Wapalestina ni wavamizi kwa mujibu wa Quran

Wapalestina ni wavamizi kwa mujibu wa Quran

Nilichogundua waislamu wengi ni maamuma ,hamjui jinsi Allah wenu anavyowatambua Wana wa Israel,

Allah wenu kwenye Quran hawajui WAPALESTINA

Hii mada hamuiwezi nileteeni Mufti mkuu
 
Si unaona walikuta watu kwenye hizo aya ulizotoa,hao watu ni akina nani?..kama walivunja masharti ya kupewa hiyo nchi,kivipi bado unang'ang'ana ahadi bado ipo?..unadandia tu vitu toka mtandaoni bila tafakuri
Haya Leta Aya Allah akiwanyang'anya Ardhi waisraeli na kuwapa WAPALESTINA
 
Kwani huo waraka ndio Biblia? Yeye katoa maandiko ndani ya quaran, na wewe lete maandiko ndani ya Biblia yake sio mambo ya waraka wa Papa ambao ni kama gazeti tu.
Papa ni muakilishi wa Yesu hapa duniani. Akisema papa amesema Yesu. Akitenda papa ametenda Yesu.
Angalia vizuri kibaraghashia chake kile kimeandikwa nini.
 
SIO KWELI

Madai haya yanaweza kukanushwa kwa kutumia msingi wa Qur'an na historia ya Uyahudi na Uislamu:

Wana wa Israeli si race bali ni kizazi cha Yakobo (Isra’il).

Katika Qur'an, Wana wa Israeli wanatajwa kama kizazi cha Nabii Yakobo (Isra’il), si kama race ya kibayolojia. Aya kama

"Enyi Wana wa Israeli! Kumbukeni neema yangu niliyokutunukuni, na ya kwamba niliwafadhilisha kuliko walimwengu" (Qur'an 2:47)

zinaonyesha kuwa "Wana wa Israeli" ni kundi la watu lililojulikana kwa historia yao na si race ya asili moja.

Musa alikuwa Myahudi kwa maana ya kabila lake.

Kwa hivyo, madai kwamba Wana wa Israeli ni race badala ya kizazi cha Yakobo na kwamba Uyahudi ni dini pekee yanakinzana na Qur'an. Wana wa Israeli ni kundi la watu waliotajwa kwa nasaba yao, na Uyahudi ni dini yao, lakini ujumbe wa Musa ulikuwa wa kujisalimisha kwa Allah, ambao ndio maana
ya Uislamu.
Ukitumia Quran hupaswi kutumia historia inayohaririwa kila siku,hasa toka kwa wanaojiita wayahudi au biblia ambayo kila mfalme aliihariri,makabila 12 ya Wana wa israel unayajua,siyo race?..hata kama makabila hayo hayapo,Wana wa yakobo bado siyo race?
Quran 61:5,musa ni mtume wa Allah,mtume wa Allah ni dini gani?
 

Attachments

  • Screenshot_2025-02-07-22-32-40-798.jpg
    Screenshot_2025-02-07-22-32-40-798.jpg
    247.1 KB · Views: 2
Unajua kusoma ?

Surat Al-Baqarah (2:122)

يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذكرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ وَأَنِّي فَضَّلْتُكُمْ عَلَى الْعَالَمِينَ
"Enyi Wana wa Israel! Kumbukeni neema yangu niliowapa ninyi, na kuwa mimi niliwafadhilisha juu ya walimwengu."

Aya hii inathibitisha kwamba Wana wa Israel walifadhiliwa na Mwenyezi Mungu, na inasisitiza kuwa walikuwa na cheo cha kipekee na nafasi ya mbaraka. Kwa tafsiri moja, hii inaweza kueleza kuwa walikuwa na haki ya ardhi hiyo.

Allah wako anawatambua wenye Ardhi ni Israel

Leta ww Aya kuwa anawatambua WAPALESTINA

Acha porojo
Wapi aya hapo katika Quran imeongelea kuwa ardhi ya Wapalestina ni ardhi ya Waisraeli ?
Acha kukurupuka
 
Hiyo Quran imejichanganya kwenye mambo mengi sana, yaani huyo muarabu angekaa aisome kwanza kabla kuja kuachia kipindi anabuni uislamu wake
Nimekua nafuatilia mwalimu Ndacha anavowaumbua waislamu hadi huruma, kama Kuna mwenye akili alipaswa auhame, sema Huwa wamekamatwa na majini hata uwaambie nini hawatakuelewa
Wauhame halafu waende wapi ambako hakuna mkanganyiko? Utatu mtakatifu nao ni utata mtupu!
 
