Wapalestina sasa kuuliwa kwa kunyimwa maji na msongamano wa makazi

Wapalestina sasa kuuliwa kwa kunyimwa maji na msongamano wa makazi

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Kucheleweshwa kwa zoezi la vikosi vya Israel kuingia Gaza kuna watu wanaamini kuwa ni woga wa Israel kupata kipigo kutoka kwa vikosi vya wanamgambo wa Hamas na wenzao huko Gaza kama ilivyokuwa huko nyuma. Hapana safari hii ni zaidi ya uwoga.

Nia safari hii ni kuwamaliza wapalestina kwa wingi kuliko safari nyingine yoyote ile kwani wakiuliwa Hamas wachache wanazaliwa wengine wanaoendeleza vita. Mbinu hiyo sasa imeweza kufanyika mbele ya walimwengu wote. Marekani na Israel wanajua wanachofanya ndio maana badala ya kutoa amri ya kusitisha vita kila siku kuna ahadi za kwenda kesho yake badala ya leo.

Jumuiya ya waarabu wanaona kinachofanyika lakini nguvu yao kubwa ni kukataa tu kukutana na Rais wa Marekani aliyepanga kukutana nao badala ya kutoa tamko kali la kufunguliwa mpaka na kupeleka mahitaji na kuiamrisha Israel ifungue maji kwa wote bila masharti.Na hiyo nayo imekuja baada kuuliwa kwa wagonjwa na madaktari kwenye shambulio la anga kwenye hospitali hapo jana ambapo watu 500 wameuliwa kwa sekunde chache tu.

Urusi ilipojitoa kwenye mkataba ya usafirishaji nafaka kati yake na Ukraine umoja wa mataifa ulitoa malalamikio na shutuma kali kwa Urusi na kutamka kuwa ni ajabu kuwa Urusi inatumia chakula kama silaha.Hiyo ilikuwa ni kwa vile mahjitaji ya ngano na bidhaa nyengine zinazoambatana nazo ni kwa ajili yao wao.

Kwa upande wa Palestina wanajua kuwa maji kwanza ni muhimu kuliko hata chakula na bado hakuna tamko la kuiambia Israel kuwa iache kutumia maji kama silaha.

Kinachoendelea ni kama kutokea kichaa mwenye nguvu akamkaba koo mnyonge fulani katikati ya barabara penye watu wengi kama pale mtaa wa sikukuu Kariakoo na kila mmoja akapita zake bila kuwaamua hata kabla ya kuuliza ugomvi wao.Akifa mnyonge yule bali hukumu na ghadhabu za Mwenyezi Mungu zitawaenea wote walioshuhudia na wakapuuza.

Hatua wanazochukua waarabu na waislamu kwa ujumla ni hafifu sana kulingana na uzito wa ukatili wanaofanyiwa wapalestina.Wakiona wanakula na kunywa na kupata usingizi mnono wanawasahau wenzao.inashangaza kumekuwa na uungwaji mkono wa wapalestina nchi za Ulaya ,Marekani na kwengineko kuliko nchi za kiarabu ambazo ni jirani zaidi na Palestina kunakotokea unyama huo.

Watu wa Ulaya na kwengineko wanajua hakuna maisha ya furaha kwa watu 90 kuishi kwenye nyumba moja isiyo na huduma kamili za kibinadamu na kila muda wakiangalia angani kusikiliza kombora ambalo linaweza likwawaangamiza wote kwa pamoja.

Waarabu wajitayarishe na mabalaa yatakayowakuta wao wenyewe kwa uzembe wao.Hii dunia ni kitu kidogo sana kwa Mwenyezi Mungu.
 
Hao sio wajinga waliwaona jinsi walivyo wachokozi huku nguvu hawana..........na kuhusu lile la kuua watu 500 ni hamas wenyewe wameua watu wao kwa ujinga walifyatua kombora likafeli sasa unataka watu wasife??
Wewe ndio wenye roho ngumu kama hao wayahudi.Kombora la kuuwa watu mia tano ni wazo la kuona wengine ni wajinga sana kuelewa.
Kombora hilo linaruka namna gani likauwa watu kutoka chini ya Ardhi.Lazima litoke angani na kutoka ndege zenye kubeba mabomu ya nguvu kubwa.Vfaa hivyo Hamas hawana.na hata kama wanavyo hawawezi kufanya unyama huo kwa wagonjwa na madaktari.
 
