Otorong'ong'o
JF-Expert Member
- Aug 17, 2011
- 37,957
- 26,414
Hahahaha...Siku hizi wanasema sio dunia tu bali hata galaxies na kwa kifupi ulimwengu (universe) wote ambao hata mwisho wake na wapi ni katikati haijajulikana.
Huko kote umenena vyema kabisa, ndiyo maana nimeondoa. Lakini katika hili la mwisho, naomba kuuliza kama unamfahamu Pengo.
"Msimamo wa TEC sometimes unatofautuana na msimamo wa kanisa"!!!! Huku ndiko kulewa kwa mvinyo mpya au mbege grade one?. Hivi unajua kanisa ni nini na TEC ni nini?. Kanisa linaanzia level ya dunia (pope) kisha level ya majimbo ( jimbo moja moja) kuna msemo wa kanisa unasema hivi penye askofu kanisa limekamilika. Askofu ni mchungaji Mkuu wa kanisa level ya jimbo. Sasa wanapokutana maaskofu wote Tanzania maana yake kanisa katoliki Tanzania limekutana na kujadiliana na kuafikiana kisha maafikiano hayo huandikwa ili jumuia ya waamini wasome na kuelewa kinachosemwa na kanisa. Kwahiyo kusema Msimamo wa TEC sometimes unakwenda kinyume na kanisa ni kwamba hujui TEC ni nini na kanisa ni nini.Kwanza akatubu ndipo mambo mengine yafuatie!
Sijui Kwanini Yule askofu mkubwa wa kanisa anashindwa kumshauri Swahiba wake atubu!
.msimamo wa TEC sometimes huwa unatofautiana na msimamo wa kanisa!
Hizi ni habari za kusadikika kwangu nachukulia kama ni fiction hazina ukweli wowote. Lakini sikuzui wewe kuamini.Tafuta kitabu kinaitwa kanisa katoliKi na siasa za Tanzania
Hapa Kwetu: Kitabu cha Dr. John C. Sivalon, M.M.
Unajua mkuu kuna watu wanajifanya wanalijua kanisa katoliki kwa kusoma vitabu vya kusadikika vya kina Yericko. Wao hawajui kabisa miongozo ya kanisa lakini ukiona wakiandika apa utadani wanalijua kwelikweli ila kwa wsiojua wanaamini hizi habari za kusadikika wanazoandikiwa na kina Yericko ambao wanatoa vijarida kujaza matumbo yao. Hata kirefu ca TEC (Tanzania Episcopal Conference) labda hawakijui."Msimamo wa TEC sometimes unatofautuana na msimamo wa kanisa"!!!! Huku ndiko kulewa kwa mvinyo mpya au mbege grade one?. Hivi unajua kanisa ni nini na TEC ni nini?. Kanisa linaanzia level ya dunia (pope) kisha level ya majimbo ( jimbo moja moja) kuna msemo wa kanisa unasema hivi penye askofu kanisa limekamilika. Askofu ni mchungaji Mkuu wa kanisa level ya jimbo. Sasa wanapokutana maaskofu wote Tanzania maana yake kanisa katoliki Tanzania limekutana na kujadiliana na kuafikiana kisha maafikiano hayo huandikwa ili jumuia ya waamini wasome na kuelewa kinachosemwa na kanisa. Kwahiyo kusema Msimamo wa TEC sometimes unakwenda kinyume na kanisa ni kwamba hujui TEC ni nini na kanisa ni nini.
Yaani mkuu maaskofu wa Katoliki ni kama watanzania wengine? Naona unawashusha.Masemaji wa kanisa ni Papa.
Na papa Ana balozi wake hapa......
Huo waraka siyo kauli ya kanisa.....ni mawazo tu ya maaskofu kama watz wengine......
Inatia moyo sana kuona Baraza la Maaskofu nchini limeanza kulaani na kukemea huu UdU wa kutisha unaoendelea nchini katika awamu hii.
Waliokuwa wanaikosoa Serikali hii dhalimu walitusiwa majina mbali mbali ikiwemo wasaliti, majizi, wapiga madili na matusi mengine chungu nzima.
Sasa hata Baraza hili la Maaskofu limechoka kuendelea kukaa kimya huku UdU nchini ukizidi kushamiri kwa kasi ya kutisha na hivyo kutishia amani ya nchi yetu.
DU apingwe kwa nguvu zote za Watanzania wenye mapenzi ya kweli na nchi yetu ili aheshimu katiba, Bunge, mahakama, sheria za nchi, sheria za manunuzi ya Serikali, sheria za kutoa fedha hazina etc.
Naendelea kusema huyu jamaa ni janga kubwa sana la Taifa letu na ni mtu hatari sana kwa mustakabali wa Taifa letu.
