Uchaguzi 2020 Wapinzani mnatambua kabisa Rais Magufuli ni mtendaji, mchapa kazi na mtekelezaji mzuri. Bado hamuoni aibu kuchukua fomu za urais!

Uchaguzi 2020 Wapinzani mnatambua kabisa Rais Magufuli ni mtendaji, mchapa kazi na mtekelezaji mzuri. Bado hamuoni aibu kuchukua fomu za urais!

Kuna tatizo la kufikiri kwa kutumia akili za kawaida ndani ya vyama vya upinzani hapa Tanzania. Sababu kwa akili za kawaida tu unaweza kupata uthubutu upi wa kupambana na rais kama Magufuli?

Chama Cha Mapinduzi kina misingi imara na thabiti ambayo kimekuwa kikiisimamia tokea kuanzishwa kwake. Na moja ya misingi ni usawa na haki kwa wote. Kwa ujumla kwa CCM binadamu wote ni sawa.

Mwaka 2015 alipopewa ridhaa ya kuwa mgombea wa CCM ni dhahiri kuwa CCM ilimpa kazi ya kutekeleza mambo muhimu kwa watanzania.
JPM ametekeleza mambo makubwa kwa muda mfupi na hii ni kwa sababu anaongoza kwa kufuata misingi ya CCM.

Aliahidi atajenga SGR kipande cha kwanza Dar to Moro kitakamilika hivi karibuni. Aliahidi kujenga JNHPP na ametekeleza na mradi huu ukikamilika utakuwa na manufaa kwa watanzania wote. Aliaahidi kuimarisha sekta ya afya na elimu na yote watanzania wameshuhudia nini kimefanyika.

Kwa ujumla Tanzania ina rais mchapa kazi ambae akiahidi kitu kwa manufaa ya watanzania lazima atekeleze.

Sasa vyama vya upinzani kama Chadema ambavyo hata kuongoza majimbo na kata ni tatizo inakuwaje wanathubutu kuchukua fomu na kutaka kuweka mgombea wa kupambana na rais kama Magufuli?

Chama kama Chadema ambacho hakiwezi kusimamia ruzuku ya ya mil 360, kitaweza vipi kuwa na rais ambae atawatekelezea maendekeo watanzania?
Akili nyanya ndio hizi, nyanya masalo kabisa.
Kajifunze maana na umuhimu wa demokrasia.Vinginevyo labda uwe hauungi mkono dhana nzima ya demokrasia.
Mwisho utatuambia kwa nini asikae tu mpaka Mungu akimpenda.
NB:Waachwe huru watu wazungumze ndio utajua vizuri nini ni nini, we unaangalia tu flyovers town, piga hilo hilo jicho lako upande wa vijijini na kwa maisha ya mtanzania wa kawaida(hapa wazembe huwa wanaleta kauli "mboga" kabisa eti ni muda wa kukaza mkanda kwa faida za kizazi cha baadae")Kipi cha wakina Wassira?😃
 
Tatizo LA magufuli Sera yake ni viwanda tena vya kujenga serekali sio vya watu binafsi vyenye masilahi binafsi ambayo vinabeba ajira kubwa na Uhuru kuongea imemshinda,tutakula barabara,ndege,
 
Mimi mkazi wa mkoa wa shinyanga kwa kweli jiwe hajafanya lolote la maana na hata mikoa jirani na shy kama kigoma, Tabora, Simiyu na Geita kafanya utopolo tupu yaani cha maana alichofanya nikuja kuzindua viwanda na lami zilizojengwa utawala wa kikwete
 
Wanadaisalam mna sababu za msingi za kumpa kura jiwe make kawajengea maflyova na kawanunulia midege, ila sie wa shy na mikoa jirani hajatufanyia lolote la maana kura zetu zipo kwa lissu
 
Sawa kwakuwa amejenga viwanda 100 nani tamnyima kura Magufuli
hatakama ccm itakaa miaka mitano bila maendeleo yyte kuitoa ni kaz maana upinzani hauna hoja muhumu na ni vigeugeu hatabiriki jukwaani n matusi mala sjui ana mguu wa hivi mala hivi na vile
 
Amini nakwambia sio tu Magufuli, hakuna mwanasiasa popote pale Tanzania anayeweza kupambana na Tundu Antipas Lissu.
Kwa uwezo wa Lissu kwenye ulingo magu anaaga mapema sana.

