WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

Naunga mkono hoja.
Kwa vile kazi ya dini zote ni kuwatayarisha tuu waumini wao kufika mbinguni, kwao hapa duniani ni safari tuu, hivyo dini zote, zifanye kazi moja tuu ya kumhubiri Mungu tuu na wasichanganye mambo ya siasa.

Hata zile shule na vyuo vya dini, vifundishe tuu injili na torati.
Na yale mashirika ya misaada ya kidini, yatoe misaada ya kueneza tuu Biblia.
Hata zile hospitali za dini, wagonjwa wakifika, wasiwatibu, bali wawaharakishe kwenda mbinguni.
P.
Hata wanasiasa ni waumini wa dini mbalimbali,hivyo wakikengeuka lazima viongozi wa dini wawakemee na kuwaonya.
 
Siasa ni nini na dini ni nini? Wataalamu mtusaidie.
 
Naunga mkono hoja.
Kwa vile kazi ya dini zote ni kuwatayarisha tuu waumini wao kufika mbinguni, kwao hapa duniani ni safari tuu, hivyo dini zote, zifanye kazi moja tuu ya kumhubiri Mungu tuu na wasichanganye mambo ya siasa.

Hata zile shule na vyuo vya dini, vifundishe tuu injili na torati.
Na yale mashirika ya misaada ya kidini, yatoe misaada ya kueneza tuu Biblia.
Hata zile hospitali za dini, wagonjwa wakifika, wasiwatibu, bali wawaharakishe kwenda mbinguni.

Na akitokea mwanasiasa kuwaomba viongozi wa dini wamuombee, then viongozi wa dini wamuombee kweli ili mapenzi ya Bwana yatimizwe juu yake, akaikamilishe safari, maana kidini, hapa duniani tuko tuu safarini.
P.
Nimekuelewa sana kaka Mayalla
 
Kanisa Katoliki Tanzania limetoa waraka kwa ajili ya kuwaandaa waamini wake kwa ajili ya kipindi cha Toba, kinachoanza rasmi Jumatano ijayo tarehe 14 Februari 2018 [ambayo ndiyo siku ya wapendanao, Valentine. tusherehekee kwa Toba eeeh tafadhalini!]. Kipindi hicho hujulikana pia kama KWARESIMA, ambacho kinahitimishwa na JUMA KUU na kisha sikukuu ya PASAKA.

Kama una haraka sana, soma ukurasa wa 11 na 12 (kurasa orijino) au ukurasa wa 14 na 15 kwa kurasa za PDF. Naambatanisha waraka huo.
Karibu! Ni nondo Kali!

=======

Maaskofu Katoliki watoa msimamo kuhusu masuala ya Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii

f1771774c03dc128b4ace4aa419e3351.jpg


031c2b5fb1cb36dcf26e0f2f70abaf9b.jpg

ceaa75236b2d1b4546253650ed852b54.jpg


----------------------

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetoa ujumbe wa Kwaresma wa mwaka 2018 ndani yake likitoa msimamo kuhusu masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini.

Ujumbe huo ulioandikwa na maaskofu wote 35 wa TEC wakiongozwa na Rais wake, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa upo katika kitabu cha kurasa 20 ikiwa ni maandalizi ya ibada hiyo ya siku 40, kipindi ambacho ni cha mfungo wa sala kukumbuka siku 40 za Kristo kufunga na kwenda jangwani.

Hali ya kisiasa

Katika ujumbe huo, TEC imesema uamuzi wa Serikali kuzuia maandamano, mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ni kwenda kinyume cha Katiba ya nchi.

Baraza hilo pia limeonya hatua ya Serikali kuvibana vyombo vya habari ikiwa pamoja na kuvifungia kwa sababu mbalimbali.

“Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambamba na kuminya uhuru wa Mahakama na Bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya kikatiba.”

Alipopigiwa simu ili kutoa maoni ya upande wa Serikali kuhusu ujumbe huo, Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbasi alisema, “Sijaliona bado tamko husika kwa hiyo siwezi kujibu hoja ambayo sijaisoma kwa sasa.”

TEC imetoa ujumbe huo katika kipindi ambacho vyama vya siasa, hasa vya upinzani vikilalamika kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara baada ya Serikali kuipiga marufuku mpaka mwaka 2020, isipokuwa kwa wabunge walioshinda uchaguzi ambao wameruhusiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yao.

Ugumu huo umetajwa na vyama hivyo kwamba unapunguza nguvu ya ushindani kwa vyama vya upinzani kukikabili chama tawala.

“Kikatiba, nchi yetu inafuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katiba na sheria mbalimbali zimeainisha utaratibu wa kazi na shughuli za vyama vya siasa. Ili kuhakikisha kwamba shughuli za vyama vya siasa zinakuwa endelevu, vyama vyenye kukidhi vigezo hupewa ruzuku kupitia bajeti ya Serikali inayopitishwa na Bunge,” unaeleza ujumbe huo.

“Hata hivyo, shughuli za, siasa bado zinaendelea kuzuiwa kwa kutumia vyombo vya dola. Maana yake ni kwamba shughuli za kiuenezi za vyama vya siasa, kama vile mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na hata mikutano ya ndani, ambayo ni haki ya kila raia, zimekoma mpaka uchaguzi mwingine. Kisheria, huu ni uvunjifu wa Katiba na sheria za nchi.”

Kuhusu vyombo vya habari, TEC imesema Serikali imepunguza wigo wa uhuru wa wananchi wa kupata habari na maoni ya kujieleza na kueleza kwamba kwa ujumla wake, mazingira hayo yatasababisha jamii kufarakana na hata kujenga chuki.

“Kumekuwapo pia hali ya vurugu katika chaguzi mbalimbali. Chaguzi hizi zinaacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine,” unasema ujumbe huo wa TEC na kuonya kuwa kama hali hiyo itaachwa, itakuja kusababisha mifarakano mikubwa itakayobomoa amani na umoja wa kitaifa.

Kiuchumi

Kuhusu uchumi, TEC imetoa mambo sita ya kujiuliza; “Tunazitumiaje mali na rasilimali nyingine tulizokabidhiwa na Mungu kama mawakili wake? Tunalipa kodi stahiki kwa ajili ya kugharamia huduma za jamii ambazo Serikali inapaswa kutoa kwa ajili ya wananchi?”

“Wale ambao tu waajiri, tunawajali wafanyakazi na wahudumu wetu kwa kuwalipa mishahara ya halali? Wale ambao tu wafanya biashara, tunalipa kodi zote kihalali?”

“Wale ambao tumepewa jukumu la kukusanya kodi, ushuru na ada nyingine kama tunafanya hivyo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu husika? Tunaepukaje na kishawishi cha rushwa, hongo, mulungula, magendo au aina yoyote ya ufisadi?”

Kijamii

Katika eneo la kijamii TEC imesema bado kuna kishawishi cha kupingana na azma ya kuboresha maisha ya kijamii.

“Hii inajidhihirisha kwa njia ya uhasama, ugomvi, ukatili kwa watoto na wanawake, ujambazi, na maovu mengine kama hayo miongoni mwa jamii yetu. Kama wamisionari tunaopaswa kuleta habari njema kwa ndugu zetu, kwa nini turuhusu roho ya namna hii ambayo kwa kweli ni roho ya Kaini inayouliza kwa jeuri kabisa,” unasema ujumbe huo.

Mambo matatu

Katika ujumbe wake, Baraza hilo limesema, “Kwa mwaka huu wa 2018 kipindi hiki ni cha kujitafakari mbele ya Mungu na kufanya toba hususan uhai wa amani yetu kwa njia ya matendo ya huruma, haki upendo na amani kwa jirani zetu.”

Limesema hiki ni kipindi chenye upekee wa aina yake kwake sababu ya mambo matatu;

“Ni katika mwaka huu ambapo Kanisa Katoliki Tanzania linaadhimisha na kusherehekea miaka 150 ya Ukatoliki Tanzania Bara, na kilele chake kitakuwa tarehe 2 Oktoba.

Mwaka huu pia utakuwa ni mwaka wa 50 tangu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania watoe tamko rasmi kuhusu mwelekeo na hatima ya nchi yetu na Mwaka huu ni mwaka wa maandalizi ya utekelezaji wa haki ya msingi ya kidemokrasia ya raia wote ya kuchagua viongozi wa Serikali zetu za mitaa, vijiji na vitongoji hapo mwakani 2019.”

Kwa sababu hizo tatu, TEC imesema, “Ni vyema tafakari yetu ya Kwaresima ikalenga katika swali ambalo, kwa namna moja au nyingine, linahusu sababu hizo tatu. Kwa njia ya swali hilo mwanadamu hudiriki kumhoji na kumuuliza Mungu na Muumba wake kuhusu hali ya binadamu mwenzake. Swali hilo ni Je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?” (Mw. 4:9).
Jiwe limegonga penyewe lakini kwa kuwa dikteta ni 'sikio la kufa' huenda asiufanyie kazi ushauri huu wa watumishi wa Mungu ambao amekuwa akiwaomba wamuombee kila kukicha. Inauma sana.
 
Kanisa Katoliki Tanzania limetoa waraka kwa ajili ya kuwaandaa waamini wake kwa ajili ya kipindi cha Toba, kinachoanza rasmi Jumatano ijayo tarehe 14 Februari 2018 [ambayo ndiyo siku ya wapendanao, Valentine. tusherehekee kwa Toba eeeh tafadhalini!]. Kipindi hicho hujulikana pia kama KWARESIMA, ambacho kinahitimishwa na JUMA KUU na kisha sikukuu ya PASAKA.

Kama una haraka sana, soma ukurasa wa 11 na 12 (kurasa orijino) au ukurasa wa 14 na 15 kwa kurasa za PDF. Naambatanisha waraka huo.
Karibu! Ni nondo Kali!

=======

Maaskofu Katoliki watoa msimamo kuhusu masuala ya Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii

f1771774c03dc128b4ace4aa419e3351.jpg


031c2b5fb1cb36dcf26e0f2f70abaf9b.jpg

ceaa75236b2d1b4546253650ed852b54.jpg


----------------------

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetoa ujumbe wa Kwaresma wa mwaka 2018 ndani yake likitoa msimamo kuhusu masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini.

Ujumbe huo ulioandikwa na maaskofu wote 35 wa TEC wakiongozwa na Rais wake, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa upo katika kitabu cha kurasa 20 ikiwa ni maandalizi ya ibada hiyo ya siku 40, kipindi ambacho ni cha mfungo wa sala kukumbuka siku 40 za Kristo kufunga na kwenda jangwani.

Hali ya kisiasa

Katika ujumbe huo, TEC imesema uamuzi wa Serikali kuzuia maandamano, mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ni kwenda kinyume cha Katiba ya nchi.