Nzi Elli Tetty Sky Eclat Salary Slip zitto junior MENGELENI KWETU tindo Saint Ivuga Erythrocyte lusungo Retired
Namshangaa saana Mh Rais anavyozidi kuwachekea hawa maaskofu
Badala ya kuendelea na kazi zao za kidini wanaingilia ingilia siasa
Hawa maaskofu wanatakiwa waadhibiwe adhabu kali hasa,ili wawe mfano kwa maaskofu wengine[emoji1321]
mume sema kweli tupu ila wakuyafanyia Kazi maneno haya ndohayupo nadhani mungemshauri turudi kwenye mfumo wa chama kimojaPage 12
"Kikatiba, nchi yetu inafuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katiba na Sheria mbalimbali zimeainisha utaratibu wa kazi na shughuli za vylma vya siasa. Ili kuhakikisha hvamba ka'"'ina shughuli z vyamavya siasa zinakuwa endelevu, vyama vyenye kukidhi vlgezo hupewa ruzuku kupitia Bajeti ya Serikali inayopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania. Hata hivyo, shughuli za, sirsa bado zinaendelea kuzuiwa kwa kutumia vyombo vya dola. Maana yake ni kwamba shughuli za kiuenezi za vyama vya siasa, kama vile mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na hata mikutano ya ndani, ambayo ni haki ya kila rua, zimekoma mpaka uchaguzi mwingine. Kisheria, huu ni uvunjifu wa Katiba na Sheria za nchi.
Vile vile baadhi ya vyombo vya habari vimefungiwa au kusimamishwa kwa muda, na hivyo kupunguza uwigo wa uhuru wa wananchi wa kupata habari, maoni na wa kujieleza. Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambaba na kuminya uhuru wa mahakama na bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya Kikatiba.
Katika mazingira haya ni rahisi kwa jamii kufarakana na hata kujenga chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu. Kumekuwapo pia hali ya vurugu katika chaguzi mbalimbali. Chaguzi hizi zinaacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine. Hali hii ni hatari kwa mustakabali wa Taifa letu. Tukiiachia hali hii izoeleke tushishangae huko mbeleni kujikuta katika mifarakano mikubwa zaidi itakayobomoa misingi ya amani na umoja wa kitaifa."
Masemaji wa kanisa ni Papa.
Na papa Ana balozi wake hapa......
Huo waraka siyo kauli ya kanisa.....ni mawazo tu ya maaskofu kama watz wengine......
huo umetoka Ijumaa, kwa hiyo kama kusomwa ingekuwa Jumapili ya jana.Jumapili ijayo nitawahi deski mbele St peters
Hakuna atajayethubutuTukiondoa sheria ya misamaha ya kodi,tutaelewana vizuri sana,hapo sielewi kitu
Wataanza kutozwa kodi shauri zao,au kuchunguzwa uraia wako.wangekuwa na ubavu huo si wangewatenga na kuwafukuza ushiriki wale wote wasababishi wa waliyoyaandika kwenye waraka wao.
Mwaka gani alitamka haya?Namfahamu sana. Rafiki yangu niliye kua naye shule alikua Askofu msaidizi wake. Na ninajua nini swali baada ya hili. Pengo siyo mropokaji kama wengine. Pengo ana wakati wake anauona muafaka anakuja na lungu lake. Sijui umri wako huko nyuma Pengo aliwasema CCM waziwazi. Unakumbuka alipowaambia CCM na serikali yake kuwa "Hittler alichaguliwa na wananchi wa ujerumani ki demokrasia na wala hakupindua nchi. Watu walichoka na muelekeo wa serikali ya wakati huo ya Ujerumani ikaamua kumuweka Hitller madarakani. Ningeoba sana ninyi watawala muangalie upya jinsi mnavyoendesha serikali isiye ya udhalimu tukaja tukamuweka Hitller wetu hapa Tanzania. Maana watu wakiwachoka na mambo yenu watampigia kura yeyote yule ili mradi wabadilishe uongozi. Hivyo msitukwaze" huyo alikua Pengo. Miaka ya 90 wakati serikali ilikua inapiga virungu mpaka wanafunzi migomo mingi ya madaktari n.k. Hivyo wengi humu ndani JF wamezaliwa juzi juzi hawamjui kabisa Pengo. Pengo alikua mwiba kwa CCM wakati huo hakuna vyama vingi.
Kumfahamu mtu haihitaji uwe umri sawa naye, haihitaji umzidi au uwe mdogo kwake, haihitaji muwe mmesoma nsye au uwe umemfundisha. Rekodi zinaongea. Aonekanavyo ndivyo alivyo. Ni kama Prof Kabudi wa Tume ya Warioba na Prof Kabudi waziri, ni watu tofauti wenye misimamo na kauli tofauti.Namfahamu sana. Rafiki yangu niliye kua naye shule alikua Askofu msaidizi wake. Na ninajua nini swali baada ya hili. Pengo siyo mropokaji kama wengine. Pengo ana wakati wake anauona muafaka anakuja na lungu lake. Sijui umri wako huko nyuma Pengo aliwasema CCM waziwazi. Unakumbuka alipowaambia CCM na serikali yake kuwa "Hittler alichaguliwa na wananchi wa ujerumani ki demokrasia na wala hakupindua nchi. Watu walichoka na muelekeo wa serikali ya wakati huo ya Ujerumani ikaamua kumuweka Hitller madarakani. Ningeoba sana ninyi watawala muangalie upya jinsi mnavyoendesha serikali isiye ya udhalimu tukaja tukamuweka Hitller wetu hapa Tanzania. Maana watu wakiwachoka na mambo yenu watampigia kura yeyote yule ili mradi wabadilishe uongozi. Hivyo msitukwaze" huyo alikua Pengo. Miaka ya 90 wakati serikali ilikua inapiga virungu mpaka wanafunzi migomo mingi ya madaktari n.k. Hivyo wengi humu ndani JF wamezaliwa juzi juzi hawamjui kabisa Pengo. Pengo alikua mwiba kwa CCM wakati huo hakuna vyama vingi.