Jamaa yangu mmoja tulikuwa tunapenda kutaniani, sura nzito tunaita Mipira ya kona au mipira iliyo kufa.(Mzaha na utani si mambo mazuri sana)
Jamaa namba mbili Yeye anakwambia hawezi fia kwa sura nzito/Ngumu ni heri akutwe na bwana Pepsi kwa Sura mvuto mithili ya Priyanka Chopra.
Nakwakweli Jamaa huwa anapata mabinti Wakali Wakali Wengine hata wakumtolea mbavuni yeye fresh tu ilimradi ni sura mvuto haichomi moyo.
Niliwahi kumtongoza bibie mwenye sura nzito penzi likachipua likamea ,likaota mizizi huku akinikaribisha katika kitanda chake alichotia shuka la mistari la kimsiri,Manemane,udi na mdalasini na tukaburudishana nafsi zetu kwa mahaba mazito.
Hakika Wanafiki tuliwaacha Midomo wazi kama wameshikwa ugoni kwa penzi letu la dhati.
Tulipoteana baada ya mizunguko na mihangaiko ya dunia,Maisha ni Safari na Sisi tuwasafiri.
Ubaguzi kwangu Mwiko Ubaguzi wa rangi Ndio kwanza napeleka kwenye ufuaji wa Nguo.
Utu Kwanza.Mengineyo yafuatie.