Waraka wa TEC wajadiliwa TV IMAAN
Mosi: Mkuu; nakubalana na utaratibu uliopendekeza.

Ni hatua njema ambapo Kwa maelezo haya bIla shaka tunakubaliana pasipo na shaka kuwa:

1. Niliandika uzi ukiwanukuu masheikh wa kiislam na makasiriko yao ya haja, dhidi ya waraka wa TEC.
2. Uzi wangu huo #1 hapo juu uliunganishwa kwenye uzi huu unaoendelea ambapo ukawa comment na kujibiwa na bwana ileje, naye kama comment.
3. Majibu ya ileje kwa namma ya maswali ninayaweka tena hapa kama rejea yako rahisi:

IMG_20230823_120842~2.jpg


4. Nami kuyaona maswali hayo nikakuribisha wewe ndugu yangu wa thamani hapa tuwasaidie masheikh na waislam hawa kutoa majibu ya kistaarabu kwa ndugu ileje na sote wenye maswali kama yake.

Pili: Kwa kuwa swali la kwanza nimelijadili kwa kina, naomba nijikite na maswali mawili yaliyobakia.

Waraka sikuusoma, kwani nilimsikiliza askofu aliyewasilsha. Sikuusoma kwasababu niliamini askofu anawasilisha waraka na hivyo hatoi maneno yake. Ikiwa ni hivyo, sikumsikia askofu akitaja waislamu. Si hilo tu, sikumsikia askofu akikejeli, kutukana wala kusema au kushawishi kuundoa uongozi uliopo. Sasa kinachonishangaza ni kuingizwa waumini wa dini; na hili, kwa maoni yangu, halikustahili.

Hapa naona nifululize na namba zangu Kwa urahisi wa rejea:

5. Kwa maneno yako umejirifhisha kuwa waraka wa TEC hauna cha kufanya na masheikh wala waislam.

Hivyo ni kauli yako Kwa swali #2 la ileje kuwa hawatajwi popote masheikh wala waislam kwenye waraka wa TEC.

Ama kuhusu swali la je DPW ni uislamu, mimi ninavyojua hiyo ni taasisi au shirika la serikali linaloshughulika na bandari na ambalo lipo Dubai. Imesadifu kuwa Dubai ni nchi/eneo linalo/inayokaliwa na Waislamu walio wengi, na hivyo halna uhusiano na dini kwani si shirika la dini wala di taasisi ya dini, na hapa napo linakuja tena swali, kwanini lihusishwe na dini.

Hapa napo niendelee na mfululizo wa namba zangu:

6. Kwa maelezo yako hapa ninakusoma kuwa DPW siyo uislam wala haina cha kufanya na masheikh wala waislam kokote duniani ikiwamo Tanzania.

Baada ya maoni hayo, huenda angalau nitakuwa nimejadili na pengine kujibu yale maswali matatu. Karibu sana Mkuu.

Sasa niombe kuyaweka maswali ya Ileje na majibu yako pamoja:

a)Atueleze waislam mnanufaika vipi na mkataba baina ya Tanzania na Dubai?

[Hili ungali hujajibu]

b) Je kuna mahali waraka wa maaskofu umewataja waislamu?

[Hapa jibu lako ni hapana]

Rejea majibu yako kutokea kwenye udadavuzi wangu #5 kutokea kwenye majibu yako hapo juu.

c) Je DPW ni uislamu?

[Hapa jibu lako ni hapana]

Rejea udadavuzi wangu #6 kutokea kwenye majibu yako hapo juu.

Hitimisho:

Maswali yote ya ileje likiwamo la kwanza ambalo hadi sasa hujalijibu chimbuko lake ni katika maelezo yangu #1 na #2. Kwamba niliandika uzi uliunganishwa kuwa comment ukiwa na captions hIi:



Asili ya swali la ileje ni kulikoni masheikh au waislam hawa wasiokuwa DPW au watajwa kwenye waraka wa TEC kuchafukwa hivi?

Sisi, yaani Mimi, Ileje na wenzetu wengi hatuwaelewi. Na wewe tunakukaribisha kutowaelewa au kutuelimisha sisi kuwaelewa.

Hadi hapa wenye kushangaa hili jambo kuhusishwa na uislamu au masheikh si wewe. Bali ni ileje, Mimi na wengine.

Wewe hapa ni kutoa majibu labda kama ungependa kuungana nasi kuwashangaa masheikh hawa.

Ni hayo tu ndugu mjumbe.
 
Waislamu someni aisee kila sehemu mnatia aibu KWA kutokusoma kwenu halafu eti kipindi kinaitwa (tunakujuza usiyoyajua) yani mjue nyie utopolo mtupu kichwani wasijue kina lissu slaa shivji na PhD kibao zilizojaa TEC achilia mbali washauri wa kitaalamu wa kikatoliki waliojaa serikalini kibao wanaotoa taarifa TEc tena za uhakika.
 
Sasa niombe kuyaweka maswali ya @Ileje na majibu yako pamoja:
Asante, Nami sasa nianze japo kwa muhtasari kuzungumza na nitaanza na pale kwenye maswali ya Ileje na majibu yangu.

a) Sheikh, angekuwa ndo miye, jibu ni kwamba hakuna Mtanzania yeyote - mwislamu, mkristo au mpagani anayefaidika na mkataba kati ya Tanzania na Dubai. Hakuna pia anayekosa. Sababu ni kuwa huo mkataba haujatekelezwa. Hivi pilipili usoila yakuwashia nini?

b) Ni kweli waraka haukuwataja waislamu. Sasa ajabu ni kutokea mtu akauliza waslamu wanavyofaidika nao. Kulikoni na waislamu?

c) DP na uislamu: Ndivyo ilivyo na umenielewa. Baada ya yote haya, kwanini bado uislamu na waislamu imekuwa ndo wanyoshewe vidole kwa mkataba huo?