Haya Leta Aya Allah akiwanyang'anya Ardhi waisraeli na kuwapa WAPALESTINA
Wewe Mungu wako akikwambia ingia nchi ya wazaram akupe iwe yako kwa masharti maalum,ukishindwa kufikia hivyo vigezo na masharti ya kuchukua nchi ya wazaram,bado utahitaji andiko lisemalo nchi ya wazaram ni nchi wazaram!?
 
Hiyo Quran imejichanganya kwenye mambo mengi sana, yaani huyo muarabu angekaa aisome kwanza kabla kuja kuachia kipindi anabuni uislamu wake
Nimekua nafuatilia mwalimu Ndacha anavowaumbua waislamu hadi huruma, kama Kuna mwenye akili alipaswa auhame, sema Huwa wamekamatwa na majini hata uwaambie nini hawatakuelewa
Fuatilia jinsi bible ilivyojichanganya kwenye kila kitu
 
Kumbukumbu la Torati 16:20

"Yaliyo haki kabisa ndiyo utakayoyafuata, ili upate kuishi na kuirithi nchi upewayo na Bwana, Mungu wako."


Zaburi 37:29
"Waadilifu wataimiliki nchi, na wataishi humo milele."


Quran 21:105
Mungu anasema kuwa

"Na hakika tulikwisha andika katika Zaburi baada ya Kumbukumbu, ya kwamba nchi watairithi waja wangu walio wema."

Ardhi ya Palestine itarudi katika mikono ya Waislam
 
Si unaona walikuta watu kwenye hizo aya ulizotoa,hao watu ni akina nani?..kama walivunja masharti ya kupewa hiyo nchi,kivipi bado unang'ang'ana ahadi bado ipo?..unadandia tu vitu toka mtandaoni bila tafakuri
Anayekudanganya walinyang'anywa ,muulize akupe Aya walipewa kina nan
 
Unajua mambo ya Divide and Rule ?

Papa hawezi kupinga uislamu kwa taarifa yako Papa Hadi misikitini anaingia Tena na viatu Huwa havui

Papa na chuo kikubwa cha waislamu cha Al Azhar University misri walisaini Hadi mkataba wa umoja na kule Dubai Kuna Jengo la kuunganisha dini ya Uislamu na Ukristo fake wa Papa

Uislamu ni dini ya wakatoliki ,nyie wafia dini na wala ubwabwa na biriani mkishashiba hamuwezi kuelewa haya

Kautafute Mkataba wa Document on Human Fraternity for World Peace and Living Together (Hati ya Udugu wa Kibinadamu kwa Amani ya Dunia na Maisha ya Pamoja), ambayo ilisainiwa tarehe 4 Februari 2019 huko Abu Dhabi, kati ya Papa Francis na Grand Imam wa Al-Azhar, Sheikh Ahmed el-Tayeb.

Hati hii inakusudia kuimarisha maelewano kati ya Waislamu na Wakatoliki, kuzuia migogoro ya kidini, na kukuza mshikamano wa kijamii duniani. Ni hatua kubwa katika juhudi za mazungumzo ya kidini kati ya Uislamu na Ukatoliki
Mbona unahangaika wewe mlokole,mikataba ya 2019 inahusiana vipi na utume wa mtu wa 570?..palikua na uwawaru hapa tz 1990s,pana umoja wa amani wa dini na madhehebu yote tz,shida nini?
 
Wewe Mungu wako akikwambia ingia nchi ya wazaram akupe iwe yako kwa masharti maalum,ukishindwa kufikia hivyo vigezo na masharti ya kuchukua nchi ya wazaram,bado utahitaji andiko lisemalo nchi ya wazaram ni nchi wazaram!?
Leta Aya kuwa Ardhi ilikuwa ya WAPALESTINA

Mbona huna Aya halafu hakuna Aya walinyang'anywa Ardhi ni mnaungaunga tu
 
Mbona unahangaika wewe mlokole,mikataba ya 2019 inahusiana vipi na utume wa mtu wa 570?..palikua na uwawaru hapa tz 1990s,pana umoja wa amani wa dini na madhehebu yote tz,shida nini?
Uislamu ni plan B ya Ukatoliki

Nani kakuambia mm mlokole ? Mm sio mfia dini kama nyie
 
Qur’an Haijasema Waisraeli Waliondolewa Milele

Katika Surat Al-Isra (17:4-7), Qur’an inasema kuwa Wana wa Israel walifanya ufisadi na wakashindwa:

بَعَثْنَا عَلَيْكُمْ عِبَادًا لَّنَا أُولِي بَأْسٍ شَدِيدٍ

"Tuliwaelekezea waja wetu wenye nguvu kali..."