Baraza hilo pia limeonya hatua ya Serikali kuvibana vyombo vya habari ikiwa pamoja na kuvifungia kwa sababu mbalimbali.

“Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambamba na kuminya uhuru wa Mahakama na Bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya kikatiba.”

Alipopigiwa simu ili kutoa maoni ya upande wa Serikali kuhusu ujumbe huo, Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbasi alisema, “Sijaliona bado tamko husika kwa hiyo siwezi kujibu hoja ambayo sijaisoma kwa sasa.”

TEC imetoa ujumbe huo katika kipindi ambacho vyama vya siasa, hasa vya upinzani vikilalamika kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara baada ya Serikali kuipiga marufuku mpaka mwaka 2020, isipokuwa kwa wabunge walioshinda uchaguzi ambao wameruhusiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yao.

Ugumu huo umetajwa na vyama hivyo kwamba unapunguza nguvu ya ushindani kwa vyama vya upinzani kukikabili chama tawala.

“Kikatiba, nchi yetu inafuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katiba na sheria mbalimbali zimeainisha utaratibu wa kazi na shughuli za vyama vya siasa. Ili kuhakikisha kwamba shughuli za vyama vya siasa zinakuwa endelevu, vyama vyenye kukidhi vigezo hupewa ruzuku kupitia bajeti ya Serikali inayopitishwa na Bunge,” unaeleza ujumbe huo.

“Hata hivyo, shughuli za, siasa bado zinaendelea kuzuiwa kwa kutumia vyombo vya dola. Maana yake ni kwamba shughuli za kiuenezi za vyama vya siasa, kama vile mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na hata mikutano ya ndani, ambayo ni haki ya kila raia, zimekoma mpaka uchaguzi mwingine. Kisheria, huu ni uvunjifu wa Katiba na sheria za nchi.”

Kuhusu vyombo vya habari, TEC imesema Serikali imepunguza wigo wa uhuru wa wananchi wa kupata habari na maoni ya kujieleza na kueleza kwamba kwa ujumla wake, mazingira hayo yatasababisha jamii kufarakana na hata kujenga chuki.

“Kumekuwapo pia hali ya vurugu katika chaguzi mbalimbali. Chaguzi hizi zinaacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine,” unasema ujumbe huo wa TEC na kuonya kuwa kama hali hiyo itaachwa, itakuja kusababisha mifarakano mikubwa itakayobomoa amani na umoja wa kitaifa.

Kiuchumi

Kuhusu uchumi, TEC imetoa mambo sita ya kujiuliza; “Tunazitumiaje mali na rasilimali nyingine tulizokabidhiwa na Mungu kama mawakili wake? Tunalipa kodi stahiki kwa ajili ya kugharamia huduma za jamii ambazo Serikali inapaswa kutoa kwa ajili ya wananchi?”

“Wale ambao tu waajiri, tunawajali wafanyakazi na wahudumu wetu kwa kuwalipa mishahara ya halali? Wale ambao tu wafanya biashara, tunalipa kodi zote kihalali?”

“Wale ambao tumepewa jukumu la kukusanya kodi, ushuru na ada nyingine kama tunafanya hivyo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu husika? Tunaepukaje na kishawishi cha rushwa, hongo, mulungula, magendo au aina yoyote ya ufisadi?”

Kijamii

Katika eneo la kijamii TEC imesema bado kuna kishawishi cha kupingana na azma ya kuboresha maisha ya kijamii.

“Hii inajidhihirisha kwa njia ya uhasama, ugomvi, ukatili kwa watoto na wanawake, ujambazi, na maovu mengine kama hayo miongoni mwa jamii yetu. Kama wamisionari tunaopaswa kuleta habari njema kwa ndugu zetu, kwa nini turuhusu roho ya namna hii ambayo kwa kweli ni roho ya Kaini inayouliza kwa jeuri kabisa,” unasema ujumbe huo.

Mambo matatu

Katika ujumbe wake, Baraza hilo limesema, “Kwa mwaka huu wa 2018 kipindi hiki ni cha kujitafakari mbele ya Mungu na kufanya toba hususan uhai wa amani yetu kwa njia ya matendo ya huruma, haki upendo na amani kwa jirani zetu.”

Limesema hiki ni kipindi chenye upekee wa aina yake kwake sababu ya mambo matatu;

“Ni katika mwaka huu ambapo Kanisa Katoliki Tanzania linaadhimisha na kusherehekea miaka 150 ya Ukatoliki Tanzania Bara, na kilele chake kitakuwa tarehe 2 Oktoba.

Mwaka huu pia utakuwa ni mwaka wa 50 tangu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania watoe tamko rasmi kuhusu mwelekeo na hatima ya nchi yetu na Mwaka huu ni mwaka wa maandalizi ya utekelezaji wa haki ya msingi ya kidemokrasia ya raia wote ya kuchagua viongozi wa Serikali zetu za mitaa, vijiji na vitongoji hapo mwakani 2019.”

Kwa sababu hizo tatu, TEC imesema, “Ni vyema tafakari yetu ya Kwaresima ikalenga katika swali ambalo, kwa namna moja au nyingine, linahusu sababu hizo tatu. Kwa njia ya swali hilo mwanadamu hudiriki kumhoji na kumuuliza Mungu na Muumba wake kuhusu hali ya binadamu mwenzake. Swali hilo ni Je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?” (Mw. 4:9).
Maaskofu wa KKKT nao wamelenga mlemle walimolenga wakatoliki. Kusema kweli nchi ipo katika ombwe la kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni. Bwana mkubwa asipojirkebisha hii nchi itamshinda.
 
Kanisa Katoliki Tanzania limetoa waraka kwa ajili ya kuwaandaa waamini wake kwa ajili ya kipindi cha Toba, kinachoanza rasmi Jumatano ijayo tarehe 14 Februari 2018 [ambayo ndiyo siku ya wapendanao, Valentine. tusherehekee kwa Toba eeeh tafadhalini!]. Kipindi hicho hujulikana pia kama KWARESIMA, ambacho kinahitimishwa na JUMA KUU na kisha sikukuu ya PASAKA.

Kama una haraka sana, soma ukurasa wa 11 na 12 (kurasa orijino) au ukurasa wa 14 na 15 kwa kurasa za PDF. Naambatanisha waraka huo.
Karibu! Ni nondo Kali!

=======

Maaskofu Katoliki watoa msimamo kuhusu masuala ya Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii

f1771774c03dc128b4ace4aa419e3351.jpg


031c2b5fb1cb36dcf26e0f2f70abaf9b.jpg

ceaa75236b2d1b4546253650ed852b54.jpg


----------------------

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetoa ujumbe wa Kwaresma wa mwaka 2018 ndani yake likitoa msimamo kuhusu masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini.

Ujumbe huo ulioandikwa na maaskofu wote 35 wa TEC wakiongozwa na Rais wake, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa upo katika kitabu cha kurasa 20 ikiwa ni maandalizi ya ibada hiyo ya siku 40, kipindi ambacho ni cha mfungo wa sala kukumbuka siku 40 za Kristo kufunga na kwenda jangwani.

Hali ya kisiasa

Katika ujumbe huo, TEC imesema uamuzi wa Serikali kuzuia maandamano, mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ni kwenda kinyume cha Katiba ya nchi.

Baraza hilo pia limeonya hatua ya Serikali kuvibana vyombo vya habari ikiwa pamoja na kuvifungia kwa sababu mbalimbali.

“Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambamba na kuminya uhuru wa Mahakama na Bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya kikatiba.”

Alipopigiwa simu ili kutoa maoni ya upande wa Serikali kuhusu ujumbe huo, Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbasi alisema, “Sijaliona bado tamko husika kwa hiyo siwezi kujibu hoja ambayo sijaisoma kwa sasa.”

TEC imetoa ujumbe huo katika kipindi ambacho vyama vya siasa, hasa vya upinzani vikilalamika kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara baada ya Serikali kuipiga marufuku mpaka mwaka 2020, isipokuwa kwa wabunge walioshinda uchaguzi ambao wameruhusiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yao.

Ugumu huo umetajwa na vyama hivyo kwamba unapunguza nguvu ya ushindani kwa vyama vya upinzani kukikabili chama tawala.

“Kikatiba, nchi yetu inafuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katiba na sheria mbalimbali zimeainisha utaratibu wa kazi na shughuli za vyama vya siasa. Ili kuhakikisha kwamba shughuli za vyama vya siasa zinakuwa endelevu, vyama vyenye kukidhi vigezo hupewa ruzuku kupitia bajeti ya Serikali inayopitishwa na Bunge,” unaeleza ujumbe huo.

“Hata hivyo, shughuli za, siasa bado zinaendelea kuzuiwa kwa kutumia vyombo vya dola. Maana yake ni kwamba shughuli za kiuenezi za vyama vya siasa, kama vile mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na hata mikutano ya ndani, ambayo ni haki ya kila raia, zimekoma mpaka uchaguzi mwingine. Kisheria, huu ni uvunjifu wa Katiba na sheria za nchi.”

Kuhusu vyombo vya habari, TEC imesema Serikali imepunguza wigo wa uhuru wa wananchi wa kupata habari na maoni ya kujieleza na kueleza kwamba kwa ujumla wake, mazingira hayo yatasababisha jamii kufarakana na hata kujenga chuki.

“Kumekuwapo pia hali ya vurugu katika chaguzi mbalimbali. Chaguzi hizi zinaacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine,” unasema ujumbe huo wa TEC na kuonya kuwa kama hali hiyo itaachwa, itakuja kusababisha mifarakano mikubwa itakayobomoa amani na umoja wa kitaifa.

Kiuchumi

Kuhusu uchumi, TEC imetoa mambo sita ya kujiuliza; “Tunazitumiaje mali na rasilimali nyingine tulizokabidhiwa na Mungu kama mawakili wake? Tunalipa kodi stahiki kwa ajili ya kugharamia huduma za jamii ambazo Serikali inapaswa kutoa kwa ajili ya wananchi?”

“Wale ambao tu waajiri, tunawajali wafanyakazi na wahudumu wetu kwa kuwalipa mishahara ya halali? Wale ambao tu wafanya biashara, tunalipa kodi zote kihalali?”

“Wale ambao tumepewa jukumu la kukusanya kodi, ushuru na ada nyingine kama tunafanya hivyo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu husika? Tunaepukaje na kishawishi cha rushwa, hongo, mulungula, magendo au aina yoyote ya ufisadi?”

Kijamii

Katika eneo la kijamii TEC imesema bado kuna kishawishi cha kupingana na azma ya kuboresha maisha ya kijamii.

