Uchaguzi 2020 Wapi kimbunga cha Bernard Membe jamani?

1. Picha lilianza kwa mbwembwe za kumpata mgombea makini, mbobezi wa siasa atakayeing'oa ccm
2. Ikafuata kumrubuni mzee Membe kuwa anakubalika nchi nzima na atampiga Pombe asubuhi kabisa
3. Membe kiburi kikamjaa akaleta jeuri kwa ccm (watu wakamtazama tu!)
4. Aliponyofolewa Lumumba, vijana wa zambarau wakamsajili kwa mbwembwe, tz ikalipuka kwa shangwe
5. Kampeni zikakaribia vijana wakajenga mazingira ya kuchomoa kale kapensheni, huku wakijua fika wana mgombea wao mfukoni
6. Bila hiyana wakambebesha bwaba Bernard ilani ya zambarau apeperushe, wakati wao wanaitambua ilani ya Ufipa
7. Bwana Kamilius akajitosa kuchukua fomu, na vijana maridadi kwa udalali wakamsindikiza Dodoma
8. Ufunguzi wa kampeni umefika, vijana wakamsukumia bwana Bwege aanzishe shoo huko kwao
9. Pesa zikaisha shushushu akakumbuka ana akaunti imenona huko Dubai, vijana walivyoinasa tu, wakamwambia "mwami vuta mpunga tukaliwashe lile tufani la kisurisuri kule Kigoma"
10. Kachero akajaa, kaenda kuvuta mpunga. (akasahau kabisa ile kauli yetu "ogopa matapeli, nyumba hii haiuzwi")
11. Vijana walipovuta tu chakwao, signal zikaita, kwa lafudhi za kilatini "hatumjui mtu huyu"
12. Mlango ukafungwa, kachero kabaki mdomo wazi, safari ya kurudi Lindi kwa mguu ikaanza, anasikia tu harufu ya "bata" kwa mbaaaali
*imeisha hiyo*
 
CCM bana, mtu akiamua kukaa kimya hamtaki, akiogea ukweli oohh anamsema Rais - sasa kwenu jema ni lipi? Membe kaamua kukaa kimya kwa sasa!!
Akijaza nyomi kwenye mkutano wake oooh hao siyo wapiga kura ni wahuni tu, mara wameenda kumshangaa mgombea. yani maccm sijui yapoje.
 
Sasa anamuunga mkono kwenye uraisi mdogo wake aitwaye Tundu Antipas Lissu.
 
Leo ni tarehe 1/10/2020, zikiwa zimebaki wiki nne kwenda kwenye jambo letu 28/10, tunakusihi Mwanadiplomasia na Kachero Mbobevu anza kuonesha makeke yako. Ndo muda muafaka wa kunuka katika ule usemi wako wa "Niguse Ninuke"

Nuka Membe, Nukaaa!!!
 
Siasa ni sayansi,, 🀣🀣🀣🀣🀣

Inawezekana anaendesha kampeni yake kisayansi zaidi. Tukijashtuka tayari goliπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Membe ni Kachero mbobezi. Kawapiga Chengactatari na anajua anachofanya. Kura yake ni kwa Lissu
 
Leo ni tarehe 1/10/2020, zikiwa zimebaki wiki nne kwenda kwenye jambo letu 28/10, tunakusihi Mwanadiplomasia na Kachero Mbobevu anza kuonesha makeke yako. Ndo muda muafaka wa kunuka katika ule usemi wako wa "Niguse Ninuke"

Nuka Membe, Nukaaa!!!
Tarehe 4 anaunga juhudi Temeke. Tusubiri.
 
Afanye kampeni tumvue uanachama. Yeye kampeni zake inatiwa afanye mikoa yakusini tu.
 
Habarini wana jamvi takribani muda umepita bila kusikia habari za mgombea urais kupitia tiketi ya Act wazalendo kachero mbobezi Bernard kamillius Membe je huyu mtu yuko wapi na anafanya nini kwa Sasa?
 
Anapiga mazoezi ya jaramba la mwisho
 
Huenda kuna mzigo aliofuata huko Oman ukafeli na kuchanganyikiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…