Aya hii haijasema kuwa walinyang’anywa ardhi milele, bali walipata adhabu ya muda kwa sababu ya uovu wao.
endelea na aya zinazofuata zinazoelezea agano walilolifanya na Mungu na ufisadi walioufanya mpaka kikawakuta kilichowakuta.

Quran ipo wazi kabisa huna pa kuichafua
 
Kwahiyo Alaumiwe Allah si ndio ?

Maana ndiye anayesema hayo maneno
1738957493850.png

Basi Firauni akataka kuwafukuza katika nchi. Kwa hivyo tukamzamisha yeye na walio kuwa pamoja naye wote.
Kwa mujibu wa Quran,ni nchi gani hapo ambayo inazungumziwa ?
 
Unajua kusoma ?

Surat Al-Baqarah (2:122)

يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذكرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ وَأَنِّي فَضَّلْتُكُمْ عَلَى الْعَالَمِينَ
"Enyi Wana wa Israel! Kumbukeni neema yangu niliowapa ninyi, na kuwa mimi niliwafadhilisha juu ya walimwengu."

Aya hii inathibitisha kwamba Wana wa Israel walifadhiliwa na Mwenyezi Mungu, na inasisitiza kuwa walikuwa na cheo cha kipekee na nafasi ya mbaraka. Kwa tafsiri moja, hii inaweza kueleza kuwa walikuwa na haki ya ardhi hiyo.
Je baada ya kufadhilishwa zaidi ya watu wengine walifanya mambo gani pindi walipoletewa mitume?
 
Kwa mujibu wa Quran Tukufu WALIOPEWA hiyo Ardhi ni Wana wa Israel,hakuna mahali Quran inawatambua WAPALESTINA,kama Kuna Aya zipo nitaomba nisaidiwe maana elimu ni Bahari

Hebu tuangalie Quran inasemaje kuhusu Ardhi kuwa ni ya Wana wa Israeli .

Uislamu Huwa unakwama kwenye historia tu ambayo mara kadhaa imekuwa ikiwaumbua

1. Surat Al-A'raf (7:137)
وَأَوْرَثْنَا الْقَوْمَ الَّذِينَ كَانُوا يُسْتَضْعَفُونَ مَشَارِقَ الْأَرْضِ وَمَغَارِبَهَا الَّتِي بَارَكْنَا فِيهَا ۖ وَتَمَّتْ كَلِمَةُ رَبِّكَ الْحُسْنَىٰ عَلَىٰ بَنِي إِسْرَائِيلَ بِمَا صَبَرُوا ۖ وَدَمَّرْنَا مَا كَانَ يَصْنَعُ فِرْعَوْنُ وَقَوْمُهُ وَمَا كَانُوا يَعْرِشُونَ


"Na tukawarithisha watu waliokuwa wakidharauliwa, mashariki ya ardhi na magharibi yake, ambayo tumebariki ndani yake. Na neno zuri la Mola wako Mlezi likatimia juu ya Wana wa Israel, kwa vile walivyosubiri. Na tukaharibu kabisa waliokuwa wakiyatenda Firauni na watu wake na walizokuwa wakizijenga."

2. Surat Al-Isra (17:104)
وَقُلْنَا مِنْ بَعْدِهِ لِبَنِي إِسْرَائِيلَ اسْكُنُوا الْأَرْضَ فَإِذَا جَاءَ وَعْدُ الْآخِرَةِ جِئْنَا بِكُمْ لَفِيفًا

"Na baada yake tukawaambia Wana wa Israel: Kaeni katika ardhi. Na utakapokuja ahadi ya Akhera tutakuleteni nyote pamoja (kutoka sehemu mbalimbali)."

3. Surat Al-Baqara (2:47)
يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذْكُرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ وَأَنِّي فَضَّلْتُكُمْ عَلَى الْعَالَمِينَ

"Enyi Wana wa Israel! Kumbukeni neema yangu niliyokuneemesheni, na kwamba niliwafadhilisha juu ya walimwengu."

4. Surat Al-Baqara (2:122)

يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذْكُرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ وَأَنِّي فَضَّلْتُكُمْ عَلَى الْعَالَمِينَ

"Enyi Wana wa Israel! Kumbukeni neema yangu niliyokuneemesheni, na kwamba niliwafadhilisha juu ya walimwengu."