“Hii inajidhihirisha kwa njia ya uhasama, ugomvi, ukatili kwa watoto na wanawake, ujambazi, na maovu mengine kama hayo miongoni mwa jamii yetu. Kama wamisionari tunaopaswa kuleta habari njema kwa ndugu zetu, kwa nini turuhusu roho ya namna hii ambayo kwa kweli ni roho ya Kaini inayouliza kwa jeuri kabisa,” unasema ujumbe huo.

Mambo matatu

Katika ujumbe wake, Baraza hilo limesema, “Kwa mwaka huu wa 2018 kipindi hiki ni cha kujitafakari mbele ya Mungu na kufanya toba hususan uhai wa amani yetu kwa njia ya matendo ya huruma, haki upendo na amani kwa jirani zetu.”

Limesema hiki ni kipindi chenye upekee wa aina yake kwake sababu ya mambo matatu;

“Ni katika mwaka huu ambapo Kanisa Katoliki Tanzania linaadhimisha na kusherehekea miaka 150 ya Ukatoliki Tanzania Bara, na kilele chake kitakuwa tarehe 2 Oktoba.

Mwaka huu pia utakuwa ni mwaka wa 50 tangu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania watoe tamko rasmi kuhusu mwelekeo na hatima ya nchi yetu na Mwaka huu ni mwaka wa maandalizi ya utekelezaji wa haki ya msingi ya kidemokrasia ya raia wote ya kuchagua viongozi wa Serikali zetu za mitaa, vijiji na vitongoji hapo mwakani 2019.”

Kwa sababu hizo tatu, TEC imesema, “Ni vyema tafakari yetu ya Kwaresima ikalenga katika swali ambalo, kwa namna moja au nyingine, linahusu sababu hizo tatu. Kwa njia ya swali hilo mwanadamu hudiriki kumhoji na kumuuliza Mungu na Muumba wake kuhusu hali ya binadamu mwenzake. Swali hilo ni Je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?” (Mw. 4:9).
*SIRI IMEFICHUKA!!!!!!*

• Maaskofu waukana Ujumbe wa Pasaka.
• Maaskofu 4 wa TEC waliouandika wajulikana
• Majina yao haya hapa, kwa taarifa za uhakika.

Nimeshtushwa sana na taarifa niliyoipata juu ya Ujumbe wa Kwaresima uliotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ulioelekezwa kwa waumini wakati huu wa toba ya Kwaresima iliyoanza Februari 14, 2018 hadi Pasaka siku ya kusherehekea ufufuko wa Bwana Yesu Kristo (Pasaka).

Mimi ni Mkatoliki wa Jimbo la Dodoma na Askofu wangu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya.

Nikiri nilianza kupata mashaka tangu mapema ujumbe huu ulipotoka, nilijiuliza sana na hivyo nikaamua kufanya juhudi za kujua kama kweli Kanisa langu Katoliki limefikia hatua hii? Naujua utaratibu na utamaduni wa kanisa langu ndio maana nilipatwa na mashaka haya.

Kwa ambao hawajausoma ujumbe huu, ulikuwa na sura nne lakini iliyoleta tafrani ni sura ya tatu yenye ujumbe kuhusu “Dalili za nyakati zetu Tanzania” hususani katika kipengele cha siasa. Imeleta tafrani kwa sababu katika eneo hili ujumbe huu umeenda kwenye masuala ambayo siku zote yamesababisha kuwepo malumbano kuwa viongozi wa dini wanaingia mambo ya kisiasa ama wanachanganya dini na siasa.

Kwa ufupi kabisa ujumbe huu umetoa shutuma na bila shaka dhidi ya Serikali inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kuwa shughuli za siasa kama vile uenezi, mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na mikutano ya ndani zinazuiwa kwa kutumia vyombo vya dola.

Ujumbe unaendelea kushutumu kuwa vyombo vya habari vimefungiwa au kusimamishwa kwa muda, uhuru wa Mahakama na Bunge unaminywa na kwamba katika mazingira haya ni rahisi kwa jamii kufarakana na hata kujenga chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu.

Ujumbe umeongeza shutuma nyingine kuwa chaguzi zinaharibiwa kwa vurugu na hivyo kuacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine na kwamba hali hiyo ni hatari kwa mustakabali wa Taifa letu, ikiachwa izoeleke tusishangae huko mbele kujikuta katika mifarakano mikubwa zaidi itakayobomoa misingi ya amani na umoja wa kitaifa.

NIMEPATA TAARIFA ZA UHAKIKA KABISA kuwa ujumbe huu haukuandikwa na Maaskofu 35 wa Kanisa Katoliki kama ilivyotolewa na Baraza la Maaskofu (TEC).

Katika shauku yangu hii ya kutaka kujua kwa nini viongozi wangu wa Kanisa lenye heshima hapa nchini wamefikia hatua hii nimepata taarifa za uhakika kuwa Maaskofu walioshiriki kuandika ujumbe huu ni wanne (nitawataja huko mbele) na Maaskofu wengine walikataa kushiriki kikao kilichofanya kazi ya kuandika ujumbe huu.

Mniwie radhi sana nimepata mashaka makubwa sana niliposoma majina ya Maaskofu waliofanya kazi ya kuandika ujumbe huu na historia zao za mahubiri yenye uchochezi mkubwa na hata mara kadhaa wametuhumiwa kwa ukabila na uchochezi na ushahidi upo.

Maaskofu walioandika ujumbe huu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya wa Jimbo Kuu la Dodoma, Mhashamu Askofu Mkuu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi wa Jimbo Kuu la Mwanza, Mhashamu Askofu Augustino Shao wa Jimbo la Zanzibar na Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi wa Jimbo la Rulenge-Ngara.

Maaskofu wengine hawakushiriki kuandika ujumbe huu na kwa kuwa wanatambua dosari iliyokuwa inafanyika wakatoa udhuru mbalimbali na kwa hivyo hao Maaskofu wanne wakaifanya kazi hiyo wakishirikiana na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Padre Raymond Saba na wakamchukua Dk. Kasala kama mshauri wa uandishi wa ujumbe huo.

Kwa kuangalia safu hiyo utaona ujumbe huu umeandikwa pasi kuwepo Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wala Mwadhama Polyacarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Nimepata taarifa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Damian Dallu aliondoka mkutanoni na kuomba udhuru baada ya kubaini mwelekeo wa ujumbe huu.

Hapo ni kujiuliza kwa nini? Na kama kuna yeyote hayaamini haya basi na awaulize viongozi hawa kama walishiriki kuandika ujumbe huo, naamini hata wao wamekwazika na kwa namna yeyote hawawezi kukubaliana na yaliyomo katika ujumbe huu hata kama watakuwa na changamoto ya kuukana hadharani kulingana na utamaduni na nidhamu ya Kanisa.

Ukiangalia Maaskofu watatu kati ya wanne walioandika ujumbe huu wanatoka Mikoa ya ama Arusha ama Kilimanjaro ambako wanasiasa wake ndio wamekuwa wakishikia bango hizo hoja walizoziandika na wao wamekuwa mara kadhaa wakipambana kutumia Ibada na shughuli za Kanisa kueneza siasa hizo.

Askofu Niwemugizi ambaye mpaka sasa ana mgogoro mkubwa na idara ya Uhamiaji kutokana na uraia wake kuwa na mashaka na yeye amekuwa akitaka kujificha kwenye kichaka cha kudai anafuatwafuatwa kwa sababu anawakosoa watawala, anafahamika kwa namna alivyojipambanua kuegemea siasa za upinzani na kuungana na wanaharakati wanaopambana na Serikali.

LAKINI kwa kungalia hizo hoja wanazozitoa kuikosoa Serikali na kutaka kujenga taharuki kwa Watanzania kuwa nchi inakwenda vibaya, mimi nimejiuliza mambo mengi sana.

Maaskofu hawa wanne wanadai shughuli za kiasiasa zimezuiliwa, hivi ni mwanasiasa gani amezuliwa kufanya siasa? Maaskofu hawa wanawasikiliza akina Freeman Mbowe, Godbless Lema, Zitto Kabwe, Tundu Lissu na genge lao linalojumuisha Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu kinachoongozwa na mwanachama wa CHADEMA Dk. Heleni Kijo-Bisimba ambao wanataka shughuli za siasa iwe ni kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya maandamano, fujo na uchochezi?

Wakawaulize wanasiasa hao ni lini wamekatazwa kufanya shughuli za siasa kwenye majimbo yao? Au kwa wao wanafurahishwa na kauli za Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kuwa Watanzania wawe tayari kufa 100 hadi 200 kwa ajili ya yeye kwenda Ikulu? Hawataki hata kumuuliza Freeman Mbowe kwa nini kaatamia uenyekiti wa CHADEMA kwa zaidi ya miaka 20?

Maaskofu hawa wanne wanashutumu kuwa vyombo vya habari vimefungiwa na vingine vimefungiwa kwa muda na hivyo kupunguza uwigo wa wananchi kupata habari, maoni na uhuru wa kujieleza. Hivi Maaskofu hawajui kuwa uhuru huu una mipaka na ni kwa mujibu wa sheria? Maaskofu hawajui vyombo vya habari vilivyofungiwa ni kwa sababu vimevunja sheria? Nimejiuliza sana hivi hata ndani ya Kanisa Katoliki hakuna mipanga ya uhuru wa kujieleza?

Labda niwaulize Maaskofu kama mnahoji hilo, Je Kanisa Katoliki lenyewe limejihoji juu ya hatua lilizomchukua Padre Felician Nkwera? Kwa ambao hawajui Padre huyu alikuwa hodari wa mahubiri na alipendwa sana na waumini akawa tishio ndani ya vigogo wa Kanisa Katoliki, matokeo yake alipigwa fitina hadi Makao Makuu Roma Italia na mwishowe alitengwa na Kanisa.

Padre Privatus Kalugendo vivyo hivyo aliweka msimamo wake na akaamua kuoa ambayo ni haki ya mwanadamu yeyote, matokeo yake alitengwa na akafukuzwa kwa tamko la Papa, ambalo huwa halipingwi.

Padre Titus Mageranga wa Iringa yalimkuta hayo hayo, na hata Askofu Jacob Koda wa Jimbo la Same Kilimanjaro naye yalimkuta hayo hayo.

Mifano ipo mingi, hivi kuna mtu anajiuliza Askofu Mkuu Norbet Wendelin Mtega yupo wapi? Askofu Mahiri kabisa aliyeliongoza Jimbo Kuu Katoliki la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba kule Songea, Ruvuma. Alipigwa fitna akaondolewa kimyakimya mpaka leo haijulikani yupo wapi na Kanisa Katoliki halijatoka kwa waumini kuwaambia alikosa nini na yupo wapi?

