Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Aache tamaa kivipi ? Binti karepiwa ndani weeee, halafu akafanywa mke.

Kazaa watoto wawili, kajengewa nyumba, kabanwa mbavu miaka kibao, tena mwanzoni kwa kurepiwa, kila aina za milalo, ya kisheria na kinyume na kisheria, huyo ni common law wife! Katoa huduma, anastahili chake, hana tamaa!
Unajua maana ya mke? Mke ni kwenye karatasi, ndio ushahidi unaompa uhalali kwenye kila kitu kuhusu mume wake, awe hai asiwe hai. Kuzaa na mtu, kujengewa sio hoja, na hakuna cha common law kama kuna mke halali wa makaratasi. Huyo binti ameshavuna alichopanda, akae kwa kutulia. Alipanda uharibifu, amevuna uharibifu

Wazungu wanasema.. Play stupid games, win stupid prizes
 
Hii naona ndio taarifa iliyo nyooka kuliko zingine,na sentensi ya mwisho umeimalizia vizuri kabisa kabisa.
Nionavyo;
-Dada wa kazi hakuwa na kosa/hana kosa.Baba wa familia, mume wa ndoa ndio tatizo hapo.
-Mke mdogo kutaka kuzika bila kumshirikisha mke mkubwa, naona kuna njama za ndugu wa mume.
Mke mdogo katumika tu.
 
Arusha Mfanyabiashara tajiri wa mawe ndugu Temu amefariki dunia na kuacha kizaazaa nyuma. Bwana huyo ana migodi, magari sita, mashamba, majumba na mahoteli na maviwanja.
Alioa mke aitwae Yasinta ndoa ya kanisani.

Akazaa nae watoto 5 Kama kawa huko chuga hawa mabilionea hua wanapenda chovyachovya.

Baba akazaa nje mtoto wa kwanza akaleta home mke alee, akanogewa akazaa mwingine tena akapeleka nyumbani mkewe alee. Mke akawa hana namna. Kiroho safi analea.
Mke nae amezaa watoto watano tena mmoja mchanga, ukijumlisha wawili wa baba wanakuwa saba.

Mama akaleta housegirl, baba alivyo na tamaa akaanza kutembea na housegirl mpaka akapata mimba. Baba akamfanya mke mdogo, akamjengea na akazaa naye watoto wawili. Yule housegirl ndo akawa na nguvu, mke mkubwa akawa anadharauliwa.

Mke kikawa kinamuuma lakini sasa ndo ashazaa watoto watano akaamua avumilie.

Mara paaap, tajiri kaumwa. Kapelekwa Muhimbili, kwa mapenzi ya Mungu akatwaliwa. Picha ndo ilianzia hapo, mke mkubwa akafika Muhimbili akashangaa anaambiwa na binamu wa mume eti kaa pembeni tutasimamia Mali za watoto na haki zao, akashangaa kiajee Sasa? Lakini kwavile yeye ndo mwenye cheti Cha ndoa akakabidhiwa mwili na cheti cha kifo.

Soma Pia: Arusha: Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauwaji watuma meseji

Ndugu na jamaa na marafiki wakaleta mwili Arusha mochwari ya Mt meru. Mke mkubwa akaelekeza mume azikwe wapi.

Sasa ndugu, marafiki na mke mdogo wakapanga pa kuzika na wakamweka kando bi mkubwa.

Siku ya kuzika bi mkubwa akaingia mahakamani kwa hati ya dharura kuomba zuio na akafanikiwa, issue ilikuwa serious kaburi lishachimbwa, mapadre ikabidi wakafanye Dua pale ya kufunga kaburi tupu na Ile pilau ya msiba wadudu waliifakamia sana.

Sasa leo amri imetolewa na mahakama mke halali amzike mume wake... Housegirl na wale ndugu hawaamini kilichotokea. Eti ndugu na marafiki wanapanga kususia maziko.

Na mke mkubwa amesema mume wangu ni mkristu na ana mke mmoja tu. Akimaliza kuzika anakusanya mali za mumewe baada ya kufungua mirathi.

Housegirl ataambulia simu na cheni za marehemu na nguo..ambazo hata hivyo bi mkubwa anaulizia vipo wapi. Housegirl amegeuka suria..ila wanae watapata mgao wa mali

Wadada wa kazi mnapoenda kufanya kazi kwenye nyumba za watu acheni tamaa kwani hamjui baba na mama wameanzia wapi na wamesotaje kupata mali. Pia ndugu na marafiki acheni upumbavu wa kuingilia mali za marehemu ikiwa ana mke na watoto
Kifo cha mmoja ni kumbusho kwa tuliobaki,
Kuna mengi ya kujifunza
 
Victim blaming. Unalalamikia house maids na ndugu badala ya mtu mwenyewe? Alilazimishwa kulala kila Kona na kuzaa nao? Hapo tatizo ni marehemu mwenyewe. Siku mkijua kukubali full accountability ya matendo yenu mtaendelea.
 
Chukua cash at bank gawa kwa idadi ya watoto kila mtoto apate zake. Sheria ya mirathi kama baba hakuacha wosia wa maandishi mtoto wa kiume mkubwa wa mke wa ndoa ndo msimamizi wa mirathi kama mke wa ndoa hana mtoto wa kiume wataangalia ni mke gani mwenye mtoto wa kiume mkubwa.
Hiyo sheria ni ki#£@m@&*÷o kweli
Ina maana watoto wa kike hawana kauli kwenye mali ya baba yao
 
Kila siku waifu akiniambia anataka alete beki 3 namuangalia kwa huruma sana.
Bora alete ndugu yake amsaidie kazi kuliko bek3.
Unam~Zoom Halafu Unasema
Kusikia Kwa Kenge Mpaka Atoke Damu Puani Na Masikioni
 
Arusha Mfanyabiashara tajiri wa mawe ndugu Temu amefariki dunia na kuacha kizaazaa nyuma. Bwana huyo ana migodi, magari sita, mashamba, majumba na mahoteli na maviwanja.
Alioa mke aitwae Yasinta ndoa ya kanisani.