Ni dhahiri, kwa maoni yangu, yanafanywa haya ili kuendeleza yale yanayosemwa ya madrasa kwa kuchukua mambo ya kuambiwa bila kuyafanyia upembuzi. Hii huenda siku moja ikawumbua watu.
 
Waislamu someni aisee kila sehemu mnatia aibu KWA kutokusoma kwenu halafu eti kipindi kinaitwa (tunakujuza usiyoyajua) yani mjue nyie utopolo mtupu kichwani wasijue kina lissu slaa shivji na PhD kibao zilizojaa TEC achilia mbali washauri wa kitaalamu wa kikatoliki waliojaa serikalini kibao wanaotoa taarifa TEc tena za uhakika.
Haya ndo yaleyale. Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza. Nawe umesoma? Kama umesoma umesoma wapi na umesoma nini?

Ikitokea ukawa umesoma, basi elimu siku hizi haimfaidii aliyesoma.

cc: brazaj
 
a) Sheikh, angekuwa ndo miye, jibu ni kwamba hakuna Mtanzania yeyote - mwislamu, mkristo au mpagani anayefaidika na mkataba kati ya Tanzania na Dubai.

Unajua swali hili ni kutokana na maelezo yao kuwahusu wao wenyewe kama masheikh, kwa niaba ya waislam na DPW kama yalivyo hapa chini?





Huoni jibu lako unalolisema hilo ndilo lililo jibu kamili sasa, la TEC na pasipokuwa na shaka yoyote?

Labda unachanganya TEC na hawa masheikh wenu, ndugu?

Hakuna pia anayekosa. Sababu ni kuwa huo mkataba haujatekelezwa. Hivi pilipili usoila yakuwashia nini?

Nilikujibu mapema hapa mkataba kunufaika au kutonufaika ni shuruti kujulikana kabla ya utekelezaji.

Manufaa huwepo kwenye vifungu vya mkataba. Mikataba ni suala la kitaalamu. Mikataba Siyo trial and error.

"Vinginevyo kulikoni kuuingia mkataba usiokuwa na manufaa?"

Nilikupa angalizo mkataba huu ukishafungwa unasemekana kutokuwa na ukomo.

b) Ni kweli waraka haukuwataja waislamu. Sasa ajabu ni kutokea mtu akauliza waslamu wanavyofaidika nao. Kulikoni na waislamu?

Kwamba hujui asili ya kuulizwa swali hilo?

Kunaulizwa waislam kunufaika kutokana na kushupaa kwa masheikh wao na DPW kana kwamba wao ni DPW au wana maslahi nao au ni wanufaika wa mkataba.

Haya yakiendelea waislam wenyewe tukiwa kimyaaa!

Zingatia wanalaumiwa wote wanaojifungananisha na DPW au mkataba huu akiwamo Mzee wa Upako hadi Phillip Mpango, mkatoliki kindaki ndaki, nk!

Isingekuwa kwa maneno ya masheikh hawa na kimya cha wafuasi wao nani angehoji ni kwa nini wanajinasibisha na mkataba huu hivi?

Au labda wewe huoni hivyo ndugu yangu?

c) DP na uislamu: Ndivyo ilivyo na umenielewa. Baada ya yote haya, kwanini bado uislamu na waislamu imekuwa ndo wanyoshewe vidole kwa mkataba huo?

Zingatia hawalaumiwi waislam wala uislam. Wanalaumiwa masheikh hawa na wafuasi wao kwa kuuhisha uislam huku waislam tukiwa kimya.

Kwa hakika ni jukumu letu sisi waislam kuwakana masheikh uchwara hawa bIla kuwasahau wafuasi wao.

Ninaamini kauli ya mzee kikwette (mwislamu) kutokuchanganya dini na siasa iliwalenga watu hawa (Siyo TEC). Ila kama kawaida wabaya wetu kama ilivyo siku zote (wale wenye kuukaanga mbuyu) wakapita nayo.

Wangelaumiwa baniyani kama wangehusishwa na viongozi wao hivi, nao wakatulia tuli!

Hujamwona yaliyomkuta wa upako na wakristo? Aliko sasa hivi anapumulia mashine.

Ni dhahiri, kwa maoni yangu, yanafanywa haya ili kuendeleza yale yanayosemwa ya madrasa kwa kuchukua mambo ya kuambiwa bila kuyafanyia upembuzi. Hii huenda siku moja ikawumbua watu.

Hakuna mtu aliye na tatizo na mwislamu au uislam. Kwani wewe unaijua dini yangu, Ileje, Prof. Shivji na wengi tu wa wasiokubaliana na masheikh hawa? Ila ni kweli kuwa kilichopo, waislam wakikaa kimya bIla kuwakemea masheikh uchwara hawa au wafuasi wao, unategemea nini ndugu kutoka kwa wengine au wale wabaya wetu?

Hivi unaelewa tunaowashangaa ni masheikh na wafuasi wao kwa ajili ya misimamo ya viongozi wao hii, ambayo aghakabu hatujaona waislam wakiikana hadharani kama waislamu?

Hapa nikuulize swali binafsi sasa:

Wewe unakubaliana na misimamo ya masheikh hawa?

Jibu lako litakuwa muhimu sana kuijua nia yako kwenye majadiliano haya nikiamini kuwa ni ya dhati ya moyo ya watu waungwana yenye kutegemewa yawe yenye tija.
 
TEC sio taasisi ya msengemnenge kama zingine,tamko lake lazima litikise na litakuwa na impact kuanzia mkataba wenyewe mpaka uchaguzi 2025
Halafu wala hawajibu mashambulizi wametulia kimyaaaa wanaendelea na sakramenti ya kipaimara
 
Huoni jibu lako unalolisema hilo ndilo lililo jibu kamili sasa, la TEC na pasipokuwa na shaka yoyote?
Ni kweli kabisa.
Labda unachanganya TEC na hawa masheikh wenu, ndugu?
Hapa kwanza nikuulize, wewe ni akina nani? mkristo au mpagani? Nauliza hivi kwa hii kauli yako ya kutumia neno 'wenu' ili nami nijue namna ya kujadilana nawe. Mihemko haitatusaidia mimi na wewe.
Vinginevyo kulikoni kuuingia mkataba usiokuwa na manufaa?"

