Wasafi Media Mtegoni. Diamond, Kusaga wavurugana

Wasafi Media Mtegoni. Diamond, Kusaga wavurugana

Kuna habari JF ni za kusoma tu na kunyuti...

Naona kuna raia wanabishana kuhusu ishu za freq spectrum hadi wanatoleana vitenzi vikurupushi...
Mjadala umekuwa mkali sana, nimechekaaaa.

Halafu hilo la frequency nimeliongeza mwishoni, wala halikuwa lengo la thread.
 
View attachment 2929146Wakurugenzi wa Wasafi Media, Joseph Kusaga na Nassib Abdul ‘Diamond Platinumz’ wanaripotiwa kukosa maelewano kati yao juu ya uendeshaji wa media hiyo inayomilikiwa na wawili hao.

Chanzo ni TRA…
Diamond ambaye amekuwa akitafutwa na maafisa kodi kwa muda mrefu, huku yeye akitumia 'janja janja' kuwakwepa, maafisa kodi hao wamehamishia majeshi kwa Joseph Kusaga.

Joseph Kusaga ambaye majukumu ya uendeshaji amemwachia Diamond, amekuwa akimpigia simu mara nyingi Diamond bila mafanikio.
Hivyo Diamond anawakwepa maafisa kodi, na huku simu za Kusaga pia hapokei.

Kusaga achoshwa na mabifu ya Diamond!
Inaarifiwa kuwa Kusaga amekuwa akilalamika mara nyingi juu ya mabifu ya Diamond na watu wengi ambayo yanaikwamisha Wasafi Media kukua.

Wakati anaanzisha media hiyo 2016, alikuwa na malengo makubwa ya kuikuza kuwa kubwa pengine kuizidi Clouds Media ambayo ni mali ya familia yao. Hivyo kupitia umaarufu wa Diamond alitegemea kuvuna wasikilizaji kutoka kila pembe ya nchi jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limefanikiwa ila kikwazo kikiwa ugomvi wa Diamond na watu wengi ambao wengi hutumia mabifu hayo kama fursa ya kuikwamisha Wasafi Media.

Kusaga Amgeukia Ali Kiba…
Habari za uhakika ni kwamba mastermind huyo wa biashara za vyombo vya habari na nyinginezo lukuki, ameelekeza nguvu zake kwa hasimu wa Diamond, Ali Kiba.

Wawili hao (Kusaga na Ali) wapo kwenye hatua za mwisho kukamilisha masuala muhimu likiwemo jina rasmi la kutumika kuitambulisha Media hiyo.

Kupitia chanzo changu makini nimefanikiwa kunasa jina linalopewa kipaumbele, Kings Media (Kings TV & Kings FM)
Pia watangazaji ambao tayari wameshawekwa kwenye list ni Abdallah Ambua ‘Dullah Planet’ aliyeng’oka EATV na EA Radio hivi karibuni, pamoja na Khalid Mohamed ‘TID’.

Kusaga na utajiri wa frequencies!
Kwa wafuatiliaji wa masuala ya media hasa radio, watakuwa wanafahamu ya kwamba hivi sasa hakuna frequency mpya hapa jijini Dar Es Salaam.

Yaani kwamba ukitaka kuanzisha redio huwezi kupata mawimbi ya kukuwezesha kusikilizwa Dar, labda ununue (frequency) ambayo inamilikiwa na wengine kisha uibadilishe kuwa redio yako.

Wajanja wa mjini wamezihodhi, akiwemo Joseph Kusaga ambaye anaarifiwa kuwa nazo kwa idadi ambayo haifahamiki.

Kupitia chanzo changu nyeti,

Nifah.
Kuna mti mmoja umemsahau Nifah Qchilah alitemwa kwenye Utangazaji na Kamati ya Maandalizi wakasema ana hasira sana hawezi kuhoji wala kutangaza..

Japo nakuamini sana story zako.huwa ni Za ndani sana hasa Za DSTV 😀😀
 
Kuna mti mmoja umemsahau Nifah Qchilah alitemwa kwenye Utangazaji na Kamati ya Maandalizi wakasema ana hasira sana hawezi kuhoji wala kutangaza..

Japo nakuamini sana story zako.huwa ni Za ndani sana hasa Za DSTV 😀😀
Q Chillah skuambiwa, chanzo kiko bize sana ndio maana.

Halafu za DSTV ninazo mpya kibao, basi tu nimechoka kuziandika.
 
Q Chillah skuambiwa, chanzo kiko bize sana ndio maana.

Halafu za DSTV ninazo mpya kibao, basi tu nimechoka kuziandika.
Ndo kisa cha Qchilla kugombana na Diamond maana hilo wazo alilipeleka kwa Wote alikiba na Diamond na chege pamoja na babutale..

Kujadili Chege na Diamond wakaondoa Jina la Qchilla..

Hebu leta za DSTV bhna vipi kuhusu Hii filamu mpya ya Nuru 😀😀
 
Ndo kisa cha Qchilla kugombana na Diamond maana hilo wazo alilipeleka kwa Wote alikiba na Diamond na chege pamoja na babutale..

Kujadili Chege na Diamond wakaondoa Jina la Qchilla..

Hebu leta za DSTV bhna vipi kuhusu Hii filamu mpya ya Nuru 😀😀
Hold on, Chegge ana role gani kwenye hizo Media hadi awepo kwenye maamuzi?
 
Mimi mwenye ni mtaalam hata hapo TCRA nina wataalam ambao nimepiga nao wengine O-Level,A-Level na Chuo. So hizi issue za Stochastic Signals, Diterministic signal,Electromagnetism, sijui Mieletronics, modulation and demodulation,Radio and TV Broadcasting, Transimission nishaachana navyo sababu nipo kwenye field nyingine japo nilivisoma chuo so ninacho kiongea na kijua.

