Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja

Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja

Wanabodi,

Tangu baada ya Uingereza kupiga kura kujitoa kwenye EU, wanabodi wetu humu ambao ni Wanzanzibari, wanashadadia sana uamuzi huo, na kushinikiza wananchi wa Zanzibar nao, wapewe fursa ya kupiga kura ya maoni kwa kuulizwa kama bado wanataka kuendelea kusalia kuwa ndani ya muungano wetu, au wanataka kujitoa!. Wanaotaka kujitoa wakishinda, utaratibu wa jinsi ya kuuvunja muungano huu adhimu ziandaliwe, tuuvunje rasmi huu muungano wetu, na tuachane kwa amani, kuliko kuendelea huku baadhi ya wenzetu ni kila siku malalamiko, manung'uniko, na ghubu lisiloisha la kutwa kucha!.

Swali kwa wenzetu wa Zanzibari, sheria ya kura ya maoni si mnayo?!, sasa nini kinachowazuia kuitumia sheria hiyo kupiga hiyo kura ya maoni kuhusu muungano?!.

Kwa msio jua kuwa wenzetu Zanzibar, waliishaipitisha sheria hiyo ya kura ya maoni toka mwaka 2010, na ndio iliyotumika kuunda SUK!.

Kura ya Maoni Zanzibar ni Sheria Nambari 6 ya 2010 kuhusu uendeshaji wa kura ya maoni ilipitishwa na Baraza la Wawakilishi mnamo mwezi wa Machi 2010 na kutiwa saini na Mheshimiwa Rais Karume mnamo mwezi wa Aprili 2010.

Tayari sheria hiyo iliishatumiwa na wananchi wa Zanzibar walipopiga kura ya maoni siku ya
Jumamosi tarehe 31 Julai 2010. Kura hiyo ilikuwa na lengo la kutafuta ridhaa ya wananchi wa visiwa hivyo vya Unguja na Pemba, kuamua iwapo wanalikubali wazo la kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010.

Auamuzi wa kupigwa kwa kura hiyo ya maoni ulianzia katika kikao cha BLW ambacho kilipitisha Azimio la Baraza kufanywa kura ya maoni (referendum) iliyowashirikisha wananchi wa Zanzibar moja kwa moja katika kupata ridhaa ya wananchi kuanzisha mfumo na muundo wa Serikali ya
Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

Kura hiyo iliendeshwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na kwa mujibu wa Kifungu cha 11(1) cha
Sheria ya Kura ya Maoni Nambari 6 ya 2010, ushindi wa Kura ya Maoni utaamuliwa kwa
wingi wa kura. Hivyo, kwa mujibu wa matokeo hayo, Wazanzibari waliopiga kura
ya NDIO kuunga mkono kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SUK ikaendwa!.

Hayo yote yalifanyika Zanzibar bila kuishirikisha JMT, hadi ninavyozungumza hapa, japo SUK inatambuliwa rasmi na serikali ya JMT, lakini hadi leo, Katiba ya JMT ya 1977, bado haitambui SUK, hakuna kipengele chochote kinachoitambua SUK, wala katiba yetu haiwatambui wale makamo wawili wa rais wa Zanzibar, bali bado inamtambua Waziri Kiongozi ambaye doesn't exist anymore!.

Mabadiliko hayo ya Katiba ya Zanzibar ya 2010, yalikiuka katiba ya JMT na kuuvunja rasmi muungano kikatiba kwa katiba hiyo kuitangaza Zanzibar kuwa ni nchi, wakati katiba ya JMT inatamka nchi ni moja tuu JMT, na kuitambua Zanzibar kama sehemu ya JMT!.

Katiba hiyo ya Zanzibar ilivunja mamlaka yote ya Bunge la JMT, na mamlaka yote ya rais wa JMT, kwa kumtangaza rais wa Zanzibar ndio mkuu wa nchi ya Zanzibar na Amiri Jeshi Mkuu wa Vokosi vya SMZ!, na kuamua sheria yoyote itakayotungwa na Bunge la JMT, haitatumika Zanzibar mpaka BLW liridhie!, hii ni dharau kiasi gani kwa rais wa JMT na Bunge la JMT?!.

Kama yote haya yaliweza kufanyika bila kuishirikisha JMT, sasa ni nini kinachowashinda Wazanzibari kujiitishia kura yake ya maoni, kuamua kama isalie katika muungano au ijitoe?!.

Sasa tumechoshwa na hizi kelele, hivyo natoa wito kwa wenzetu Wazanzibari, waamue moja, ama waache kelele watulie, ama wafikie maamuzi waamue!.

Nawatakia Jumapili Njema.

