenyekiti wa Maisha Mbowe?
 
Naam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…