Na kwa jinsi Magu alivyoharibu kwenye kilimo na Sera zake za ajabu si korosho, si mbaazi, si ufuta si mahindi bei zimeharibika vibaya sana , kwa jinsi alivyoharibu kwenye uchumi hadi biashara kufungwa, makampuni kufungwa ivyo watu kupoteza ajira. Kwa jinsi magu alivyoharibu sekta binafsi hadi suala la ajira limeharibuika vibaya kuna vijana maelfu wamegraduate tangu 2015 na hawana ajira nina uhakika Lissu anampiga Magu mapema sana
nmefurahi unvyompenda lissu hahaaaa
 
Ninawashangaa sana baadhi ya watanzania walio ni fikra ndogo na upeo mdogo wa kufanya upembuzi yakinifu juu ya nani atashinda u rais mwaka huu.yani unakuta mtu anasimama kabisa na kusema eti Lissu anauwezo wa kumkabili Magufuli (best president ever).

Naombeni niwaambie hakuna mtu anayeweza mkabili Dkt. Magufuli hata kidogo, mimi nasema atakae weza mkabili Magufuli nitatoa milioni tano cash.

Dkt. Magufuli sio wa mchezo kama mnavodhani, amefanya makubwa na nchi inaenda vizuri sana. Eleweni basi. Mnajisumbua wapinzani

Amewahi shinda nn bila kubebwa
 
We bwege nini? Ruzuku ya Chadema mlilipa kijanja Mbowe bil 8. Takukuru lazima wapeleke mahakamani. Ccm haina matumizi mabaya ya ruzuku kama unavyosema ndio maana inatumia vyema hata pesa za walipa kodi kuleta maendeleo kwa kuwabana mafisadi.
Kununua watu toka upinzani na kuwarundika ccm ni matumizi sahihi ya hizo fedha au ni ufisadi??
 
Mleta mada nakubaliana nawe kwa aslimia 100% Lissu ni kiongozi mzuri wa watu pamoja na Maendeleo yao lakini Magufuli ni mtawala wa watu na Maendeleo ya vitu.
Mfano Lissu awezi kusema vyama flani visifanye Siasa ila chama chake ndiyo kifanye Siasa.. Ila Magufuli anaweza ilo tena sana.Lissu awezi kukubali wastaafu wasilipwe mafao yao kwa wakati,vijana wasipate ajira au watumishi wasipandishwe mishahara.. Ila Magufuli anaweza kufanya hivyo zaidi ya sana.
 
Ndo demokrasia hiyo bwashee, wewe humpendi hata kidogo mimi nampenda. Tukutane kwenye kampeni
okay tusiishiee kwenye kampeni tu na hata upigaji kuraa "kumchagua kiongozi ni haki yako" ila naamini kura yako imeishahalibikaaa rafiki yangu
 
Ninawashangaa sana baadhi ya watanzania walio ni fikra ndogo na upeo mdogo wa kufanya upembuzi yakinifu juu ya nani atashinda u rais mwaka huu.yani unakuta mtu anasimama kabisa na kusema eti Lissu anauwezo wa kumkabili Magufuli (best president ever).

Naombeni niwaambie hakuna mtu anayeweza mkabili Dkt. Magufuli hata kidogo, mimi nasema atakae weza mkabili Magufuli nitatoa milioni tano cash.

