Warusi waikimbia ngome nyingine kaskazini kwa Kherson, kama kawa Ukraine waendeleza kipigo


Mkuu hujajibu swali langu: Nimesema hivi tusiwe tuna entertain double standard NATO na USA wanapofanya mambo ya ndio sivyo - Dunia inagugumia kimya kimya,kisa? Muhusika na Merikani an untouchable, lakini linapo kuja suala la Putin na Ukraine US inaiitisha vikao vya UNSC fasta inalazimisha baadhi ya mataifa yaunge mkono madai ya US dhidi ya Russia wanao kataa kuingizwa kwenye camp US wanatishiwa kuwekewa vikwazo na kunyimwa misaada ya maendeleo - yaani Umoja wa Mataifa unageuzwa kuwa kitengo cha ku-support foreign policy za Kimerikani. Je,umoja wa mataifa ulianzishwa kwa madhumuni yepi?Sidhani kama ulianzishwa ili baadae utekwe nyara na na mataifa yenye nguvu kijeshi.
 
Kwamba hayo majimbo sio , America ?


Swali ni: yalipatikana kwa njia zipi, kihalali au kwa kulazimishwa kwa mtutu wa bunduki,kuna evidece gani ya kuthibitisha kwamba majimbo tajwa hapo juu Serikali ya Merikani iliwahi kupisha walao referundum, si walipora kinguvu tu bila ya kuwashirikisha wenyeji - leo hii Merikani na mataifa mengine mazaba zabina wanajaribu kumkalia kooni Putin as if kafanya makosa makubwa sana - wanajifanya kusahau ukatiri na mauuaji NATO/US walio wahi kuyatenda hapa Duniani.
 

Mkuu hata vita ya VietNam US ilishindwa kutokana na msaada wa silaha zilizo kuwa zinatolewa na Urusi - je, Merikani iliwahi kuivimbia Urusi hata siku moja kutoka na msaada wao wa silaha kwa VietCong? Hakuna.
 
Sasa mkuu; hayo unayosema si yalifanyika zamani kama sikosei ilikuwa ni ww11 na mataifa wakaona sio vema na hivyo wakakaa na kukubaliana mipaka ya mataifa mbalimbali itakuwa vipi na ramani zikachorwa na kila nchi ikakubaliana nayo ili amani iwepo. Hoja ya makundi ya kikabila (Ethnic groups) ikakomeshwa na ndo maana yapo baadhi ya makabila yanapatikana ndani na nje ya mipaka ya baadhi ya nchi nyingi duniani.
Kwa mantiki hiyo inakuwa ni kioja na ni kuanzisha vurugu isiyo na tija kwa taifa moja e.g.. Russia kukiuka taratibu za UN kwamba mipaka iliyowekwa iheshimike na kuanza kuchukua maeneo ya nchi jirani ya Ukraine kwa madai kwamba maeneo hayo 4 yanaongea lugha ya Kirusi. Ni sawa na Kenya waanze kudai maeneo ya Longido,Monduli, Namanga au Loliondo kwa madai wapo watu wanaongea Kimaasai huko Kajiado Kenya. Maendeleo yamefikia hatua ya kuachana na Ukabila na kwa sasa ni Utaifa ndo umeshika hatamu.
 
Mkuu hata vita ya VietNam US ilishindwa kutokana na msaada wa silaha zilizo kuwa zinatolewa na Urusi - je, Merikani iliwahi kuivimbia Urusi hata siku moja kutoka na msaada wao wa silaha kwa VietCong? Hakuna.
Ni kweli mkuu ila kwa mwendo huu tukiwa tujadali pasipo mihemko yetu, mkuu bado una imani kuwa Urusi anaweza weka battle na Marekani?
 

Mnacho sahau ni kwamba Ukraine ilikuwa ni sehemu ya Soviet Union - Russia ilikubali wa hiari yake kuiachilia Ukraine iwe huru, hakuna aliye walazimisha Warusi kuipatia uhuru Ukraine, hakuna.

Tatizo la Ukraine linasabishwa kwa kiasi kikubwa na hulka za Zelensky na wafadhili wake wakubwa - mfano kwa nini Zelensky anawatisha tisha ethnic Ruasians kwamba wasizungumze lugha ya kirusi hata wakiwa wanazungumza na
familia zao,je,sisi hapa Tanzania tumewahi kuweka sheria ya raia kukatazwa kuzungumza lugha zao za asili wanapokuwa majimboni mwao ya asili?? Serikali ya Zelensky ilifikia hatua mpaka ya kufunga raia wanao zungumza Kirusi,wakafungia TV ,radio na magezi yaliyo kuwa yanatumia lugha ya Kirusi, sasa mlitegemea raia wa kusini mashariki mwa Ukraine wangefanya nini ili kuepusha unyanyasaji wa Serikali ya Zelensky husio na kifani dhidi yao - ndio maana majimbo hayo ya kusini mashariki yaliomba msaada kutoka kwa jeshi la Putin ili kukomesha udhalimu walio kuwa wanatendewa na Zelensky na gege lake ovu la Azov neo NAZI, hizo ndizo sababu za msingi zilizo ilazimu Russian kuingilia kati, lakini nchi za magharibi zinajifanya kulifumbia macho suala hilo - badala yake kumulaahumu na kumshutumu Putin 24X7. kujifanya wao ni malaika.
 
Super power with Soviet era tactics,
Vifaru msafara kilometer 74 unaviswaga kwenda kyiv....mwenzako anakausha tu msafara usonge..hivi niwaulize nyie Mbagala Russians ule msafara na Askari wake mbona mpaka Leo haujarudi Wala kufika kyiv?
Kwa ufupi hakurudisha kifaru hata kimoja, na pale ndo alipoteza elites wengi maana lengo la ule msafara ulikuwa kumtoa Zelensky Kyiv, hivyo hawakwenda watu waliotoka mafunzoni jana, alipelekea wataalamu haswaa

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Urusi hakumuachia ukraine. USSR ilipovunjika na kusababisha nchi 15 kujitangazia uhuru.
Its not like hizi nchi zilikuwa mateka wa urussi.
 
Hata watu wake wanamshangaa, maana kwa sasa hasongi mbele
Hajui mipaka ya maeneo aliyotwaa

Anarudi nyuma kwa kisingizio cha kujipanga

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Putin ni dhaifu ndio maana anatumia nguvu kubwa sana kujimwambafai resources anazotumia kwenye vita hii ni kubwa mno kuilinganisha na Ukraine
Kwa ufupi kamzawadia Ukraine vifaa vingi sana

Kawapa EU na West zana zake, hivyo wanamsoma kirahisi

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…