Nilikupa angalizo mkataba huu ukishafungwa unasemekana kutokuwa na ukomo.
Sasa naona huenda hatujafahamiana. Mimi nimesema kwa Kuwa mkataba haujatekelezwa hauna manufaa. Utamuulizaje mtu huyu mwanao aliyetumboni, bado hajaja duniani unanufaika naye vipi? Halafu utarajie jibu gani?

Kulikoni kuuingia mkataba usio na manufaa au wenye manufaa. Wewe ukiona hauna manfaa, mwingine anaona unayo manufaa.
Kwamba hujui asili ya kuulizwa swali hilo?

Kunaulizwa waislam kunufaika kutokana na kushupaa kwa masheikh wao na DPW kana kwamba wao ni DPW au wana maslahi nao au ni wanufaika wa mkataba
Hivi Hapa nami naweza kuuliza wakristo wana nini kwa kutoa tamko la TEC? yaani TEC inawakilsha wakristo wote? Nafahamu hapa kwetu madhehebu kadhaa ya kikristo.

Hili la kunufaika nimeshalisema, sitaki kulirejea.
Zingatia wanalaumiwa wote wanaojifungananisha na DPW au mkataba huu akiwamo Mzee wa Upako hadi Phillip Mpango, mkatoliki kindaki ndaki, nk!
Najadili kilichoandikwa sijadili yaliyomo kichwani mwako. Ukishindwa kujenga hoja afadhali utulie tu mkuu. Kama hoja ni wanaojifunganisha na DP yule, na wewe iweje uchanganye waislamu tu. Ni mhemko? Ni kutokujua? Au ugomvi
Kwa hakika ni jukumu letu sisi waislam kuwakana masheikh uchwara hawa bIla kuwasahau wafuasi wao.
Kauli hii ya Kikwete wala haina matatizo. Ulishamsikia Zawadini anasema kuhusu hilo?
.
Hakuna mtu aliye na tatizo na mwislamu au uislam. Kwani wewe unaijua dini yangu, @Ileje, Prof. Shivji na wengi tu wa wasiokubaliana na masheikh hawa? Ila ni kweli kuwa kilichopo, waislam wakikaa kimya bIla kuwakemea masheikh uchwara hawa au wafuasi wao, unategemea nini ndugu kutoka kwa wengine au wale wabaya wetu?
Kusema ni kitu kngine na kutekeleza ni kitu kingine. Mimi nimesemea kauli ya Ileje na kauli yako. Hao wengine sijawahi kuwagusa. Nimesemea hayo kwa kuchanganya kwenu waliomo na wasiokuwemo.

Hili la kutegemea nini kwa wabaya wetu mimi na wewe. Hao wabaya wetu mimi na wewe ni nani?
Wewe unakubaliana na misimamo ya masheikh hawa?
Swali hili umeliuliza mara nyingi nami nikajibu. Sasa najibu kwa mara ya mwsho: Mimi nakubaliana na masheikh wanaposema wanaunga mkono mkataba, iwapo hivyo vipengele vinavyozungumziwa, serikali itaona kuna haja ya kuvifanyia marekebisho au itaamua kuviacha kama vilivyo.
 
Ni kweli kabisa.
Hii ni hatua njema sana kwa hakika. Hapa ikiwa ninakuelewa sawasawa kuwa:

"Sote kwa umoja wetu, na tuwakemee wote wakiwamo masheikh hawa na wafuasi wao kama lengo ni kutaka kutupeleka kwenye ubaguzi ukiwamo wa kidini ambako hakuhusiki kabisa na jambo hili."

Suala la DPW si la dini, kabila, kanda, jinsia, nk. Hili ni suala la kimkataba ambao kama hauna maslahi, haipo shaka kuwa hautufai.

Hapa kwanza nikuulize, wewe ni akina nani? mkristo au mpagani? Nauliza hivi kwa hii kauli yako ya kutumia neno 'wenu' ili nami nijue namna ya kujadilana nawe. Mihemko haitatusaidia mimi na wewe.

JF kuruhusu anonymity yaani kuficha utambulisho wa watu ni pamoja na haya ya udini yasiyo na maana yakiwamo nilipo, kabila, ajira, mtandao wa simu, umri, nk.

Aghalabu dini yangu haibatilishi lolote katika mjadala huu.

Hapa tofautisha waislam na masheikh kwa upande mmoja na masheikh hawa na wafuasi wao ninaothubutu kuwaita uchwara kwa upande mwingine.

Zingatia hata huyu ni sheikh wa kiislam niliye na heshima kubwa kwake:



Kwani wewe wamwona je huyu ndugu?

Matumizi ya neno wenu Wala yasikutie kimuhemuhe.

Kiongozi yeyote ni wenu kama mnaona anawafaa hali sisi wengine tukiona hatufai. Vivyo hivyo ni wetu kama anatufaa hata kama nyie hawafai.

Huu ndiyo ulio uungwana kutokea pande za kwetu kwa kiongozi yeyote: awe mkristo, muislam, baniyani, Buddha, mpagani, nk.

Sasa naona huenda hatujafahamiana. Mimi nimesema kwa Kuwa mkataba haujatekelezwa hauna manufaa. Utamuulizaje mtu huyu mwanao aliyetumboni, bado hajaja duniani unanufaika naye vipi? Halafu utarajie jibu gani?

Kulikoni kuuingia mkataba usio na manufaa au wenye manufaa. Wewe ukiona hauna manfaa, mwingine anaona unayo manufaa.

