Uchaguzi 2020 Washauri wa Lissu mitandaoni wana tatizo kubwa la kiufahamu

Natamani sana wagombea walio serious hasa wa Ccm, Cdm na Act wafanyiwe mdahalo maalumu . Ili uwezo wa hawa watu uwe wazi kwa kila mTz.

Lakini naamini kijani hawatakuwa tayari .
Hakuna mgombea mwenye maono kama JPM. Kuingia kwenye mdahalo na Lissu na Membe ni kujidharirisha.
 
mkuu mbona unaruka ruka tu na hueleweki "umesema wasimpangie cha kusema au cha kufanya" why wewe unataka kuwapangia wana jf chakuongea? waachwe watu wazungumze mitizamo yao wala haitaleta athari katika upande wowote...

hakunaga mchuano usiokua na mbwembwe hivo hizo tambo za maneno ndo mbwembwe za uchaguzi, tuweni wafuasi wazuri tusio na mihemko yakuwalimit wengine cha kusema akati wao hatulimit chakusema.
 
Kuna Hardtalk moja ya BBC na Mh Lissu kuhusu Homosexuality...pale nilifunga imani yangu yote kwake yule msela
 
Je umezingatia hii aya!?


Kuna wakati ni sahihi watu kuandika mitazamo na mawazo yao lakini isifike ukampangia mtu cha kusema ama cha kufanya...kila mmoja ana hulka yake...na hulka hazifanani hata kama nyie ni pacha
 
Nimeisoma mkuu.
Siyo kwamba mtu anakupangia cha kusema lakini anakuonesha pale ambapo hujaona kwa maana hakuna mtu mkamilifu kama ulivyosema kila mtu na hulka yake.

Anakuonesha hali halisi inakutaka useme na ufanye nini kwa wakati huo. Hulka ya mtu haiwezi kuwa utetezi ukizingatia huyo mtu anaomba tumpe nguvu ya kisheria au uhalali wa kuidhinisha kifo cha mtu kisheria, anaomba tumpe nguvu ya kauli yake aweze kuamrisha watu waende vitani na huko unazungumzia maisha ya watu.

Yaani hapo namzungumzia mtu ambae anaweza kuwa raisi na kusaini hukumu ya kifo, anaweza kuwa amiri jeshi mkuu akatuma majeshi yaende vitani kwa neno lake tu.

Such important person must be impeccable with his word, He can not be driven by his own negative or bad characters (hulka). Kifupi ni kama kila anayekupa kura anakupa uamue hatima ya maisha yake na ya nduguze wasioweza kupiga kura.

Ikiwa mtu kama huyo anaendeshwa na hulka yake ambayo inaweza kuwa siyo nzuri au siyo rafiki na dhamana kubwa anayopewa inaweza kuwa hatari na majanga kwa taifa.
 
[emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545]nimekupata vema sana..japo hapo kwenye hulka nadhani kwa mchujo na michakato chama iliyopitia naona wamejiridhisha
 
Natamani sana wagombea walio serious hasa wa Ccm, Cdm na Act wafanyiwe mdahalo maalumu . Ili uwezo wa hawa watu uwe wazi kwa kila mTz.

Lakini naamini kijani hawatakuwa tayari .

Kwa mgombea kutokuwa tayari kutokea kwenye mdahalo hiyo ni rasmi kuwa hafai.

Hana cha kueleza hana cha kutupa ndiyo maana atalazimika kuingia mitini.

Mdahalo ni fursa ya mgombea kueleza sera zao. Asiyetaka kutumia fursa hii ni ishara kuwa itakuwa hana Mpango wa kutupa tunayotaka kama wapiga kura. Yaani hitajio letu la mgombea:

 
[emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545]nimekupata vema sana..japo hapo kwenye hulka nadhani kwa mchujo na michakato chama iliyopitia naona wamejiridhisha
Chama hawajakosea kumpa awawakilishe sababu yalikuwa maamuzi ya wengi ndani ya chama tunaamini walikuwa sahihi, muhimu hapo yeye kama mwakilishi wa chama kuna wakati lazima afuate kile alichotumwa na chama.
Hapo namaanisha chama ndiyo kiratibu afanye nini, wapi na aseme nini, ingawa kuongeza yake binafsi si vibaya mradi ahakikishe hatavuruga malengo na taswira ya chama chake.

Alamsiki mkuu.
 
Asante [emoji1545][emoji1545][emoji1545]...uwe na usiku mwema...
 
Mashana ulijiandikisha kupiga kwenye daftari la mpiga kura?. Nakumbuka nilitumia nguvu nyingi sana kuwazuia wafuasi wenu.
 
Nasubiri baada ya uchaguzi nione komenti zako.
Ndiyo maana nasema wallah mwaka huu nimeamua kwenda kudhalilika na foleni la njaa ya kutwa nzima siku ya uchaguzi.

Tufanye sasa hii ni kama ligi.

Nataka kuongeza nguvu ya kukata ngebe mwaka huu, ninataka upande ninaoushabikia ukishindwa uniguse na nijihisi kuwa nimeshindwa mimi.

Ninajua tutashinda kwa haki asubuhi na mapema hata kabla kura hazijamalizika kuhesabiwa, isipokuwa sasa nataka mazingira ya upigaji kura na kuhesabu kuwekwe wazi ili baada ya matokeo mtu asije kuleta fyoko fyoko zake kwa kisingizio cha kuporwa,awe kama amemwagiwa maji ya mtungini asubuhi ya kipupwe atoke ameufyata.

nitamlaani sana yeyote atakayechezesha rafu za matokeo kama ilivyokuwa kwa serikali za mtaa, huyo asivumiliwe na afanywe ni adui na1 wa taifa asulubishwe, tunataka uchaguzi ulio huru na haki.

Mimi nataka Jpm ashinde na atashinda tu kwa sababu upinzani wameshanyang'anyana kura tayari, wameshindwa kuweka mgombea mmoja ili wampigie mbiu ya sapoti.

Eti kila kiongozi wa upinzani anautaka urais!

Wengine aibu watakazoambulia baada ya matokeo, zitafanana kwa karibu na aibu za matokeo ya kura za maoni za wagombea nafasi za kuchaguliwa ubunge!

Hivi kuna faida gani kugombea nafasi ya uraisi huku ukijua kabisa unaenda kushindwa?

Ama ni hizi posho na ruzuku?

Tuombe afya njema Mungu atuwezeshe kufika mwezi wa 10 kutokomeza ubishi huu.
 
Hahaaaa umemaliza kila kitu na nyengine hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…