Akazaa nae watoto 5 Kama kawa huko chuga hawa mabilionea hua wanapenda chovyachovya.

Baba akazaa nje mtoto wa kwanza akaleta home mke alee, akanogewa akazaa mwingine tena akapeleka nyumbani mkewe alee. Mke akawa hana namna. Kiroho safi analea.
Mke nae amezaa watoto watano tena mmoja mchanga, ukijumlisha wawili wa baba wanakuwa saba.

Mama akaleta housegirl, baba alivyo na tamaa akaanza kutembea na housegirl mpaka akapata mimba. Baba akamfanya mke mdogo, akamjengea na akazaa naye watoto wawili. Yule housegirl ndo akawa na nguvu, mke mkubwa akawa anadharauliwa.

Mke kikawa kinamuuma lakini sasa ndo ashazaa watoto watano akaamua avumilie.

Mara paaap, tajiri kaumwa. Kapelekwa Muhimbili, kwa mapenzi ya Mungu akatwaliwa. Picha ndo ilianzia hapo, mke mkubwa akafika Muhimbili akashangaa anaambiwa na binamu wa mume eti kaa pembeni tutasimamia Mali za watoto na haki zao, akashangaa kiajee Sasa? Lakini kwavile yeye ndo mwenye cheti Cha ndoa akakabidhiwa mwili na cheti cha kifo.

Soma Pia: Arusha: Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauwaji watuma meseji

Ndugu na jamaa na marafiki wakaleta mwili Arusha mochwari ya Mt meru. Mke mkubwa akaelekeza mume azikwe wapi.

Sasa ndugu, marafiki na mke mdogo wakapanga pa kuzika na wakamweka kando bi mkubwa.

Siku ya kuzika bi mkubwa akaingia mahakamani kwa hati ya dharura kuomba zuio na akafanikiwa, issue ilikuwa serious kaburi lishachimbwa, mapadre ikabidi wakafanye Dua pale ya kufunga kaburi tupu na Ile pilau ya msiba wadudu waliifakamia sana.

Sasa leo amri imetolewa na mahakama mke halali amzike mume wake... Housegirl na wale ndugu hawaamini kilichotokea. Eti ndugu na marafiki wanapanga kususia maziko.

Na mke mkubwa amesema mume wangu ni mkristu na ana mke mmoja tu. Akimaliza kuzika anakusanya mali za mumewe baada ya kufungua mirathi.

Housegirl ataambulia simu na cheni za marehemu na nguo..ambazo hata hivyo bi mkubwa anaulizia vipo wapi. Housegirl amegeuka suria..ila wanae watapata mgao wa mali

Wadada wa kazi mnapoenda kufanya kazi kwenye nyumba za watu acheni tamaa kwani hamjui baba na mama wameanzia wapi na wamesotaje kupata mali. Pia ndugu na marafiki acheni upumbavu wa kuingilia mali za marehemu ikiwa ana mke na watoto
Hizi ndizo sababu zinazofanya familia za watu weusi zishindwe kurithishana utajiri kutoka kizazi kimoja kwenda kingine, huku ni kukosa discipline kwa matajiri wetu weusi
Sijawahi kuona wala kusikia tajiri abood ana nyumba ndogo au mambo kama haya
Na abood na ndugu zake wanaishi kwenye same household ,very disciplined hawa wenzetu ,mswahili akipata pesa basi atataka kutomba mademu wote mjini bila ya kuangalia shida atakayoipa kizazi chake, sasa hawa wanawake wataishia kumaliza hela mahakamani na kurogana , typica africans
 
Siku ya kuzika bi mkubwa akaingia mahakamani kwa hati ya dharura kuomba zuio na akafanikiwa, issue ilikuwa serious kaburi lishachimbwa, mapadre ikabidi wakafanye Dua pale ya kufunga kaburi tupu na Ile pilau ya msiba wadudu waliifakamia sana
View attachment 3113672
Siku ya kuzika bi mkubwa akaingia mahakamani kwa hati ya dharura kuomba zuio na akafanikiwa, issue ilikuwa serious kaburi lishachimbwa, mapadre ikabidi wakafanye Dua pale ya kufunga kaburi tupu na Ile pilau ya msiba wadudu waliifakamia sana
View attachment 3113672
😂
 
Nimeshuhudia picha kama hili.

Ila kilichotokea ni mke mkubwa na watoto kumtenga mume.

Mume akaondoka home, akaenda kuoa mke mwingine.

Alipofariki vikaanza vita vya mali.
 
Mahakama huwa haichagui msimamizi wa mirathi. Bali inamthibitisha tu.

Ni ndugu wenyewe ndio mtampendekeza kwenye muhtasari wa kupeleka mahakamani.

Na ukifoji tu msala
Na kama huyo mke hatakaa vizuri na ndugu, muhtasari kuupata inakuwa kimbembe. Hizi mali zitaua watu. Malumbano yote hayo ni sababu aliyekufa ni yajiri, angekuwa kapuku, hata michango ya msiba inausua sua, na watu wakizika tu hakuna anayetaka hata kujua watoto wa marehemu watasaidiwaje
Sikaki mali ya mtu mimi. Vya kwangu vinanitosha.
 
Back
Top Bottom