Hapa ni muhimu sana kutambua hatujafahamiana kabisa. Zingatia mantiki badala ya kucheza na kiswahili ambacho sote sisi ni wabobezi, bila kusahau maneno matupu hayavunji mfupa:

1. Tambua Mikataba ni suala la kisheria.
2. Faida na hasara kwa mkataba huchambuliwa na watalaamu. Nilikuorodheshea manguli wenye kofia za u Prof, DKt na wanasheria wasomi kwenye hilo. Kina yakhe kama mimi na wewe, tupa kule!

Ni wazi kuwa hukunielewa. Kwamba ungali huelewi mbona itakuwa shughuli?

Hasara za mkataba wa DPW ni nyingi na mojawapo ni huko kutokuwa na ukomo kama wabobezi wanavyotwambia.

Faida na hasara hung'amuliwa kitalaamu kabla ya utekelezaji.

Hapa ndiyo maana wenye akili zao wako kimya, kuwaachia manguli wa sheria kuchakata hili vilivyo.

Hivi Hapa nami naweza kuuliza wakristo wana nini kwa kutoa tamko la TEC? yaani TEC inawakilsha wakristo wote? Nafahamu hapa kwetu madhehebu kadhaa ya kikristo.

TEC ni wakristo. Tamko lao halijawakilisha wakristo bali watanzania wote. Humo tumo wakristo, waislam hata na wapagani. Tamko lao tunakubaliana nalo sisi dhidi ya hawa masheikh uchwara na wafuasi wao wenye kutaka kulifanya jambo hili kuwa ni la kidini.

Sisi pamoja na mzee kikwette tunawaasa masheikh hao na wafuasi wao, wasichanganye dini na siasa. Kwamba katu mkataba wa DPW au tamko la TEC halina cha kufanya nao wala, ukristo, uislam, nk kama dini.

Hapa nilikutegemea nawe kuwa upande wetu Ili tushirikiane sote kuwaelekeza kwa staha mamburula hao wasiostaraabika wala kuwa na uelewa wowote.

Hili la kunufaika nimeshalisema, sitaki kulirejea.

Hili la kunufaika si suala la kulisemea. Ni suala la kulielewa. Zingatia ninaongea mantiki na si maneno matupu. Hatua mbele hupigwa mantiki inapoeleweka. Ina maana gani kufanya mazungumzo au majadiliano yasiyokuwa na mantiki?

Kuwa hutaki Kwa sababu hutaki tu? Huko ni kushupaa wakiita kukaza ubongo. Tofautisha kuwa na ubongo na kupania maembe mahala pake.

Najadili kilichoandikwa sijadili yaliyomo kichwani mwako. Ukishindwa kujenga hoja afadhali utulie tu mkuu. Kama hoja ni wanaojifunganisha na DP yule, na wewe iweje uchanganye waislamu tu. Ni mhemko? Ni kutokujua? Au ugomvi

Hakuna nilipokuitisha kujadili yaliyopo kichwani kwangu ambayo unajua wazi kuwa huyajui na hutakaa uyajue. Nilidhani tunajadili ninayoandika hapa na kwa kuamini tunajadiliana kwa malengo yenye tija. Kwa sababu hiyo Siyo Siri kuwa nilikuwa nimeyapa umhuhimu wake majadiliano haya.

Nimekwambia sina na wala hatuna matatizo na dini ya mtu bali masheikh hawa na wafuasi wao wenye kutaka kulifungamanisha suala hili la DPW na uislamu.

Ningependa ulielewe hili Ili tusiwe tunalirudia rudia maana liko wazi mno ndugu yangu. Beberu akiliita "trivial". Ambayo ni sawa sawa na sifuri kujumlisha namba au namba kuzidisha na moja.

Tafadhali kama majadiliano haya Yana umhuhimu wowote kwako pia, tujadiliane tukishawishiana kwa hoja.

Hoja haikimbiwi wala kupiga kwa rungu. Siyo kwa kurukia rukia mambo bila msingi wowote. Huo ndiyo ulio uungwana ndugu yangu.

Kauli hii ya Kikwete wala haina matatizo. Ulishamsikia Zawadini anasema kuhusu hilo?
.
Hii inatia moyo. Hata hivyo ni muhimu kutambua ninachoandika hapa si tu kile ambacho zawadini ana tatizo nacho. Nijulie wapi vyote usivyo na matatizo navyo Ili nisiviweke hapa? Au nijueje vyote ulivyo na matatizo navyo ili tu kuwa ndivyo niviweke hapa?

Kusema ni kitu kngine na kutekeleza ni kitu kingine. Mimi nimesemea kauli ya Ileje na kauli yako. Hao wengine sijawahi kuwagusa. Nimesemea hayo kwa kuchanganya kwenu waliomo na wasiokuwemo.

Kauli yako hii ya tofauti za kusema na kutenda nilishakufahamisha ni potofu. Wewe si malaika. Hapa pia nilikwambia kusema hutangulia kutenda. Hapa tunaandika kwa maana ya kuongea. Tunayoyaandika ndiyo tunayoyaamini, tunayoyasema na kuyatenda. Wewe ni nani kuyahoji tuyasemayo kuwa labda hatutayatenda ndugu? Ileje, mimi, si kuwa tuko peke yetu. Hata kina Prof. Shivji waislam hao, nao ni wenzetu.

Nimesema mara nyingi tatizo letu si masheikh wala waislam bali masheikh uchwara hawa na wafuasi wao. Mbaya zaidi wakiutumia uislam kuwachafua waislam, waislam wenyewe wakiwa wameufyata vilivyo.

Hili la kutegemea nini kwa wabaya wetu mimi na wewe. Hao wabaya wetu mimi na wewe ni nani?

Wabaya wetu nilisha kufahamisha wazi wazi na "link" nikakupa na "like" ukanipa.