Na hili halipo Tanzania tu, huo ndio utamaduni wa Kanisa hili kwamba katika ngazi hizo za vigogo wakubwa, ukienda tofauti na matakwa yao bila kujali una haki au huna haki unafukuzwa, unafichwa Roma ama unawekwa popote duniani ama unapotezwa kabisa maana inakuwa hakuna mawasiliano na nyumbani wala ndugu zako. Wakatoliki wanaujua ukweli huu. Nausema kwa sababu walioanzisha kufukunyua mambo ya kuvuruga nchi ni vizuri wajue kuwa hata wao sio wasafi hivyo na sisi waumini tunajua mengi ila tunaheshimu tu.

Maaskofu hawa wanne wanasema vyombo vya habari vinafungiwa, nimewaza sana na nikakumbuka jinsi viongozi hawa hawa wa Kanisa Katoliki kule nchini Rwanda walipotumia kituo cha redio kueneza chuki miongoni mwa Wanyarwanda na kusababisha mauaji ya halaiki mwaka 1994, ambapo watu takribani Milioni 1 waliuawa kikatili kwa kuchinjwa, kuchomwa moto na kupondwapondwa kwa madai kuwa ni mende.

Kwa wasiojua mauaji ya halaiki ya Rwanda yaliibukia kwenye ukabila lakini fukuto lilianza zamani na miongoni mwa waliokuwa wanatengeneza fukuto hilo ni viongozi wa Kanisa Katoliki ambalo lina mizizi mikubwa nchini Rwanda.

Askofu Rwemugizi ambaye ana mgogoro na idara ya Uhamiaji kwa madai kuwa sio raia wa Tanzania bali nchi jirani anaujua ukweli huu na anajua vizuri madhara ya mchezo anaoufanya, naamini ama anashauku ya kuona tena mauaji yale ama anafanya kwa malengo mahususi.

Maaskofu hawa wanne wanasema Mahakama na Bunge vinaingiliwa, lakini hawajasema ni wapi mihimili hii imeingiliwa.

Kwa ujumbe unaotoka kwa jina la chombo kikubwa kama Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) nilitegemea kusoma mifano na uthibitisho wa kuingiliwa kwa mihimili hii.

Hii ni hatari kubwa sana kutoa tuhuma nzito kama hizo dhidi ya mihimili ya dola halafu ukaacha zinaelea hewani. Watoke tena Maaskofu hawa wanne waseme kwa uwazi na kwa uthibitisho kuwa mihimili hii imeingiliwa hapa na hapa na hapa.

Maaskofu hawa wanne wanasema chaguzi zinafanywa kwa vurugu na zinaacha chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu. Japo kuwa kauli hii imeachwa inaelea lakini kwa namna yoyote Maaskofu wanatuhumu kuwa wanaoshindwa kwenye chaguzi nyingi hapa nchini ambao ni vyama vya upinzani ndio wanaobaki na hasira na chuki.

Hapa Maaskofu wanataka kutuambia kuwa ni Tanzania peke yake ambako wanaoshindwa kwenye uchaguzi ndio wananuna? Hivi kwenye chaguzi za ndani ya CHADEMA wanaokosa huwa hawanuni? Ina maana Maaskofu huwa hawaoni vurugu ambazo hutokea kwenye mataifa mbalimbali wakiwemo jirani zetu wa Kenya hata Taifa kubwa la Marekani ambao wamefanya uchaguzi karibuni? Mimi nilidhani jukumu la maaskofu lingekuwa kuponya kwa imani makovu ya uchaguzi hasa kwa wanaoshindwa na badala yake wanataka hapa Tanzania ndio paonekane pana tatizo kubwa na wanatuma ujumbe wa kuwachochea wananchi waikasirikie Serikali.

HITIMISHO.
Kwa sisi Wakatoliki hiki kilichofanywa na Maaskofu hawa wanne ni lazima kikemewe kwa nguvu zote. Naamini Kanisa linao Maaskofu wazuri, wacha Mungu na wanaotambua umuhimu wa Kanisa katika nchi, wanatambua umuhimu wao katika kuimarisha ustawi wa jamii badala ya kuivuruga.

Na hata katika mahubiri ya leo Jumapili ya Matawi (Machi 25, 2018) tumewasikia Maaskofu na Mapadre wazuri wakihubiri Injili juu ya Mateso ya Yesu na kusulubiwa kwake kwa ajili ya wanadamu. Wanafanya kazi ya Mungu ya kuwajenga waumini kwa imani, kutubu dhambi na kushika njia iliyonyooka, wametufundisha mambo muhimu katika maisha ya ukristo na kamwe viongozi hawa hawawi na mahubiri ya mihemko na siasa zinazoleta chuki na uchochezi.

Tunajenga Taifa la wachapakazi, nchi yetu ipo nyuma sana kimaendeleo, Maaskofu na Mapadre wetu wazuri wanahubiri matumaini, wanawaombea viongozi wa Serikali kuwa watumishi bora, wenye hofu ya Mungu, wanaviombea vyombo vya haki kutenda haki na wanawaombea Watanzania na dunia nzima kupigania amani, upendo, mshikamano na udugu badala ya kushabikia kauli na uchochezi wa kuleta vita, mapigano, malumbano na fitna.

Maaskofu na Mapadre Wakatoliki wazuri wanawahimiza Watanzania kufanya kazi mashambani na makazini ili kujipatia kipato halali kwa kuwa imeandikwa asiyefanya kazi na asile, wanawahimiza Watanzania kutovunja sheria na kuheshimu mamlaka zote badala ya kuchochea watu wakeshe kwenye maandano, malumbano na mapambano na Serikali.

Naamini mtazamo huu sio wa kwangu pekee yangu, naamini wapo Wakatoliki wengi ambao wamechukizwa na sehemu ya ujumbe huu wa Kwaresima ulioandikwa na Maaskofu hawa wanne, nawaomba tusiyumbishwe na hilo, tuendelee kuipenda nchi yetu na kuungana na Serikali hasa wakati huu ambapo kiongozi wa nchi Mhe. Rais Magufuli anafanya mambo makubwa ya kimageuzi katika uchumi, ustawi wa jamii, kutetea wanyonge na kudhibiti wizi wa mali za umma.

Natambua kuwa Baraza la Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) nao wamefanya makosa haya haya yaliyofanywa na TEC, natambua vinara wa kutoa Ujumbe wa Pasaka wa KKKT ni watu wa mlengo gani, natambua kwa nini wamekasirishwa hivyo lakini hili wacha niwaachie waumini wa KKKT wenyewe, mimi nipo na hawa wa kwangu Kanisa Katoliki.

Kwa Maaskofu wote na viongozi wengine wa dini, naomba niseme Tanzania ninayoijua mimi ina watu ambao wapo makini sana hasa linapokuja suala la nchi yao, sisi Watanzania tunapenda amani, tunapenda upendo, sisi ni ndugu sana, hatujazoea vurugu, hatupendi ukabila na ukanda, tunawapenda majirani kama Yesu alivyosema na ndio maana hao wanasiasa walioasisi haya mnayoyasema leo wameshindwa kwenye uwanja wa siasa na sasa wanataka kuwatumia nyie kwenye makanisa.

Ninachokiona kwa kuwa mmesahau kuwa Makanisani kwenu kuna waumini wenye milengo tofauti ya siasa tunakokwenda mtayavuruga Makanisa, kwa Kanisa Katoliki itakuwa ni mtihani mkubwa kwa sababu hakuna utaratibu wa Askofu kupigiwa kura ili aendelee ama asiendelee kama ilivyo kwa Makanisa mengine, kwa hiyo kitakachotokea ni kuendelea kukimbiwa na waumini kama ambavyo mmewapoteza waumini wengi kwenda kwenye makanisa ya Kilokole.

Kwa makanisa yenye uchaguzi wa Maaskofu ninachokiona ni kuendeleza mitafaruku ambayo mpaka leo inazitafuna baadhi ya Dayosisi zenu. Tena huku mlikoingia ndio kubaya zaidi maana sasa vyama vya siasa vitaanza kushindana kuweka Maaskofu wao. Inawezekana msilione hili lakini mkae mkijua kuwa litakapofika hapo hamtaweza kulidhibiti.

CHADEMA walipoanzisha kumchukua Mwana CCM Lazaro Nyalandu walidhani CCM watakaa kimya, walichokipata na wanachoendelea kukipata wote mnaona. Sasa na nyinyi mmeamua kuingia kwenye siasa za kushabikia hoja za CHADEMA na kutumwa na CHADEMA kuichokonoa Serikali ya CCM, mjiangalie siku CCM nao wakiingia huko Makanisani kwenu mjue shughuli itakuwa pevu.

Nawaombeni msituharibie Kanisa. Acheni Makanisa yafanye kazi yake ya kuhubiri Injili, siasa waachieni wanasiasa, harakati waachieni wanaharakati na vita waachieni wanajeshi. Polycarp Mdemu soma na hii hapa uone ukweli ulivyo,na Pengo kwenye ujumbe wa wito vijana Bagamoyo amekataa hilo.

Julius Kindonga
Mkazi wa Dodoma
Machi 25, 2018
 
Jiwe limegonga penyewe lakini kwa kuwa dikteta ni 'sikio la kufa' huenda asiufanyie kazi ushauri huu wa watumishi wa Mungu ambao amekuwa akiwaomba wamuombee kila kukicha. Inauma sana.
*SIRI IMEFICHUKA!!!!!!*

• Maaskofu waukana Ujumbe wa Pasaka.
• Maaskofu 4 wa TEC waliouandika wajulikana
• Majina yao haya hapa, kwa taarifa za uhakika.

Nimeshtushwa sana na taarifa niliyoipata juu ya Ujumbe wa Kwaresima uliotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ulioelekezwa kwa waumini wakati huu wa toba ya Kwaresima iliyoanza Februari 14, 2018 hadi Pasaka siku ya kusherehekea ufufuko wa Bwana Yesu Kristo (Pasaka).

Mimi ni Mkatoliki wa Jimbo la Dodoma na Askofu wangu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya.

Nikiri nilianza kupata mashaka tangu mapema ujumbe huu ulipotoka, nilijiuliza sana na hivyo nikaamua kufanya juhudi za kujua kama kweli Kanisa langu Katoliki limefikia hatua hii? Naujua utaratibu na utamaduni wa kanisa langu ndio maana nilipatwa na mashaka haya.

Kwa ambao hawajausoma ujumbe huu, ulikuwa na sura nne lakini iliyoleta tafrani ni sura ya tatu yenye ujumbe kuhusu “Dalili za nyakati zetu Tanzania” hususani katika kipengele cha siasa. Imeleta tafrani kwa sababu katika eneo hili ujumbe huu umeenda kwenye masuala ambayo siku zote yamesababisha kuwepo malumbano kuwa viongozi wa dini wanaingia mambo ya kisiasa ama wanachanganya dini na siasa.