Wewe ndio wenye roho ngumu kama hao wayahudi.Kombora la kuuwa watu mia tano ni wazo la kuona wengine ni wajinga sana kuelewa.
Kombora hilo linaruka namna gani likauwa watu kutoka chini ya Ardhi.Lazima litoke angani na kutoka ndege zenye kubeba mabomu ya nguvu kubwa.Vfaa hivyo Hamas hawana.na hata kama wanavyo hawawezi kufanya unyama huo kwa wagonjwa na madaktari.
Unapambana eehh..........wewe mmakonde upalestina umeutolea wapi?? ......kingine kama hamas waliua watu 1300 na kujeruhi zaidi ya 600 unataka Israeli iwachekee kisa walisema alwa akbar?..........waendelee kusema tu alwa akbar uku na wenyewe wakiwahishwa kwenda kupata bikra 72
 
Wewe ndio wenye roho ngumu kama hao wayahudi.Kombora la kuuwa watu mia tano ni wazo la kuona wengine ni wajinga sana kuelewa.
Kombora hilo linaruka namna gani likauwa watu kutoka chini ya Ardhi.Lazima litoke angani na kutoka ndege zenye kubeba mabomu ya nguvu kubwa.Vfaa hivyo Hamas hawana.na hata kama wanavyo hawawezi kufanya unyama huo kwa wagonjwa na madaktari.
Huo ndio ukweli missile imefeli imekung'uta hospital Israel wapo tayari ku prove hilo na hapo ndo mtajua mnawatetea vichaa.
 
Unapambana eehh..........wewe mmakonde upalestina umeutolea wapi?? ......kingine kama hamas waliua watu 1300 na kujeruhi zaidi ya 600 unataka Israeli iwachekee kisa walisema alwa akbar?..........waendelee kusema tu alwa akbar uku na wenyewe wakiwahishwa kwenda kupata bikra 72
Kwanini vifo vya waisrael unaviona ni vya thamani kuliko vifo vya wapalestina.
 
Kucheleweshwa kwa zoezi la vikosi vya Israel kuingia Gaza kuna watu wanaamini kuwa ni woga wa Israel kupata kipigo kutoka kwa vikosi vya wanamgambo wa Hamas na wenzao huko Gaza kama ilivyokuwa huko nyuma. Hapana safari hii ni zaidi ya uwoga.

Nia safari hii ni kuwamaliza wapalestina kwa wingi kuliko safari nyingine yoyote ile kwani wakiuliwa Hamas wachache wanazaliwa wengine wanaoendeleza vita. Mbinu hiyo sasa imeweza kufanyika mbele ya walimwengu wote. Marekani na Israel wanajua wanachofanya ndio maana badala ya kutoa amri ya kusitisha vita kila siku kuna ahadi za kwenda kesho yake badala ya leo.

Jumuiya ya waarabu wanaona kinachofanyika lakini nguvu yao kubwa ni kukataa tu kukutana na Rais wa Marekani aliyepanga kukutana nao badala ya kutoa tamko kali la kufunguliwa mpaka na kupeleka mahitaji na kuiamrisha Israel ifungue maji kwa wote bila masharti.Na hiyo nayo imekuja baada kuuliwa kwa wagonjwa na madaktari kwenye shambulio la anga kwenye hospitali hapo jana ambapo watu 500 wameuliwa kwa sekunde chache tu.

Urusi ilipojitoa kwenye mkataba ya usafirishaji nafaka kati yake na Ukraine umoja wa mataifa ulitoa malalamikio na shutuma kali kwa Urusi na kutamka kuwa ni ajabu kuwa Urusi inatumia chakula kama silaha.Hiyo ilikuwa ni kwa vile mahjitaji ya ngano na bidhaa nyengine zinazoambatana nazo ni kwa ajili yao wao.

Kwa upande wa Palestina wanajua kuwa maji kwanza ni muhimu kuliko hata chakula na bado hakuna tamko la kuiambia Israel kuwa iache kutumia maji kama silaha.

Kinachoendelea ni kama kutokea kichaa mwenye nguvu akamkaba koo mnyonge fulani katikati ya barabara penye watu wengi kama pale mtaa wa sikukuu Kariakoo na kila mmoja akapita zake bila kuwaamua hata kabla ya kuuliza ugomvi wao.Akifa mnyonge yule bali hukumu na ghadhabu za Mwenyezi Mungu zitawaenea wote walioshuhudia na wakapuuza.