Kwanza kitendo cha kuhold maanake serikali inakosa mapato kwa hiyo frequency yeyewe, pili kupitia hiyo frequency serikali inakosa kodi kupitia wafanyakazi wa hiyo redio sababu nao wanakuwa walipa kodi. Halafu dunia ya sasa technology ipo very sophisticated sio rigid kama mnavyo fikiri.
Mkuu unabisha tu ila huwezi kupata frequency ya DSM kwasaaa TCRA. ndio maana wengi wanachukua za zenji wanafunga Busta dar. Kuhusu kuhodh ipo Sana Kuna jamaa dodom anazo tatu kazi yake ni kuzilipia kodi tu ile ya mwaka..nchi hii uhuni ni mwingi Sana.

Ila Kama unaweza kupata frequency ya DSM njoo PM nitakulipa
 
View attachment 2929146Wakurugenzi wa Wasafi Media, Joseph Kusaga na Nassib Abdul ‘Diamond Platinumz’ wanaripotiwa kukosa maelewano kati yao juu ya uendeshaji wa media hiyo inayomilikiwa na wawili hao.

Chanzo ni TRA…
Diamond ambaye amekuwa akitafutwa na maafisa kodi kwa muda mrefu, huku yeye akitumia 'janja janja' kuwakwepa, maafisa kodi hao wamehamishia majeshi kwa Joseph Kusaga.

Joseph Kusaga ambaye majukumu ya uendeshaji amemwachia Diamond, amekuwa akimpigia simu mara nyingi Diamond bila mafanikio.
Hivyo Diamond anawakwepa maafisa kodi, na huku simu za Kusaga pia hapokei.

Kusaga achoshwa na mabifu ya Diamond!
Inaarifiwa kuwa Kusaga amekuwa akilalamika mara nyingi juu ya mabifu ya Diamond na watu wengi ambayo yanaikwamisha Wasafi Media kukua.

Wakati anaanzisha media hiyo 2016, alikuwa na malengo makubwa ya kuikuza kuwa kubwa pengine kuizidi Clouds Media ambayo ni mali ya familia yao. Hivyo kupitia umaarufu wa Diamond alitegemea kuvuna wasikilizaji kutoka kila pembe ya nchi jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limefanikiwa ila kikwazo kikiwa ugomvi wa Diamond na watu wengi ambao wengi hutumia mabifu hayo kama fursa ya kuikwamisha Wasafi Media.

Kusaga Amgeukia Ali Kiba…
Habari za uhakika ni kwamba mastermind huyo wa biashara za vyombo vya habari na nyinginezo lukuki, ameelekeza nguvu zake kwa hasimu wa Diamond, Ali Kiba.

Wawili hao (Kusaga na Ali) wapo kwenye hatua za mwisho kukamilisha masuala muhimu likiwemo jina rasmi la kutumika kuitambulisha Media hiyo.

Kupitia chanzo changu makini nimefanikiwa kunasa jina linalopewa kipaumbele, Kings Media (Kings TV & Kings FM)
Pia watangazaji ambao tayari wameshawekwa kwenye list ni Abdallah Ambua ‘Dullah Planet’ aliyeng’oka EATV na EA Radio hivi karibuni, pamoja na Khalid Mohamed ‘TID’.

Kusaga na utajiri wa frequencies!
Kwa wafuatiliaji wa masuala ya media hasa radio, watakuwa wanafahamu ya kwamba hivi sasa hakuna frequency mpya hapa jijini Dar Es Salaam.

Yaani kwamba ukitaka kuanzisha redio huwezi kupata mawimbi ya kukuwezesha kusikilizwa Dar, labda ununue (frequency) ambayo inamilikiwa na wengine kisha uibadilishe kuwa redio yako.

Wajanja wa mjini wamezihodhi, akiwemo Joseph Kusaga ambaye anaarifiwa kuwa nazo kwa idadi ambayo haifahamiki.

Kupitia chanzo changu nyeti,

Nifah.
Kuna redio inabifu kma clouds huyo kusaga mwenyewe kadhulumu ndgu zake...madj wake wanabifu na wasanii kibao toka enzi ya ruge
 
Kusaga akiwemo?

Karanga zilikuwa zinatengenezwa na kiwanda kinaitwa Smart Industry Limited...

Hicho kiwanda kiliingia makubaliano na Wasafi/Diamond (kutumia jina lake Diamond + promotion) na pia Big Joe (promotion kupitia media zake)...

Baadaye wakashindwana kwenye kulipana, Diamond kupitia Wasafi akafungua kesi dhidi ya hicho kiwanda na hao wenye kiwanda wakafungua kesi dhidi ya Diamond na Kusaga...

Biashara ikaishia hapo...
 
Kusaga kwenye biashara hana rafiki wala adui, leo yupo na wewe (business partner) kesho anawekeza kwingine biashara hiyohiyo.
Akili kubwa ya biashara ile.
Sasa Dai hapokei simu halafu wanakua wote,inakuja kweli?
Kwanini asimwambie alichotaka kumwambia muda huo wakikutana?
Diamond kwasasa ni mkubwa,hata akiachiwa kile kituo,anaendesha.
 
Hata mimi nahisi hivyo, sikuwa nafahamu mwaliko wa Kusaga kwenye hiyo show yake wakati naandika hapa.

Nimeenda kucheki baada ya kuandika namuona Kusaga na Nape, imekaa kitaalamu sana.
Sana Humuoni na Mkuu wa Mkoa RC..
Pia humuoni Mwana FA huoni Viongozi wa Serkali zaidi ya 12 walioalikwa?
 
Back
Top Bottom