Kwa ufupi kabisa ujumbe huu umetoa shutuma na bila shaka dhidi ya Serikali inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kuwa shughuli za siasa kama vile uenezi, mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na mikutano ya ndani zinazuiwa kwa kutumia vyombo vya dola.

Ujumbe unaendelea kushutumu kuwa vyombo vya habari vimefungiwa au kusimamishwa kwa muda, uhuru wa Mahakama na Bunge unaminywa na kwamba katika mazingira haya ni rahisi kwa jamii kufarakana na hata kujenga chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu.

Ujumbe umeongeza shutuma nyingine kuwa chaguzi zinaharibiwa kwa vurugu na hivyo kuacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine na kwamba hali hiyo ni hatari kwa mustakabali wa Taifa letu, ikiachwa izoeleke tusishangae huko mbele kujikuta katika mifarakano mikubwa zaidi itakayobomoa misingi ya amani na umoja wa kitaifa.

NIMEPATA TAARIFA ZA UHAKIKA KABISA kuwa ujumbe huu haukuandikwa na Maaskofu 35 wa Kanisa Katoliki kama ilivyotolewa na Baraza la Maaskofu (TEC).

Katika shauku yangu hii ya kutaka kujua kwa nini viongozi wangu wa Kanisa lenye heshima hapa nchini wamefikia hatua hii nimepata taarifa za uhakika kuwa Maaskofu walioshiriki kuandika ujumbe huu ni wanne (nitawataja huko mbele) na Maaskofu wengine walikataa kushiriki kikao kilichofanya kazi ya kuandika ujumbe huu.

Mniwie radhi sana nimepata mashaka makubwa sana niliposoma majina ya Maaskofu waliofanya kazi ya kuandika ujumbe huu na historia zao za mahubiri yenye uchochezi mkubwa na hata mara kadhaa wametuhumiwa kwa ukabila na uchochezi na ushahidi upo.

Maaskofu walioandika ujumbe huu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya wa Jimbo Kuu la Dodoma, Mhashamu Askofu Mkuu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi wa Jimbo Kuu la Mwanza, Mhashamu Askofu Augustino Shao wa Jimbo la Zanzibar na Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi wa Jimbo la Rulenge-Ngara.

Maaskofu wengine hawakushiriki kuandika ujumbe huu na kwa kuwa wanatambua dosari iliyokuwa inafanyika wakatoa udhuru mbalimbali na kwa hivyo hao Maaskofu wanne wakaifanya kazi hiyo wakishirikiana na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Padre Raymond Saba na wakamchukua Dk. Kasala kama mshauri wa uandishi wa ujumbe huo.

Kwa kuangalia safu hiyo utaona ujumbe huu umeandikwa pasi kuwepo Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wala Mwadhama Polyacarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Nimepata taarifa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Damian Dallu aliondoka mkutanoni na kuomba udhuru baada ya kubaini mwelekeo wa ujumbe huu.

Hapo ni kujiuliza kwa nini? Na kama kuna yeyote hayaamini haya basi na awaulize viongozi hawa kama walishiriki kuandika ujumbe huo, naamini hata wao wamekwazika na kwa namna yeyote hawawezi kukubaliana na yaliyomo katika ujumbe huu hata kama watakuwa na changamoto ya kuukana hadharani kulingana na utamaduni na nidhamu ya Kanisa.

Ukiangalia Maaskofu watatu kati ya wanne walioandika ujumbe huu wanatoka Mikoa ya ama Arusha ama Kilimanjaro ambako wanasiasa wake ndio wamekuwa wakishikia bango hizo hoja walizoziandika na wao wamekuwa mara kadhaa wakipambana kutumia Ibada na shughuli za Kanisa kueneza siasa hizo.

Askofu Niwemugizi ambaye mpaka sasa ana mgogoro mkubwa na idara ya Uhamiaji kutokana na uraia wake kuwa na mashaka na yeye amekuwa akitaka kujificha kwenye kichaka cha kudai anafuatwafuatwa kwa sababu anawakosoa watawala, anafahamika kwa namna alivyojipambanua kuegemea siasa za upinzani na kuungana na wanaharakati wanaopambana na Serikali.

LAKINI kwa kungalia hizo hoja wanazozitoa kuikosoa Serikali na kutaka kujenga taharuki kwa Watanzania kuwa nchi inakwenda vibaya, mimi nimejiuliza mambo mengi sana.

Maaskofu hawa wanne wanadai shughuli za kiasiasa zimezuiliwa, hivi ni mwanasiasa gani amezuliwa kufanya siasa? Maaskofu hawa wanawasikiliza akina Freeman Mbowe, Godbless Lema, Zitto Kabwe, Tundu Lissu na genge lao linalojumuisha Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu kinachoongozwa na mwanachama wa CHADEMA Dk. Heleni Kijo-Bisimba ambao wanataka shughuli za siasa iwe ni kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya maandamano, fujo na uchochezi?

Wakawaulize wanasiasa hao ni lini wamekatazwa kufanya shughuli za siasa kwenye majimbo yao? Au kwa wao wanafurahishwa na kauli za Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kuwa Watanzania wawe tayari kufa 100 hadi 200 kwa ajili ya yeye kwenda Ikulu? Hawataki hata kumuuliza Freeman Mbowe kwa nini kaatamia uenyekiti wa CHADEMA kwa zaidi ya miaka 20?

Maaskofu hawa wanne wanashutumu kuwa vyombo vya habari vimefungiwa na vingine vimefungiwa kwa muda na hivyo kupunguza uwigo wa wananchi kupata habari, maoni na uhuru wa kujieleza. Hivi Maaskofu hawajui kuwa uhuru huu una mipaka na ni kwa mujibu wa sheria? Maaskofu hawajui vyombo vya habari vilivyofungiwa ni kwa sababu vimevunja sheria? Nimejiuliza sana hivi hata ndani ya Kanisa Katoliki hakuna mipanga ya uhuru wa kujieleza?

Labda niwaulize Maaskofu kama mnahoji hilo, Je Kanisa Katoliki lenyewe limejihoji juu ya hatua lilizomchukua Padre Felician Nkwera? Kwa ambao hawajui Padre huyu alikuwa hodari wa mahubiri na alipendwa sana na waumini akawa tishio ndani ya vigogo wa Kanisa Katoliki, matokeo yake alipigwa fitina hadi Makao Makuu Roma Italia na mwishowe alitengwa na Kanisa.

Padre Privatus Kalugendo vivyo hivyo aliweka msimamo wake na akaamua kuoa ambayo ni haki ya mwanadamu yeyote, matokeo yake alitengwa na akafukuzwa kwa tamko la Papa, ambalo huwa halipingwi.

Padre Titus Mageranga wa Iringa yalimkuta hayo hayo, na hata Askofu Jacob Koda wa Jimbo la Same Kilimanjaro naye yalimkuta hayo hayo.

Mifano ipo mingi, hivi kuna mtu anajiuliza Askofu Mkuu Norbet Wendelin Mtega yupo wapi? Askofu Mahiri kabisa aliyeliongoza Jimbo Kuu Katoliki la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba kule Songea, Ruvuma. Alipigwa fitna akaondolewa kimyakimya mpaka leo haijulikani yupo wapi na Kanisa Katoliki halijatoka kwa waumini kuwaambia alikosa nini na yupo wapi?

Na hili halipo Tanzania tu, huo ndio utamaduni wa Kanisa hili kwamba katika ngazi hizo za vigogo wakubwa, ukienda tofauti na matakwa yao bila kujali una haki au huna haki unafukuzwa, unafichwa Roma ama unawekwa popote duniani ama unapotezwa kabisa maana inakuwa hakuna mawasiliano na nyumbani wala ndugu zako. Wakatoliki wanaujua ukweli huu. Nausema kwa sababu walioanzisha kufukunyua mambo ya kuvuruga nchi ni vizuri wajue kuwa hata wao sio wasafi hivyo na sisi waumini tunajua mengi ila tunaheshimu tu.

Maaskofu hawa wanne wanasema vyombo vya habari vinafungiwa, nimewaza sana na nikakumbuka jinsi viongozi hawa hawa wa Kanisa Katoliki kule nchini Rwanda walipotumia kituo cha redio kueneza chuki miongoni mwa Wanyarwanda na kusababisha mauaji ya halaiki mwaka 1994, ambapo watu takribani Milioni 1 waliuawa kikatili kwa kuchinjwa, kuchomwa moto na kupondwapondwa kwa madai kuwa ni mende.

Kwa wasiojua mauaji ya halaiki ya Rwanda yaliibukia kwenye ukabila lakini fukuto lilianza zamani na miongoni mwa waliokuwa wanatengeneza fukuto hilo ni viongozi wa Kanisa Katoliki ambalo lina mizizi mikubwa nchini Rwanda.

Askofu Rwemugizi ambaye ana mgogoro na idara ya Uhamiaji kwa madai kuwa sio raia wa Tanzania bali nchi jirani anaujua ukweli huu na anajua vizuri madhara ya mchezo anaoufanya, naamini ama anashauku ya kuona tena mauaji yale ama anafanya kwa malengo mahususi.

Maaskofu hawa wanne wanasema Mahakama na Bunge vinaingiliwa, lakini hawajasema ni wapi mihimili hii imeingiliwa.

Kwa ujumbe unaotoka kwa jina la chombo kikubwa kama Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) nilitegemea kusoma mifano na uthibitisho wa kuingiliwa kwa mihimili hii.

Hii ni hatari kubwa sana kutoa tuhuma nzito kama hizo dhidi ya mihimili ya dola halafu ukaacha zinaelea hewani. Watoke tena Maaskofu hawa wanne waseme kwa uwazi na kwa uthibitisho kuwa mihimili hii imeingiliwa hapa na hapa na hapa.

Maaskofu hawa wanne wanasema chaguzi zinafanywa kwa vurugu na zinaacha chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu. Japo kuwa kauli hii imeachwa inaelea lakini kwa namna yoyote Maaskofu wanatuhumu kuwa wanaoshindwa kwenye chaguzi nyingi hapa nchini ambao ni vyama vya upinzani ndio wanaobaki na hasira na chuki.

Hapa Maaskofu wanataka kutuambia kuwa ni Tanzania peke yake ambako wanaoshindwa kwenye uchaguzi ndio wananuna? Hivi kwenye chaguzi za ndani ya CHADEMA wanaokosa huwa hawanuni? Ina maana Maaskofu huwa hawaoni vurugu ambazo hutokea kwenye mataifa mbalimbali wakiwemo jirani zetu wa Kenya hata Taifa kubwa la Marekani ambao wamefanya uchaguzi karibuni? Mimi nilidhani jukumu la maaskofu lingekuwa kuponya kwa imani makovu ya uchaguzi hasa kwa wanaoshindwa na badala yake wanataka hapa Tanzania ndio paonekane pana tatizo kubwa na wanatuma ujumbe wa kuwachochea wananchi waikasirikie Serikali.