Dkt. Magufuli sio wa mchezo kama mnavodhani, amefanya makubwa na nchi inaenda vizuri sana. Eleweni basi. Mnajisumbua wapinzani
Bahati nzuri umeongea propaganda badala ya fact ukweli ni kwamba magufuli anachukiwa mno na watanzania waliowengi na ndio maana amepewa ulinzi kuliko maraisi wote waliomtangulia pia ujue watanzania wamezoea shida na mateso hivyo wanaofagilia jpm Ni wale ambao wanakamilisha msemo u cant fight them join them sasa lisu na wengine wengi malaki kwa malaki ambao hawawaungi mkono ni kwamba they can fight you that's y the won't join you waliowaunga mkono wamezoea mateso hivyo wanajiunga na mtesi wao wakidhani watapata faraja ya mateso Yao jiulize kwanini mpaka Leo kuna walimu wanajiita wapambe na wapenzi waccm wakati wanajua CCM ilichowafanyia ?
 
okay tusiishiee kwenye kampeni tu na hata upigaji kuraa "kumchagua kiongozi ni haki yako" ila naamini kura yako imeishahalibikaaa rafiki yangu
Ndugu demokrasia ni kuchagua navkuchaguliwa kwa uhuru. Naamini TUNDU LISSU anafaa, naamini atafanya makubwa kwa maslahi mapana ya Tanzania. Naamini akishinda ndo itakuwa mwanzo wa demokrasia na maendeleo ya kweli kwa Tanzania.
kuna madogo nawaona mtaani wamemaliza vyuo tangu 2015 na wanahangaika hawana ajira, wamekata tamaa na wanasikitisha sana. Nikitembea Tanzania nikiona jinsi mipango miji ilivyo mibovu, jinsi watu wanashindwa hata kuwekwa kwenye maeneo mazuri yaliyojengwa na kupangwa vizuri kufanyia biashara, ninavyoona makampuni yakifa na watu wakikosa ajira inanifanya ntake sera mbadala ambazo naamini zitaivusha nchi yetu.

Ni wakati wa watu wengine kupewa serikali. Demokrasia ya kweli ndo chanzo cha maendeleo ya kweli
 
Ninawashangaa sana baadhi ya watanzania walio ni fikra ndogo na upeo mdogo wa kufanya upembuzi yakinifu juu ya nani atashinda u rais mwaka huu.yani unakuta mtu anasimama kabisa na kusema eti Lissu anauwezo wa kumkabili Magufuli (best president ever).

Naombeni niwaambie hakuna mtu anayeweza mkabili Dkt. Magufuli hata kidogo, mimi nasema atakae weza mkabili Magufuli nitatoa milioni tano cash.

Dkt. Magufuli sio wa mchezo kama mnavodhani, amefanya makubwa na nchi inaenda vizuri sana. Eleweni basi. Mnajisumbua wapinzani
Inawezekana hata hiyo milioni 5 hujawahi kuiona wala kuishika... magufuri ndo nn kwamba hatuna mtu wa kushindana naye?? Angekuwa mtu bora asingekubali fomu achukue pekeyake...ni rais mbovu na muoga tangu kuundwa kwa Taifa la Tanzania
 
Ninawashangaa sana baadhi ya watanzania walio ni fikra ndogo na upeo mdogo wa kufanya upembuzi yakinifu juu ya nani atashinda u rais mwaka huu.yani unakuta mtu anasimama kabisa na kusema eti Lissu anauwezo wa kumkabili Magufuli (best president ever).

Naombeni niwaambie hakuna mtu anayeweza mkabili Dkt. Magufuli hata kidogo, mimi nasema atakae weza mkabili Magufuli nitatoa milioni tano cash.

Dkt. Magufuli sio wa mchezo kama mnavodhani, amefanya makubwa na nchi inaenda vizuri sana. Eleweni basi. Mnajisumbua wapinzani
Buku 7
 
Bila tume huru hawawezi shinda ila kukiwa na haki huyo unaemsifia ni mweupe mno ndio maana hata fomu katoa moja ungeshangaa angetoa fom zaidi ya moja yani hata ndani hawamtaki !!! Ulishaona awamu IPI fom inatolewa moja???
Mnamkuza kama Mungu lakin he doesn't deserve such status !!!!
Ajira hakuna
Ameshindwa hata kuongeza mishahara watumishi wanaishi kimaskini mno kuliko awamu zote
Anatamba yeye anajua wakiongea wengine itakua......
Ukabila ndo usiseme ???
Unamjibu buku 7 vzr namna hii hawa co kwamba ukwel hawaujui la hasha wanqujua ila tu wameamua kuweka maslah mbele we mquote andika buku 7 umemaliza
 
Back
Top Bottom