Wapinzani tuwe na busara za kisiasa. Mikutano ya kisiasa sio ishu ya maana hata huko USA na Magharibi chaguzi zikiisha siasa zinahamia bungeni.

Usichokijua ni bora ukae kimya, maana kama hujui umuhimu wa mikutano ya hadhara ya vyama siasi nakushauri uachane na mambo ya siasa!.
 
Umechukua hatua gani kwa hayo yote unayoyalalamikia?
 
Hao wabunge watarajiwa sera zao wakazinadi wapi ili wachaguliwe na kuingia bungeni kulifanya bunge liwe na meno? Wakazinadi sera zao chumbani kwa wake na wanaume zao?
 
Kwani lile ni bunge? Niambie nani aliyeshinda kihalali mle ndani? Mikutano inawaweka sawa wananchi kwamba wakiibiwa kura wawe tayari kufa kutetea haki Yao. Siyo wewe unayepelekwa kama ling'ombe
 

Ungemweleza faida za mikutano ya kisiasa ili shutuma yako dhidi yake iwe na maana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…