Bandari ipo pale pale kama ilivyokusudiwa na QUEEN kwa kuwa tayari vyombo vyote viliombwa kutoa ridhaa wamekubali bandari ipewe kwa mwekezaji DP World. Vyombo hivyo ni wananchi kupitia bunge na serikali kupitia rais. Hao wananchi wa sasa walikuwa wapi wakati walipoambiwa waende dodoma kutoa maoni? Hakuna katika hao wa TEC ambae alienda bungeni kati ya wale wananchi 72. Wakenya wanatumia TEC kufifisha na kisa kukwamisha juhudi za makusudi za serikali za kuwatoa watanzania ktk dimbwi la umasikini.
TAHADHARI KWA BUNGE
Mimi kama mtanzania wa kawaida naiomba serikali kuepushia mbali aibu itakayoipata bunge ikiwa TEC watasikilizwa kwani kazi ya kushauri,kupendekeza na kukubari au kukataa mkataba ilikuwa ni ya bunge.
Bunge naliomba kuazimia kutobariki tena mkata wa aina yoyote ikiwa bandari haitaenda kwa mwekezaji dpw.
Nahitimisha kwa kulitaka kanisa kupitia TEC waombe msamaha kwa wabunge na serikali.
Kwa serikali naomba hayo makanisa yakaripoti kwa msajili dini kwa kosa la kukusanya taarifa.