Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Ila sheria ni ngumu sana ... sasa kikao cha ukoo na ndugu kisipokaa itakuwaje??? Nani atateuliwa kuwa msimamizi wa mirathi???... is it not automatic kuwa mke wa marehemu ndio msimamizi wa mirathi directly???... wanasheria tusaidieni.
 
Arusha Mfanyabiashara tajiri wa mawe ndugu Temu amefariki dunia na kuacha kizaazaa nyuma. Bwana huyo ana migodi, magari sita, mashamba, majumba na mahoteli na maviwanja.
Alioa mke aitwae Yasinta ndoa ya kanisani.

Akazaa nae watoto 5 Kama kawa huko chuga hawa mabilionea hua wanapenda chovyachovya.

Baba akazaa nje mtoto wa kwanza akaleta home mke alee, akanogewa akazaa mwingine tena akapeleka nyumbani mkewe alee. Mke akawa hana namna. Kiroho safi analea.
Mke nae amezaa watoto watano tena mmoja mchanga, ukijumlisha wawili wa baba wanakuwa saba.

Mama akaleta housegirl, baba alivyo na tamaa akaanza kutembea na housegirl mpaka akapata mimba. Baba akamfanya mke mdogo, akamjengea na akazaa naye watoto wawili. Yule housegirl ndo akawa na nguvu, mke mkubwa akawa anadharauliwa.

Mke kikawa kinamuuma lakini sasa ndo ashazaa watoto watano akaamua avumilie.

Mara paaap, tajiri kaumwa. Kapelekwa Muhimbili, kwa mapenzi ya Mungu akatwaliwa. Picha ndo ilianzia hapo, mke mkubwa akafika Muhimbili akashangaa anaambiwa na binamu wa mume eti kaa pembeni tutasimamia Mali za watoto na haki zao, akashangaa kiajee Sasa? Lakini kwavile yeye ndo mwenye cheti Cha ndoa akakabidhiwa mwili na cheti cha kifo.

Soma Pia: Arusha: Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauwaji watuma meseji

Ndugu na jamaa na marafiki wakaleta mwili Arusha mochwari ya Mt meru. Mke mkubwa akaelekeza mume azikwe wapi.

Sasa ndugu, marafiki na mke mdogo wakapanga pa kuzika na wakamweka kando bi mkubwa.

Siku ya kuzika bi mkubwa akaingia mahakamani kwa hati ya dharura kuomba zuio na akafanikiwa, issue ilikuwa serious kaburi lishachimbwa, mapadre ikabidi wakafanye Dua pale ya kufunga kaburi tupu na Ile pilau ya msiba wadudu waliifakamia sana.

Sasa leo amri imetolewa na mahakama mke halali amzike mume wake... Housegirl na wale ndugu hawaamini kilichotokea. Eti ndugu na marafiki wanapanga kususia maziko.

Na mke mkubwa amesema mume wangu ni mkristu na ana mke mmoja tu. Akimaliza kuzika anakusanya mali za mumewe baada ya kufungua mirathi.

Housegirl ataambulia simu na cheni za marehemu na nguo..ambazo hata hivyo bi mkubwa anaulizia vipo wapi. Housegirl amegeuka suria..ila wanae watapata mgao wa mali

Wadada wa kazi mnapoenda kufanya kazi kwenye nyumba za watu acheni tamaa kwani hamjui baba na mama wameanzia wapi na wamesotaje kupata mali. Pia ndugu na marafiki acheni upumbavu wa kuingilia mali za marehemu ikiwa ana mke na watoto
Duh kumbe ndivyo ilivyokuwaga? Niliona title kwa millard ila sikufuatilia.
 
shida ilianzia kwa mke mdg kutaka kujiweka mbele angekua mpole haya yasinge mkuta

sema wapambe wake wanamwendesha na kumshauri hovyo wakiwa na lengo apate mali zote wazitumbue

iran na israel wachapane tu tujue moyo sio kukaa na hisia za kibwege bwege za nani atapigwa
Wanawake hao ndio walivyo akipata nafasi ya kuwa mchepuko tayari anajiona mke. Ukiwa mzembe lazma atakuharibia kwa wife akiamini anaweza pindua meza aolewe yeye.

Mungu aniepushe na tamaa za kutamani na kuzaa watoto wa nje. Huleta migogoro sana siku ya msiba.
 
Mabinti waache tamaa, watapigwa na kitu kizito hawatakuwa na pakukimbilia

binti aache tamaa kivipi ? Binti karepiwa ndani weeee, halafu akafanywa mke.

Kazaa watoto wawili, kajengewa nyumba, kabanwa mbavu miaka kibao, tena mwanzoni kwa kurepiwa, kila aina za milalo, milalo ya kisheria na kinyume na kisheria, huyo ni wife, common law wife! Hana tamaa, katoa huduma, anastahili chake!
 
Aache tamaa kivipi ? Binti karepiwa ndani weeee, halafu akafanywa mke.

