WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

Ngoja tuone kama watatumiwa TRA maana katoliki wana miradi mingi
Sidhani kama Serikali itakuwa na haraka sana kuanza ligi na Kanisa Katoliki. ni kitu kimoja kumhoji uraia Askofu NiweMugizi, au kukagua mpaka nguo za ndani za mke wa Askofu Kakobe, lakini ni kitu kingine kabisa kuanzisha ligi na Kanisa Katoliki lenyewe.
 
Hii ina afya
Ujumbe uwawashe sawasawa wale wote wanaokiuka haki za binadamu na watanzania kwaujumla
 
Hiki kifungu kwenye waraka wa hawa jamaa kina mantiki; "Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambamba na kuminya uhuru wa Mahakama na Bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya kikatiba.” Ni kweli kwamba wabunge wamezuiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yao? Hii inadhihirisha kwamba hawa watu hawajui kinachoendelea na badala yake wameandika kile walichoambiwa na hao waliotaka habari hii iandikwe kwa namna ya kizushi na sio kiuahalisisa!
 
Mmenikosha maaskofu wangu. Nadhani Maaskofu wa DRC wamewapa somo. Sasa naahidi kuongeza mchango wa Tegemeza Jimbo kwa mwaka huu mpaka laki moja. Nilishaacha kuchangia kabisa kwa sababu ya Pengo!

Mkuu,

usiache kuchangia kanisa kwa ajili ya Pengo na D'Salaam yake. Wakikuudhi changia jimbo lolote achana na D'Salaam ya Pengo.

By the way Pengo ataondoka na kuiacha D'Salaam kwa askofu mwingine anayekidhi kama tatizo la Rulenge lilivyodhibitiwa kwa kumleta NiweMugizi kuisambaratisha Jumuiya ya Mshikamano.
 
Uongozi wa nchi yetu hauna utaratibu wa kujibu waraka.Ingekuwa hivyo ingebidi kuwe na mtu maalum wa kujibu nyaraka za kanisa maana ni nyingi mno na ni za kila wakati.Wametoa mawazo yao tunawadhukuru lakini nchi inasonga mbele kwa taratibu za kinchi na sio za kanisa.Kanisani tuonane hukohuko na ni lazima tuje kusali kwani tuna muhitaji Mungu vilevile.

Kaulize tawala ziliaoznguka huko ulaya kwa wazo kama hilo ndipo ujue nguvu ya kanisa katika taratibu za nchi.
 
Kuna kipi kipya katika Waraka huo na hasa katika maeneo hayo ya siasa, uhuru wa vyombo vya habati na uchumi? Si ni hayo hayo raia wamekuwa wakiyapigia kelele na watawala wakiweka pamba masikioni ikifikia viongozi kadhaa kutunga sheria kwa maagizo ya majukwaani! Labda kwa vile Kanisa Katoliki Tanzania limesema tutaona mabadiliko
 
Masemaji wa kanisa ni Papa.
Na papa Ana balozi wake hapa......
Huo waraka siyo kauli ya kanisa.....ni mawazo tu ya maaskofu kama watz wengine......

Hata mimi ni msemaji wa kanisa maadamu nilipata sakramenti ya kipaimara na nina uwezo wa kuhubiri katekism ya kanisa mradi nisiipotoshe.
 
Kwa akili ndogo za Chuttle-man, badala ya kufuata ushauri ataanza kuwatisha.

Huyu MTU hata akitubu ni kazi bure
 
Wakatoliki wenzangu, tuwe makini tunapoeleza complicated issues la sivyo hatutaeleweka. Ukisema kwamba ule waraka wa askofu Paul Ruzoka hauna nguvu kwa sababu ni askofu mmoja basi unamaanaisha kwamba una nguvu kwenye jimbo lake yaani Tabora tu.

Kifupi ni kwamba Pengo alichemka kipindi kile na alikiri uzembe wake wa kutousoma. Ikumbukwe TEC waliombwa maoni ya TEC ili yaende kwenye Tume ya Warioba.

Kamati ya askofu Paul Ruzoka imepewa mamlaka na TEC kupeleka na ndiyo yaliyokweda kwa Warioba na siyo askofu mmoja wa jimbo moja linaitwa D'Salaam.

Tukiri tu kwamba Pengo alipotoka.

Ilikuwa Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu, chini ya Askofu Mkuu Paulo Ruzoka. Ni kweli Rais wa TEC ndiye msemaji wa Kanisa Katoliki Tanzania. ndiyo maana siyo rahisi Kardinali Pengo kuukana waraka huu. itamletea matatizo makubwa sana.

Ipo tofauti. Zile Nyaraka za 2010 za Kanisa Katoliki kama kaulimbiu ya kuwaandaa waumini kwa uchaguzi mkuu, na hata ule wa karibuni zaidi ambao Kardinali Pengo aliukana, zilitolewa na kamati za Baraza la Maaskofu. tofauti ni kwamba ile inakuwa imeidhinishwa na askofu mhusika wa kamati. hapo utaona jina la Askofu mmoja tu ambaye ndiye mkuu wa Kamati husika. na pia Waraka unakuwa na nguvu ya kushauri tu, si wa kimamlaka kwa nchi nzima. ndio maana Pengo aliukana bila kuwa na wasiwasi.

Huu wa sasa umetolewa na Baraza lenyewe la Maaskofu na wameusaini Maaskofu wote wa nchi nzima. hapo sasa waraka huu una nguvu za kutumika kama nyenzo ya uinjilishaji kwa taifa zima. Ni kauli rasmi ya Kanisa Katoliki Tanzania na Maaskofu wote kwa kweli wanalazimika kuuheshimu. Ni tofauti kubwa sana na Historia imeandikwa.
 
Nadhani umenipa ushauri mzuri. Ila tu kwenye jumuiya sasa wanajua kabisa una uwezo na huchangii michango km hiyo hawatakuelewa! Ni shida!
Mkuu,

usiache kuchangia kanisa kwa ajili ya Pengo na D'Salaam yake. Wakikuudhi changia jimbo lolote achana na D'Salaam ya Pengo.

By the way Pengo ataondoka na kuiacha D'Salaam kwa askofu mwingine anayekidhi kama tatizo la Rulenge lilivyodhibitiwa kwa kumleta NiweMugizi kuisambaratisha Jumuiya ya Mshikamano.[/QUO
 
Hiki kifungu kwenye waraka wa hawa jamaa kina mantiki; "Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambamba na kuminya uhuru wa Mahakama na Bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya kikatiba.” Ni kweli kwamba wabunge wamezuiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yao? Hii inadhihirisha kwamba hawa watu hawajui kinachoendelea na badala yake wameandika kile walichoambiwa na hao waliotaka habari hii iandikwe kwa namna ya kizushi na sio kiuahalisisa!
Unajuwa Sugu amewekwa jela kwa kesi bailable kwa tuhuma gani?

Kama unawashwa sema tukukabidhi kwa Alhad ana Vaseline ya kutosha.
 
Back
Top Bottom