HITIMISHO.
Kwa sisi Wakatoliki hiki kilichofanywa na Maaskofu hawa wanne ni lazima kikemewe kwa nguvu zote. Naamini Kanisa linao Maaskofu wazuri, wacha Mungu na wanaotambua umuhimu wa Kanisa katika nchi, wanatambua umuhimu wao katika kuimarisha ustawi wa jamii badala ya kuivuruga.

Na hata katika mahubiri ya leo Jumapili ya Matawi (Machi 25, 2018) tumewasikia Maaskofu na Mapadre wazuri wakihubiri Injili juu ya Mateso ya Yesu na kusulubiwa kwake kwa ajili ya wanadamu. Wanafanya kazi ya Mungu ya kuwajenga waumini kwa imani, kutubu dhambi na kushika njia iliyonyooka, wametufundisha mambo muhimu katika maisha ya ukristo na kamwe viongozi hawa hawawi na mahubiri ya mihemko na siasa zinazoleta chuki na uchochezi.

Tunajenga Taifa la wachapakazi, nchi yetu ipo nyuma sana kimaendeleo, Maaskofu na Mapadre wetu wazuri wanahubiri matumaini, wanawaombea viongozi wa Serikali kuwa watumishi bora, wenye hofu ya Mungu, wanaviombea vyombo vya haki kutenda haki na wanawaombea Watanzania na dunia nzima kupigania amani, upendo, mshikamano na udugu badala ya kushabikia kauli na uchochezi wa kuleta vita, mapigano, malumbano na fitna.

Maaskofu na Mapadre Wakatoliki wazuri wanawahimiza Watanzania kufanya kazi mashambani na makazini ili kujipatia kipato halali kwa kuwa imeandikwa asiyefanya kazi na asile, wanawahimiza Watanzania kutovunja sheria na kuheshimu mamlaka zote badala ya kuchochea watu wakeshe kwenye maandano, malumbano na mapambano na Serikali.

Naamini mtazamo huu sio wa kwangu pekee yangu, naamini wapo Wakatoliki wengi ambao wamechukizwa na sehemu ya ujumbe huu wa Kwaresima ulioandikwa na Maaskofu hawa wanne, nawaomba tusiyumbishwe na hilo, tuendelee kuipenda nchi yetu na kuungana na Serikali hasa wakati huu ambapo kiongozi wa nchi Mhe. Rais Magufuli anafanya mambo makubwa ya kimageuzi katika uchumi, ustawi wa jamii, kutetea wanyonge na kudhibiti wizi wa mali za umma.

Natambua kuwa Baraza la Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) nao wamefanya makosa haya haya yaliyofanywa na TEC, natambua vinara wa kutoa Ujumbe wa Pasaka wa KKKT ni watu wa mlengo gani, natambua kwa nini wamekasirishwa hivyo lakini hili wacha niwaachie waumini wa KKKT wenyewe, mimi nipo na hawa wa kwangu Kanisa Katoliki.

Kwa Maaskofu wote na viongozi wengine wa dini, naomba niseme Tanzania ninayoijua mimi ina watu ambao wapo makini sana hasa linapokuja suala la nchi yao, sisi Watanzania tunapenda amani, tunapenda upendo, sisi ni ndugu sana, hatujazoea vurugu, hatupendi ukabila na ukanda, tunawapenda majirani kama Yesu alivyosema na ndio maana hao wanasiasa walioasisi haya mnayoyasema leo wameshindwa kwenye uwanja wa siasa na sasa wanataka kuwatumia nyie kwenye makanisa.

Ninachokiona kwa kuwa mmesahau kuwa Makanisani kwenu kuna waumini wenye milengo tofauti ya siasa tunakokwenda mtayavuruga Makanisa, kwa Kanisa Katoliki itakuwa ni mtihani mkubwa kwa sababu hakuna utaratibu wa Askofu kupigiwa kura ili aendelee ama asiendelee kama ilivyo kwa Makanisa mengine, kwa hiyo kitakachotokea ni kuendelea kukimbiwa na waumini kama ambavyo mmewapoteza waumini wengi kwenda kwenye makanisa ya Kilokole.

Kwa makanisa yenye uchaguzi wa Maaskofu ninachokiona ni kuendeleza mitafaruku ambayo mpaka leo inazitafuna baadhi ya Dayosisi zenu. Tena huku mlikoingia ndio kubaya zaidi maana sasa vyama vya siasa vitaanza kushindana kuweka Maaskofu wao. Inawezekana msilione hili lakini mkae mkijua kuwa litakapofika hapo hamtaweza kulidhibiti.

CHADEMA walipoanzisha kumchukua Mwana CCM Lazaro Nyalandu walidhani CCM watakaa kimya, walichokipata na wanachoendelea kukipata wote mnaona. Sasa na nyinyi mmeamua kuingia kwenye siasa za kushabikia hoja za CHADEMA na kutumwa na CHADEMA kuichokonoa Serikali ya CCM, mjiangalie siku CCM nao wakiingia huko Makanisani kwenu mjue shughuli itakuwa pevu.

Nawaombeni msituharibie Kanisa. Acheni Makanisa yafanye kazi yake ya kuhubiri Injili, siasa waachieni wanasiasa, harakati waachieni wanaharakati na vita waachieni wanajeshi. Polycarp Mdemu soma na hii hapa uone ukweli ulivyo,na Pengo kwenye ujumbe wa wito vijana Bagamoyo amekataa hilo.

Julius Kindonga
Mkazi wa Dodoma
Machi 25, 2018
 
nahisi huu utakuwa sindano ya moto kama ule wito wa kutubu wa Kutubu wa Kakobe
*SIRI IMEFICHUKA!!!!!!*

• Maaskofu waukana Ujumbe wa Pasaka.
• Maaskofu 4 wa TEC waliouandika wajulikana
• Majina yao haya hapa, kwa taarifa za uhakika.

Nimeshtushwa sana na taarifa niliyoipata juu ya Ujumbe wa Kwaresima uliotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ulioelekezwa kwa waumini wakati huu wa toba ya Kwaresima iliyoanza Februari 14, 2018 hadi Pasaka siku ya kusherehekea ufufuko wa Bwana Yesu Kristo (Pasaka).

Mimi ni Mkatoliki wa Jimbo la Dodoma na Askofu wangu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya.

Nikiri nilianza kupata mashaka tangu mapema ujumbe huu ulipotoka, nilijiuliza sana na hivyo nikaamua kufanya juhudi za kujua kama kweli Kanisa langu Katoliki limefikia hatua hii? Naujua utaratibu na utamaduni wa kanisa langu ndio maana nilipatwa na mashaka haya.

Kwa ambao hawajausoma ujumbe huu, ulikuwa na sura nne lakini iliyoleta tafrani ni sura ya tatu yenye ujumbe kuhusu “Dalili za nyakati zetu Tanzania” hususani katika kipengele cha siasa. Imeleta tafrani kwa sababu katika eneo hili ujumbe huu umeenda kwenye masuala ambayo siku zote yamesababisha kuwepo malumbano kuwa viongozi wa dini wanaingia mambo ya kisiasa ama wanachanganya dini na siasa.

Kwa ufupi kabisa ujumbe huu umetoa shutuma na bila shaka dhidi ya Serikali inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kuwa shughuli za siasa kama vile uenezi, mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na mikutano ya ndani zinazuiwa kwa kutumia vyombo vya dola.

Ujumbe unaendelea kushutumu kuwa vyombo vya habari vimefungiwa au kusimamishwa kwa muda, uhuru wa Mahakama na Bunge unaminywa na kwamba katika mazingira haya ni rahisi kwa jamii kufarakana na hata kujenga chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu.

Ujumbe umeongeza shutuma nyingine kuwa chaguzi zinaharibiwa kwa vurugu na hivyo kuacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine na kwamba hali hiyo ni hatari kwa mustakabali wa Taifa letu, ikiachwa izoeleke tusishangae huko mbele kujikuta katika mifarakano mikubwa zaidi itakayobomoa misingi ya amani na umoja wa kitaifa.

NIMEPATA TAARIFA ZA UHAKIKA KABISA kuwa ujumbe huu haukuandikwa na Maaskofu 35 wa Kanisa Katoliki kama ilivyotolewa na Baraza la Maaskofu (TEC).

Katika shauku yangu hii ya kutaka kujua kwa nini viongozi wangu wa Kanisa lenye heshima hapa nchini wamefikia hatua hii nimepata taarifa za uhakika kuwa Maaskofu walioshiriki kuandika ujumbe huu ni wanne (nitawataja huko mbele) na Maaskofu wengine walikataa kushiriki kikao kilichofanya kazi ya kuandika ujumbe huu.

Mniwie radhi sana nimepata mashaka makubwa sana niliposoma majina ya Maaskofu waliofanya kazi ya kuandika ujumbe huu na historia zao za mahubiri yenye uchochezi mkubwa na hata mara kadhaa wametuhumiwa kwa ukabila na uchochezi na ushahidi upo.

Maaskofu walioandika ujumbe huu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya wa Jimbo Kuu la Dodoma, Mhashamu Askofu Mkuu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi wa Jimbo Kuu la Mwanza, Mhashamu Askofu Augustino Shao wa Jimbo la Zanzibar na Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi wa Jimbo la Rulenge-Ngara.

Maaskofu wengine hawakushiriki kuandika ujumbe huu na kwa kuwa wanatambua dosari iliyokuwa inafanyika wakatoa udhuru mbalimbali na kwa hivyo hao Maaskofu wanne wakaifanya kazi hiyo wakishirikiana na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Padre Raymond Saba na wakamchukua Dk. Kasala kama mshauri wa uandishi wa ujumbe huo.

Kwa kuangalia safu hiyo utaona ujumbe huu umeandikwa pasi kuwepo Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wala Mwadhama Polyacarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Nimepata taarifa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Damian Dallu aliondoka mkutanoni na kuomba udhuru baada ya kubaini mwelekeo wa ujumbe huu.

Hapo ni kujiuliza kwa nini? Na kama kuna yeyote hayaamini haya basi na awaulize viongozi hawa kama walishiriki kuandika ujumbe huo, naamini hata wao wamekwazika na kwa namna yeyote hawawezi kukubaliana na yaliyomo katika ujumbe huu hata kama watakuwa na changamoto ya kuukana hadharani kulingana na utamaduni na nidhamu ya Kanisa.

Ukiangalia Maaskofu watatu kati ya wanne walioandika ujumbe huu wanatoka Mikoa ya ama Arusha ama Kilimanjaro ambako wanasiasa wake ndio wamekuwa wakishikia bango hizo hoja walizoziandika na wao wamekuwa mara kadhaa wakipambana kutumia Ibada na shughuli za Kanisa kueneza siasa hizo.