Pasco
NB. Pasco wa JF ni muumini wa falsafa ya Nyerere kuhusu muungano, Nchi Moja, Serikali Moja chini ya Rais Mmoja wa JMT!, ila pia ni mtu mwenye maslahi fulani binafsi na Zanzibar!.

Rejea.
Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, Then "Twende kwenye Serikali Moja!.

Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?
Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?! .
Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano?
Je, wajua kuwa kuna uwezekano Tanzania sio nchi halali Kisheria ...
Zanzibar: Japo SMZ ya SUK sio de jure tena bali ni de facto ...
CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima .
Je, kunahitajika affirmative action ili Mzanzibari aweze tena
Muundo wa Serikali Tatu ni Illegal, Unjustifiable, na Ni Kuvunja ...
Kumbe Sultan Jamshid Alifurahia Kuuawa kwa Karume!. Alitaraji ..
Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein ...
Zanzibar Issue: Kwanini watu wanapiga kelele tu bila kuchukua ...
Balozi Karume: 'CCM pekee iwe inasimamisha mgombea urais Zanzibar
Kuna haja ya kuhofia kurudiwa Uchaguzi Zanzibar? |
Mbowe Alipua Bomu la Siri ya Ushindi Wa CCM Zanzibar
Imethibitishwa pasi na shaka kuwa CUF Ilishinda, Zanzibar ...
Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano ...
Inawezekana Vipi Zanzibar Hakuna Div I, Div II, wala Div III , Wao ..
Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na .

Huu ni uchonganishi, samahani uchochezi.
 
Well said ndugu Pasco. Lakini nani ataitisha hiyo kura ya maoni? Maana mtu mmoja aliwahi kusema "usiitishe kura ya maoni kama una uhakika wa kushinda."

Nionavyo mimi ni kwamba kwa sasa mtu anayetakiwa kuanzishwa na kusimamia jambo hili hana uhakika wa kushinda. Kwa hali ya Zanzibar ilivyo sasa, kuanzisha kura ya maoni kuhusu muungano ni sawa na kufukua makaburi. Acha tu "makaburi yapumzike".
 
Tukimaliza Zanzibar nataka kura ya makabila.
Ni lini makabila yetu yalikubaliana uwepo wa Tanganyika?
Mkataba wa makabila kuunda Tanganyika uko wapi?
 
Mwenye maamlaka ya kuitisha kura ya maoni ni serikali . Serikali ya CCM kwame haiwezi kuitisha kura ya maoni kuhusu Muungano. Ni hapo tu gharama za Muungano zitakuwa too costly ndipo Tanganyika itaachia Zanzibar. Too costly maana yake umwagikaji wa damu ya wanzibari hadi mataifa makuu kuinglia kati. East Timor ni funzo kwa wanzibari.
 
Wananchi wa Zanzibar hawana haki ya kujiuliza kuwa wanataka muungano au hawataki kwa kuwa hata huu Muungano ulipoundwa hawakuulizwa kama wanataka Muungano au hawataki.
Anayebisha atafute muda asome historia.

Waingereza waliamua kuingia Euro na sasa wanaamua kutoka. Hii ni tofauti ya Zanzibar na Muungano wa Tanzania
 
Wananchi wa Zanzibar hawana haki ya kujiuliza kuwa wanataka muungano au hawataki kwa kuwa hata huu Muungano ulipoundwa hawakuulizwa kama wanataka Muungano au hawataki.
Anayebisha atafute muda asome historia.

Waingereza waliamua kuingia Euro na sasa wanaamua kutoka. Hii ni tofauti ya Zanzibar na Muungano wa Tanzania
Twisted logic. Every man has God given right to determine his destiny. CCM ipende isipende.
 
Dahhhh Pasco I hope kuna mtu kutoka serikalini
Atasoma na kufikisha huu ujumbe wako mahali
Hoja nzito.
 
Mko poa tu kwa vile nyie ndio watawala. Uongo muungano haukuumizini msingekuwa wakali kwa wazanzibari wanaoukataa Muungano. Zanzibar ina Katiba yake na hakuna katiba supreme dhidi ya nyengine. Neno zuri la kusema Katiba zinakinzana
Huo "utawala" wa Tanganyika juu ya Zanzibar haumsadii chochote Mtanganyika na wala hauwezi kutuhadaa tusione mzigo tunaoubeba.

Watanganyika tusikubali ka Zanzibar haka katukwamishe mambo yetu, kametunyima Katiba Mpya haka, tumekwama kupitisha masuala yetu muhimu ya kitaifa kwa sababu ya "muundo wa Muungano." Mbona tuliweza kujivua brainwashing nyingine za Nyerere kama Azimio la Arusha na Chama kimoja, kwa nini hili li ndumba la Muungano tunashindwa na mwenyewe ashakufa? I don't understand this baloney for the life of me.