Ninaiweka tena hapa kukupa nafasi nyingine ya kujikumbusha nayo kwa raha zako:

Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa

Swali hili umeliuliza mara nyingi nami nikajibu. Sasa najibu kwa mara ya mwsho:

Ninao uhakika sijakuuliza lolote zaidi ya mara moja popote, kama jibu lako limekuwa toshelevu. Ndiyo maana nimelazimika kutumia neno labda kiungwana kila nilipokuwa sina jibu lako la moja kwa moja kwenye lolote ili kufanikisha kuweza kupiga hatua.

"Izingatiwe kama ulivyo wewe hata miye siko nao muda mwingi kiasi hicho, wa kupoteza kwenye jambo au mambo yenye kurudiwa rudiwa pasipokuwa na ulazima wala tija."

Kwamba labda uliulizwa zaidi ya mara moja? Basi tambua jibu lako halikuwa wazi wala kujitosheleza kuweza kuona sehemu hiyo imeeleweka.

Mimi nakubaliana na masheikh wanaposema wanaunga mkono mkataba, iwapo hivyo vipengele vinavyozungumziwa, serikali itaona kuna haja ya kuvifanyia marekebisho au itaamua kuviacha kama vilivyo.

Wewe labda useme hapa unakubaliana na Maaskofu wa TEC maana hao ndiyo wanaosema ulicho summarize hapo juu. Summary hiyo ndiyo yetu sisi sote wa aina ya kina ileje na wote wenye kuwashangaa hao masheikh na wafuasi wao bila exception.

Masheikh hawa na wafuasi wao hakuna wanaposema, kutamka au kuashiria vifungu au vipengele vyovyote vya mkataba huu.

Nimekupa clips mbili au hapa nikuongeze nq nyingine zaidi?

"Nionyeshe wapi wanatamka neno kipengele cha mkataba."

Masheikh hawa na wafuasi wao wanasema udini, ukristo, uislam, nk. Wamejaa Shari dhidi ya TEC na dhidi ya wakristo au yeyote mwenye kuupinga mkataba huu au kuwa na mawazo tofauti na wao.

Ndiyo maana sisi wengine bila kujali dini wala itikadi zetu, tunajiuliza kulikoni ndugu zetu hawa na kupagawa huku?

Hali kadhalika na wewe kama uko nao, au kumbe uko nao tunajiuliza kulikoni ndugu yetu huyu suala hili lisilowahusu waislamu au masheikh mbona kutaka kutuletea uchuro wao ya Rabi?

Kwamba labda wewe ni au si mmoja wapo ndiyo maana nikakualika kistaarabu tujuzane labda tukawaelewa?

Lau wewe si mmoja wao tusaidiane kuwaelewesha kwani kwa mawazo yetu wengine, hawa ndugu kwa wanakoelekea wamepotoka kukubwa (big time).

Kufikia hapa nikadhani niupanue uwanja kwa kuwaita ndugu wastaarabu wengine ili kuwa sehemu ya mjadala huu japo kwa taarifa ikiwapendeza. Hii ikizingatiwa, hii nchi ni yetu sote na hasa kama ungali ukikaza ubongo kama masheikh hayo.

Cc: Pascal Mayalla, Elli, tpaul, Ileje, denooJ na ndugu wapambanaji wengine.
 
Hii ni hatua njema sana kwa hakika. Hapa ikiwa ninakuelewa sawasawa kuwa:

"Sote kwa umoja wetu, na tuwakemee wote wakiwamo masheikh hawa na wafuasi wao kama lengo ni kutaka kutupeleka kwenye ubaguzi ukiwamo wa kidini ambako hakuhusiki kabisa na jambo hili."

Suala la DPW si la dini, kabila, kanda, jinsia, nk. Hili ni suala la kimkataba ambao kama hauna maslahi, haipo shaka kuwa hautufai.



JF kuruhusu anonymity yaani kuficha utambulisho wa watu ni pamoja na haya ya udini yasiyo na maana yakiwamo nilipo, kabila, ajira, mtandao wa simu, umri, nk.

Aghalabu dini yangu haibatilishi lolote katika mjadala huu.

Hapa tofautisha waislam na masheikh kwa upande mmoja na masheikh hawa na wafuasi wao ninaothubutu kuwaita uchwara kwa upande mwingine.

Zingatia hata huyu ni sheikh wa kiislam niliye na heshima kubwa kwake:

View attachment 2727125

Kwani wewe wamwona je huyu ndugu?

Matumizi ya neno wenu Wala yasikutie kimuhemuhe.

Kiongozi yeyote ni wenu kama mnaona anawafaa hali sisi wengine tukiona hatufai. Vivyo hivyo ni wetu kama anatufaa hata kama nyie hawafai.

Huu ndiyo ulio uungwana kutokea pande za kwetu kwa kiongozi yeyote: awe mkristo, muislam, baniyani, Buddha, mpagani, nk.



Hapa ni muhimu sana kutambua hatujafahamiana kabisa. Zingatia mantiki badala ya kucheza na kiswahili ambacho sote sisi ni wabobezi, bila kusahau maneno matupu hayavunji mfupa:

1. Tambua Mikataba ni suala la kisheria.
2. Faida na hasara kwa mkataba huchambuliwa na watalaamu. Nilikuorodheshea manguli wenye kofia za u Prof, DKt na wanasheria wasomi kwenye hilo. Kina yakhe kama mimi na wewe, tupa kule!

Ni wazi kuwa hukunielewa. Kwamba ungali huelewi mbona itakuwa shughuli?

Hasara za mkataba wa DPW ni nyingi na mojawapo ni huko kutokuwa na ukomo kama wabobezi wanavyotwambia.

Faida na hasara hung'amuliwa kitalaamu kabla ya utekelezaji.

Hapa ndiyo maana wenye akili zao wako kimya, kuwaachia manguli wa sheria kuchakata hili vilivyo.