Askofu Niwemugizi ambaye mpaka sasa ana mgogoro mkubwa na idara ya Uhamiaji kutokana na uraia wake kuwa na mashaka na yeye amekuwa akitaka kujificha kwenye kichaka cha kudai anafuatwafuatwa kwa sababu anawakosoa watawala, anafahamika kwa namna alivyojipambanua kuegemea siasa za upinzani na kuungana na wanaharakati wanaopambana na Serikali.

LAKINI kwa kungalia hizo hoja wanazozitoa kuikosoa Serikali na kutaka kujenga taharuki kwa Watanzania kuwa nchi inakwenda vibaya, mimi nimejiuliza mambo mengi sana.

Maaskofu hawa wanne wanadai shughuli za kiasiasa zimezuiliwa, hivi ni mwanasiasa gani amezuliwa kufanya siasa? Maaskofu hawa wanawasikiliza akina Freeman Mbowe, Godbless Lema, Zitto Kabwe, Tundu Lissu na genge lao linalojumuisha Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu kinachoongozwa na mwanachama wa CHADEMA Dk. Heleni Kijo-Bisimba ambao wanataka shughuli za siasa iwe ni kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya maandamano, fujo na uchochezi?

Wakawaulize wanasiasa hao ni lini wamekatazwa kufanya shughuli za siasa kwenye majimbo yao? Au kwa wao wanafurahishwa na kauli za Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kuwa Watanzania wawe tayari kufa 100 hadi 200 kwa ajili ya yeye kwenda Ikulu? Hawataki hata kumuuliza Freeman Mbowe kwa nini kaatamia uenyekiti wa CHADEMA kwa zaidi ya miaka 20?

Maaskofu hawa wanne wanashutumu kuwa vyombo vya habari vimefungiwa na vingine vimefungiwa kwa muda na hivyo kupunguza uwigo wa wananchi kupata habari, maoni na uhuru wa kujieleza. Hivi Maaskofu hawajui kuwa uhuru huu una mipaka na ni kwa mujibu wa sheria? Maaskofu hawajui vyombo vya habari vilivyofungiwa ni kwa sababu vimevunja sheria? Nimejiuliza sana hivi hata ndani ya Kanisa Katoliki hakuna mipanga ya uhuru wa kujieleza?

Labda niwaulize Maaskofu kama mnahoji hilo, Je Kanisa Katoliki lenyewe limejihoji juu ya hatua lilizomchukua Padre Felician Nkwera? Kwa ambao hawajui Padre huyu alikuwa hodari wa mahubiri na alipendwa sana na waumini akawa tishio ndani ya vigogo wa Kanisa Katoliki, matokeo yake alipigwa fitina hadi Makao Makuu Roma Italia na mwishowe alitengwa na Kanisa.

Padre Privatus Kalugendo vivyo hivyo aliweka msimamo wake na akaamua kuoa ambayo ni haki ya mwanadamu yeyote, matokeo yake alitengwa na akafukuzwa kwa tamko la Papa, ambalo huwa halipingwi.

Padre Titus Mageranga wa Iringa yalimkuta hayo hayo, na hata Askofu Jacob Koda wa Jimbo la Same Kilimanjaro naye yalimkuta hayo hayo.

Mifano ipo mingi, hivi kuna mtu anajiuliza Askofu Mkuu Norbet Wendelin Mtega yupo wapi? Askofu Mahiri kabisa aliyeliongoza Jimbo Kuu Katoliki la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba kule Songea, Ruvuma. Alipigwa fitna akaondolewa kimyakimya mpaka leo haijulikani yupo wapi na Kanisa Katoliki halijatoka kwa waumini kuwaambia alikosa nini na yupo wapi?

Na hili halipo Tanzania tu, huo ndio utamaduni wa Kanisa hili kwamba katika ngazi hizo za vigogo wakubwa, ukienda tofauti na matakwa yao bila kujali una haki au huna haki unafukuzwa, unafichwa Roma ama unawekwa popote duniani ama unapotezwa kabisa maana inakuwa hakuna mawasiliano na nyumbani wala ndugu zako. Wakatoliki wanaujua ukweli huu. Nausema kwa sababu walioanzisha kufukunyua mambo ya kuvuruga nchi ni vizuri wajue kuwa hata wao sio wasafi hivyo na sisi waumini tunajua mengi ila tunaheshimu tu.

Maaskofu hawa wanne wanasema vyombo vya habari vinafungiwa, nimewaza sana na nikakumbuka jinsi viongozi hawa hawa wa Kanisa Katoliki kule nchini Rwanda walipotumia kituo cha redio kueneza chuki miongoni mwa Wanyarwanda na kusababisha mauaji ya halaiki mwaka 1994, ambapo watu takribani Milioni 1 waliuawa kikatili kwa kuchinjwa, kuchomwa moto na kupondwapondwa kwa madai kuwa ni mende.

Kwa wasiojua mauaji ya halaiki ya Rwanda yaliibukia kwenye ukabila lakini fukuto lilianza zamani na miongoni mwa waliokuwa wanatengeneza fukuto hilo ni viongozi wa Kanisa Katoliki ambalo lina mizizi mikubwa nchini Rwanda.

Askofu Rwemugizi ambaye ana mgogoro na idara ya Uhamiaji kwa madai kuwa sio raia wa Tanzania bali nchi jirani anaujua ukweli huu na anajua vizuri madhara ya mchezo anaoufanya, naamini ama anashauku ya kuona tena mauaji yale ama anafanya kwa malengo mahususi.

Maaskofu hawa wanne wanasema Mahakama na Bunge vinaingiliwa, lakini hawajasema ni wapi mihimili hii imeingiliwa.

Kwa ujumbe unaotoka kwa jina la chombo kikubwa kama Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) nilitegemea kusoma mifano na uthibitisho wa kuingiliwa kwa mihimili hii.

Hii ni hatari kubwa sana kutoa tuhuma nzito kama hizo dhidi ya mihimili ya dola halafu ukaacha zinaelea hewani. Watoke tena Maaskofu hawa wanne waseme kwa uwazi na kwa uthibitisho kuwa mihimili hii imeingiliwa hapa na hapa na hapa.

Maaskofu hawa wanne wanasema chaguzi zinafanywa kwa vurugu na zinaacha chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu. Japo kuwa kauli hii imeachwa inaelea lakini kwa namna yoyote Maaskofu wanatuhumu kuwa wanaoshindwa kwenye chaguzi nyingi hapa nchini ambao ni vyama vya upinzani ndio wanaobaki na hasira na chuki.

Hapa Maaskofu wanataka kutuambia kuwa ni Tanzania peke yake ambako wanaoshindwa kwenye uchaguzi ndio wananuna? Hivi kwenye chaguzi za ndani ya CHADEMA wanaokosa huwa hawanuni? Ina maana Maaskofu huwa hawaoni vurugu ambazo hutokea kwenye mataifa mbalimbali wakiwemo jirani zetu wa Kenya hata Taifa kubwa la Marekani ambao wamefanya uchaguzi karibuni? Mimi nilidhani jukumu la maaskofu lingekuwa kuponya kwa imani makovu ya uchaguzi hasa kwa wanaoshindwa na badala yake wanataka hapa Tanzania ndio paonekane pana tatizo kubwa na wanatuma ujumbe wa kuwachochea wananchi waikasirikie Serikali.

HITIMISHO.
Kwa sisi Wakatoliki hiki kilichofanywa na Maaskofu hawa wanne ni lazima kikemewe kwa nguvu zote. Naamini Kanisa linao Maaskofu wazuri, wacha Mungu na wanaotambua umuhimu wa Kanisa katika nchi, wanatambua umuhimu wao katika kuimarisha ustawi wa jamii badala ya kuivuruga.

Na hata katika mahubiri ya leo Jumapili ya Matawi (Machi 25, 2018) tumewasikia Maaskofu na Mapadre wazuri wakihubiri Injili juu ya Mateso ya Yesu na kusulubiwa kwake kwa ajili ya wanadamu. Wanafanya kazi ya Mungu ya kuwajenga waumini kwa imani, kutubu dhambi na kushika njia iliyonyooka, wametufundisha mambo muhimu katika maisha ya ukristo na kamwe viongozi hawa hawawi na mahubiri ya mihemko na siasa zinazoleta chuki na uchochezi.

Tunajenga Taifa la wachapakazi, nchi yetu ipo nyuma sana kimaendeleo, Maaskofu na Mapadre wetu wazuri wanahubiri matumaini, wanawaombea viongozi wa Serikali kuwa watumishi bora, wenye hofu ya Mungu, wanaviombea vyombo vya haki kutenda haki na wanawaombea Watanzania na dunia nzima kupigania amani, upendo, mshikamano na udugu badala ya kushabikia kauli na uchochezi wa kuleta vita, mapigano, malumbano na fitna.

Maaskofu na Mapadre Wakatoliki wazuri wanawahimiza Watanzania kufanya kazi mashambani na makazini ili kujipatia kipato halali kwa kuwa imeandikwa asiyefanya kazi na asile, wanawahimiza Watanzania kutovunja sheria na kuheshimu mamlaka zote badala ya kuchochea watu wakeshe kwenye maandano, malumbano na mapambano na Serikali.

Naamini mtazamo huu sio wa kwangu pekee yangu, naamini wapo Wakatoliki wengi ambao wamechukizwa na sehemu ya ujumbe huu wa Kwaresima ulioandikwa na Maaskofu hawa wanne, nawaomba tusiyumbishwe na hilo, tuendelee kuipenda nchi yetu na kuungana na Serikali hasa wakati huu ambapo kiongozi wa nchi Mhe. Rais Magufuli anafanya mambo makubwa ya kimageuzi katika uchumi, ustawi wa jamii, kutetea wanyonge na kudhibiti wizi wa mali za umma.

Natambua kuwa Baraza la Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) nao wamefanya makosa haya haya yaliyofanywa na TEC, natambua vinara wa kutoa Ujumbe wa Pasaka wa KKKT ni watu wa mlengo gani, natambua kwa nini wamekasirishwa hivyo lakini hili wacha niwaachie waumini wa KKKT wenyewe, mimi nipo na hawa wa kwangu Kanisa Katoliki.

Kwa Maaskofu wote na viongozi wengine wa dini, naomba niseme Tanzania ninayoijua mimi ina watu ambao wapo makini sana hasa linapokuja suala la nchi yao, sisi Watanzania tunapenda amani, tunapenda upendo, sisi ni ndugu sana, hatujazoea vurugu, hatupendi ukabila na ukanda, tunawapenda majirani kama Yesu alivyosema na ndio maana hao wanasiasa walioasisi haya mnayoyasema leo wameshindwa kwenye uwanja wa siasa na sasa wanataka kuwatumia nyie kwenye makanisa.