Kazaa watoto wawili, kajengewa nyumba, kabanwa mbavu miaka kibao, tena mwanzoni kwa kurepiwa, kila aina za milalo, ya kisheria na kinyume na kisheria, huyo ni common law wife! Katoa huduma, anastahili chake, hana tamaa!
Wewe ni mpuuzi.. uwe raped uzae na watoto tena wawili?????...
 
Hio ipo sana arusha, mabinti na wanawake mijanamke ya mjini tena wengine wanatembea na magnjwa kama ukimwi wanamendea waume za watu wenye mali , usipokua makin ukiondoka unaiacha famiilia kwenye migogoro isiyokua na lazima, unawapa shida watoto wako na mkeo pia mana inabid arekebishe usenge wako ulioufanya duniani,
kama una mke tulia na mkeo, n zaid kama una hela mpendezeshe unavyotaka awe kama wengine unaowatamani, hakika hutoweka sehem zako za siri kwa hao mashankupe ya mjini yenye magonjwa lukuki na kutaka mali za bure.
 
Siyo kosa la Mahouse girl! Ni makosa ya Mama wenye nyumba!
Mama ukiruhusu housegirl tayari jua huyo ni mke mwenza wako!
Na wanatafutaga upenyo tu kidogo tu, na mke unaruhusu binti anamfulia boksa mumeo, mara amtengee maji ya kuoga mara chakula, mara akirud ampokee, na faza unaruhusu tu,
na wao wanatafuta maisha wanaangalia fursa penye upenyo anapita na gepu ukishtuka mimba ya miezi 8..mamaeh..
 
Arusha Mfanyabiashara tajiri wa mawe ndugu Temu amefariki dunia na kuacha kizaazaa nyuma. Bwana huyo ana migodi, magari sita, mashamba, majumba na mahoteli na maviwanja.
Alioa mke aitwae Yasinta ndoa ya kanisani.

Akazaa nae watoto 5 Kama kawa huko chuga hawa mabilionea hua wanapenda chovyachovya.

Baba akazaa nje mtoto wa kwanza akaleta home mke alee, akanogewa akazaa mwingine tena akapeleka nyumbani mkewe alee. Mke akawa hana namna. Kiroho safi analea.
Mke nae amezaa watoto watano tena mmoja mchanga, ukijumlisha wawili wa baba wanakuwa saba.

Mama akaleta housegirl, baba alivyo na tamaa akaanza kutembea na housegirl mpaka akapata mimba. Baba akamfanya mke mdogo, akamjengea na akazaa naye watoto wawili. Yule housegirl ndo akawa na nguvu, mke mkubwa akawa anadharauliwa.

Mke kikawa kinamuuma lakini sasa ndo ashazaa watoto watano akaamua avumilie.

Mara paaap, tajiri kaumwa. Kapelekwa Muhimbili, kwa mapenzi ya Mungu akatwaliwa. Picha ndo ilianzia hapo, mke mkubwa akafika Muhimbili akashangaa anaambiwa na binamu wa mume eti kaa pembeni tutasimamia Mali za watoto na haki zao, akashangaa kiajee Sasa? Lakini kwavile yeye ndo mwenye cheti Cha ndoa akakabidhiwa mwili na cheti cha kifo.

Soma Pia: Arusha: Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauwaji watuma meseji

Ndugu na jamaa na marafiki wakaleta mwili Arusha mochwari ya Mt meru. Mke mkubwa akaelekeza mume azikwe wapi.

Sasa ndugu, marafiki na mke mdogo wakapanga pa kuzika na wakamweka kando bi mkubwa.

Siku ya kuzika bi mkubwa akaingia mahakamani kwa hati ya dharura kuomba zuio na akafanikiwa, issue ilikuwa serious kaburi lishachimbwa, mapadre ikabidi wakafanye Dua pale ya kufunga kaburi tupu na Ile pilau ya msiba wadudu waliifakamia sana.

Sasa leo amri imetolewa na mahakama mke halali amzike mume wake... Housegirl na wale ndugu hawaamini kilichotokea. Eti ndugu na marafiki wanapanga kususia maziko.

Na mke mkubwa amesema mume wangu ni mkristu na ana mke mmoja tu. Akimaliza kuzika anakusanya mali za mumewe baada ya kufungua mirathi.

Housegirl ataambulia simu na cheni za marehemu na nguo..ambazo hata hivyo bi mkubwa anaulizia vipo wapi. Housegirl amegeuka suria..ila wanae watapata mgao wa mali

Wadada wa kazi mnapoenda kufanya kazi kwenye nyumba za watu acheni tamaa kwani hamjui baba na mama wameanzia wapi na wamesotaje kupata mali. Pia ndugu na marafiki acheni upumbavu wa kuingilia mali za marehemu ikiwa ana mke na watoto
Nyumba ikigonga gari ni habari ila gari ikigonga nyumba si habari..kati ya ndugu 'bilionea marehemu' na house girl nani alimuanza mwenzie?
 
Back
Top Bottom