Waraka wa TEC umesomwa kwenye Jumuia yangu ya Mt. Marcelino. Tunawashukuru Maaskofu. Kesho utasomwa vigangoni na Parokiani Mt. Antoni wa Padua

Waraka wa TEC umesomwa kwenye Jumuia yangu ya Mt. Marcelino. Tunawashukuru Maaskofu. Kesho utasomwa vigangoni na Parokiani Mt. Antoni wa Padua

Leo Mambo yamependeza sana, Waraka wa TEC unaofafanua Mkataba wa Bandari za Tanzania na DPW ya Dubai wenye ujumbe mwanana wa Sauti ya Watu ni Sauti ya Mungu.
Yaliyojitokeza ni waumini kuuelewa na kuukubali. Pembezoni nimeteta na Mh. Mbunge wa Jimbo letu, Ni muumini wa Jumia hii, kwa ufupi anasema waraka huu na yeye na wengine umewapa amani, wamepata pa kushikia, Nafsi zao zilisongwa sana kwenye vikao ndani ya chama. lakini sasa wametua mzigo. Wanasubiri kama utarudi bungeni au utatupwa kapuni. Niliyyapata kwa waumini mchanganyiko, akina mama, wazee wa familia, wafanya biashara na mmoja mtu muhimu serikalini.
1. Wao kama WAKATOLIKI na Watanzania wako tayari kuulinda, kuutetea Waraka huu hata kama ni kimyakimya.
2. Serikali sasa iwe makini sana, kumbuka dini haina mipaka eneo la kazi, tumechanganyana humo, wako wabunge, mahakimu, mapolisi, wanajeshi, wakulima, walimu, madaktari, wafanyakazi bandarini, yaani popote na kwa kawaida WUMINI HUWA HATUPINGI MAELEKEZO YA KIROHO, KWA SASA KUTOKUBALIANA NA MKATABA WA BANDARI NI SUALA LA KIROHO.
3. Ujumbe huu ukiwa na hoja muhimu ni vema zijibiwe kwa uwazi na weledi, halafu waumini na viongozi wetu kiroho tukiyaelewa majibu yenu Spika, Rais, Prof. Mbarawa tutarudi kwa waumini kuwaambia mmeeleweka .

Asanteni kwa Sasa. Kesho nitahudhuria misa ya Kwanza, Asanteni Maaskofu.
Ohooooo
 
Hatuvai kobazi, tunavaa viatu kama kawaida.
Karibu kanisani, usiabudu sanamu
Ntakuja na nyama yangu ya nguruwe niwe inajitafunia taratibu wakati na sikiliza mahubiri ya makasiriko ya wavaa kubazi
 
Ntakuja na nyama yangu ya nguruwe niwe inajitafunia taratibu wakati na sikiliza mahubiri ya makasiriko ya wavaa kubazi
Hutakatazwa maana hatupambani na mtu, hiyo ni kazi ya Mungu atajitetea
 
Mama anaendeleza kuwapa vidonda vya tumbo na magonjwa ya moyo:



Kwenye mioyo yao kuna maradhi na atawazidishia Allah maradhi.

Aamiin .
 
Moja ya kanuni ya Wakatoliki ni utii kwa mamlaka ya Kanisa...kwa hiyo hilo tamko la TEC ni msimamo was Wakatoliki Tanzania nzima...na Sina shaka Papa kule Vatican ameshajulishwa kabla ya waraka/tamko kutoka....

Mizizi ya Wakatoliki imejikita ndani ya jamii mijini na vijijjnii....dah serikali kazi wanayo kwa hili...
Kuna wanasiasa miongoni mwa hao viongozi wetu, kuna mwana CHADEMA mmoja anaitwa padre Kitina, anaongea kiungwana kabisa kumbe ana ajenda zake za kisiasa.
 
Huu waraka ni Zaid ya mkutano wa hadhara, huu waraka ni Zaid ya mechi ya Simba na Yanga, huu waraka unafanya mwanamke mzanzibar ashindwe Kula na kunywa.
 
Ni uoga wa waarabu unaosumbua viongozi wetu wa kanisa. Wanasahau kuwa waarabu ni wamiliki tu wa biashara nzima lakini watendaji wote huku chini ni watu wa mataifa mengine.

Ni sawa na Man City, wamiliki ni waarabu wenyewe lakini makocha na wataalam wengine wote ni watu wa mataifa mengine.

Tatizo kubwa la Tanzania ujuaji ni mwingi sana, mtanzania wa kawaida anajua kila kitu, kocha ni yeye, daktari wa timu ni yeye, mtaalam wa misuli ni yeye, profesa wa sheria ni yeye yaani tunajua kila kitu.
 
Back
Top Bottom