Shigongo acha unafiki,unajifanya kukasirishwa na zecomedy kumsema mashaka matongo kuwa kafirisika?kwa wasiojua ni kwamba ERIC JAMES SHIGONGO ndio aliochangia mashaka matongo kufirisika kwani alinunua gazeti la AMANI ambalo lilikuwa linatolewa na kampuni ya mashaka matongo(hapa ni kwamba,eric baada ya kuona kuwa mashaka matongo ndie mpinzani wake mkubwa wa biashara za magazeti ya udaku na gazeti alilokuwa analitoa mashaka la AMANI linauzwa sana akaamua kumzunguka mashaka kwa kwenda kwa mmiliki wa gazeti na kumlaghai kisha kulinunua,kwani mashaka alikuwa anatumia jina la AMANI kwa mkataba baada ya mmiliki kushindwa kuliendesha na mashaka ndio aliolipandisha chati AMANI na likawa linanunuliwa sana,pia haikuishia hapo kwani shigongo akamlaghai kwa vijisenti mpiga picha aliyekuwa anaongoza kwa kupiga picha za udaku aitwae issa mnally hivyo issa akaamia kwa shigongo),kuanzia hapo mashaka matongo akaanza kuyumba kibiashara na mwishowi kufunga biashara,akakosa pesa ya kulipa nyumba aliyokuwa amepanga sinza akarudi kwenye nyumba yake ya yombo.
kwa wasiomjua shigongo watakuwa wanawaona zecomedy wana dhambi kwa jinsi shigongo alivyoandika huo waraka lakini nataka kuwaambia kuwa huyu jamaa(shigongo) ndio zake kuandika waraka pindi anapotofautiana na watu hasa wasaniii,keshawaandikia waraka wasanii kibao mmojawapo ni solothang mara baada ya solothang kutoa wimbo wa KILIO CHANGU,akimpaka shigongo na shindano lake la mkali wa hiphop,hivyo hiyo ndio style yake
shigongo katika waraka wake ameongelea kuhusu kumtoa dudubaya aliyekuwa anakaribia kufungwa,nataka kuwaakikishia wanajf kuwa shigongo alifanya hivyo kwa sababu na sio kama ni huruma ndio iliyomfanya kwenda kumtoa dudubaya,waswahili wanasema adui wa adui yako ni rafiki yako,hivyo hapa ilikuwa hivi,Shigongo na clouds hawapatani kitambo(sijui kwa sasa),clouds waliandaa show ya mr nice ambae alikuwa adui ya dudubaya na siku ya show dudubaya akamvamia mr nice kwenye stage hivyo clouds wakaapa kumfunga dudubaya,hapo ndipo shigongo kwa kuwa yeye na clouds ni maadui akaamua kujiingiza kwenye hio kesi na kumtoa dudubaya.
huyu ndio shigongo ambaye anajifanya na kujionesha kwa watu kuwa yeye ni msafi na mwenye moyo wa huruma kumbe ni mnafiki na anayependa kuchonganisha na kuchochea mambo kwa manufaa ya magazeti yake ya udaku