TEC ni wakristo. Tamko lao halijawakilisha wakristo bali watanzania wote. Humo tumo wakristo, waislam hata na wapagani. Tamko lao tunakubaliana nalo sisi dhidi ya hawa masheikh uchwara na wafuasi wao wenye kutaka kulifanya jambo hili kuwa ni la kidini.

Sisi pamoja na mzee kikwette tunawaasa masheikh hao na wafuasi wao, wasichanganywe dini na siasa. Kwamba katu mkataba wa DPW au tamko la TEC halina cha kufanya nao wala, ukristo, uislam, nk kama dini.

Hapa nilikutegemea nawe kuwa upande wetu Ili tushirikiane sote kuwaelekeza kwa staha mamburula hao wasiostaraabika wala kuwa na uelewa wowote.



Hili la kunufaika si suala la kulisemea. Ni suala la kulielewa. Zingatia ninaongea mantiki na si maneno matupu. Hatua mbele hupigwa mantiki inapoeleweka. Ina maana gani kufanya mazungumzo au majadiliano yasiyokuwa na mantiki?

Kuwa hutaki Kwa sababu hutaki tu? Huko ni kushupaa wakiita kukaza ubongo. Tofautisha kuwa na ubongo na kupania maembe mahala pake.



Hakuna nilipokuitisha kujadili yaliyopo kichwani kwangu ambayo unajua wazi kuwa huyajui na hutakaa uyajue. Nilidhani tunajadili ninayoandika hapa na kwa kuamini tunajadiliana kwa malengo yenye tija. Kwa sababu hiyo Siyo Siri kuwa nilikuwa nimeyapa umhuhimu wake majadiliano haya.

Nimekwambia sina na wala hatuna matatizo na dini ya mtu bali masheikh hawa na wafuasi wao wenye kutaka kulifungamanisha suala hili la DPW na uislamu.

Ningependa ulielewe hili Ili tusiwe tunalirudia rudia maana liko wazi mno ndugu yangu. Beberu akiliita "trivial". Ambayo ni sawa sawa na sifuri kujumlisha namba au namba kuzidisha na moja.

Tafadhali kama majadiliano haya Yana umhuhimu wowote kwako pia, tujadiliane tukishawishiana kwa hoja.

Hoja haikimbiwi wala kupiga kwa rungu. Siyo kwa kurukia rukia mambo bila msingi wowote. Huo ndiyo ulio uungwana ndugu yangu.


.
Hii inatia moyo. Hata hivyo ni muhimu kutambua ninachoandika hapa si tu kile ambacho zawadini ana tatizo nacho. Nijulie wapi vyote usivyo na matatizo navyo Ili nisiviweke hapa? Au nijueje vyote ulivyo na matatizo navyo ili tu kuwa ndivyo niviweke hapa?



Kauli yako hii ya tofauti za kusema na kutenda nilishakufahamisha ni potofu. Wewe si malaika. Hapa pia nilikwambia kusema hutangulia kutenda. Hapa tunaandika kwa maana ya kuongea. Tunayoyaandika ndiyo tunayoyaamini, tunayoyasema na kuyatenda. Wewe ni nani kuyahoji tuyasemayo kuwa labda hatutayatenda ndugu? Ileje, mimi, si kuwa tuko peke yetu. Hata kina Prof. Shivji waislam hao, nao ni wenzetu.

Nimesema mara nyingi tatizo letu si masheikh wala waislam bali masheikh uchwara hawa na wafuasi wao. Mbaya zaidi wakiutumia uislam kuwachafua waislam, waislam wenyewe wakiwa wameufyata vilivyo.



Wabaya wetu nilisha kufahamisha wazi wazi na "link" nikakupa na "like" ukanipa.

Ninaiweka tena hapa kukupa nafasi nyingine ya kujikumbusha nayo kwa raha zako:

Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa



Ninao uhakika sijakuuliza lolote zaidi ya mara moja popote, kama jibu lako limekuwa toshelevu. Ndiyo maana nimelazimika kutumia neno labda kiungwana kila nilipokuwa sina jibu lako la moja kwa moja kwenye lolote ili kufanikisha kuweza kupiga hatua.

"Izingatiwe kama ulivyo wewe hata miye siko nao muda mwingi kiasi hicho, wa kupoteza kwenye jambo au mambo yenye kurudiwa rudiwa pasipokuwa na ulazima wala tija."

Kwamba labda uliulizwa zaidi ya mara moja? Basi tambua jibu lako halikuwa wazi wala kujitosheleza kuweza kuona sehemu hiyo imeeleweka.



Wewe labda useme hapa unakubaliana na Maaskofu wa TEC maana hao ndiyo wanaosema ulicho summarize hapo juu. Summary hiyo ndiyo yetu sisi sote wa aina ya kina ileje na wote wenye kuwashangaa hao masheikh na wafuasi wao bila exception.

Masheikh hawa na wafuasi wao hakuna wanaposema, kutamka au kuashiria vifungu au vipengele vyovyote vya mkataba huu.

Nimekupa clips mbili au hapa nikuongeze nq nyingine zaidi?

"Nionyeshe wapi wanatamka neno kipengele cha mkataba."

Masheikh hawa na wafuasi wao wanasema udini, ukristo, uislam, nk. Wamejaa Shari dhidi ya TEC na dhidi ya wakristo au yeyote mwenye kuupinga mkataba huu au kuwa na mawazo tofauti na wao.

Ndiyo maana sisi wengine bila kujali dini wala itikadi zetu, tunajiuliza kulikoni ndugu zetu hawa na kupagawa huku?

Hali kadhalika na wewe kama uko nao, au kumbe uko nao tunajiuliza kulikoni ndugu yetu huyu suala hili lisilowahusu waislamu au masheikh mbona kutaka kutuletea uchuro wao ya Rabi?