Ninachokiona kwa kuwa mmesahau kuwa Makanisani kwenu kuna waumini wenye milengo tofauti ya siasa tunakokwenda mtayavuruga Makanisa, kwa Kanisa Katoliki itakuwa ni mtihani mkubwa kwa sababu hakuna utaratibu wa Askofu kupigiwa kura ili aendelee ama asiendelee kama ilivyo kwa Makanisa mengine, kwa hiyo kitakachotokea ni kuendelea kukimbiwa na waumini kama ambavyo mmewapoteza waumini wengi kwenda kwenye makanisa ya Kilokole.

Kwa makanisa yenye uchaguzi wa Maaskofu ninachokiona ni kuendeleza mitafaruku ambayo mpaka leo inazitafuna baadhi ya Dayosisi zenu. Tena huku mlikoingia ndio kubaya zaidi maana sasa vyama vya siasa vitaanza kushindana kuweka Maaskofu wao. Inawezekana msilione hili lakini mkae mkijua kuwa litakapofika hapo hamtaweza kulidhibiti.

CHADEMA walipoanzisha kumchukua Mwana CCM Lazaro Nyalandu walidhani CCM watakaa kimya, walichokipata na wanachoendelea kukipata wote mnaona. Sasa na nyinyi mmeamua kuingia kwenye siasa za kushabikia hoja za CHADEMA na kutumwa na CHADEMA kuichokonoa Serikali ya CCM, mjiangalie siku CCM nao wakiingia huko Makanisani kwenu mjue shughuli itakuwa pevu.

Nawaombeni msituharibie Kanisa. Acheni Makanisa yafanye kazi yake ya kuhubiri Injili, siasa waachieni wanasiasa, harakati waachieni wanaharakati na vita waachieni wanajeshi. Polycarp Mdemu soma na hii hapa uone ukweli ulivyo,na Pengo kwenye ujumbe wa wito vijana Bagamoyo amekataa hilo.

Julius Kindonga
Mkazi wa Dodoma
Machi 25, 2018
 
Ameandika Padre Titus Amigu

*VIONGOZI WA DINI KUINGIA WOGA HATA KUSEMA UONGO*.

Dini hazijaanza jana, wala siasa hazijaanza jana. Kwa Wakristo Wakatoliki, kwa woga, watu wanafuja vipaimara vyao na sakramenti ya Daraja inayowafanya wawe makuhani, manabii na wafalme hapa ulimwenguni. Hao wanapatwa na woga kiasi hiki wanasema uongo wa kwamba dini haipaswi kuhusiana na siasa.
Ni uongo kabisa kwani hata Pasaka yenyewe, tunayoisherehekea kila mwaka, ni matunda ya mwingiliano wa dini na siasa. Wayahudi wanaokolewa kutoka katika mikono ya Farao (mwanasiasa). Musa alikuwa mtu wa dini lakini alipambana na Farao, mwanasiasa. Kumbe, kudai dini isihusiane na dini siyo tu woga unaowashika viongozi wa dini isipokuwa ni pia ishara ya kutoyajua Maandiko. Tangu mwanzo wa Biblia hata mwisho wake, watu wa dini walihusiana na wanasiasa. Abrahamu alihusiana na Melkizedeki, mfalme. Tena alihusiana na Farao kule Misri hata akalazimika kusema uongo wa kwamba Sara si mkewe akiogopa kuuawa. Yusufu alihusiana kisiasa na Farao sawia na Putifa na mkewe.
Musa ndiyo tusiseme alihusiana na Farao. Mapigo kumi dhidi ya Wamisri shauri lenyewe lilikuwa siasa, utumwa. Na tunajua pigo la kumi na mbili, kuuawa kwa wazaliwa wa kwanza wa wanyama na wanadamu wa Wamisri ndilo lililo asili ya sikukuu ya Pasaka. Tupo pamoja?
Naomba niendelee na mifano. Samweli alihusiana na wanasiasa Sauli na Daudi. Elisha alihusiana na akina Ahabu na Jezebeli. Isaya alihusiana na akina Sairusi. Yeremia alihusiana na siasa za wafalme wengi hata akatupwa katika shimo la simba. Danieli na wenzake walihusiana na akina Nebukadreza na Belshaza. Manabii wote walihusiana na wafalme ama wakiwaunga mkono na kuwashauri au kuwaonya na kuwasahihisha. Yohane Mbatizaji alimkanya mwanasiasa Herodi Antipasi akalipia kwa shingo lake. Yesu mwenyewe alihusiana na wanasiasa kama akina Herode na Pilato. Mbona tunakumbuka kwamba Yesu alihukumiwa na Pilato,
Hatimaye, mitume nao walihusiana na wanasiasa, wengine wakali sana wakawatoa roho zao. Hata kitabu cha mwisho cha Biblia (ndiyo Ufunuo) ni mahusiano kati ya Dola ya Rumi na Wakristo. Makaisari walikuwa wanasiasa. Kaisari Konstantino aliyelisaidia Kanisa kupata nafuu ya madhulumu alikuwa mwanasiasa. Je, hatumsifu kwa kuwa mtu mwema?
Baada ya mitume, watakatifu mbalimbali walihusiana pia na wanasiasa kwa kuwaunga mkono au kuwakanya. Akina Thomas More na John Fisher walipotezaje maisha yao? Maximilian Kolbe alikufa katika muktadha gani? Kwa nini Baba watakatifu walioishi wakati wa biashara ya utumwa na hata wakati wa mauaji ya kimbari yaliyoendeshwa na Adolf Hilter dhidi ya Wayahudi wanalaumiwa kwa kutokuwa na misimamo ya kuwatetea wanyonge?
Si hivyo tu, historia ya Kanisa imejaa hati zinazohusika na mambo ya siasa. Rerum Novarum ina muktadha upi? Gadium et Spes ina muktadha gani, kwa nini tuseme Kanisa Ulimwenguni? Ulimwengu wa wapi wanaoishi wanadini peke yao pasipo dola, nchi na mataifa? Sasa inakuwaje ajabu au haramu kwetu sisi tunaoishi katika karne hii kujihusisha kwa namna yake na siasa?
Tusijipinge wenyewe. Kwa nini kila tunaposali sala za waumini tunaiombea serikali na viongozi wao? Tunawaombeaje ikiwa mambo yao hayatuhusu? Lakini ukweli ni huu. Tunaishi katika ulimwengu mmoja na wanasiasa. Ni katika ulimwengu huo huo tunamoaswa kufanya utume. Yesu Kristo hajawapa Wakristo ulimwengu wao peke yao (Yn 16:33).
Kama ndivyo, tutawezaje kuzungumzia mambo ya haki, amani na upatanisho pasipo kuwagusa wanasiasa na watawala ambao ndio wenye vyombo vinavyohusika na hayo? Anawezaje mwanadini kuzungumzia haki bila kuigusa nchi na watawala wake? Anawezaje mwanadini kuzungumzia haki na amani pasipo kuwagusa polisi na mahakimu?
Nadhani kama Wakristo wasingelikuwa raia wa nchi za ulimwengu huu na wanasiasa wasingelikuwa waamini wa dini za ulimwengu huu, dini na siasa vingeliweza kutenganishwa vizuri kabisa. Lakini kama waamini tusingelikuwa raia tusingelilipa kodi na wala tusingelishiriki chaguzi zozote na wanasiasa nao wasingelikuwa waamini tusingeliwatazamia waje kusali wala kushika amri yoyote ya Mungu. Kumbe basi, woga wetu usitufanye tuseme uongo wa kutaka dini na siasa visigusane, tunamuumiza sana Yesu aliyekuwa jasiri namba moja.
Ukweli ni kwamba wanadini siasa inatuhusu na wanasiasa dini inawahusu. Nani aliyesema mwanadini hawezi kuwa mwanasiasa na mwanasiasa hawezi kuwa mwanadini? Tusipotoshe mambo kwa woga wetu. Kumbe, kinachohitajika ni busara na kujali uwiano wa kusifiana, kuhimizana, kujadiliana na kuonyana ili wote tusiukose uzima wa milele. La sivyo, waamini na viongozi wao wasiseme wanashiriki ofisi za unabii na ufalme za Yesu Kristo!
Aidha, kukutana dini na siasa si ajabu. Kama tumetumwa ulimwenguni tukawafanye watu wote wanafunzi wa Yesu tusistaajabu kukutana na wafanyabiashara, wanasiasa, wema na wabaya. Acha nikumbuke wimbo wa zamani. Ni hivi kila mwamini, kwa sababu ya utume wake wa kimisionari ambao kwao anatakiwa kukutana na watu wote, anapaswa kujiimbisha wimbo wa zamani wa “Wote ni abiria wangu”, maana yake wanasiasa na siasa zao wamo kati ya abiria wake.*

*Ndimi mzee wenu Pd. Titus Amigu.*
 
Huu waraka ni msimamo wa kanisa.Hata kama Pengo hakuweko wakati ukiandikwa, kama maaskofu 34 waliobaki wameuafiki, uwepo wa Pengo usingeubadili waraka huu. Inawezekana wapo maaskofu wengine ambao hawauafiki 100% lakini wengi wameuafiki ndio maana umekua msimamo wa kanisa.

Mambo mengine ni bora kukaa kimya.
 
Ulishawahi kujiuliza kwa nini CATHOLIC wana IDARA YA PROPANGANDA?!

PROPANGANDA ni SIASA.

Unafahamu CATHOLIC huiishi na kuamua SIASA za eneo husika kwamba hivi ndivyo siasa ya nchi iendeshwe?

Kwa taarifa yako IDARA YA PROPANGANDA ya CATHOLIC ndicho chombo cha juu ktk eneo husika CHENYE KUFANYA TAFITI/UPELELEZI na kuamua SIASA za eneo husika.

Chombo hicho hupambania kanisa kwa nguvu na akili nyingi ili tu lidumu kuwa hai.

Hao ndiyo huelekeza kipi na wapi kifanyike kwa wakati husika. IDARA hiyo ndicho chombo pekee ktk baraza chenye kuwasiliana moja kwa moja VATICAN!

ILIMUELEWA KARDINALI?

Jipe maswali,je ni kweli kanisa linaweza kutoa waraka bila yeye tena Askofu mkuu wa moja ya majimbo makuu hapa nchini kuelewa?!MCHEZO!

Sasa ktk msafara wa MAMBA kenge HUWEPO.Mwisho kenge huingizwa KINGI!

Jamani hao watu wanaposema HILO NI FUMBO LA IMANI MSIFIKIRI ni WAJINGA!
 
Back
Top Bottom