5. Surat Al-Ma'idah (5:24-26)

Aya hizi zinaeleza jinsi Wana wa Israel walivyokataa kuingia katika ardhi hiyo kwa hofu ya watu waliokuwa wakiishi humo, na adhabu yao ya kupotea kwa miaka 40 jangwani:

قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّ فِيهَا قَوْمًا جَبَّارِينَ وَإِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا حَتَّىٰ يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِن يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِنَّا دَاخِلُونَ ۝ قَالَ رَجُلَانِ مِنَ الَّذِينَ يَخَافُونَ أَنْعَمَ اللَّهُ عَلَيْهِمَا ادْخُلُوا عَلَيْهِمُ الْبَابَ فَإِذَا دَخَلْتُمُوهُ فَإِنَّكُمْ غَالِبُونَ ۖ وَعَلَى اللَّهِ فَتَوَكَّلُوا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ ۝ قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا أَبَدًا مَّا دَامُوا فِيهَا فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ ۝ قَالَ فَإِنَّهَا مُحَرَّمَةٌ عَلَيْهِمْ أَرْبَعِينَ سَنَةً يَتِيهُونَ فِي الْأَرْضِ فَلَا تَأْسَ عَلَى الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ

("Wakasema: Ewe Musa! Hakika humo mna watu wenye nguvu na sisi hatutaingia humo mpaka wao watoke humo. Wakishatoka, basi tutaingia. Watu wawili miongoni mwao waliomuogopa Mwenyezi Mungu na ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha walisema: Waingilieni kwa kupitia mlango, mtakapoingia humo mtakuwa washindi. Na kwa Mwenyezi Mungu mtegemee ikiwa nyinyi ni waumini. Wakasema: Ewe Musa! Hatutaingia humo kamwe maadamu wao wamo. Basi nenda wewe na Mola wako mpigane, sisi tunakaa hapa. Musa akasema: Hakika ardhi hiyo imeharamishwa kwao kwa muda wa miaka arubaini, watatangatanga katika ardhi. Basi usiwaonee huruma hao watu wapotovu.")

Aya hizi zinaeleza historia ya Wana wa Israel na ardhi waliyopewa ,hivo WAPALESTINA ni wavamizi
Fahamu kwamba Israel asili yake haikuwa Nchi na haijawahi kuwa Nchi mpaka mwaka 1948 baada ya vita ya pili ya dunia wazungu wa Britain wakalitangaza hilo Taifa la Israel.

Israeli si taifa. Ni jina la Mtume. Nabii huyo ambaye baba yake aliitwa Yakobo, Wana hao wa Israeli walijulikana kuwa makabila 12 ya Israeli. Watu hawa wanaunda wale tunaowaita "Mayahudi" siku hizi, lakini Kiislamu wanaitwa Wana wa Israili, hivyo ndivyo Allah S.W.T anawaita. Neno Israeli halijawahipo kuhusishwa na serikali ni jambo jipya.

Narudia tena Israel ni Jina maalum la Nabii Yakub (AS) alilopewa na Allah (SWT). Haina uhusiano wowote na Nchi ya Kishetani ambayo imelitumia vibaya na kuliteka nyara jina la Nabii wa Mungu.

Umetumia muda mwingi kwenda kwenye Quran tukufu na kuleta hapa baadhi ya aya ingawa ziko na nyengine nyingi umeziacha, lakini katika aya hizo zote ulizoleta na ulizoziacha hakuna mahali zinatafsiri kwamba Israel ni Nchi (State) never (بَنِي إِسْرَائِيلَ) hili neno bani Israel maana yake ni watu wa ukoo Prophet Yakub na si (Nchi/State)

Hao kina Netanyahu na wenzake waliletwa hapo kwenye ardhi ya Palestina kama Diaspora baada ya hiyo vita ya pili ya dunia na kuanza kukatiwa vipande vya ardhi kila siku wanasogea mbele mpaka sasa zamai hizi imefikia halii hii uionayo. na wameletwa hapo kimkakati ili Nchi za ulaya na marekani waweze kupata mahali pa kudhibiti dola za kiarabu (Mashariki ya kati) kutokana na raslimali walizonazo walizobarikiwa lakini pia kujaribu kudhibiti mataifa ya kiislam yenye nguvu duniani na kupenyeza mila zao za kishenzi ili kuwavuruga waislamu.

Nafkiri baada ya kuapta muda kusoma maelezo haya hutakuja tena hapa na kasumba zako kama ulivyolishwa.
 
Back
Top Bottom