Kwamba labda wewe ni au si mmoja wapo ndiyo maana nikakualika kistaarabu tujuzane labda tukawaelewa?

Lau wewe si mmoja wao tusaidiane kuwaelewesha kwani kwa mawazo yetu wengine, hawa ndugu kwa wanakoelekea wamepotoka kukubwa (big time).

Kufikia hapa nikadhani niupanue uwanja kwa kuwaita ndugu wastaarabu wengine ili kuwa sehemu ya mjadala huu japo kwa taarifa ikiwapendeza. Hii ikizingatiwa, hii nchi ni yetu sote na hasa kama ungali ukikaza ubongo kama masheikh hayo.

Cc: Pascal Mayalla, Elli, tpaul, Ileje, denooJ na ndugu wapambanaji wengine.
MUNGU akubariki saaaaaana, umefafanua Kwa weledi na utulivu wa hali ya Juu sana sana. MUNGU akubariki saaaaaana hakika hata Mimi nimejifunza
 
MUNGU akubariki saaaaaana, umefafanua Kwa weledi na utulivu wa hali ya Juu sana sana. MUNGU akubariki saaaaaana hakika hata Mimi nimejifunza

Tuko pamoja mkuu hii nchi ni yetu sote. Watu kama hawa:



Tusiache kuwakemea bila kujali dini zetu.

Cc: Zawadini
 
Tambua Mikataba ni suala la kisheria.
2. Faida na hasara kwa mkataba huchambuliwa na watalaamu. Nilikuorodheshea manguli wenye kofia za u Prof, DKt na wanasheria wasomi kwenye hilo. Kina yakhe kama mimi na wewe, tupa kule!
Ni wapi nilisema mkataba si swala la kisheria?

Hili la faida na hasara kuchambuliwa kitaalamu sijawahi kulikataa au kulibishia. Usizungumze yasokuwepo. Nilichozungmza ni kungizwa sote kuulizwa tunavyonufaika wakati mkataba hata haujatekelezwa. Usizunguke mbuyu.
 
Ni wapi nilisema mkataba si swala la kisheria?

Kwani ukisema kujua faida au hasara za mkataba kufahamika ni hadi utekelezwe, kwamba katu si kabla kumbe maana yake nini ndugu yangu?

Au tangu lini utekelezaji wa lolote kwa minajili ya kupima faida au hasara ukawa wenye ulazima wa kuhitaji unguli kama ule wa kina Shivji ndugu yangu?

Hili la faida na hasara kuchambuliwa kitaalamu sijawahi kulikataa au kulibishia.

Kama hili kumbe walikubali, basi bila shaka utakuwa sasa umeifuta kauli yako kuwa tulikuwa hatujafahamiana..

"Hivyo bila ya shaka sasa utakuwa wauona umhuhimu wa hoja ya bwana Ileje kuwa: kulikoni kumhoji awaye yote kuhusiana ni faida zipi wenzetu wanaoukingia kifua wanaweza kuwa wameziona hata kabla ya utekelezaji wake. Vivyo hivyo na kwa wenye kuziona hasara."

Kwamba hapa sasa rasmi bila ya shaka tutakuwa tumetoka, na tena kwa kauli moja.

Usizungumze yasokuwepo.

Hapa kwa hakika sikuelewi una maana gani?

Ni wazi kuwa tunazungumza yaliyokuwapo ndugu yangu.

"Tuyazungumzie vipi hapa yasiyokuwapo?"

Kulikoni kuanza kuongelea majini au maruhani hapa ambayo uelewa wetu kwake ni wa kufikirika?

Nilichozungmza ni kungizwa sote kuulizwa tunavyonufaika wakati mkataba hata haujatekelezwa. Usizunguke mbuyu.

Hapa tena unajichanganya. Msikie ndugu yetu huyu hapa, kuhusiana na mkataba huu:



1. TICTS walikuwa wakitoa 7 Tr/-?
2. DPW watatoa 27Tr/-?
3. Waziri mkuu ni msemaji wa Serikali?
4. Hoja ya huyu ndugu ni ipi?
5. Makosa ya Shivji ni rangi yake?
6. Anao weledi upi huyu kumtaka Mama Samia kuwapuuza manguli kama Shivji na eti asikizwe mburula yeye kwenye lenye maslahi na nchi hii?
7. Huyu anao weledi gani wa kuyajua yaliyoko kwenye mkataba hata wa kuuza nyanya tu?

Kuuzunguka mbuyu ni nadhani ni kuwaendekeza mburura kama hawa bIla kuwachana live, kwa kujidanganya kuwa eti ni wenzetu.

Hawa si wenzetu. Hawa ni adui zetu na tena ni mzigo Kwa taifa hili.

"Zingatia tulikubaliana tangia awali aliyekuwa akihojiwa na Ileje alikuwa ni sheikh yule si wewe, wala muislam yeyote."

Kumbuka tulikubaliana nawe kuwa hapa tulitokea kujaribu kumjibia au kumnanga kwa vile hayuko JF.

"Kulikoni sasa wewe kutaka kujifanya hili ni lako?"

Si tulikubaliana kuepuka kuihepa hoja kwa kujifanya wakristo au waislam zaidi kwenye hoja isiyokuwa na chembe ya udini?

Humphrey Polepole alikuwa na maneno sahihi kabisa kuwahusu watu kama sheikh huyu na wafuasi wao:

 
Kwani ukisema kujua faida au hasara za mkataba kufahamika ni hadi utekelezwe, kwamba katu si kabla kumbe maana yake nini ndugu yangu?