Nyerere alisema nchi kubwa zinaungana sisi tunataka kutengana, well, Nyerere has been proven wrong in Europe, Waingereza wamesema miungano sio yote ina manufaa, miungano ya kijinga jinga ya wadogo kuungana na kuwanyonya wakubwa haina faida.

Barack Obama alivyokwenda UK kuwaasa wabaki EU, Boris Johnson akamwambia, wewe Obama, there's no way in hell America ingekubali kubanwa kwenye ki muungano kama hiki cha kuamuliwa mambo na nchi nyingine, noooo way! Which is true, US inashadadia Mahakama ya the Hague lakini yenyewe haimo!

Tanganyika, sio Zanzibar, sisi Tanganyika hatutaki Muungano, I don't give a monkey's what Zanzibar thinks, na hatuwasubiri Wazanzibar waamue au watuamulie, sisi Tanganyika tumechoka kunyonywa, tunataka kujitoa!
 
Twisted logic. Every man has God given right to determine his destiny. CCM ipende isipende.

It's a wrapped logic, which is in fact leaving the Zanzibaris and Tanganyikans ( if they exist) in the middle of nowhere to decide their fate.
God given right is universally accepted and doctrinally true however millions are denied those rights by those who rule over them.
 
Tanganyika, sio Zanzibar, sisi Tanganyika, I don't give a monkey's what Zanzibar thinks na hatuwasubiri Wazanzibar waamue au watuamulie, sisi Tanganyika tumechoka kunyonywa, tunataka kujitoa!
Huo ni Ubunuwasi wa kutufanya wazanzibari tuzidi kuendelea kukuroma wakati Tanganyika inazidi kula uroda! Janja hiyo imepitwa na wakati. Zanzibar tunataka nchi yetu
 
Wananchi wa Zanzibar hawana haki ya kujiuliza kuwa wanataka muungano au hawataki kwa kuwa hata huu Muungano ulipoundwa hawakuulizwa kama wanataka Muungano au hawataki.
Anayebisha atafute muda asome historia.

Waingereza waliamua kuingia Euro na sasa wanaamua kutoka. Hii ni tofauti ya Zanzibar na Muungano wa Tanzania
Ni kweli, lakini kama wananchi hawakuhusika hasa upande wa Zanzibar ambao ulikuwa hauna kiongozi aliechaguliwa na wananchi wenyewe kinyume na bara inatafsirika kuwa Zanzibar ni koloni la bara. HIvyo kudai uhuru kuutoka kwa mkoloni huyu mweusi si kosa na ni haki.
 
Mwenye maamlaka ya kuitisha kura ya maoni ni serikali . Serikali ya CCM kwame haiwezi kuitisha kura ya maoni kuhusu Muungano. Ni hapo tu gharama za Muungano zitakuwa too costly ndipo Tanganyika itaachia Zanzibar. Too costly maana yake umwagikaji wa damu ya wanzibari hadi mataifa makuu kuinglia kati. East Timor ni funzo kwa wanzibari.
Mungu apishe mbali
 
Ni kweli, lakini kama wananchi hawakuhusika hasa upande wa Zanzibar ambao ulikuwa hauna kiongozi aliechaguliwa na wananchi wenyewe kinyume na bara inatafsirika kuwa Zanzibar ni koloni la bara. HIvyo kudai uhuru kuutoka kwa mkoloni huyu mweusi si kosa na ni haki.

Upo sahihi Kabisa.
Ukipita kwenye vikao vya raia huko Unguja( JAWS CORNER IN PARTICULAR) watu wanaelewa vizuri Sana juu ya Muumgano huu lakini hawana namna ya kuitisha hicho kinachoitwa "kura ya maoni" ili kuamua hatma Yao.
 
Tunaongea sana ila katika duania hakuna taifa linalojitambua linaruhusu kataifa kadogo kujiuendesha karibu na mipaka yake. Ndo yaliyopo Macao, Taiwan, Hong Kong, Gilblatar, hata visiwa vingi vidogo vinavyo zunguka Marekani, UK, Uholanzi, Ufaransa, Uturuki, Urusi, n.k.

Kwa maana moja hata nyingine, huwa watawala hawako radhi kuachia maeneo kama haya. Sisi tunalalamika ila itabaki hivyo.
 
Tunaongea sana ila katika duania hakuna taifa linalojitambua linaruhusu kataifa kadogo kujiuendesha karibu na mipaka yake. Ndo yaliyopo Macao, Taiwan, Hong Kong, Gilblatar, hata visiwa vingi vidogo vinavyo zunguka Marekani, UK, Uholanzi, Ufaransa, Uturuki, Urusi, n.k.

Kwa maana moja hata nyingine, huwa watawala hawako radhi kuachia maeneo kama haya. Sisi tunalalamika ila itabaki hivyo.
 
Back
Top Bottom