safuher
JF-Expert Member
- Feb 11, 2019
- 11,837
- 17,412
- Thread starter
- #21
Raisi ni raisi tu,hii sio hoja ya kukamatia kwa sababu ipo kihisia zaidi kuliko uhalisia.Atazuiwa na wahafidhina wa chama chake. Hawa ndiyo hawataki kusikia ishu ya katiba mpya.
Mambo kibao kayafanya ambayo yanasemwa kihisia kama unavyosema kwamba wahafidhina wanakerekwa lakini ni hisia tu kusema wahafidhina wanakerekwa.
Mfano teuzi zake sasa hivi watu husema anawakwra mpaka wahafidhina, hivyo kama kaweza kuwakera kwa hili pia anaweza kuwakera kwa katiba na wasimfanye chochote zaidi ya kulalamika.
Kauli zake kuhsu mikakati anayochukus dhidi ya korona,hili pia inasemwa kwamba wahafidhina wanakereka lakini wanasema kihisia kama unavyosema wewe,kwa hiyo kama kawakera katika jambo hili anaweza pia kuwakera katika katiba na bado isiwe kitu.
Once mama akishasema kwamba sasa naanza mchakato wa katiba mpya,hao wahafidhina unaowasema wote wataanza kusapoti mchakato huo na kujidai wao ndio wazalendo.
Lakini sasa watu wanaenda na upepo wa mama tuu maadamau hajaona umuhimu wake kwa sasa basi nao wahafidhina unaowasema wanaenda na biti hilo hilo