Au tangu lini utekelezaji wa lolote kwa minajili ya kupima faida au hasara ukawa wenye ulazima wa kuhitaji unguli kama ule wa kina Shivji ndugu yangu?
Na hapa ndo unajibu swali langu?
Hivyo bila ya shaka sasa utakuwa wauona umhuhimu wa hoja ya bwana @Ileje kuwa: kulikoni kumhoji awaye yote kuhusiana ni faida zipi wenzetu wanaoukingia kifua wanaweza kuwa wameziona hata kabla ya utekelezaji wake. Vivyo hivyo na kwa wenye kuziona hasara."
Rejea tena kauli iliyotoka kwa Ileje, halafu ujadili hiyo kauli. Ama hujui maana ya kilichoandikwa au unashupaza shingo; na yote ni tatizo.
Hapa kwa hakika sikuelewi una maana gani?

Ni wazi kuwa tunazungumza yaliyokuwapo ndugu yangu.

"Tuyazungumzie vipi hapa yasiyokuwapo?"

Kulikoni kuanza kuongelea majini au maruhani hapa ambayo uelewa wetu kwake ni wa kufikirika?
Hapa nami naona ajabu; au tumerogwa na ushabiki?
Hapa tena unajichanganya. Msikie ndugu yetu huyu hapa, kuhusiana na mkataba huu:
Ni yaleyale. Sasa kwenye hili na huyu nafunga mdomo kwani nisingependa kujichosha kwa kuwa hatufahamiani kwenye lugha, nami naamini sijadiliani na mtoto mdogo.
Zingatia tulikubaliana tangia awali aliyekuwa akihojiwa na @Ileje alikuwa ni sheikh yule si wewe, wala muislam yeyote."
Rejea tena ya Ileje halafu angalia tena huu mjadala wako.
Kulikoni sasa wewe kutaka kujifanya hili ni lako?"
Hili unalijua jibu lake na hivyo halstahiki kujibiwa nami.
Si tulikubaliana kuepuka kuihepa hoja kwa kujifanya wakristo au waislam zaidi kwenye hoja isiyokuwa na chembe ya udini?

Ni wapi nilihepa hoja. Nimehepa hoja au najadili hoja iliyotolewa?
 
Naona Waraka Sasa umefika Kila pahala, haujamuacha MTU salama! Naam wanaushambulia Kwa hakika though hakuna tangible points hapa!

Masheikh hawa wanaamini Waraka wa TEC utaleta taharuki. Wanafanya reference ya mambo ya ESCROW.

Wanasema tamko la TEC linataka kuleta taharuki Kwa wananchi na chuki Kwa wananchi dhidi ya serikali ya CCM.
Wana uwezo wa kuujadili waraka?
Labda useme wanawajadili watoa waraka.
 
Mwalimu Nyerere kasema,"vijana twendeni vitani"....ooh oooh nalia, nangojea pijooo kupanda.
 
Na hapa ndo unajibu swali langu?
Rejea tena kauli iliyotoka kwa Ileje, halafu ujadili hiyo kauli. Ama hujui maana ya kilichoandikwa au unashupaza shingo; na yote ni tatizo.
Hapa nami naona ajabu; au tumerogwa na ushabiki?
Ni yaleyale. Sasa kwenye hili na huyu nafunga mdomo kwani nisingependa kujichosha kwa kuwa hatufahamiani kwenye lugha, nami naamini sijadiliani na mtoto mdogo.
Rejea tena ya Ileje halafu angalia tena huu mjadala wako.
Hili unalijua jibu lake na hivyo halstahiki kujibiwa nami.

Ni wapi nilihepa hoja. Nimehepa hoja au najadili hoja iliyotolewa?

Kufikia hapa ninadhani tunaweza kufanya majumuisho kwa maswali yote matatu ya bwana Ileje kama alivyokuwa kayaleta kwetu.

Ni muhimu kuwa na kumbukumbu za wazi ya nini tumejadili, nini tumemaliza, nini tumekubaliana na nini kinabakia.

"Tuepuke kurudi nyuma au kurudia tulikokwisha kukubaliana."

Hapa yalikuwa maswali ya ileje na tulipokuwa tumefikia na kwa kauli moja:

Screenshot_20230825-081021.jpg


Tulikuwa tumebakiwa na swali la kwanza tu.

Kumbuka hapa chini yalikuwa maelezo yako kulihusu swali hilo:

Screenshot_20230825-084605.jpg


Kwamba ukisisitiza faida au hasara kwa mtu au kundi ni hadi mkataba umeshatekelezwa tu, na kuwa si vinginevyo.

Hapa pia ukikazia msimamo wako huo:

Screenshot_20230825-091211.jpg


Kwamba hatimaye huyu hapa ni wewe tena kwenye jambo hilo hilo:

Screenshot_20230825-082711.jpg


Utaona kuwa, kufikia hapa
ulikuwa umeridhia uhalali wa faida na hasara kujulikana kitalaamu (kisheria). Hivyo ulikuwa umefika kwenye nafasi sasa ya kujibu swali la bwana ileje, tena pasipokuwa na kigugumizi chochote.

"Kwamba, nikadhani ulichokuwa unachosubiriwa sasa ilikuwa ni majibu yako (ya moja kwa moja) tu kwenye swali hili Moja linalobakia kwa sheikh huyu:"

a)Atueleze waislam mnanufaika vipi na mkataba baina ya Tanzania na Dubai?

Hilo likiwa ni swali kwa sheikh huyu kutokana na maelezo yake ya ufasaha sana haya kwa niaba ya wafuasi wake:



Majibu yako tafadhali.
 
Zawadini si ajabu kuwa majibu hapo juu huna. Bila shaka umejua kuwa kumbe huu si mjadala wa kidini, kiitikadi wala kikanda.

Tambua masheikh uchwara na wafuasi wao wanawakosea sana waislam.

"Ama kwa hakika pana waislam wengi tu wako na watumishi kama huyu:"



Pia wako wengi tu wasiokuwa na mburura kama huyu:

 
Watu wenyewe walivyovaa, hii inaonuesha uwezo wa kiuchambuzi Hawana.Tuwasamehe ila ni uzembe wao wa kutokwenda shule.
 
Back
Top Bottom