Hatua wanazochukua waarabu na waislamu kwa ujumla ni hafifu sana kulingana na uzito wa ukatili wanaofanyiwa wapalestina.Wakiona wanakula na kunywa na kupata usingizi mnono wanawasahau wenzao.inashangaza kumekuwa na uungwaji mkono wa wapalestina nchi za Ulaya ,Marekani na kwengineko kuliko nchi za kiarabu ambazo ni jirani zaidi na Palestina kunakotokea unyama huo.

Watu wa Ulaya na kwengineko wanajua hakuna maisha ya furaha kwa watu 90 kuishi kwenye nyumba moja isiyo na huduma kamili za kibinadamu na kila muda wakiangalia angani kusikiliza kombora ambalo linaweza likwawaangamiza wote kwa pamoja.

Waarabu wajitayarishe na mabalaa yatakayowakuta wao wenyewe kwa uzembe wao.Hii dunia ni kitu kidogo sana kwa Mwenyezi Mungu.
Hammas walipovamia sherehe ya Supernova na kuua wayahudi 260 huo umoja wa mataifa,umoja wa waarabu ulikuwa wapi kutoa matamko makali dhidi ya hammas ila vitendo vya Israel kujilinda vinaonekana vitolewe matamko wafia dini acheni unafiki na upendeleo tafuteni haki na usawa

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
 
Huo ndio ukweli missile imefeli imekung'uta hospital Israel wapo tayari ku prove hilo na hapo ndo mtajua mnawatetea vichaa.
Tumia akili yako vyema.Usifanye ushabiki kwa wanyonge wanapoonewa.Kinachofuata kutoka kwa muumba wa Ulimwengu kinaweza kuwa na madhara kwa dunia nzima na sisi tulio mbali tukaingia kwenye dhiki kama za wapalestina.
 
Tumia akili yako vyema.Usifanye ushabiki kwa wanyonge wanapoonewa.Kinachofuata kutoka kwa muumba wa Ulimwengu kinaweza kuwa na madhara kwa dunia nzima na sisi tulio mbali tukaingia kwenye dhiki kama za wapalestina.

Subiria footages mnataka tuwasikilize nyie tuu? ndio maana jana kwenye mahojiano na BBC msemaji wa Israel amewaambia BBC msikimbilie kutangaza vitu bila balanced stories na wamesema watatoa footages muone hayo machizi yenu yanalipua watu wao.

Una mtazamo gani kwa watu waliouliwa October 7th?
 
Subiria footages mnataka tuwasikilize nyie tuu? ndio maana jana kwenye mahojiani na BBC msemaji wa Israel amewaambia BBC msikimilie kutangaza vitu bila balanced stories na wamesema watatoa footages muone hayo machizi yenu yanalipua watu wao.
Kwa kudanganya Israel hawawezekani.Mara kadhaa wamepeleka hizo footage UN zikaonekana ni uongo mtupu.
 
Hammas walipovamia sherehe ya Supernova na kuua wayahudi 260 huo umoja wa mataifa,umoja wa waarabu ulikuwa wapi kutoa matamko makali dhidi ya hammas ila vitendo vya Israel kujilinda vinaonekana vitolewe matamko wafia dini acheni unafiki na upendeleo tafuteni haki na usawa

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
Unazungumza kama kwamba huo mzozo umeanza juzi oktoba 7.Jiulize hao watu walikuwa wapi Israel ikivunja mikataba na matamko yote ya UN.
Kama watu wao waliouliwa ni 260 au 1300 si wamesema ni Hamas basi wawafuate hao hao Hamas mbona sasa wameshauwa karibu raia 4000 na wanaendelea.Huoni kuwa nia sio Hamas pekee bali ni wapalestina wote.
 
Sasa ni jukumu la Hamas kupeleka footages za ukweli, otherwise bomu lolote likirushwa na yeyote linaweza ku detonate.
Ile hali iliyoonekana na vyombo vyote vya habari hawajashawishika kuwa shambulio lilie ni la Hamas.Hakuna shida ya footage unayoidai.
 
Ile hali iliyoonekana na vyombo vyote vya habari hawajashawishika kuwa shambulio lilie ni la Hamas.Hakuna shida ya footage unayoidai.
Kushawishika maana yake nini? Vita haina kushawishika ni facts tuu, migambo imekosea projection imejibamiza risasi mguuni kwao.
 
Back
Top Bottom